JavaScript

This website requires the use of Javascript Explain This   to function correctly. Performance and usage will suffer if it remains disabled.
Hifadhi ili kusoma baadaye
Inapatikana katika lugha hizi:
Liko Wapi Kanisa la Mungu Leo hii?
Photo of a CongregationNew York, Marekani Photo of a CongregationJamaika Photo of a CongregationPeru Photo of a CongregationIdaho, Marekani Photo of a CongregationIndia Photo of a CongregationUbelgiji Photo of a CongregationKenya Photo of a CongregationArkansas, Marekani Photo of a CongregationAfrika Kusini Photo of a CongregationUingereza Photo of a CongregationNigeria Photo of a CongregationOhio, Marekani

Yesu alisema, “Nitalijenga Kanisa Langu.†Kuna shirika moja linalofundisha ukweli wote wa Biblia, na limeitwa kuishi kwa “kila neno la Mungu.†Je, unajua namna ya kulipata? Kristo alisema lita:

  • Fundisha “yote†Aliyoagiza
  • Kuwa na washiriki walioitwa na kuwekwa wakfu kwa ile kweli
  • Kuwa “kundi dogoâ€
Habari za Mwandishi
Photo of David C. PackDavid C. Pack 

Mwanzilishi na Mchungaji Mkuu wa Kanisa la Mungu Rejeshwa, Mhariri-Mkuu wa Jarida la Ukweli Halisi, na sauti ya programu ya Ulimwengu Ujao, Daudi C. Pack amewafikia mamilioni wengi ulimwenguni na kweli za Biblia zilizo na nguvu sana—zisizojulikana karibu kwa wote. Ameandika vitabu na vijitabu 80, mwenyewe ameanzisha zaidi ya mikusanyiko 50, na alionekana kama mgeni kwenye Kituo cha Historia (The History Channel). Bwana Pack alihudhuria Chuo cha Mabalozi huko Pasedena, Kalifonia, aliingia katika huduma ya Kanisa la Ulimwengu Mzima mwaka 1971, na yeye binafsi alifundishwa na mwanzilishi wake, Herbert W. Armstrong.

Uwezekano Wa Kustaajabisha Wa Mwanadamu

na David C. Pack

Jiandae kuduwazwa—kustaajabishwa amini usiamini! Ukweli wa ajabu umebaki mafichoni—umezuiliwa—usieleweke kwa wanadamu wote kwa miaka 2,000. Ulimwengu uliodanganywa umezuiliwa usielewe KIJENZI MUHIMU KINACHOKOSEKANA katika kumaliza matatizo ya mwanadamu. Wanasayansi, wanateolojia, waelimishaji na wanafalsafa wamebaki kuwa wajinga kuhusu ukweli wa kwa nini mwanadamu yupo. Na bado, UKWELI HUU WA KUSHANGAZA—MAARIFA HAYA YA AJABU—yamekuwepo wakati wote. Lakini walio wengi hawaelewi watafute wapi. Kristo alikuja kama MLETA HABARI akifunua matukio yajayo—akifafanua kabla HABARI NJEMA kwa ajili ya wanadamu wote. Hii ndiyo simulizi ya kushangaza ya injili ya kweli ambayo Aliileta—na jinsi inavyokuhusisha WEWE!

Utangulizi

Tumaini la kila Mkristo ni siku moja kupokea “wokovuâ€, huku wengi wakidhani kwamba “kwenda mbinguni†ndio thawabu kubwa kabisa anayoweza kupata kila mtu duniani. Hiki ndicho kinachoonekana kuwa kilele—mafanikio ya juu kabisa na ridhaa hitimishi!—ya majaaliwa ya mwanadamu.

Lakini je, hii ni kweli? Au kuna kitu kikubwa zaidi kilicho mbele ya kila mwanadamu aliyepata kuzaliwa?

Wazo la “kuelekea mbinguni†limejengwa katika udhanifu wa kizamani—juu ya kile ambacho wengi wameambiwa kwamba Biblia inasema kuhusu maisha baada ya kifo. Matokeo yamekuwa kwamba, wachache wanaofikiri juu ya kilichoko mbele baada ya maisha haya, hawaongelei juu ya “uwezekano†mwingine wowote, iwe kwa mtu mmoja mmoja, ama kwa ubinadamu, kwa jumla. Hata hivyo wachache ndio wanaotaka kutumia muda kuupata UNDANI!

Ukweli wa kushangaza ni kwamba Biblia hufundisha kitu tofauti kabisa—na KIKUBWA MNO!—kuliko mtazamo huu pendwa unaoaminiwa na wengi miongoni mwa watu wanaohudhuria makanisa yote yanayojulikana sana leo.

Tatizo ni hili hapa—hii ndiyo sababu kwamba ni wachache wanafahamu sababu ya kuzaliwa kwao. Watu wengi kamwe hawajishughulishi wenyewe na MASWALI MAKUBWA KABISA ya maisha mpaka wanapokabiliwa na kifo, ama chao wenyewe au cha mtu wao wa karibu. Hata hapo vilevile, wengi huwa na shauku ya juu juu. Wale wachache ambao wako tayari kuchukua mtazamo wa karibu juu ya namna gani wataishi milele yote hawajui mahali pa kupata MAJIBU DHAHIRI kwa maswali yao. Hii ni kwa sababu ama hawajui jinsi ya kujifunza Biblia wao wenyewe au wanaamini kuwa wanapaswa kusikiliza majibu ya “watu wasomi†ambao “wamefundishwa†na ambao “wanajua habari ya mambo haya.†Na wameagizwa “kukubali kwa imani†mambo yanayohusu kile kitakachotokea baada ya maisha haya wakiambiwa kwamba hayawezi kueleweka.

Cha kusikitisha, wakitumia njia rahisi, wengi kwa kupenda hubaki vipofu, wanakubali yasiyo-majibu bila wao kupinga.

Mataifa ya dunia yanapiga mbio kuelekea wakati wa mwisho, msukosuko wa kutisha wa ulimwengu—mgogoro uliotabiriwa kutokea mwishoni mwa zama hii. Kuongezeka kwa hofu ya vita, ughaidi, njaa, magonjwa, jinai, uchafuzi wa mazingira, kuvunjika kwa familia, na matatizo mengine yanayoonekana kutotatulika yanayozidi kuwa mabaya zaidi, yakiwahusisha wengi zaidi na zaidi, na hali hii inakumba mataifa yote.

Ushahidi ni mwingi sasa kwamba mwisho wa ustaarabu uliopo umekaribia. Wengi wanaoshangaa “Hali hii yote inaelekea wapi?â€, “Mungu anafanya nini?†na “Je, hii ndio yote iliyopo?†wanataka majibu ya wazi—DHAHIRI!—yanayothibitika kwa maswali haya na mengine yanayofanana nayo.

Swali kubwa kabisa ni “Je, Mungu ana MPANGO MKUU?â€, na kama jibu ni ndiyo, mpango huo ni nini? Jibu ni kwamba Anao, na umebeba mambo mengi mazito ya kusisimua—ambayo UNAWEZA kuyajua yote. Utajifunza kwamba kusudi la Mungu halitanguki, kwamba haliwezi kupinduliwa au kushindwa.

Unaweza pia kujua sehemu yako ndani yake. Kwa hakika, kama utasoma kitabu chote, utajua hivi punde.

Kitabu hiki kinajibu kila moja ya maswali muhimu ambayo yanatakiwa kuwa katika mawazo yako, kikijumuisha mengine mengi ambayo usingeweza hata kupata kuyauliza—lakini unahitaji kuyafahamu. Hakuna unachokitarajia [unachokitazamia] katika moja ya majibu yote. Wala majibu haya si yale ambayo “wasomi†wanaoitwa “wanazuoni na wanateolojia†hufundisha, kwa sababu hakuna wanaoweza kufundisha kile ambacho kamwe hawakufundishwa—kile ambacho kamwe hawakuwahi kujifunza.

Uliwekwa duniani kutimiza KUSUDI LA KUSTAAJABISHA—unashikilia uwezekano ambao unapita mbali sana matazamio yako yote makuu uliyonayo. Jiandae sasa KUDUWAZWA kuhusu ni nini hasa—na KUVUVIWA kupita mawazo yako ya juu kabisa!

Sura ya Kwanza – Jinsi Ambavyo Dini Imezuia Ujumbe wa Kristo Kwa Miaka 2,000!

Ukweli wa injili—kusudi la Mungu la kushangaza kwa ajili ya mwanadamu—umefichwa kutoka kwa ulimwengu. Huelezea kwa nini ulizaliwa. Ni maarifa ya ajabu sana yatakayokuacha mdomo wazi! Ufahamu huu wa kustaajabisha sasa umefunuliwa—sambamba na njama za kuuhafifisha!

Mabilioni sasa wamedanganywa, vivyo hivyo mabilioni huko nyuma. Hata wewe umeambiwa uongo. Ushawishi kamili umetokea, na dini zote za ulimwengu zimechangia katika hili. Maarifa ya mustakabali wako wa ajabu—UWEZEKANO wako wa KUSTAAJABISHA—umefichwa kutoka kwako!

Wengi hushangaa na kuwa na wasiwasi kuhusu yasiyojulikana—na nini kiko katika mustakabali wao. Wengine wana hofu kwamba hata hawana mustakabali. Bado wengine wanahofu kwamba ustaarabu hauna mustakabali. Huhitaji kamwe tena kuwa katika mashaka kuhusu mustakabali wako—au wa ubinadamu.

Laiti kama ubinadamu ungejua kile ambacho Mungu ameuandalia! Ila uzuiaji wa makusudi wa ukweli umeficha maarifa haya kutoka machoni pa wengi isipokuwa kwa wachache. Unaweza kuwa tofauti—mmoja wa wachache ambao hawajadanganywa!

Ulimwengu umeamini injili ya uongo kwa miaka 2,000. Kwa ujumla umechukulia kwamba Yesu Kristo ndiye injili badala ya Mjumbe wake. Ujumbe—kiini—cha injili siyo Kristo. Kwa kusisitiza juu Yake—Mjumbe—walaghai wa kidini wamefaulu kuuzuia na kuufunika Ujumbe Aliouleta!

Maarifa muhimu ya jinsi ambavyo mwanadamu angekuwa ametatua matatizo yake na kuuelewa Mpango Mkuu wa Mungu yamefichwa kutoka kwa ulimwengu, yakiuacha gizani. Mwanadamu hajui yeye ni nini au sababu ya kuwepo kwake. Hajui njia ya mafanikio tele, amani na mambo yote mema maishani. Injili ingekuwa imemwonyesha mwanadamu suluhisho kwa matatizo yake tele yasiyotatulika.

Na bado, isipokuwa mtume Yohana, mitume wengine wote wa awali waliuawa kwa ajili ya kufundisha ukweli wa kusudi la Mungu la kustaajabisha. Yesu alisulubishwa kwa sababu watu hawakutaka kusikia Ujumbe Wake!

Ufahamu sahihi wa injili ya kweli hufunua maarifa ya muhimu sana. Hujumuisha upana wa uelewa ambao hauwezi kugunduliwa kwa uchunguzi wa kisayansi. Kila inayofikiriwa kuwa “dini kuu†ya ulimwengu imesaidia kuuhafifisha. Wanateolojia wao hawaelewi wala hawako tayari kuufundisha. Tutaona kwamba wameuzuilia ufunguo mkuu unaofungua kusudi la kuwepo kwako—UWEZEKANO WAKO WA KUSTAAJABISHA!

Jinsi gani hii ilitokea? Na ni nani aliye nyuma ya uzuiaji huu wa maarifa?

Mdanganyifu Mkuu

Kwa wasioelewa, Biblia ni kitabu chenye kauli za kushtua. Hufunua ukweli wa kushtusha, usioeleweka kabisa hata kwa wale wanaodai kuifahamu. Lakini kuna kauli chache zinazoduwaza zaidi ya ile inayopatikana katika Ufunuo 12:9. Fungu hili husema moja kwa moja kwamba mwovu Shetani—ambaye yuko—“audanganyaye ulimwengu WOTE.â€

Akiwa “mfalme wa UWEZO wa anga†(Efe. 2:2), Shetani ameshawishi, ongoza, tawala na kuwadanganya kabisa halaiki wasiotilia shaka.

Kwa hakika huu ni ufunuo wenye kuduwaza—kiasi kwamba wengi kirahisi tu huupuuzia au kuukataa, wakiamini kwamba haiwezekani kuwa kweli. Lakini fungu hili liko ndani ya Biblia yako. Na ulimwengu mzima unabaki umedanganyika kuhusu ukweli kwamba umedanganywa!

Biblia husema kwamba, tangu uasi wake kabla mwanadamu hajaumbwa, Shetani “ameyadhoofisha mataifa†kwa kiwango kikubwa (Isa. 14:12) na “kuwadanganya mataifa†(Ufu. 20:3) katika ufahamu na maarifa muhimu yanayofafanua kusudi la Mungu. Udanganyifu wake umekamilika. Baadaye tutachambua kwa undani jinsi anavyofanya kazi hii.

Mungu wa Ulimwengu Huu

Biblia pia humwita ibilisi “mungu wa ulimwengu huuâ€â€”ufunuo mwingine wa kushtua! Hiki ndicho kile 2 Wakorintho 4:4 husema: “ambao ndani yao mungu wa dunia hii amepofusha fikra zao wasioamini, isiwazukie nuru ya injili ya utukufu.â€

Shetani huupofusha ulimwengu usiione injili ya kweli kwa sababu binafsi. Injili huelezea ufalme wa Mungu unaokuja hivi karibuni—Serikali ya Mungu itawalayo ulimwengu mzima. Bila shaka, Shetani anatafuta kuwaziba watu wasiuelewe ukweli huu wa ajabu, akiwa hataki “nuru†iangazie kusudi la Mungu la kustaajabisha kwa ajili ya mwandamu. Anataka ubinadamu, kwa jumla na mmoja mmoja, ufikiri kwamba hauna mustakabali! Kwa hakika, ibilisi anatambua kwamba kuwasili kwa ufalme wa Mungu humaanisha kwamba yeye ataondolewa kutoka nafasi yake ya sasa (Ufu. 20:2-3) ya kuushawishi ulimwengu mzima kama mungu ambaye ubinadamu humwabudu bila habari. Hataruhusiwa tena kudanganya au kuyaangusha mataifa. Pia anatambua kwamba kamwe hawezi kupata kile ambacho Mungu amewaahidia wanadamu.

Katika Yohana 12:31, 14:30 na 16:11, Kristo alimrejelea Shetani kama “mkuu wa ulimwengu huu.†Mafungu haya husema kuwa siku moja ibilisi atahukumiwa. Tumia muda kidogo uyasome! Yohana 12:31 huziweka sambamba hukumu ya ulimwengu huu na hukumu ya Shetani. Kwa nini? Kwa sababu ulimwengu huu ni wake! Kauli ya Paulo iliyovuviwa kwa hakika hufunua kwamba yeye ni “mungu†wake halisi.

Huu ni ukweli dhahiri kutoka ndani ya Biblia yako! Ustaarabu wa mwanadamu, pamoja na tamaduni zake, njia na mifumo, viko chini ya utawala wa ibilisi!

Fikiri. Kama Shetani ameudanganya ulimwengu wote, basi huu hauwezi kuwa ulimwengu wa Mungu. Na kwa kuwa ulimwengu wote umedanganywa, umekatwa kutoka kwa Mungu. Watu waliodanganyika hawajui kusudi la kuwepo kwao, na wanaendesha maisha yanayoakisi ujinga huu (Isa. 59:1-2; Yer. 5:25).

Tungeweza kuuliza: Jinsi gani kiumbe mmoja anaweza kudanganya zaidi ya watu bilioni sita na nusu? Ziko njia mbili za msingi.

Kwanza, Ufunuo 12:9 huhitimisha na, “akatupwa hata nchi, na malaika zake wakatupwa pamoja naye.†Angalia inasema kwamba, “malaika zake.†Viumbe hawa, anaowaongoza, wanajulikana kama pepo wabaya (au malaika walioanguka), na wanamsaidia Shetani katika jukumu lake kama mdanganyifu mkuu. Kwa hiyo, Shetani hafanyi kazi peke yake—ana mamilioni ya viumbe roho waliodanganyika (malaika walioanguka) ambao humsaidia.

Lakini yako mengi zaidi ya kuelewa. Iko njia ya pili, iliyo na umuhimu sawa ambayo kwayo Shetani amefaulu sana kuwadanganya watu wengi hivyo—na kuficha uwezekano wao wa ajabu kutoka machoni pao.

Shetani Ana Watumishi

Jamii ya Kikristo inawakilishwa na mamia ya madhehebu na vikundi tofauti vinavyoshindana na kupingana. Kinachodhaniwa kuwa Ukristo huonekana katika kila mwonekano wa kufikirika wa “sura, ladha, rangi na umbile asili†vya imani na tamaduni. Wengi wamedhania kuwa hii ndiyo hali halisi ya mambo katika ulimwengu wa “Kikristoâ€â€”kwamba hii ndiyo njia ambayo Mungu ameitaka.

Jinsi gani wamekosea!

Weka namna nyingine, hii inamaanisha kwamba wako mamia ya maelfu, na pengine mamilioni, ya waalimu wa dini wanaowakilisha na kufundisha imani za aina hizi za Ukristo zinazotofautiana na zisizokubaliana. Wengi wanaohudhuria makanisa haya tofauti tofauti wamedhania kwamba hawa wote kwa ujumla lazima wawe ni watumishi wa Mungu—kwamba wanawakilisha na kufundisha kile ambacho Mungu anataka kifundishwe. Hakuna hatari zaidi ya hii—au MAKOSA ya dhahiri—udhanifu!

Sasa hapa bado kuna kauli moja zaidi ya kushtusha!

Akiwa ndiye mungu wa ulimwengu uliodanganyika kabisa, ambao ni lazima ujumuishe aina zote za Ukristo zinazotofautiana na dini zingine, Shetani anao mawakala wake mwenyewe. Anawatumia mawakala hawa kueneza mafundisho yake ya uongo bila kujulikana. Ndiyo, ameweza kupata mafanikio haya makubwa kwa sababu anao WATUMISHI WAKE MWENYEWE! Bila shaka, mawakala wake—watumishi wake—wao wenyewe wamedanganyika wakiamini kwamba ni watumishi wa Mungu. Baadhi hufundisha vipengele vichache vya ukweli wa Mungu, lakini kwa hakika hakuna chochote cha kweli Zake muhimu!

Sasa angalia 2 Wakorintho 11:13-15. Mtume Paulo alionya dhidi ya werevu ambao watumishi wa Shetani huutumia kudanganya kwa mafanikio: “Maana watu kama hao ni mitume wa uongo, watendao kazi kwa hila, wanaojigeuza wawe mfano wa mitume wa Kristo. Wala si ajabu. Maana Shetani mwenyewe hujigeuza awe mfano wa malaika wa nuru. Basi si neno kubwa watumishi wake nao wakijigeuza wawe mfano wa watumishi wa haki, ambao mwisho wao utakuwa sawasawa na kazi zao.â€

Hili ni andiko la wazi, linaloshtua sana. Bado, ni kweli kwamba watumishi wa Shetani huonekana kuwa watumishi wa Mungu. Elewa hili! Shetani haneni moja kwa moja na wanadamu. Hutenda kazi kupitia watumwa wake—watumishi wake!

Na huu hapa ndio uongo mkuu wa watumishi hawa wa uongo: Ibilisi anawatumia kama vyombo vyake kwa ajili ya kueneza injili ya uongo kuhusu Nafsi ya Yesu Kristo—badala ya Ujumbe Wake wa ufalme wa Mungu, ule ambao Kristo aliuleta. Ukweli mkuu ambao watumishi, wanateolojia na wanadini wa ulimwengu huu huukataa ndio uwezekano wa kustaajabisha ambao kila mwanadamu anao.

Mafungu yafuatayo yanaendeleza maelezo ya Paulo kuhusu kazi za watumishi wa uongo. Yanaonyesha hatari inayoendelea ya mawakala wa Shetani wakitafuta kujipenyeza ndani ya Kanisa la kweli kuwapofusha watumishi wa kweli wa Mungu mara ya pili wasiuelewe ukweli wa ajabu wa injili ili wawarudishe gizani. Angalia: “Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa hila yake, asije akawaharibu fikra zenu [ndugu wa Korintho], mkauacha unyofu na usafi kwa Kristo. Maana yeye ajaye [akiongelea wahubiri wa uongo] akihubiri Yesu mwingine… au mkipokea roho nyingine… au injili nyingine msiyoikubali…†(11:3-4).

Paulo alionya dhidi ya roho “nyingine†ambayo hata iliweza kuingia katika Kanisa la kweli. Roho hii hii nyingine ilipotosha ukweli kuhusu injili na Kristo halisi wa Biblia. Kihistoria, Ukristo bandia wa leo ulionekana mara ya kwanza mara tu baada ya kifo na ufufuo wa Kristo.

Pia, jiulize mwenyewe: Kama Kristo ni injili, basi kwa nini kunukuu “Yesu mwingine†na “injili nyingine†kama makosa mawili tofauti ya mafundisho?

Tutarudi kwa hili.

Maonyo ya Agano Jipya

Agano Jipya lina maonyo mengi dhidi ya walaghai, wadanganyifu na matapeli ambao wangejaribu kuingia katika Kanisa la kweli wajipatie wafuasi na kuwaongoza katika mafundisho ya uongo. Wengi miongoni mwa mitume, kwa namna moja au nyingine, kwa hakika walilionya kila kusanyiko dhidi ya hatari hii. Ni mfumo huu huu wa Ukristo wa uongo ambamo watu wengi wamezaliwa na kutumikia maisha yao ndani yake.

Mtume Petro alionya dhidi ya waalimu wa uongo “miongoni mwenu (Kanisa).†Angalia: “Lakini kuliondokea manabii wa uongo katika wale watu, kama vile kwenu kutakavyokuwako WAALIMU WA UONGO, watakaoingiza kwa werevu uzushi wa kupoteza, wakimkana hata Bwana aliyewanunua, wakijiletea uharibifu usiokawia. Na WENGI watafuata ufisadi wao; na kwa hao njia ya kweli itatukanwa. Na katika kutamani watajipatia faida kwenu kwa maneno yaliyotungwa†(2 Pet. 2:1-3).

Haya ni maneno makali. Kama vile manabii wa uongo walivyosumbua Israeli ya zamani, vivyo hivyo Kanisa limeshambuliwa na “waalimu wa uongo†katika karne zote ambao, kwa “maneno yaliyotungwa,†waliwashawishi “wengi†wawafuate. Lengo lilikuwa ni kuwavuta watu watoke kwenye “njia ya UKWELI.â€

Mtume Yuda, ndugu mdogo wa Kristo, yeye naye alikuwa wazi katika onyo lake moja kwa moja: “Wapenzi, nilipokuwa nikifanya bidii sana kuwaandikia habari ya wokovu…ili niwaonye kwamba mwishindanie imani waliyokabidhiwa watakatifu mara moja tu. Kwa maana kuna watu WALIOJIINGIZA kwa siri, watu walioandikiwa tangu zamani hukumu hii, makafiri, wabadilio neema ya Mungu wetu kuwa ufisadi [leseni ya kuvunja Amri za Mungu]…†(fu. 3-4).

Shtaka hili rasmi huwaelezea wale ambao “walijiingiza†na kuwasababisha baadhi kutoipigania “imani ambayo ilikabidhiwa mara moja tu.†Angalia inasema kwamba baadhi ya hawa wazushi walikuwa “wameandikiwa tangu zamani.†Kwa sababu walikuwa makafiri, waliwafundisha wengine wavunje amri ya Mungu pia. Tutachunguza Matendo 8 hivi punde ili kuelewa vizuri watu hawa walitoka wapi. Mfumo na mafundisho yao si mapya kabisa.

Yohana aliandika karibu sura nzima ya maneno ya onyo la Kristo mwenyewe kwa kondoo Wake wote wa wakati ujao. Kristo habakizi kitu chochote anapoelezea asili ya kweli ya viongozi na waalimu wa uongo. Hizi hapa ni dondoo kutoka sura hiyo:

“Yeye asiyeingia mlangoni katika zizi la kondoo [Kanisa]… huyo ni MWIVI naye ni MNYANG'ANYI…mchungaji wa kondoo [Kristo na watumishi wake waaminifu]... kondoo humfuata, kwa maana waijua sauti yake. MGENI hawatamfuata kabisa, bali watamkimbia; kwa maana hawazijui sauti za WAGENI…Basi Yesu aliwaambia tena…Mimi ndimi mlango wa kondoo. Wote walionitangulia ni WEVI na WANYANG'ANYI; lakini kondoo hawakuwasikia. Mimi ndimi mlango; mtu akiingia kwa mimi, ataokoka; ataingia na kutoka, naye atapata malisho. MWIVI haji ila aibe na kuchinja na kuharibu; mimi nalikuja ili wawe na uzima, kisha wawe nao tele. Mimi ndimi mchungaji mwema. Mchungaji mwema huutoa uhai wake kwa ajili ya kondoo. Mtu wa MSHAHARA…humwona MBWA-MWITU...na kukimbia; na MBWA-MWITU huwakamata na kuwatawanya. YULE hukimbia kwa kuwa ni mtu wa MSHAHARA; wala mambo ya kondoo si kitu kwake†(10:1-13).

Tumia muda kuisoma sura hii yote. Angalia kujirudiarudia kwa maneno “mbwa-mwituâ€, “mgeniâ€, “mwiviâ€, “mnyang’anyi†na “mtu wa mshaharaâ€â€”hawa wa mwisho ni wale ambao huliacha kundi, wakitafuta matakwa binafsi. Katika historia yote ya Kanisa, wakati maadui walipowatishia watu wa Mungu, watumishi wengi walilitelekeza kundi, na kondoo wengi walidanganywa na kufagiliwa mbali kutoka Kanisa la Mungu na ukweli.

Pamoja na Wakorintho, Paulo pia aliyaonya makusanyiko mengine. Hiki hapa ndicho alichowaambia Wagalatia walipokuwa wametumbukia kwenye mafudisho ya uongo: “Mlikuwa mkipiga mbio vizuri; ni nani aliyewazuia msiitii KWELI? Kushawishi huku hakukutoka kwake yeye anayewaita ninyi. Chachu kidogo huchachua donge zima†(5:7-9).

Wagalatia walikuwa wameiacha njia. Hawakuelewa kwamba mafundisho ya uongo kidogo (“chachuâ€) hatimaye huenea (kama chachu kwenye unga uliokandwa) kwenye “donge zima†la kweli nyingi za Mungu. Tutakuja kuona kwamba Wagalatia hawa walikuwa wanapoteza uelewa wao wa injili.

Siri ya Kuasi

Sasa geukia onyo alilolitoa Paulo kwa Wathesalonike, ambamo aliongelea juu ya “siri ya kuasi†iliyokuwa tayari inatenda kazi katika Kanisa la karne ya kwanza. Muktadha wa pale (fu. 3) pia una maelezo ya matukio ambayo hutangulia muda mfupi kabla ya Kurudi kwa Kristo. “Ukengeufu†na kufunuliwa kwa “mtu wa kuasi…mwana wa uharibifu†vitatokea kwanza kabla ya Kurudi kwa Kristo Mara ya Pili. Aliandika, “Maana ile siri ya kuasi hivi sasa inatenda kazi†(2 Thes. 2:7). Paulo alielewa kwamba matukio fulani yalikuwa “tayari†yanatokea Kanisani wakati huo, vile vile kama ambavyo yatakuja kutokea, mara nyingine tena, mwishoni mwa zama.

Kitabu cha Matendo huelezea matukio katika Samaria na hutoa mambo ya muhimu yanayopaswa kufikiriwa: “Siku zile kukatukia adha kuu ya kanisa lililokuwa katika Yerusalemu; wote wakatawanyika katika nchi ya Uyahudi na Samaria, isipokuwa hao mitume… Lakini wale waliotawanyika wakaenda huko na huko wakilihubiri neno. Filipo akatelemka akaingia mji wa Samaria… Ikawa furaha kubwa katika mji ule†(8:1, 4-5, 8).

Wakati ukweli dhahiri wa Neno la Mungu unapohubiriwa kwa wale ambao akili zao zimefunguliwa, hakika huleta “furaha kubwa.â€

Baadaye, mafungu kadhaa humrejelea mtu mmoja aitwaye Simoni Mchawi—ambaye mara nyingi huitwa Simoni Magusi na wanahistoria mbalimbali wa kanisa. Mtu huyu alikuwa na mvuto mkubwa katika eneo la Samaria ambalo wakazi wake wengi walikuwa watu wa Mataifa. Alikuwa sehemu ya mfumo wa siri ambao Paulo aliwaonya Wathesalonike dhidi yake (ona pia Ufu. 17:5, kisha baadaye kwenye kitabu hiki). Mfumo huu huu wenye nguvu, ambao hapo awali uliongozwa na Simoni, umeendelea kutafuta kuingia ndani ya Kanisa la kweli.

Sasa angalia: “Na mtu mmoja, jina lake SIMONI, hapo kwanza alikuwa akifanya uchawi katika mji ule, akiwashangaza watu wa taifa la Wasamaria, akisema ya kuwa yeye ni mtu mkubwa. Wote wakamsikiliza tangu mdogo hata mkubwa, wakisema, Mtu huyu ni uweza wa Mungu, ule Mkuu. Wakamsikiliza, kwa maana amewashangaza muda mwingi kwa uchawi wake†(fu. 9-11).

Biblia hufafanua ni “neno†gani ambalo Filipo alikuwa anahubiri: “Lakini walipomwamini Filipo, akizihubiri habari njema za UFALME WA MUNGU, na jina lake YESU KRISTO, wakabatizwa, wanaume na wanawake†(fu. 12). Angalia kwamba hawa watu wa Samaria walibatizwa tu pale “walipoamini†ujumbe huu—ufalme wa Mungu—si fikra bandia za uongo zilizobuniwa-kibinadamu.

Hapa kuna yale ambayo Paulo aliwaandikia Waefeso. Aya hii inaelezea ofisi mbalimbali ambazo Kristo alizianzisha ndani ya huduma Yake ya Agano Jipya. Hufafanua makusudi ya ofisi hizo katika kuwajenga, kuwaunganisha na kuwakamilisha ndugu wa Kanisa la Mungu. Angalia: “Naye alitoa wengine kuwa MITUME, na wengine kuwa MANABII; na wengine kuwa WAINJILISTI na wengine kuwa WACHUNGAJI na WAALIMU; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo; ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu. Lakini tuishike KWELI katika upendo na kukua hata tumfikie yeye katika yote, yeye aliye kichwa, Kristo†(4:11-15).

Huu ni mfululizo mwingine wa maonyo makali kwa watu wa Mungu. Kristo alikusudia kwamba kondoo Wake wawasikilize watumishi wa kweli na wagundue “upepo wa elimu†ya uongo ambayo inaweza kuja imefunganishwa katika njia za “ujanja†na “hila.â€

Karibu na mwisho wa huduma ya Paulo, muda mfupi kabla hajaenda kushitakiwa kwa ajili ya maisha yake, alikutana na wazee wote waliokuwa wamekusanyika huko Efeso. Ulikuwa ni mkutano wenye hisia kali, kwa sababu alijua kuwa asingewaona tena. Alitumia muda kuwakumbusha wajibu wao na kile ambacho alikuwa amewaagiza mara kwa mara kwa kipindi zaidi ya miaka mitatu! Wajibu ambao Paulo aliuelezea unabaki kuwa jukumu la watumishi wa kweli wa Mungu leo.

Kwa uangalifu angalia jinsi Paulo alivyosisitizia umuhimu wa kwamba alikuwa amehubiri ufalme wa Mungu: “Na sasa, tazameni, mimi najua ya kuwa ninyi nyote niliowahubiria UFALME WA MUNGU… hamtaniona uso tena. Jitunzeni… na lile kundi lote…kulilisha kanisa lake Mungu…Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu MBWA-MWITU WAKALI wataingia kwenu, wasilihurumie kundi; tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao. Kwa hiyo KESHENI, mkikumbuka ya kwamba miaka mitatu, usiku na mchana, sikuacha kumwonya kila mtu kwa machozi†(Matendo 20:25, 28-31).

Kile ambacho Paulo alionya dhidi yake kilitokea. Wazushi si tu waliingia katika kusanyiko la Efeso lakini katika maeneo mengine mengi ya Kanisa la Mungu na kuwachochea wafuate uelewa na vitendo vya udanganyifu. Wanahistoria wa Kanisa kwa kawaida hurejelea kipindi kuanzia katikati ya karne ya kwanza BK hadi katikati ya karne ya pili BK kama “karne iliyopotea.â€

Katika kipindi hiki, Kanisa linaloonekana kubadilika kabisa katika mwonekano, kufikia kiasi cha karibu kutotambulika. Waumini wa kweli waliosalia, waliokuwa wachache, wa hali ya chini, walilazimika kukimbia na kuwaacha wengi waliokuwa wanaonekana, waliokuwa wamegeukia makosa. Maarifa juu ya kusudi la Mungu la ajabu kwa ajili ya uwepo wa mwanadamu yakawa yamepotea miongoni mwa walio wengi ambao walifagiliwa mbali kwenye wokovu wa uongo.

Tangu hapo karne ya kwanza, wakati Kristo alipoanzisha Kanisa Lake, lililazimika kuupigania ukweli. Watu wa Mungu walipaswa kuwa waangalifu wakati wote—wenye kujihadhari sana—kuhusu hatari ya watumishi wa uongo wakijipenyeza miongoni mwao na kupotosha baadhi au mafundisho yote ya Mungu. Na hawa walaghai wakati wote huhubiri injili ya uongo. Kumbuka, Paulo aliwaonya Wakorintho kwamba walikuwa “wamedanganywa†kwa kukubali “injili nyingine†(2 Kor. 11:4). (Kitabu changu kipana Liko Wapi Kanisa la Kweli? – na Historia Yake ya Ajabu! huchambua somo hili la kusisimua kwa undani.)

Katika sura inayofuata, tutaona kwa nini injili ya KWELI—na kuja kwa UFALME WA MUNGU—hushikilia majibu kwa matatizo makubwa ya mwanadamu. Jiandae kwa ajili ya ufahamu wa kushtua—na mambo ya kweli!

Sura ya Pili – Injili ya Kweli—na Uwezekano Wako wa Kustaajabisha Vyafunuliwa!

Fundisho moja kuu kabisa katika Biblia ni maarifa ya injili ya kweli. Unaelekea kujifunza ni kwa nini.

Elewa. Iko injili moja tu iliyo sahihi. Zingine zote ni upotoshaji, uliobuniwa na Shetani kuubadili ukweli wa Ujumbe wake wa ajabu. Ni ufahamu huu wa muhimu sana ambao mara nyingi watumishi wa Shetani huonekana kuupotosha kwanza.

Pale mwanzoni kabisa mwa huduma Yake, Kristo alifundisha, “Tubuni na kuiamini INJILI†(Marko 1:15). Lakini injili ya kweli ni nini? Je ziko zaidi ya moja ambazo Mungu anaziridhia? Majibu kwa hili na maswali mengine yanapatikana ndani ya Biblia—na kwa hakika ni MUHIMU kwako kuyaelewa. Lakini majibu yamebaki mafichoni kwa walio wengi sana.

Maarifa Mengi ya Uongo

Maelfu ya vitabu vipya vya kidini huchapishwa kila mwaka nchini Marekani! Vile vile kuna madhehebu na vikundi tofauti zaidi ya elfu mbili nchini Marekani! Ila, mkanganyiko na kutokukubaliana kuhusu majibu kwa maswali makuu ya maisha miongoni mwa wanaodai kuwa Wakristo, au katika ulimwengu mzima, umeongezeka zaidi kuliko wakati wowote. KWA NINI? Kwa nini yako maarifa mengi, na kwa wakati huo huo kuna ujinga mwingi juu ya ukweli kuhusu maswali MAKUU ya maisha?

Majibu yote kwa maswali haya yanahusiana moja kwa moja na INJILI!

Walio wengi wamefundishwa—na wanaamini—kwamba injili ni kuhusu Nafsi ya Yesu Kristo. Hakika, jukumu la Kristo ni somo la muhimu mno, lakini Yeye si injili. Biblia huonyesha kwamba jina la Yesu Kristo huhubiriwa sambamba na injili. Kwa mara nyingine, jukumu Lake ni la muhimu sana kwa Ukristo na ni lazima lieleweke, lakini Yeye si injili!

Baadhi hutangaza “injili ya wokovu†au “injili ya neema.†Wengine huamini “injili ya miujiza†au “injili ya ujamaa†au “injili ya vyakula†au “uponyaji†au “imani.†Bado wengine tu hufukiria “muziki wa injili†wanaposikia neno hili. Haya yote ni mawazo ya kibinadamu ambayo hupuuza ukweli wa Biblia!

Hebu turudi kwenye Marko 1, na tuangalie fungu la 14: “Hata baada ya Yohana kutiwa gerezani, Yesu akaenda Galilaya, akiihubiri Habari Njema ya UFALME WA MUNGU.†[injili ya ufalme wa Mungu] Hii ndiyo injili aliyohubiri Yesu. Na ni katika muktadha huo huo alisema, “Tubuni, na KUIAMINI INJILI.†Lakini, injili gani? Injili ya “ufalme wa Mungu.†Fungu la kwanza hurejelea ujumbe huu linaposema, “Mwanzo wa Injili ya Yesu Kristo.†Injili ya Kristo ilikuwa juu ya UFALME WA MUNGU—si kitu kingine! Mtu awaye yote hana budi kuiamini injili hiyo, si bandia au mbadala. Ulimwengu kwa-njia-rahisi hauijui injili hii!

Wachache wanatambua. Lakini kwa nini? Kwa nini ni wachache sana leo-hii wanaoelewa vizuri mustakabali wa kustaajabisha wa mwito wa Kikristo? Paulo alivuviwa kufafanua: “Lakini, kama ilivyoandikwa, Mambo ambayo jicho halikuyaona wala sikio halikuyasikia, (Wala hayakuingia katika moyo wa mwanadamu,) Mambo ambayo Mungu aliwaandalia wampendao. Lakini Mungu ametufunulia sisi kwa Roho. Maana Roho huchunguza yote, hata mafumbo ya Mungu†(1 Kor. 2:9-10). Pasipo Mungu kuifungua akili, haiwezekani kuelewa mambo ya Mungu. Vile vile haiwezekani hata kuja kwa Mungu (Yohana 6:44, 65). Kwa hakika, fungu hili linasema kwamba kusudi la Mungu halijawahi kuingia katika fikra za mwanadamu!

Mungu, kwa kusudi Lake la ajabu sana, amefunua ukweli wa injili kwa wachache sana kwa wakati huu—na amewaweka ndani ya Kanisa Lake. Walimwengu waliosalia wamepofushwa. Elewa hili! Ibilisi hataki wanadamu wafurahie kile ambacho yeye amenyimwa milele—uanakaya [kuwa memba] katika Familia ya Mungu, ambao utajifunza.

Wengi hawataamka dhidi ya udanganyifu—madanganyo kwa halaiki—wa “Ukristo†uliopotoshwa unaokataa kweli dhahiri za Biblia! Mpango wa Mungu kwa ajili ya wanadamu unaduwaza­­—usioweza kulinganishwa na chochote ambacho mwanadamu amekiunda kichukue mahali pake. Ulimwengu unapuuza maandiko yaliyo wazi, na dhahiri yapatikanayo kote katika Neno la Mungu kuhusu ufalme wa Mungu. Kitabu hiki kinafafanua ukweli wa kustaajabisha ambao wengi huupuuza—na kinafunua kile ambacho chaweza kuwa mustakabali wako!

Onyo Kali Kutoipotosha Injili

Somo hii ni la muhimu mno kiasi kwamba Mungu alimvuvia mtume Paulo kutoa onyo hili kwa Wagalatia kipindi kile na kwetu sasa: “Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi yeye aliyewaita katika neema ya Kristo na kugeukia injili ya namna nyingine. Wala si nyingine; lakini wapo watu wawataabishao na kutaka kuigeuza injili ya Kristo. Lakini, ijapokuwa sisi au malaika kutoka mbinguni atawahubiri ninyi injili yoyote isipokuwa hiyo tuliyowahubiri, na alaaniwe. Kama tulivyotangulia kusema, na sasa, nasema tena, mtu awaye yote akiwahubiri ninyi injili yoyote isipokuwa hiyo mliyoipokea, na alaaniwe†(1:6-9).

Hii ni kauli nzito sana! Baadaye kidogo, Paulo alisisitizia tumaini lake kwamba “kweli ya INJILI ikae pamoja nanyi†(2:5). Kwa hivyo iko injili moja ya kweli—na zingine zote za uongo. Sasa unaweza kuelewa vyema onyo la Paulo katika Wagalatia 5:7-9, lililorejelewa hapo awali.

Ingawa baadhi hudai kuwa Paulo alifundisha injili tofauti au injili ya nyongeza, ni wazi kwamba hakufanya hivyo. Kinyume na hilo, Mungu alimtumia Paulo kuonya dhidi ya kuruhusu fundisho la uongo kama hilo kwa kutangaza laana kwa mtu awaye yote, malaika au hata mtume yeyote—“Lakini, ijapokuwa sisi [akimaanisha, mitume]… atawahubiri ninyi injili nyingine yoyoteâ€â€”anayechagua kukiuka amri hii (1:8)

Andiko zito kiasi gani—na ONYO!

Paulo alieleza kwamba mitume waliaminiwa na Mungu kuhifadhi injili ya kweli. Angalia 1 Wathesalonike 2:4: “Bali kama vile tulivyopata kibali kwa Mungu tuwekewe amana Injili, ndivyo tunenavyo; si kama wapendezao wanadamu, bali wampendezao Mungu anayetupima mioyo yetu.†Huo ni wajibu usioweza kuchukuliwa kirahisi. Watumishi wa kweli daima watafundisha kile ambacho Mungu ameamuru, si kile kinachowafurahisha wanadamu (ikiwa ni pamoja na “wasomi†wa Biblia). Hivyo, dai lolote kwamba Paulo alifundisha injili tofauti au ya pili (inayodhaniwa kuwa ni juu ya Kristo au ya “amaniâ€) haiwezekani. Kwa hakika angekuwa anatangaza laana juu yake yeye mwenyewe!

Yesu Alitabiriwa Kuleta Injili

Yesu alikuja kama mtangazaji akibeba tangazo. Kila mahali alikoenda Alitoa tangazo hilo hilo kuhusu kuja kwa SERIKALI BORA itawalayo-ulimwengu itakayosimamishwa wakati wa Kurudi Kwake.

Alipokuwa akinena kwa kundi la wasikilizaji jangwani, Kristo alifafanua kusudi Lake—wajibu Wake. Angalia jinsi Alivyofafanua utume Wake: “Akawaambia, Imenipasa kuihubiri habari njema ya UFALME WA MUNGU katika miji mingine pia; maana kwa sababu hiyo nalitumwa (Luka 4:43).

Mathayo anaangazia zaidi suala hili: “Naye alikuwa akizunguka katika Galilaya yote, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri HABARI NJEMA YA UFALME, na kuponya ugonjwa na udhaifu wa kila namna katika watu†(Math. 4:23). Kazi ya Kristo ilikuwa ni kupeleka ujumbe wa ufalme wa Mungu katika miji yote ya Israeli. “Alitumwa†kwa kusudi hili.

Katika Agano la Kale, Yesu alitabiriwa kuja kama MJUMBE. Angalia Malaki 3:1: “Angalieni, namtuma mjumbe wangu [Yohana Mbatizaji], naye ataitengeneza njia mbele Yangu; naye Bwana, mnayemtafuta, atalijilia hekalu lake ghafla; naam, yule MJUMBE [Kristo] wa agano, mnayemfurahia.â€

Kristo alikuwa “MJUMBEâ€, si ujumbe wenyewe. Ujumbe Wake kuhusu ufalme wa Mungu ndiyo kiini hasa—kitovu!—cha Biblia nzima.

Sasa linganisha aya katika Malaki na nyingine katika Agano Jipya: “Torati na manabii vilikuwapo mpaka Yohana [maandiko ya Agano la Kale pekee ndiyo yaliyohubiriwa mpaka Yohana Mbatizaji]; tangu wakati huo habari njema ya UFALME WA MUNGU hutangazwa, na kila mtu hujiingiza kwa nguvu†(Luka 16:16). Kumbuka kwamba, katika Marko, Kristo alihubiri “ufalme wa Mungu†na akauita injili.

Shetani, aliyejua kwamba Kristo alitabiriwa kuhubiri Ujumbe ambao anauchukia, kupitia Mfalme Herode, alitafuta Kumuua Akiwa angali mtoto mchanga. Hii ndiyo sababu ibilisi pia alitafuta kumjaribu kule nyikani (Math. 4:1-11). Alijua kuwa kama angefaulu katika jaribio moja wapo, basi angevuruga Mpango wa Mungu na kubaki na mamlaka juu ya mataifa ya ulimwengu. Pia tutajifunza zaidi juu ya hili baadaye.

Maana ya “Injiliâ€

Neno “injili†ni neno la Kiingereza cha zamani lenye maana ya “god spell†yaani habari njema. Neno “ufalme†pia ni neno la Kiingereza cha zamani, lenye maana rahisi ya serikali. Tunaweza kusema kwa usahihi kwamba Kristo alihubiri “habari njema ya serikali ya Mungu.†Tutajifunza juu ya nani, nini, wapi, lini, kwa nini na ni vipi HABARI NJEMA hii inahusiana na unabii mkuu wa Biblia.

Neno injili linapatikana mara 101 katika Biblia. Wakati mwingine linapatikana pekee yake, na wakati mwingine “ya ufalme†hulifuatia. Wakati mwingine hujumuisha “ya ufalme wa Mungu†au usemi unaolingana na huo “ya ufalme wa mbinguni.†Angalia kwamba inasema, “wa mbinguni,†siyo “huko mbinguni.†Ni ufalme wa mbinguni na kuna tofauti kubwa. Kama ilivyo kwamba ufalme wa Mungu, si ufalme katika Mungu, vivyo hivyo ni kweli kuhusu ufalme wa mbinguni au ufalme wa mbingu. Hili ni jambo muhimu kulielewa.

Kote katika Agano Jipya, neno “ufalme†hupatikana mara 27, “ufalme wa Mungu†mara 75 na “ufalme wa mbinguni†mara 34. Ni wazi kwamba yote haya ni kitu kimoja na yanafanana.

Sasa elewa jambo hili. Somo la ufalme wa Mungu si tu kwamba ni mada kuu katika Agano Jipya, lakini pia ndio mada kuu katika Biblia NZIMA. Bado, ajabu ni kwamba, wengi wanaelewa kidogo au hawajui kabisa habari zake. Watumishi wa makanisa ya ulimwengu huu hawaijui injili ya kweli na kamwe hawahubiri juu yake. Kwa hivyo, karibu ulimwengu mzima unasimama katika ujinga kamili kuhusu moja ya ukweli mkuu katika Neno la Mungu. Ni ajabu, lakini ni kweli!

Pia, wale WOTE ambao wakati mmoja walijifunza ukweli huu lazima wawe makini wakati wote, usije ukawaponyoka (Ebr. 2:1).

Mitume Walihubiri Injili ya Kweli

Kuna ushahidi gani kwamba waandishi wengine wa Agano Jipya walihubiri ujumbe huu huu? Ni mwingi sana!

Petro alihubiri ufalme. Angalia: “Maana hivi mtaruzukiwa kwa ukarimu kuingia katika UFALME wa milele wa Bwana wetu, Mwokozi wetu Yesu Kristo†(2 Pet. 1:11).

Ndivyo alivyofanya mtume Yakobo: “Ndugu zangu wapenzi, sikilizeni, Je! Mungu hakuwachagua maskini wa dunia wawe matajiri wa imani na warithi wa UFALME aliowaahidia wampendao?†(2:5).

Maelezo ya Mathayo hutaja usemi “injili ya ufalme†mara tatu tofauti. Huu hapa ni mfano mwingine ambao ni karibu sawa na 4:23, iliyokwisha kunukuliwa: “Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri HABARI NJEMA YA UFALME, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina†(9:35).

Katika mingi ya mifano Yake, Kristo alifundisha mambo ya msingi ya ufalme wa Mungu. Mathayo peke yake, hasa kwa njia ya mifano, hufanya rejea zaidi ya hamsini kwa ufalme wa Mungu unaokuja.

Luka ameandika kuwa Yesu Kristo aliwaagiza wanafunzi wake kuhubiri ujumbe huu huu: “Akawaita wale Thenashara...Akawatuma wautangaze UFALME WA MUNGU†(9:1-2). Muda mfupi baadaye, aliwatuma wengine sabini waende kuhubiri, nao pia walibeba ujumbe wa “UFALME WA MUNGU†(10:1, 9).

Yohana ameyaandika maneno ya Kristo mbele ya Pontio Pilato usiku ule aliposalitiwa. Hiki ni kiashiria muhimu kukielewa. Kristo alisema, “UFALME Wangu si wa ulimwengu huu [jamii hii ya sasa]†(Yohana 18:36). Baadaye tutagundua undani wa jinsi ambavyo serikali ya Mungu itasimamishwa duniani.

Kumbuka kwamba Filipo, shemasi, alihubiri ufalme kwa Wasamaria (Matendo 8:12).

Tambua kwamba katika kuhubiri alitenganisha ufalme na Kristo: “Lakini walipomwamini Filipo…kuhusu ufalme wa Mungu, na jina lake Yesu Kristo, wakabatizwa, wanaume na wanawake.â€

Filipo hakuhubiri injili ya ufalme pekee, lakini pia aliitofautisha na fundisho juu ya Yesu Kristo. Tumia muda kusoma habari hii yote. Kumbuka mjumbe sio ujumbe. Kristo si injili. Hata hivyo, Husimama kando yake moja kwa moja na atatawala dunia nzima wakati ufalme utakaposimamishwa.

Hivyo basi Luka, mwandishi wa Matendo, hutofautisha zaidi kati ya kuhubiri juu ya ufalme wa Mungu na kuhubiri juu ya Yesu Kristo! Wakati yote ni ya muhimu sana, ni wazi kwamba ni masomo mawili tofauti!

Tumetatua tatizo ambalo baadhi ya watu hudai kwamba Paulo alihubiri “injili tofauti.†Kwa hakika hawa hawana habari kwamba ni Paulo ambaye Mungu alimtumia kutangaza laana kwa yeyote aliyefanya hivyo (Gal. 1:8-9). Tumeona kwamba Paulo alihubiri ufalme wa Mungu. Hata hivyo, utaona mafungu mawili katika Matendo, ambayo huonyesha kwamba hakupuuzia somo la pili juu ya jukumu la Kristo katika mchakato wa wokovu.

Kwanza, hebu tuthibitishe kwamba Paulo alihubiri ufalme wa Mungu kwa watu wa Mataifa. Matendo 19:8 husema: “Akaingia ndani ya sinagogi, akanena kwa ushujaa kwa muda wa miezi mitatu, akihojiana na watu, na kuwavuta katika mambo ya UFALME WA MUNGU.†Yako maeneo mengi katika nyaraka zake ambapo Paulo alifundisha ufalme kwa makanisa mbalimbali ya watu wa Mataifa. Ujumbe wake ulikuwa huo huo wakati wote, akiendelea kuhubiri na kurejelea ufalme wa Mungu.

Chunguza hili kutoka Matendo 20:25: “Niliowahubiria UFALME WA MUNGU…wamtubie Mungu, na kumwamini Bwana wetu Yesu Kristo†(fu. 21). Maelezo haya yanaweka wazi kwamba Paulo alihubiri injili hiyo hiyo—pia sambamba na jukumu la Kristo—kwa Wayahudi na watu wa Mataifa. (Kimsingi Waefeso walikuwa waongofu kutoka kwa watu wa Mataifa.)

Kisha, angalia sura ya 28:30-31: “Na Paulo akakaa muda wa miaka miwili mizima katika nyumba yake aliyokuwa ameipanga, akawakaribisha watu wote waliokuwa wakimwendea, akihubiri habari za UFALME WA MUNGU, na kuyafundisha mambo ya Bwana Yesu Kristo.†Kama Filipo, Paulo alielewa kuwa injili na Yesu Kristo alikuwa ni nani, yalikuwa ni masomo mawili tofauti.

Mwisho, angalia aya moja zaidi mahali ambapo Paulo alibainisha tofauti kati ya injili na Nafsi ya Kristo, kwa kurejelea tena kwa ufupi 2 Wakorintho 11:4: “Maana yeye ajaye akihubiri Yesu mwingine ambaye sisi hatukumhubiri… au injili nyingine msiyoikubali, mnatenda vema kuvumiliana naye†(maelezo ya pembeni kwa usahihi hutamka usemi wa mwisho “na mimiâ€). Paulo aliwahimiza Wakorintho kuwakataa waalimu wa uongo na kushikilia kile alichokuwa amewafundisha. Kwa wazi alitofautisha mafundisho ya Yesu wa uongo na injili ya uongo kama makosa mawili tofauti.

Jiulize mwenyewe tena: Kama Kristo ni injili, basi kwa nini Paulo (mara nne) na Filipo huyaongelea kama mambo mawili tofauti?

Kila Nabii wa Agano la Kale Alihubiri Ufalme

Wengi wamedhani kwamba injili ni ujumbe wa Agano Jipya peke yake. Hakuna kitu ambacho kinaweza kuwa mbali na ukweli kama hiki! Kwa hakika Biblia imejaa maeneo, katika Agano la Kale na Jipya, yanayoelezea vipengele mbalimbali na unabii kuhusu ufalme wa Mungu.

Hebu tuchunguze kauli ya kushangaza ya Petro inayopatikana katika Matendo 3:19-21: “Tubuni basi, mrejee, ili dhambi zenu zifutwe, zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako kwake Bwana; apate kumtuma Kristo Yesu mliyewekewa tangu zamani; ambaye ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya vitu vyote, zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu.â€

Angalia kwamba Petro anarejelea Kuja kwa Kristo—“kuwako kwake Bwana†(fu. 19), na fungu la 20 likisema kwamba Mungu “apate kumtuma Kristo Yesu.†Fungu la 21 huelezea ufalme wa Mungu kama “kufanywa upya vitu vyote.†Petro alitamka kwamba huku “kufanywa upya†(Kristo akisimamisha ufalme Wake) ni zamani ambazo “zilinenwa na Mungu kwa… manabii Wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu.â€

Hii ni kauli ya kushangaza! Lakini je, ni kweli?

Inawezekana kweli Mungu alimtumia kila mmoja wa manabii wake kutangaza ufalme Wake? Kwa nini wasomi wa Biblia na watu wa dini hupuuzia hili—au hata kulikataa hapo hapo? Hebu tuchunguze Agano la Kale.

Wahubiri-Kabla ya Gharika

Yuda aliandika, “Na Henoko [Babu-mkuu wa Nuhu]…alitoa maneno ya unabii…akise- ma, Angalia Bwana YUAJA… ili afanye hukumu juu ya watu WOTE†(fu. 14-15). Ni wazi hii humrejelea Yesu Kristo akirudi kusimamisha serikali, inayoyatawala mataifa YOTE.

Katika 2 Petro 2:5, Nuhu hurejelewa kuwa “mhubiri wa haki wa naneâ€. Yuda aliandika kuwa Henoko alikuwa wa “saba kutoka Adamu.†Hivyo, Nuhu aliyemfuatia, anarejelewa kuwa wa “nane.†Ukianza na Habili, ukimjumlisha na Henoko, kulikuwa na wanaume saba ambao walibeba jukumu hili hapo nyuma kabla ya Nuhu. Maisha ya wanaume hawa wanane yalienea kipindi chote kati ya Adamu na Gharika na wote walihubiri ujumbe huo huo.

Uchunguzi makini wa Yuda hufunua kuwa Henoko alihubiri kuhusu dhambi na haki. Wakati mengi yanaweza kusemwa kuhusu kipindi hiki cha karne kumi-na-sita-na-nusu, inatosha kusema, watu hawa wote walizungumzia ujumbe ule ule. Kumbuka Petro alisema, “…tokea mwanzo wa ulimwengu.â€

Nani mwingine alihubiri ufalme wa Mungu?

Ibrahimu, Musa, Samweli na Daudi

Je, kuna ushahidi kwamba injili ilihubiriwa katika kipindi kilichofuata baada ya Gharika?

Katika Mwanzo 12:3, Mungu alimwambia Ibrahimu, “Katika wewe jamaa zote za dunia watabarikiwa.†Fungu hili pia limerejelewa kwenye Wagalatia 3:8, lakini limesemwa tofauti kidogo: “…katika wewe [Ibrahimu] mataifa yote watabarikiwa.†Fungu hili hili husema kwamba injili “ilihubiriwa zamani kwa Ibrahimu.â€

Hii inavutia! Si tu kwamba Ibrahimu alihubiriwa injili (bila shaka na Melkizedeki—Kristo), lakini pia ilihubiriwa katika Mwanzo, kupitia maandiko ya Musa, kuhusu Ibrahimu! Sasa fikiri. Inawezekanaje mataifa yote ya dunia kubarikiwa isipokuwa Kristo atakuwa amesimamisha serikali Yake duniani?

Ingawa Musa hakuwa “mhubiri wa haki†au mtume, alikuwa nabii na mwamuzi, na mtu wa kwanza ambaye Mungu alimwinua kuwaongoza Israeli. Pengine hukuwahi kumfikiria Musa kama mmoja wa waliohubiri injili. Bado, Biblia hufunua kwamba alihubiri, kwa Israeli wa zamani, walipokuwa jangwani. Tuliona kwamba Mwanzo 12:3, hurejelea injili, kama ilivyo Hesabu 24:17-19, na mafungu haya yote yaliandikwa na Musa.

Matendo 3:22 kwa wazi husema Musa alitangulia kunena kwamba Mungu atamwinua Yesu Kristo kama Nabii mkuu (Torati 18:15) kuhubiri kwa ulimwengu mzima (Matendo 3:23) wakati wa Kurudi Kwake! Wengi wanaelewa tu juu ya Musa kuwaongoza Israeli kutoka Misri, na hawajui kabisa jinsi Mungu alivyomtumia katika njia hii.

Waebrania 3:9 na 4:2 pia huonyesha kwamba Musa alihubiri injili kwa Israeli wa zamani. “Maana ni kweli, sisi nasi tumehubiriwa habari njema vile vile kama hao [Israeli wa zamani]†(4:2). Mafungu haya, pamoja na Matendo 3, huonyesha kwamba hii ilijumuisha kipindi chote mpaka—na cha—Samweli!

Matendo 3:24 humrejelea Samweli pia kama aliyehubiri injili. Angalia: “Naam, na manabii wote tangu Samweli na wale waliokuja baada yake, wote walionena [ikimaanisha kila mmoja], walihubiri habari za siku hizi [Kuja kwa Kristo na ufalme wa Mungu].†Hizi ni kauli nzito na za wazi. Haziwezi kufunikwa. Jiwezeshe mwenyewe kutumia muda kutafakari juu ya kile ulichokisoma. Fungu hili linatamka, “manabii WOTE wa Mungu…wote walionena…walihubiri habari za siku hizi.â€

Hatimaye, ingawa kila mtu anajua kuwa Daudi alikuwa mfalme, karibu hakuna anayefahamu kwamba alihubiri ufalme wa Mungu. Katika Zaburi 67:4, aliandika, “… Maana kwa haki Wewe [Bwana] utawahukumu watu, na kuwaongoza mataifa walioko duniani.†Kauli hii ni kielelezo dhahiri kwa serikali ya Mungu inayokuja.

Isaya, Yeremia, Ezekieli na Danieli

Nabii Isaya alitoa kauli za wazi kabisa kuhusu ufalme wa Mungu, kuhusu vile utakavyotokea na kuleta amani kwa mataifa yote duniani. Vile vile aliweka wazi kwamba ufalme wa Mungu huhusisha SERIKALI. Angalia “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na UWEZA WA KIFALME utakuwa begani mwake; Naye ataitwa Jina Lake, Mshauri wa Ajabu, Mungu Mwenye Nguvu, Baba wa Milele, Mfalme wa Amani. Maongeo ya ENZI Yake na amani hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na UFALME wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza; Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele†(9:6-7).

Unabii huu uko wazi mno kiasi kwamba hauhitaji ufafanuzi zaidi!

Nabii Yeremia alitangulia kusema, “Tazama siku zinakuja, asema BWANA, nitakapomchipushia Daudi Chipukizi la Haki [Kristo]; naye atamiliki mfalme, atatenda kwa hekima, naye atafanya hukumu na haki katika nchi. Katika siku zake Yuda ataokolewa, na Israeli atakaa salama, na jina lake atakaloitwa ni hili, BWANA NI HAKI YETUâ€(23:5-6; pia soma fu. 7-8).

Kama ilivyo kwa Isaya, mafungu haya hayahitaji ufafanuzi zaidi. Yeremia anatoa maelezo ya wazi ya matukio ambayo yanaweza kuelezewa tu kama kipindi baada ya ufalme wa Mungu kuwa umekwisha kuja duniani. Hivyo, alihubiri injili kwa Nyumba ya Yuda.

Kitabu cha Ezekieli huelezea wakati ambapo Mungu atawakusanya watu Wake kutoka matekani watakakochukuliwa siku zijazo. Hiki ni kipindi kinachofuata mara tu baada ya Dhiki Kuu (Math. 24:21-22)—kipindi cha maafa kwa wazao wa leo wa Israeli wa zamani. Sasa angalia: “Maana nitawatwaa kati ya mataifa, nami nitawakusanya na kuwatoa katika nchi zote, na kuwarudisha katika nchi yenu wenyewe†(36:24).

Mafungu kumi yanayofuata huelezea kipindi cha ujenzi mpya na mafanikio ambayo yanaweza kutokea tu baada ya Kurudi kwa Kristo. Chukua muda uyasome.

Danieli aliandika hivi: “Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha UFALME ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa ENZI yake; bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele†(2:44).

Je, nabii huyu alihubiri ufalme wa Mungu? Biblia hujibu ndiyo—na tutakuja kuona baadaye kuwa alifanya hivyo katika maeneo mengine mengi!

Manabii Wadogo Wote

Inaweza kuonyeshwa kwamba, kwa njia moja au nyingine, wale wote ambao hujulikana kama “Manabii Wadogo†walihubiri injili ya ufalme wa Mungu (inawezekana kuacha Yona.) Kumbuka, kuuona usemi “injili ya ufalme wa Mungu†si njia pekee ya kuielezea injili! Mafungu ya Mwanzo 12:3 na Wagalatia 3:8 yamekwisha kudhihirisha hili.

Yapitie tena mafungu yafuatayo. Katika kila fungu, utaona kuwa yanarejelea ufalme wa Mungu, moja kwa moja au kwa namna nyingine: Hosea 2:16, 19; 3:5; Yoeli 2:21-27; Amosi 9:11-15; Obadia 21; Mika 4:1-3; Habakuki 2:14; Zefania 3:14-20; Zakaria 14:1-3, 8-9; Malaki 3:1-3.

Baada ya kusoma maandiko haya, ni wazi kwamba Petro alikuwa sahihi, na kwamba “...zije zamani za kufanywa [urejeshaji] upya vitu vyote zilizonenwa na Mungu kwa kinywa cha manabii wake watakatifu tokea mwanzo wa ulimwengu,†ambazo zaweza kutokea tu pale serikali ya Mungu itakapokuja duniani.

Ni muhimu sana kusema jambo moja la mwisho. Matendo 3:21 husema, “Mungu amenena kwa kinywa cha…†Injili ya ufalme ni ujumbe kutoka kwa Mungu.

Lazima iwe wazi kwamba ni MUNGU anayenena kupitia kwa aina yoyote ya mtumishi Anayemtumia—nabii, mzee, mwamuzi, shemasi, mhubiri wa haki, mfalme, mchungaji, mwinjilisti au mtume! Kama kweli mtu alikuwa mtumishi wake, wakati wote Mungu alinena ujumbe huu huu kupitia kwake—“tokea mwanzo wa ulimwenguâ€!

Je, Kuna Injili Iliyojitenga ya Yesu Kristo?

Kama ilivyotajwa, Marko 1:1 huzungumzia “Mwanzo wa injili ya Yesu Kristo.†Hebu tuulize: Je, “injili ya Yesu Kristo†ni tofauti—injili—ya pili? Je, Paulo alisahau kwamba kulikuwa na injili nyingine kando ya ile inayohusu ufalme?

Jibu ni “Hapana†ya msisitizo! Lakini wahubiri wengi hufundisha kwamba injili ya Yesu Kristo ni kuhusu Kristo, pia wakidai kwamba Yeye ndiye ufalme wa Mungu na kwamba injili ya ufalme ni Kristo. Tumekwisha kuona kwamba huu ni uongo, na hautokani na Biblia kabisa! Injili ya Yesu Kristo ni injili Yake—ujumbe Wake kuhusu ufalme wa Mungu!

Tumeona kwamba Yesu alikuwa Mjumbe aliyetumwa kutoka kwa Mungu akiwa na TANGAZO! Haikuwa kuhusu Yeye Mwenyewe—ilihusu ufalme wa Mungu ukija kutawala juu ya dunia yote. Katika Yohana 12:49-50, Yesu alisema, “Kwa sababu Mimi sikunena kwa nafsi Yangu tu; bali Baba aliyenipeleka, Yeye mwenyewe ameniagiza nitakayonena na nitakayosema. Nami najua ya kuwa agizo Lake ni uzima wa milele; basi hayo ninenayo Mimi, kama Baba alivyoniambia, ndivyo ninenavyo.†Lazima iwe wazi sasa kwamba Kristo alitenda kama mjumbe—kama MSEMAJI kwa ajili ya ufalme wa Mungu.

Katika Yohana 14:24, Yesu alisema, “nalo neno mnalolisikia silo Langu, ila ni Lake Baba aliyenipeleka.†Kristo alileta ujumbe wa Baba—sio Wake mwenyewe. Jambo hili sasa lazima liwe limekuwa wazi kabisa. Kumbuka, alisema katika Luka 16:16 kwamba “Torati na manabii vilikuwapo [hubiriwa] mpaka Yohana; tangu wakati huo habari njema ya ufalme wa Mungu hutangazwa.â€

Hicho ndicho Kazi hii inafanya leo. Kupitia kitabu hiki, na vingine vingi, ukweli wa ufalme wa Mungu unahubiriwa kwako na kwa mamilioni wengine.

Ufalme wa Mungu Unakuja

Usifanye kosa lolote! Wakati hali ya ulimwengu inakaribia migogoro ya mwisho, hakuna mwanadamu aliyeweza kuleta serikali moja yenye kutawala dunia nzima ambayo ingeweza kufanikiwa. Yesu Kristo atarudi hivi karibuni na kusimamisha ufalme WAKE.

Wanafunzi hawakuelewa ni lini Kristo angesimamisha serikali ya Mungu duniani. Ilimlazimu kuwaeleza kwa kutumia mfano. Angalia: “Waliposikia hayo, aliongeza kusema mfano, kwa sababu alikuwa karibu na Yerusalemu, na wao walidhani ya kuwa UFALME WA MUNGU utaonekana mara†(Luka 19:11). Mfano huu mrefu hufafanua kwamba muda mrefu ungepita kabla ufalme haujaja.

Kabla ya kupaa Kwake mbinguni, katika Matendo 1, baada ya kukutana mara kadhaa na wanafunzi Wake, Kristo alikutana nao mara moja na ya mwisho. Mpaka mwisho kabisa, Aliendelea kuwafafanulia zaidi ufalme wa Mungu. Lakini walibaki wamekanganyikiwa kuhusu ni lini utasimamishwa: “hata siku ile alipochukuliwa juu... [alikuwa] akiyanena mambo yaliyouhusu UFALME WA MUNGU… Basi walipokutanika, wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo unapowarudishia Israeli UFALME?†(fu. 2-3, 6).

Kristo alifafanua, “Si kazi yenu kujua nyakati wala majira…†(fu. 7). Hata leo hatuwezi kujua hasa ni lini utakuja, lakini tunaweza kujua kuwa uko karibu.

Sasa angalia Danieli 7:18: “Lakini watakatifu wake Aliye juu wataupokea ufalme, na kuumiliki huo ufalme milele, naam hata milele na milele.†Kisha fungu la 22 husema, “Hata akaja huyo Mzee wa Siku [hapa ni Kristo, na Baba ametajwa kwenye fungu la 13], nao watakatifu Wake Aliye juu wakapewa hukumu; na majira yakawadia watakatifu waumiliki ufalme.â€

Mwisho, angalia fungu la 27: “Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu Wake Aliye Juu; ufalme wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka [watawala] watamtumikia na kumtii.â€

Danieli alijua kwamba siku moja watakatifu watatawala na Kristo duniani!

Hubiri la kwanza la Yesu lililoandikwa, huitwa “Hubiri juu ya Mlima,†husema kwamba “wapole watairithi nchi†(Math. 5:5). Kwa hakika, Kristo alikuwa anamnukuu Daudi, aliyeandika ripoti hii katika Zaburi 37:11—ni mahali pengine Daudi alipoitangaza injili. Maneno yaliyotumika hapo ni yale yale. Unabii mwingine pia huonyesha kwamba siku moja Daudi mwenyewe atatawala juu ya makabila yote ya Israeli (ona Ezekieli 34) ndani ya ufalme wa Mungu.

Angalia mafungu matatu tofauti katika Ufunuo. Kristo amenukuliwa kupitia Yohana akisema, “Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja Nami katika kiti Changu cha enzi, kama Mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba Yangu katika kiti Chake cha enzi†(3:21). Pia 2:26-27: “Na yeye ashindaye…nitampa mamlaka juu ya mataifa: naye atawachunga kwa fimbo ya chuma.†Mwisho, “ukawafanya kuwa UFALME na MAKUHANI kwa Mungu wetu; nao wanamiliki juu ya nchi†(5:10).

Je, dini yoyote iliyoundwa imekuambia kuhusu mojawapo ya mafungu haya? Bila shaka hakuna kabisa. Japokuwa yamekuwepo ndani ya Biblia kwa maelfu ya miaka.

Si ajabu kwamba Kristo alipokuwa akishtakiwa kwa ajili ya maisha Yake, Aliongeza zaidi kwenye ripoti Yake iliyonukuliwa mapema katika kitabu, “UFALME Wangu sio wa ulimwengu huu. Kama UFALME Wangu ungekuwa wa ulimwengu huu, watumishi Wangu wangenipigania, nisije nikatiwa mikononi mwa Wayahudi: Lakini UFALME Wangu si wa kutoka hapa†(Yohana 18:36). Katika majibizano haya, Pilato alikuwa amemuuliza, “Wewe u mfalme basi?†Kristo alijibu, “Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya Mimi nalikuja ulimwenguni…†(fu. 37).

Yesu alielewa kikamilifu kwamba Alizaliwa kuwa Mfalme!

Kristo Kuwa Mfalme

Kuja kwa Kristo Mara ya Kwanza lilipaswa kuwa tukio kubwa. Isaya alitabiri kuzaliwa Kwake na bikira: “Kwa hiyo BWANA Mwenyewe atawapa ishara. Tazama, bikira atachukua mimba, atazaa mtoto Mwanamume, naye atamwita jina lake Imanueli†(7:14).

Kabla ya kuzaliwa kwa Yesu, malaika alimtokea Mariamu kumfafanulia kusudi la Mungu na kile kilichokuwa kinaenda kumtokea: “Mwezi wa sita, malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda mpaka mji wa Galilaya, jina Lake Nazareti, kwa mwanamwali… Mariamu†(Luka 1:26-27).

Kuanzia fungu la 30, Gabrieli anaelezea zaidi kuhusu Kristo na jinsi ambavyo hatimaye atatawala kwenye kiti cha enzi cha Daudi. Angalia: “Malaika akamwambia, Usiogope, Mariamu, kwa maana umepata neema kwa Mungu. Tazama, utachukua mimba na kuzaa mtoto Mwanamume; na jina Lake utamwita YESU. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye Juu, na Bwana Mungu atampa KITI CHA ENZI cha Daudi, baba Yake. ATAIMILIKI nyumba ya Yakobo hata milele, na UFALME Wake utakuwa hauna mwisho†(fu. 30-33).

Kristo kamwe hakuwa na shaka kuhusu utume na kusudi la maisha Yake. Hii ndiyo sababu alifululiza kuhubiri ufalme wa Mungu popote alipokwenda.

Isaya aliongea kwa undani zaidi kuhusu jinsi ambavyo ufalme wa Mungu utaenea duniani, hatimaye kufunika mataifa yote: “Na itakuwa katika siku za mwisho, mlima wa nyumba ya BWANA utawekwa imara juu ya milima, nao utainuliwa juu ya vilima; na mataifa yote watauendea makundi makundi. Na mataifa mengi watakwenda na kusema, Njoni, twende juu mlimani kwa Bwana, nyumbani kwa Mungu wa Yakobo, naye atatufundisha njia Zake, nasi tutakwenda katika mapito Yake maana katika Sayuni itatoka sheria, na neno la Bwana katika Yerusalemu. Naye atafanya hukumu katika mataifa mengi, atawakemea watu wa kabila nyingi; nao watafua panga zao ziwe majembe, na mikuki yao iwe miundu; taifa halitainua upanga juu ya taifa lingine, wala hawatajifunza vita tena kamwe†(2:2-4).

Unabii ulio sawa na huu umerudiwa kwa msisitizo katika Mika 4:1-3. Aya hizi hutabiri kwamba ufalme wa Mungu utaenea ulimwenguni. Hii ndiyo sababu mfano mmoja wa Kristo ulilinganisha ufalme na chachu (Luka 13:20-21), ambayo daima husambaa na kujaa ilimowekwa. Kusudi kuu la maisha yako ni kushiriki kuieneza SERIKALI ya Mungu kwa wakati ujao.

Mbele ya jengo la Umoja wa Mataifa kuna sanamu ya mtu mkubwa akifua panga kuwa jembe. Nimeiona mara nyingi sana, kwa sababu niliendesha huduma za kanisa mtaani hapo mkabala na mahali ilipo kwa miaka kadhaa. Lakini hakuna mtu anayeonekana kutilia maanani tena, au hata kuamini, unabii wa kushangaza unaoelezewa na sanamu hili maarufu.

Yesu Kristo alikuja kuwa MFALME ambaye siku moja ATATAWALA duniani. Atakaporudi, mateso, masikitiko, huzuni na matatizo yote ya dunia na maovu vitatoweka—na amani ya dunia “itajitokeza,†halisi sambamba na furaha kuu, mapatano na mafanikio tele kwa mataifa yote. Hakuna serikali ya mwanadamu iliyoweza kuleta mambo haya hata kwa nchi moja duniani. Hiki ndicho kiini cha injili ambayo Kristo aliileta.

Je, unaiamini? Utaiamini?

Bado Ufalme wa Mungu Lazima Uhubiriwe Leo

Katika unabii wa Mlima wa Mizeituni kwenye Mathayo 24 (na 25), Kristo aliulizwa kuhusu matukio ambayo yangekuwa ishara ya Kuja Kwake Mara ya Pili na mwisho wa ulimwengu (zama). Alijibu kwamba matukio na hali mbalimbali tofauti vitatokea kwanza.

Tukio moja linalotangulia Kurudi kwa Kristo limeelezewa katika fungu la 14: “Tena habari njema ya ufalme itahubiriwa katika ulimwengu wote, kuwa ushuhuda kwa mataifa yote; hapo ndipo ule mwisho utakapokuja.†Injili ya kweli ilitabiriwa kuhubiriwa mpaka “mwisho utakapokuja.†Hii inamaanisha wazi kwamba mtu fulani atakuwa anaihubiri sasa, katika zama yetu, kwa sababu mwisho bado haujaja.

Historia kidogo: Maarifa ya injili ya kweli yalirejeshwa na Herbert W. Armstrong (1892-1986). Injili ilikuwa haijahubiriwa kwa ulimwengu kwa takribani karne 19 mpaka bwana Armstrong alipoanza kuihubiri mwezi Januari 1934, wakati unabii wa Mathayo 24:14 ulipoanza kufunuliwa. Elewa! Tangu karne ya kwanza ulimwengu wote haukuwahi kusikia ujumbe huu. Kwa kipindi chote cha huduma ya miaka 52, mpaka kifo chake mwaka 1986, Mungu alimtumia bwana Armstrong kuwafikishia ufahamu huu mamia ya mamilioni. Huyu ndiye mtu aliyenifundisha mimi injili ya kweli na ambaye chini yake nilifunzwa kuweza kuupeleka ujumbe huu huu kwa ulimwengu.

Kumbuka, mwisho bado haujaja. Kwa hiyo, Kanisa la Mungu Rejeshwa linaendeleza utume huu, kwa ujasiri likihubiri ukweli huu mkuu kati ya kweli za kiunabii. Kuwasili kwa ufalme wa Mungu ni hakika—hakuna shaka! Utakapofika, wewe pia unaweza kuwa sehemu yake.

Mpango wa Miaka-7,000

Ukiwa umetengwa na Mungu kwa sababu ya dhambi (Isa. 59:1-2), ubinadamu umeamini uongo wa mungu wa dunia hii kwa miaka 6,000. Muhula wa Mpango wa Mungu kwa wanadamu utachukua miaka 7,000. Wachache wameelewa hili. Wengi wameelewa kwa usahihi angalau mafungu machache yanayoelezea Utawala wa Kristo wa miaka 1,000 unaokuja, utakaoanza wakati wa Kurudi Kwake (Ufu. 20:4-6). Lakini hawajui chochote kuhusu Mungu kutenga miaka 6,000, au siku-milenia sita za “juma la siku-saba,†kwa ajili ya utawala wa mwanadamu, chini ya Shetani, kabla ya miaka 1000 ya “siku†ya saba. Tuko karibu sana na mwisho wa “siku ya sita.â€

Hebu tuelewe! Biblia inasema, “Lakini, wapenzi, MSILISAHAU neno hili, kwamba kwa Bwana siku moja ni kama miaka elfu, na miaka elfu ni kama siku moja†(2 Pet. 3:8; Zab. 90:4). Kwa hakika, wengi “wamepuuza†karibu KILA KITU ambacho Biblia hufundisha.

Lakini unaweza kujua!

Mwanadamu (chini ya utawala wa Shetani usioonekana) amepewa “siku†sita, au miaka 6,000, kujaribu njia zake, serikali, dini, falsafa, mifumo ya maadili na mitindo ya elimu. Chini ya ushawishi wa Shetani, ametenda dhambi na uasi kwa maagizo ya Mungu kipindi hiki chote. Na ameshajaribu kutibu athari zote mbaya zilizojitokeza, badala ya chanzo, ambacho ni uvunjaji wa amri za Mungu. Mungu anauruhusu ubinadamu kujifunza masomo magumu, machungu. Walio wengi ambao kamwe hawakuwahi kujua thamani ya ukweli wa Mungu, lazima wajifunze kwamba njia zao wenyewe hazifai kitu!

Muda mfupi ujao, ulimwengu utashuhudia kutimia kwa Ufunuo 11:15: “Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo Wake, Naye atamiliki hata milele na milele.â€

Yesu Kristo alizaliwa kuwa Mfalme ambaye atatawala mataifa yote ya dunia milele akisaidiwa na wafalme wengine walio roho: “Na upanga mkali hutoka kinywani Mwake ili awapige mataifa kwa huo. Naye atawachunga kwa fimbo ya chuma… ana jina limeandikwa katika vazi Lake na paja Lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA†(Ufu. 19:15-16).

Je, kuna mtu yeyote aliyewahi kukuambia juu ya aya hizi? Sikuwahi kujifunza habari zake au hata kuzisikia katika kanisa la ujana wangu—na bado, ndizo hizi hapa, zimeandikwa kwa maana ya wazi bila utata kwa wote watakaotii.

Ufalme wa Mungu Wafafanuliwa

Mathayo 6:33 inasema, “Bali utafuteni kwanza ufalme wa Mungu, na haki Yake…â€

Kama unatafuta kitu fulani kwanza katika maisha, ingekuwa vyema ukaelewa ni nini hasa unachotafuta.

Lengo kuu katika sura hii si kufafanua kwa undani ufalme wa Mungu. (Hii itafanyika baadaye). Ni kufafanua fasili ya injili ya kweli na uwezekano wa kustaajabisha wa ubinadamu.

Hivyo hebu tuelewe. Neno “ufalme†kwa urahisi humaanisha serikali. Kwa hakika, huwezi kuwa na serikali bila taifa la kutawala. Kwa hivyo, ufalme kwa uchache ni taifa moja pamoja na serkali yake.

Kuna vipengele vinne vya muhimu kwa ufalme wowote: (1) Ardhi, mali au eneo—liwe kubwa ama dogo. Kwa maneno mengine, ni lazima pawepo na mipaka halisi inayotambulisha eneo la ufalme; (2) mtawala, mfalme, mtawala mkuu au gavana anayeongoza serikali, (3) watu au wananchi wanaoishi katika eneo la utawala, na (4) mfumo wa sheria na kanuni sambamba na muundo msingi wa serikali. Hakuna ufalme uliokamilika bila kuwa na mambo haya yote ya msingi.

Lakini mambo haya yanahusika vipi na ufalme wa Mungu? Wengi hawajui mambo ya msingi ya ufalme wa Mungu. Je ni ufalme halisi wenye mahali halisi duniani, wenye watu na sheria, zikisimamiwa na mtawala? Wengi huamini ufalme ni kitu fulani kilichomo katika mioyo ya watu. Wengine wanaamini kuwa uko mahali popote utakapoona kanisa fulani. Bado wengine wanaamini kwamba ni Yesu Kristo mwenyewe. Baadhi wanaamini kwamba uko hapa duniani sasa na wengine wanaamini kwamba haujaja bado, lakini hawaelewi—hawana wazo—jinsi utakavyotokea.

Tunaweza kuuliza: Jinsi gani mtu anauingia ufalme wa Mungu?

Ni Lazima Mtu azaliwe Mara ya Pili Kuuingia Ufalme

Paulo aliandika kwamba Kristo ni “mzaliwa wa kwanza kutoka kwa wafu†(Kol. 1:18), na pia “mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi†(Rum. 8:29). Yakiunganishwa, mafungu haya yanaonyesha kwamba Yesu ni mzaliwa wa kwanza tu kutoka kwa wafu, na wengine wengi watafuatia. Lakini ni lini, na katika nini, hawa wengine watazaliwa?

Katika Yohana 3:3, Kristo alimwambia Nikodemo, “Amin, amin [hii humanisha kweli, kweli], nakuambia, Mtu ASIPOZALIWA MARA YA PILI, hawezi kuuona ufalme wa Mungu.†Katika fungu la 6, Kristo anaendelea, “Kilichozaliwa kwa mwili ni mwili; na kilichozaliwa kwa Roho ni roho.†Kwa urahisi tu amini maana dhahiri ya fungu hili. Ni lazima mtu afanyike roho ili KUUONA ufalme wa Mungu.

Paulo alifundisha, “nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu†(1 Kor. 15:50). Mafungu mawili yanayofuata hufafanua kuwa ufufuo utatokea wakati wa Parapanda ya Saba (mwisho), wakati “wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika.â€

Kristo atarudi wakati Parapanda ya Saba ya Ufunuo 11 italia. Huu ndio wakati ambao ufufuo wa wafu utatokea. Usilielewe vibaya tukio hili la upeo wa juu kabisa, litakaloelezwa kwa uangalifu zaidi baadaye. Inatosha kusema hapa, watu ambao hapo kabla walikuwa wanadamu wa nyama watabadilishwa kuwa roho—watazaliwa mara ya pili—na kuingia katika ufalme wa Mungu. Hakuna watu halisi wanaoweza kuuingia ufalme.

Yohana 4:24 inasema, “Mungu ni Roho.†Chini ya Baba, Kristo anaongoza ufalme Wake, ambao unaundwa na viumbe roho. Wakati wa Kurudi Kwake Kristo, kama mwanakaya [memba] wa Familia ya Mungu, atakuwa na wadogo wengi “ndugu wakiume na wakike,†watakaokuwa wamefuzu kutawala pamoja Naye.

Fikiria namna hii: Uko ufalme wa mimea, ufalme wa wanyama, falme za wanadamu na ufalme wa malaika. Vile vile kuna ufalme wa Mungu.

Sasa angalia Mwanzo 1:26: “Na tumfanye mtu kwa mfano WETU, kwa sura YETU.†Wakijirejelea wao wenyewe, Yule anayeongea anasema, “Sisi,†“Wetu†na “Yetu.†Huu ni uthibitisho kwamba katika Uungu wako zaidi ya mmoja—kwa sasa wako wawili! Katika andiko hili, neno la Kiebrania kwa ajili ya Mungu ni Elohim. Neno hili ni la wingi katika umoja kama kundi, timu, kamati au familia. Maneno haya yote yanawakilisha kitu kimoja, chenye washiriki kadhaa au watu.

Kwa hivyo, tutaona kwamba Biblia inafundisha kwamba yuko Mungu mmoja, mwenye nafsi mbili—Baba na Kristo—na wengine wengi zaidi kuongezewa baadaye. Mara ya kwanza Mungu atakapoongeza wana wengi katika Familia Yake ni pale ufalme wa Kristo unaposimamishwa. Lakini kuuingia ufalme wa Mungu halitakuwa jambo la moja kwa moja kwa mtu yeyote.

Yako Masharti Kuuingia Ufalme

Tunasoma katika sehemu kadhaa ambapo Kristo alisema ni wale tu wanaoshinda ndio watakaourithi ufalme na kutawala pamoja Naye. Kuna zaidi ya kuwepo katika ufalme wa Mungu kuliko kuutamani tu. Kuna MASHARTI ya kufuzu ambayo lazima yatimizwe.

Yesu alimwaambia kijana tajiri aliyeuliza kuhusu uzima wa milele, “…ukitaka kuingia katika uzima, zishike amri†(Math. 19:17). Alifafanua kwamba mtu ni sharti azishike Amri Kumi ili aweze kuokolewa, na akanukuu tano kati yake.

Sasa dhambi ni nini? Kwa kuwa kuitenda huleta mauti (Rumi 6:23), si ni vyema ukajua ni nini? 1 Yohana 3:4 imerekodi, “Dhambi ni uvunjaji wa sheria.†Hii ni sheria ile ile ambayo kijana tajiri aliambiwa ni sharti aitii ili aweze kuurithi uzima wa milele.

Wengi hudai kuwa Wakristo—kuwa wafuasi wa Kristo. Wanadai “kumwamini Kristo†na hudai kuwa “watafutaji wa ukweli,†wakati hawataki ukweli halisi wa Biblia kabisa. Angalia majibizano haya marefu ambayo Yesu Kristo aliyafanya na Mafarisayo: “Basi Yesu akawaambia wale Wayahudi waliomwamini [hawa walikuwa “wauminiâ€], Ninyi mkikaa katika NENO LANGU, mmekuwa wanafunzi Wangu kweli kweli; tena mtaifahamu KWELI, nayo hiyo KWELI itawaweka huru…lakini mnatafuta kuniua kwa sababu NENO LANGU halimo ndani yenu…Lakini sasa mnatafuta kuniua Mimi, mtu ambaye nimewaambia ILIYO KWELI, niliyoisikia kwa Mungu…Mungu angekuwa Baba yenu, mngenipenda Mimi; kwa maana nalitoka kwa Mungu...Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo? Ni kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia NENO LANGU… Nami, kwa sababu nasema iliyo KWELI, hamnisadiki [bado inasema “walimwaminiâ€]...Nami nikisema KWELI, mbona ninyi hamnisadiki?†(Yohana 8:31-32, 37, 40, 42-46). Yesu anaendelea katika maelezo kwa kuwashutumu kwa wazi wale ambao watadai kuwa Wakristo wakati kwa hakika ni “wa baba (yao) ibilisi.â€

Wengi hudai kuwa “wanamjua Yesu†wakati kwa hakika hawajui chochote juu ya Kristo wa kweli wa Biblia. Kama alivyosema, kwa hakika “hawawezi kusikia†maneno ya Kristo—KWELI—ingawa wanaweza kufikiri kuwa wanasikia: “Yeye asemaye, NIMEMJUA, wala hazishiki amri Zake, ni mwongo, wala KWELI haimo ndani yake†(1 Yohana 2:4). Ulimwengu umejawa na mamia ya mamilioni ya “Wakristo†wa aina hii, wakifuata aina ya Yesu, lakini hawaijui kweli.

Wengi wasiouishi Ukristo, hujiingiza katika Kanisa la kweli. Lakini hatimaye wote huondoka. Yohana aliendelea, “Walitoka kwetu, lakini hawakuwa wa kwetu. Maana kama wangalikuwa wa kwetu, wangalikaa pamoja nasi. Lakini walitoka ili wafunuliwe kwamba si wote walio wa kwetu†(fu. 19). Nimeliona hili mara nyingi. Wengi wanaonekana kuamini juu ya Kristo, si kumwamini Yeye hakika—yaani kuamini kile alichokisema, na akasema KUTENDA!

Kumbuka maneno ya Kristo katika Marko 1:15: “TUBUNI, na kuiamini injili.†Toba ni kutoka dhambini (Matendo 3:19). Mkristo ni yule aliyegeuka kutoka—ametubu—dhambi zake, na amebatizwa (2:38) na kuongoka (3:19). Kwa maisha ya kushinda dhambi, Mkristo hufuzu kwa (ingawa hawezi kuchuma) wokovu na kuzaliwa katika roho kuingia ufalme wa Mungu.

Uwezekano Wako wa Kustaajabisha

Kumbuka Mungu alisema kwamba aliwaumba wanadamu kwa “sura†na “mfano†Wake. Fungu hili humaanisha kile linachokisema. Mungu alikuumba wewe ili uwe “kama†Yeye kwa kila namna. Kwa njia ya Roho Yake kuingia katika mawazo ya kila mtoto Wake mpya aliyeongoka, maisha mapya kabisa ya roho yametungwa. Katika wakati huo, “kiinitete†kidogo cha roho-kilichotungika hutokea, kikiwa tayari kukua na kuendelea katika mwonekano mzima wa roho, kwa mantiki hiyo tunaweza kusema, kwanza “kijusi,†kisha kuzaliwa.

Agano la Kale na Jipya kwa pamoja huweka wazi kabisa jambo hili! Wakati baadhi wana uelewa usio dhahiri kwamba Wakristo kwa namna fulani, wanakuwa “wana wa Mungu,†hakuna aliyewahi kufikiria jambo hili: “Wapenzi, sasa tu wana wa Mungu, wala haijadhihirika bado tutakavyokuwa; lakini twajua ya kuwa atakapodhihirishwa, tutafanana NAYE; kwa maana tutamwona kama alivyo†(1 Yohana 3:2). Tafakari maarifa haya ya kuduwaza, yasiyojulikana karibu na wote wanaojidhani kuwa Wakristo! Siku moja tutafanana kabisa na Kristo. Warumi 8:16 inasema kwamba sisi ni “watoto†wa Mungu na “warithi†pamoja na Kristo.

Mfalme Daudi pia alielewa jambo hili miaka elfu moja mapema alipoandika, “Bali mimi nikutazame uso wako katika haki, Niamkapo nishibishwe KWA SURA YAKO†(Zab. 17:15). Bila kutegemea, fungu hili huondolea mbali wazo la “njozi nzuri†ya kufikirika iliyosambazwa na kanisa la ulimwengu—kwamba watu hawatauona uso wa Mungu katika maisha yajayo. Daudi alielewa kwamba tutamwona Mungu—na uso kwa uso. Vivyo hivyo Yohana. Wote walielewa kuwa, kwenye Ufufuo—“tutakapoamkaâ€â€”tutakuwa kamili kama Mungu, katika umbo na tabia.

Kwa hivyo, Mungu anazaliana Mwenyewe katika wanadamu ambao wamepokea Roho Yake Takatifu. Anaumba watoto watakaofanana Naye kwa kila namna!

Lakini Petro aliandika kwamba ni lazima Wakristo “WAKUE katika neema, na katika kumjua Bwana wetu na Mwokozi Yesu Kristo†(2 Petro 3:18). Wakristo wanapaswa—na lazima—wakue katika maisha haya ya sasa. Ili wapewe mamlaka ya kiungu na nguvu, kama warithi-pamoja na Kristo, lazima wafuzu, kwa kujenga tabia takatifu ya haki ya Mungu katika maisha yao.

Paulo alifafanua kwamba jukumu la mtumishi mwaminifu katika Kanisa ni kulilisha kundi. Yesu alisema, “Nitalijenga Kanisa Langu†(Math. 16:18). Ni Kanisa—Kanisa LILE—ambalo ni “Yerusalemu wa juu…mama yetu sisi†(Gal. 4:26; Ebr. 12:22-23). Kama alivyo mama yeyote, Kanisa hutunza na kulisha watoto wake—na amekuwa akifanya hivyo kwa miaka 2,000. (Jukumu la Kanisa kama mama yetu litafafanuliwa zaidi katika Sura ya Kumi.)

Andiko la Kustaajabisha

Kitabu cha Waebrania kinafunua Kusudi la Mungu la kustaajabisha kwa uwazi kama kioo. Muktadha huanza katika Sura ya 1. Tazama picha ya wokovu ikifunuka.

Kwanza, elewa kwamba Mungu aliumba malaika wawe “roho watumikao†wakitumwa kuwahudumu wale “watakaourithi wokovu†(fu. 14). Hili ndilo jukumu lao katika mpango wa Mungu. Malaika hawajapewa nafasi ya kuwa wanakaya [memba] katika Familia ya Mungu. Hii ndiyo sababu Shetani (kama malaika aliyeanguka) anachukia sana wazo kwamba wanadamu wa nyama, wadhaifu, wa hali ya chini wanaweza kupokea kile ambacho hakikutolewa kwake wala hawezi kukipata.

Paulo ananukuu sehemu mbili katika Zaburi: “Kwa maana Alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe Mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa Kwake Baba, Na Yeye atakuwa Kwangu Mwana?...†(fu. 5). Kamwe Mungu hajawahi kusema hili kwa malaika yeyote!

Kisha Paulo ananukuu zaburi nyingine, akifafanua kile ambacho kimekuwa kusudi la Mungu: “KITI Chako CHA ENZI, Mungu, ni cha milele na milele; Na fimbo ya UFALME Wako ni fimbo ya adili…†(fu. 8). Fimbo hutumika kama alama ya utawala au mamlaka—na katika ufalme Wake ni Mungu aliye na nguvu zote.

Mwisho, Paulo analiuliza swali lile lile kwa namna nyingine kuhusu malaika: “Je! Yuko malaika aliyemwambia wakati wo wote, Uketi mkono Wangu wa kuume Hata nitakapoweka adui Zako chini ya Miguu Yako? Je! Hao wote si roho watumikao, wakitumwa kuwahudumu wale watakaourithi wokovu?†(fu. 13-14).

Hii inaweka jukwaa kwa ajili ya kile ambacho lazima tukifahamu! Hebu tutafakari vilivyo mustakabali wa kustaajabisha ambao Mungu ameandaa kwa ajili ya wale wote wanaomtumikia.

Mfululizo wa mafungu ya kushangaza unaendelea katika sura ya 2. Paulo alimnukuu Daudi (kutoka Zaburi 8:4-6) alipouliza swali hilo la muhimu-kuliko yote, “Mwanadamu ni nini hata Umkumbuke?†(fu. 6). Kwa kuwa Mungu ni wa milele, na huketi juu ya ulimwengu wote na ndiye mwenye uweza wote chini Yake, sio ajabu Daudi aliuliza, na Paulo akarudia, swali hili lilio kiini cha maisha.

Jibu la kushangaza huanza katika fungu linalofuata: “Umemfanya [mwanadamu] mdogo punde kuliko malaika, Umemvika taji ya utukufu na heshima, Umemtawaza juu ya kazi za mikono Yako.â€

Hatimaye Mungu atashiriki utawala wa uumbaji Wake wote na Wana Wake. Kwa mara nyingine, Kristo ni wa kwanza tu wa Wana wengi. Kuzaliwa kwa mtoto wa kwanza hakuzuii kuzaliwa kwa wana wengine (na mabinti) kwa familia hiyo. Ninao wana wawili na mimi ni mzaliwa wa kwanza wa kiume nikiwa na kaka mdogo. Baba yangu alikuwa kijana wa pili, akiwa na kaka yake na kuendelea.

Paulo anaendelea kufafanua kwamba Mungu anapanga kuwapa Wana Wake nguvu nyingi ajabu na mamlaka: “Umeweka VITU VYOTE chini ya miguu yake. Kwa maana katika kuweka vitu vyote chini yake hakusaza KITU kisichowekwa chini yake. Lakini sasa bado hatujaona vitu vyote kutiwa chini yake†(fu. 8). Bado hili halijatokea—lakini litatokea hivi karibuni.

Mungu anaposema kwamba “vitu vyote†vitawekwa chini ya miguu ya mwanadamu, hicho ndicho anachomaanisha! Ulimwengu usiopimika, pamoja na mamilioni kwa kipawa cha nne cha nyota na trilioni moja ya galaksi, vitawekwa chini ya mamlaka ya wanadamu watakaokuwa wamezaliwa katika Familia ya Mungu. Kwa hakika, tafsiri ya Biblia ya Moffatt hulitafsiri neno la Kigiriki “vitu vyote†kama “ULIMWENGU.â€

Kwa kweli haya ni maarifa ya kuduwaza! Tumia muda kuyashika. Furahia kile ambacho kinaweza kuwa mustakabali WAKO!

Kabla ya kuendelea, angalia fungu la kushangaza kuhusu kipengele kingine kinachohusiana cha wokovu ambacho hakikueleweka kabla. Tumeona kwamba Wakristo wanasubiri wokovu wa kustaajabisha ajabu. Lakini uumbaji kwa ujumla nao unasubiri kwa hamu kubwa kufunuliwa kwa wale wana wapya watakaoongezwa kwenye Familia ya Mungu. Soma mafungu yafuatayo kwa uangalifu kutoka Biblia ya Revised Standard Version:

“Kwa maana viumbe vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu. Kwa maana viumbe vyote [vitu vyote katika ulimwengu unaojulikana] pia vilitiishwa chini ya ubatili; si kwa hiari Yake, ila kwa sababu Yake Yeye aliyevitiisha katika tumaini; kwa kuwa viumbe vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa WATOTO WA MUNGU. Kwa maana twajua ya kuwa viumbe vyote [kila kitu] pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa. Wala si hivyo tu; ila na sisi wenyewe [Wakristo] tulio na malimbuko ya Roho, sisi [WACHACHE wanaoitwa sasa] pia tunaugua katika nafsi zetu, tukikutazamia [kufanywa] wana†(Rumi 8:19-23).

“Wana wote wa Mungu†wajao hatimaye watauweka huru uumbaji ambao sasa uko utumwani, na uliotabiriwa kuendelea kuwa mbaya zaidi. Dunia iliyooza na kujeruhiwa, jua, mwezi na nyota—ulimwengu!—utafanywa upya hivi karibuni na kurudishwa kwenye hali ya uzuri, usawa na utulivu chini ya uongozi wa Kristo na watakatifu waliofufuliwa.

“Kuleta Wana Wengi Kwenye Utukufuâ€

Sasa tunaweza kuendelea na maelezo ya muhimu sana katika Waebrania 2: “Ila twamwona Yeye aliyefanywa mdogo punde kuliko malaika, yaani, Yesu, kwa sababu ya maumivu ya mauti, amevikwa taji ya utukufu na heshima, ili kwa neema ya Mungu aionje mauti kwa ajili ya kila mtu. Kwa kuwa ilimpasa Yeye, ambaye kwa ajili Yake na kwa njia Yake vitu vyote vimekuwapo, akileta WANA WENGI WAUFIKILIE UTUKUFU, kumkamilisha Kiongozi mkuu wa wokovu wao kwa njia ya mateso†(fu. 9-10).

Aya hii inafunua uwezekano wa kushangaza uliopangwa kwa ajili ya Wakristo wote. Wakati Kristo atakaporudi, Paulo anafunua kwamba watakuwepo “WANA WENGI†watakaoufikilia “utukufu†kwa njia ya “Kiongozi mkuu wa wokovu wetu.â€

Fungu la 11 husema kwamba Kristo “haoni haya kuwaita [wale wana wengine wengi—sisi] ndugu.†Hawa ndio wale ambao kwao Kristo huitwa “mzaliwa wa kwanza.†Kwa kweli, mtu aliyetungwa ameitwa kuufikilia “utukufu†na kuwa mmoja wa “wana wengi.†Mateso na dhabihu ya Kristo ndivyo vinavyomfanya kuwa “Kiongozi mkuu wa wokovu waoâ€â€”na awezekanaye kabisa kuwa wako!

Ni uwezekano wa kustaajabisha namna gani kwa wale ambao Kristo anawaita…ndugu.†Sasa angalia fungu hili la mwisho: “Maana Yeye atakasaye na hao wanaotakaswa wote pia watoka kwa mmoja. Kwa ajili hii Haoni haya kuwaita ndugu†(fu. 11). Kristo na watakatifu wanashiriki wokovu ule ule.

Fungu hili linaonyesha kwamba Wakristo “wametakaswa†(tengwa). Kwa namna gani? Yohana anasema, “Uwatakase [Wakristo waliotungwa] kwa ile kweli; NENO LAKO NDIYO KWELI†(Yohana 17:17).

Tamaduni na hadithi zinazoshabikiwa na wanadamu, kuhusu maisha baada ya kifo au kitu kingine chochote, huanguka vinapochunguzwa. Wakristo, wakiwa wametoka kwenye ulimwengu uliodanganyika na kukanganyikiwa, wametengwa kutoka ulimwenguni kwa ile KWELI!

Kama Kristo “haoni haya kuwaita (sisi) ndugu,†hivyo basi sisi, wana wa Mungu waliotungwa, lazima tusione haya kuitetea ile kweli inayotutakasa—na kweli ya injili (Fil. 1:17). Ni lazima “tukue†kwa Kristo (Efe. 4:13) na tuyashike mafundisho ya kweli ya Mungu. Ni lazima TUFUZU ili siku moja tusimame kando ya Kristo juu ya “vitu vyote.â€

Sasa rudi nyuma. Unakiona kilichoelezwa hapa? Lengo la kushangaza la Mkristo ni kuzaliwa katika ufalme wa Mungu—kufanyika nafsi roho AKITAWALA chini ya Kristo, kama mwana halisi wa Mungu. Kipi chaweza kuwa cha ajabu zaidi—cha UTUKUFU zaidi!—kwa ajili ya Mkristo kukitazamia?

Kristo Anarudi

Mathayo 24:27 inasema kwamba Kristo atakaporudi, Kuja Kwake kutakuwa kama umeme uking’aa kutoka mashariki hata magharibi. Hili litakuwa ni tukio litikisalo dunia yote, isiwezekane kulikosa.

Danieli aliongea juu ya Kristo kuja katika “mawingu ya mbinguni†(7:13). Kabla ya Kurudi Kwake, Mungu anampa rasmi MAMLAKA kutawala ulimwengu. Watakatifu hawawezi kupewa mamlaka na Kristo mpaka Yeye atakapopewa mamlaka kwanza. Hapo ndipo atakapoweza kuwapa nguvu wengine. Angalia: “Naye AKAPEWA [Kristo] mamlaka, na utukufu, na UFALME, ili watu wa kabila zote, na taifa zote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka Yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na UFALME Wake ni ufalme usioweza kuangamizwa†(fu. 14).

Lakini wajibu wa Mkristo katika maisha haya ni KUFUZU kuwa sehemu ya ufalme wa Mungu. Si ajabu Kristo alisema, “Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa, naye atawachunga kwa fimbo ya chuma…kama Mimi nami nilivyopokea kwa Baba Yangu†(Ufu. 2:26-27) na mafungu machache baadaye, “Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja nami katika kiti changu cha enzi…†(3:21). Kristo atakaporudi, watakatifu watawala pamoja Naye!

Msisimko wa maisha ya milele utakuwa hauna maelezo. Tutakuwa na uweza wa Mungu, kamwe hatutajisikia kuchoka, mateso, maumivu au uovu wa aina yoyote ile. Matazamio ya miradi mipya, mafanikio ya kustaajabisha na furaha isiyosemeka vitadumu milele.

Nani ambaye asingeyataka haya? Kwa nini mwanadamu hakuwahi kujua kwamba hii imekuwa HATIMA yake wakati wote—kwamba mateso yote na kukata tamaa kwa mwanadamu vingeweza kuondoshwa, kama mwanadamu angefahamu asili ya hulka ya mwanadamu, chanzo cha uovu wa kila namna—na kuishinda?

KWA NINI ulimwengu uko katika vurugu ya kutisha kama ulivyo? KWA NINI mwanadamu aliahidiwa uzima wa milele, bado akaumbwa kwa mavumbi ya ardhi—wa kufa—awezaye kufa? KWA NINI—na kwa jinsi gani—anatofautiana na wanyama? KWA NINI yeye anaweza kufikiri na kuwaza—kutatua matatizo na kupata jawabu—ili hali wanyama hawawezi? KWA NINI mawazo ya mwanadamu yana uwezo zaidi kuliko ubongo wa mnyama yeyote? Tofauti kati yao ni nini hasa?

Endelea kusoma ili kupata MAJIBU DHAHIRI ambayo wanasayansi, wanateolojia, wanafalsafa na waelimishaji wameyakosa!

Sura ya Tatu – Kabla ya Historia na Kuumbwa kwa Mwanadamu

Ulimwengu umefika karne ya ishirini-na-moja. Mababu zangu wote walizaliwa katika karne ya kumi-na-tisa. Ndani ya kipindi hicho—miaka mia moja na kidogo tu—ulimwengu umebadilika kiasi cha kutotambulika. Mwanadamu sasa anasimama kwenye mstari wa [kizingiti cha] kujimaliza na silaha za maangamizi, huku tishio la ughaidi likienea duniani kote.

Hali za ulimwengu zinazidi kuwa za kuogofya zaidi huku habari za kila siku zikionekana kuwa mbaya zaidi kuliko za siku iliyopita. Matukio yanapiga mbio kuelekea mgogoro mkubwa mwishoni mwa zama hii.

Ilitokeaje mpaka maovu haya ya kuogofya na mateso ya kutisha yakaufikia ulimwengu mzima?

Na kwa nini viongozi wa ulimwengu wameshindwa kuimarisha nchi wanazozitawala na pia ulimwengu kwa ujumla? Tatizo ni nini?

Kwa nini maendeleo katika maarifa, sayansi na teknolojia havijamwokoa mwanadamu kutoka kwenye matatizo yake?

Kwa nini ustaarabu umesimama katika ukingo wa maangamivu—hata kutoweka—bila kuwa na namna ya kuingilia na kuuokoa?

Wengi wanajua kuna kitu hakiendi sawa—lakini hawajui ni kitu gani. Wanaodhaniwa kuwa wataalamu hawana majibu ya maswali makuu ya maisha. Wachache wanaelewa kuwa kuna kusudi kubwa ambalo Mungu anatekeleza hapa chini. Wachache zaidi wanaelewa kusudi hilo ni nini—na hawaelewi nguvu zinazotenda kazi ambazo zimeudhibiti ustaarabu tangu hapo mwanadamu alipoonekana duniani kwa mara ya kwanza.

Utekaji Nyara Mkubwa Kuliko Wowote

Wengi wanadhani kuwa mambo yako vile yalivyo kwa sababu mwanadamu aliibuka hadi kuifikia hali aliyopo sasa. Mtazamo huu umeingizwa kwenye elimu ya wakati huu lakini ni uongo—msimamo­—wa MAKOSA kabisa­. Uibukaji ni hadithi ya kubuni iliyotengenezwa na wanadamu walioongozwa kwenye nadharia hii na yule anayetafuta kuwapofusha wakazi wote wa dunia wasiuone mpango wa Mungu wa kustaajabisha—kusudi Lake la kuduwaza kwa ajili ya ubinadamu.

Wale wanaoshikilia nadharia ya uibukaji wamezuiwa—kwa hakika wamefungwa!—wasitambue kwa nini hali ya mambo iko vile ilivyo duniani. Na watawala wengi, viongozi na wabunifu wanajisikia kunaswa na mwelekeo na hali ya mambo, na mtiririko wa jumla wa matukio ya ulimwengu, wasiweze kufanya chochote juu yake. Kwa hakika wamenaswa. Lakini tunahitaji kuelewa ni kwa nini.

Huu sio ulimwengu wa Mungu. Umekatwa kutoka Kwake na umeshikiliwa mateka na MTEKAJI MKUU asiyeonekana. Wanadamu wote wamedanganywa katika kuamini maneno laini [ya kuchombeza] ya MTEKAJI huyu mkuu, wakifikiria wao wenyewe kwamba wana afadhali zaidi kuwa chini ya uangalizi na uongozi wake. Namwongelea Shetani ibilisi na utekaji mateka wake—miaka 6,000 iliyopita—wa Adamu na Hawa na wakazi wote wa sayari Dunia baada ya hapo! Tangu hapo ulimwengu umebaki kuwa mateka kwa kupenda.

Mtu yeyote anayesoma magazeti anaelewa utekaji mateka. Uhalifu huu huwakumba hasa viongozi wa juu wa makampuni makubwa, ambao kuachiliwa kwao ni kwa njia ya kulipa fidia.

Watekaji nyara nao hutenda kwa njia iyo hiyo, isipokuwa uhalifu huu kawaida huhusisha utekaji wa ndege, basi au aina nyingine ya gari likiwa limejaa wahanga.

Wengi wa wahanga wa utekaji hubaki wafungwa mpaka mtu fulani ama athubutu kuwaokoa au fidia ilipwe. Dunia sasa iko katika hali ya mateka, ikihitaji ukombozi usio wa kawaida—kuokoa—kwa kulipa fidia.

Hapa kuna mashaka ya mwanadamu wa leo: Fikiria mwenyewe ukikitwaa kitabu chenye sura ishirini na unajaribu kukielewa kwa kuanzia kusoma sura ya mwisho. Ungepotea, usiweze kabisa kuelewa maana ya wahusika na matukio yanayoelezewa. Kwa namna hiyo hiyo, hakuna watakaoweza kuelewa matukio katika ulimwengu wa sasa kwa sababu hawana msingi mathubuti kuhusu nini kilitokea katika sura za nyuma za uwepo wa mwanadamu duniani. Na ndiyo sura ya kwanza kabisa ya simulizi ya ubinadamu iliyo ufunguo kwa sura zote “kumi-na-tisa†zinazofuata.

Ulimwengu kabla ya Mwanadamu

Tunahitaji kuchunguza kipindi kabla ya historia, wakati kabla ya kuonekana kwa mwanadamu duniani, kuelewa jinsi Shetani alivyotokea kuwa kama alivyo.

Mwanzo 1:1 husema, “Hapo mwanzo Mungu aliziumba mbingu na nchi.†Andiko hili linaweka jukwaa la kujifunza kwetu.

Kitabu cha Ayubu kinaelezea vizuri zaidi wakati Mungu alipoiumba dunia, miaka mabilioni iliyopita. Mungu alimwuliza Ayubu mfululizo wa maswali: “Ulikuwa wapi nilipoiweka misingi ya nchi? Haya! Sema, kama ukiwa na ufahamu. Ni nani aliyeamrisha vipimo vyake, kama ukijua? Au ni nani aliyenyosha kamba juu yake?... Hapo nyota za asubuhi zilipoimba pamoja, Na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?†(38:4-5, 7).

“Nyota†hizi zilikuwa malaika (Ufu. 12:4), pia hueleza kama “wana wa Mungu.†(Bila shaka, nyota halisi haziimbi.) Angalia kwamba inasema “zote†kabisa “zilipiga kelele†na “kuimba pamoja.â€

Ayubu 38 ni andiko la kushangaza linalofunua kwamba mwanzoni mwa uumbaji wa vitu vinavyoonekana kulikuwa na amani, umoja na furaha. Lakini huu sio mwanzo hasa wa uumbaji wa Mungu—ni maelezo ya mwanzo wa uumbaji Wake wa vitu vinavyoonekana—wa vitu vyote vilivyotengenezwa kwa maada [mata].

Mwanzo halisi wa vitu vyote—mahali maelezo ya uumbaji wa Mungu unapoanza hasa—haupatikani katika kitabu cha Mwanzo 1, bali ni katika Agano Jipya, katika Yohana 1. Hapa ndipo Biblia imerekodi nani au nini kilikuwepo kabla ya uumbaji uliorekodiwa katika kitabu cha Mwanzo.

Hivi ndivyo Yohana anavyoandika juu ya wakati wa mwanzo kabisa ambao Biblia imeurekodi: “Hapo mwanzo kulikuwako Neno, naye Neno alikuwako kwa Mungu, naye Neno alikuwa Mungu. Huyo mwanzo alikuwako kwa Mungu. Vyote [“ulimwengu†– tafsiri ya Moffatt ya neno hilo hilo katika Waebrania 1:2] vilifanyika kwa Huyo; wala pasipo Yeye hakikufanyika CHO CHOTE kilichofanyika†(1:1-3). Hii inajumuisha kila kitu.

Lakini “Neno†ni nani? Yohana anajibu mafungu machache baadaye: “Naye Neno alifanyika mwili, akakaa kwetu; (nasi tukauona utukufu Wake, utukufu kama wa Mwana pekee atokaye kwa Baba); amejaa neema na kweli†(fu. 14). Mungu-Kiumbe pekee aliyefanyika mwili ili kukaa pamoja na watu ni Yesu. Hakuwahi kuwa mwili mpaka Alipokuja duniani kuwa Mwokozi wa wanadamu.

Katika Kigiriki asilia, mtajo “Neno†hakika humaanisha “Msemaji.†Kristo alifanyika Mwana wa Mungu pale tu alipozaliwa kama mwanadamu, Alikuwa Kiumbe wa milele—Alikuwa “hana baba, hana mama, hana ukoo, hana mwanzo wa siku zake, wala mwisho wa uhai wake†(Ebr. 7:3).

Kwa dhahiri, mafungu haya humwongelea Kristo kabla na baada ya kuzaliwa Kwake kama mwanadamu. Tena, ni Mungu-Kiumbe mmoja “aliyefanyika mwili na kukaa kwetu.†Lakini Yohana 1:1 hufunua zaidi! Angalia inasema kwamba Kristo, Neno, “alikuwa†Mungu na pia alikuwa “pamoja na†Mungu. Hii inawezekana tu kama Viumbe WAWILI tofauti wanaelezewa. Viumbe hawa WAWILI wa milele—Nafsi—walikuwepo kabla ulimwengu unaoonekana haujaumbwa. Walikuwepo tokea mwanzo na muda wote kabla ya hapo.

Waefeso 3:9 inathibitisha Yohana 1: “Mungu...aliyeviumba vitu vyote kwa Yesu Kristo.†Akiwa “Nenoâ€â€”Msemaji—kwa milele yote, kipindi chote cha huduma Yake, Kristo alisema mara nyingi kwamba Aliamuru tu kile ambacho Mungu alimtaka akiseme. Kwa kuwa Kristo alikuwa “Neno,†tunaweza kuelewa kwa nini Zaburi 33 inasema, “Kwa Neno la BWANA mbingu [ulimwengu] zilifanyika, Na jeshi lake lote kwa pumzi ya kinywa chake… Maana Yeye alisema, ikawa†(Fu. 6, 9).

Zaburi 33 imepanuliwa katika Wakolosai 1. Fungu la 12 huzungumza juu ya Baba na juu ya “Mwana…Wake†(fu. 13) “naye ni mfano wa Mungu asiyeonekana…Kwa kuwa katika Yeye [Kristo] vitu vyote [ulimwengu] viliumbwa, vilivyo mbinguni na vilivyo juu ya nchi, vinavyoonekana na visivyoonekana; ikiwa ni viti vya enzi, au usultani, au enzi, au mamlaka; vitu vyote viliumbwa kwa njia Yake, na kwa ajili Yake. Naye amekuwako kabla ya vitu vyote, na vitu vyote hushikana katika Yeye†(fu. 15-17).

Tumemaliza kutoa muhtasari wa ripoti ya Biblia kuhusu nafsi na hali ya mambo yaliyokuwepo kipindi chote kabla ya historia! Si malaika wala kitu chochote kinachoonekana kilikuwepo pamoja na Mungu. Ni hawa Viumbe wawili wa hali ya juu kabisa walikuwepo—PEKE YAO—kwa milele yote ya nyuma.

Viumbe hawa walikuwa Mungu, wakiwa na nguvu zisizo na kikomo za akili na uwezo wa kuumba. Hii ndiyo sababu Waliumba mwanadamu, muda mrefu baada ya kuumbwa kwa ulimwengu unaoonekana—aliye na akili yenye uwezo wa kuumba. Hii inaenda sawa na mtindo wa nguvu na uwezo wa kuumba wa Mungu mwenyewe.

Wanadamu wanaweza kusanifu, kuchora ramani na kujenga kitu chochote kile wanachochagua. Uwezo mkubwa wa kufikiria, kuwaza, kufanya maamuzi na kutekeleza malengo waliyojipangia huwatofautisha wanadamu na wanyama.

Kama Mungu asingetengeneza kitu kingine chochote, hebu fikiria tu jinsi gani NGUVU yao ilivyo ya kustaajabisha—kwamba waliweza kuumba akili ya mwanadamu, ikiwa na uwezekano unaoonekana kutokuwa na kikomo.

Lakini Ayubu 38 inafunua kwamba malaika waliumbwa kabla ya ulimwengu unaoonekana, ambao ulitangulia kuonekana kwa mwanadamu pengine kwa miaka mabilioni.

Malaika wameumbwa kwa roho. Ni viumbe halisi, lakini hawakutengenezwa kwa maada [mata]. Walipewa maisha ya milele toka muda walipoumbwa. Ingawa hawana nguvu kama Mungu, roho hawa walioumbwa wana nguvu nyingi zaidi kuliko wanadamu wa kawaida. Walikuwa kilele cha uumbaji wa Mungu kwa kipindi chote cha miaka mabilioni kabla ya historia.

Ulimwengu Wakati wa Kuumbwa kwa Mwanadamu

Sasa lazima tuchunguze kuumbwa kwa mwanadamu na nini Mungu alisema kuhusu “chombo†Chake kilipokuwa kimekamilika.

Mwanzo ni kitabu cha mianzo. Sura zake 50 zinaelezea kipindi cha zaidi ya miaka 2,000. Kwa hivyo, hakikuandikwa kuonyesha kila kitu. Badala yake, huwakilisha mtazamo kwenye matukio makuu yenye umuhimu zaidi katika historia ya mwanadamu. Juma la uumbaji na kipindi kilichofuata mara baada ya hapo vimeelezewa katika sura tatu za kwanza.

Mwanzo 1:1 inasema, “Hapo mwanzo Munguâ€â€”lakini Anayezungumza ni nani, akijiita Mwenyewe kuwa Mungu? Musa aliandika vitabu vitano vya kwanza vya Agano la Kale katika lugha ya Kiebrania. Tuliona kuwa neno la Kiebrania lililotafsiriwa “Mungu†ni Elohim, neno lenye maana sawa na timu, kundi, familia au kanisa. Mungu ni Familia moja—Mungu mmoja—yenye Wenye Uhai WAWILI.

Mungu na Kristo hufurahia umoja na makubaliano kamili. Wanaakisi upendo mkamilifu kwa wengine, kujali na kushirikiana. Baba ndiye kiongozi mkuu wa Familia ambayo wahusika wake wawili walichagua kuipanua. Kwanza, Mungu aliwaumba malaika na kisha ulimwengu wote, pamoja na dunia. Mwanadamu akafuata.

Kumbuka, Mungu alisema, “Na tufanye [zaidi ya mmoja] mtu kwa sura YETU, kwa mfano WETU†(Mwa. 1:26). Kama inavyoonekana, ni wazi walikuwepo zaidi ya nafsi moja zilizohusika katika uumbaji wa mwanadamu.

Fungu la 25 linaonyesha kwamba kila mnyama aliumbwa kwa “jinsi yake.†Angalia: “Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake; Mungu akaona ya kuwa ni vyema.â€

Fungu la 27 linaendelea, “Mungu akaumba mtu kwa mfano Wake, kwa mfano wa Mungu alimwumba, mwanamume na mwanamke aliwaumba.†Huu ni ufunguo wa kuelewa kwamba kusudi hasa la Mungu ni kuzaliana yeye Mwenyewe. Familia ya mwanadamu na kuzaliana kwa mwanadamu ni mfano wa mpango huu. Fungu la 28 huanza na kauli ya muhimu: “Na Mungu akawabariki, na Mungu akawaambia, Zaeni mkaongezeke, na kuijaza dunia.â€

Mafungu mawili yanayofuata hufafanua kwamba Mungu alikabidhi uumbaji Wake wote (wanyama, mimea, n.k.) kwa utawala wa mwanadamu—mamlaka juu ya vyote. Mwanzo 2:19 inaelezea jinsi Mungu alivyoleta wanyama wote kwa Adamu “kuona angewaitaje.â€

Maelezo ya Mwanzo 1 humalizia na fungu lenye umuhimu mkubwa la 31: “Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana.â€

Katika sura ya 2, Mungu aliwapa Adamu na Hawa uchaguzi ambao wangekabiliana nao (sura 3) kati ya Mti wa Uzima na “mti wa ujuzi wa mema na mabaya.†Katika uchaguzi huu, wangepewa fursa ya kuamua baina ya “hulka takatifu†ya Mungu (2 Pet. 1:4)—kujenga na kukuza tabia Yake—au kuchukua hulka ya Shetani ya dhambi.

Kama Adamu angekubali kwa hiari kutii maagizo ya Mungu, angeweza kufuzu kumwondoa Shetani na kurejesha Serikali ya Mungu duniani. Tutaona kwamba Shetani alikuwa ameasi na kuipindua serikali ya Mungu duniani.

Je Uweza wa Mungu Kuumba una Kikomo?

Tungeweza kuuliza, pamoja na uwezo Wake wa kuumba unaoonekana kutokuwa na mpaka, je kuna kitu chochote ambacho hata Mungu mwenyewe hawezi kuumba mara moja? Je Mungu ana mipaka yoyote? Je kuna kitu kimoja—cha aina yoyote—ambacho kiko nje ya uwezo Wake kukiumba papo hapo?

Ndiyo—kitu kimoja! Na ni cha MUHIMU-MNO.

Mungu hawezi kuumba, tabia kamilifu, takatifu, ya haki walionayo Baba na Yesu Kristo. Kabla ya kuendelea, pata ufahamu huu wa muhimu mno akilini mwako. Mungu hawezi kubandika tabia Yake katika usiku mmoja—kwa uweza wa kimungu. Na bado sifa hii ya muhimu kuliko zote lazima ipatikane ndani ya mtu ili Mungu afikie hatima ya kusudi Lake la kuumba.

Aina hii ya tabia ni uwezo wa kuchagua, kutenda na kuishi njia sahihi, hata dhidi ya mivuto na majaribu ya tamaa binafsi. Ni kujisalimisha kikamilifu, kwa kigezo cha uhuru wa maamuzi, kwa Mungu na njia Yake kamilifu ya maisha—kwa hiari bila shinikizo. Ni kujisalimisha kwa serikali ya Mungu na Sheria ya Mungu.

Sifa hii ya akili—TABIA—haiwezi kujengwa kwa usiku mmoja. Ni mchakato wa maisha yote. Tabia ni lazima ijengwe kwa njia ya uchaguzi mara kwa mara (kwa msaada wa Mungu) kuishi na kutenda kilicho sahihi. Mungu hawezi kupenyeza ndani ya mtu bila kufikiri. Hujengwa kupitia mitihani na majaribu ya kila aina. Watu wenye uhuru wa maamuzi lazima waendelee kujiachilia kwa Mungu na kuchagua kutenda haki, tena na tena, mpaka itakapokuwa sehemu ya TABIA yao halisi, ya ndani!

Umuhimu wa maarifa haya—ufahamu huu wa muhimu sana—hauwezi kusemwa kupita kiasi.

Malaika waliumbwa na uhuru wa maamuzi. Walipewa akili yenye uwezo wa kufanya uchaguzi, maamuzi. Walikuwa na uwezo wa kutafakari na kufikiri kutatua matatizo na kupanga utashi wao. Mungu alifunua njia Yake ya kweli ya maisha kwa viumbe hawa huru. Na aliwaruhusu kuchagua njia ambayo wangeifuata.

Yuda 6-7 inafunua kwamba Mungu aliwaweka malaika duniani kama “enzi yao…makao yao.†Kusudio Lake lilikuwa kwamba waitumie dunia kama uwanja wa majaribio—uwanja wa kuthibitisha—kujenga tabia.

Ulimwengu kabla ya Adamu ulijawa na viumbe wakubwa “kabla ya historia.†Huu ulikuwa wakati kabla ya historia, kama inavyomhusu mwanadamu. Watu waliumbwa baadaye, kipindi kile Shetani na mapepo wake walitawala dunia akiwa Lusifa na moja-ya-tatu ya malaika—hata wakati wa kubadilika kwao katika hulka.

Ni wazi, uwezekano uliokuwa wa malaika hapo kabla, sasa ni wa wanadamu.

Nini Kilibadilisha Kila Kitu?

Tuliona kwamba Ayubu 38 ilielezea jinsi dunia ilivyoumbwa katika hali nzuri ajabu, malaika wakifurahi sana na kuimba. Uumbaji wote kwa ujumla ulikuwa katika furaha kuu. Hii ina maana kwamba hapakuwepo na mapepo wakati wa uumbaji katika Mwanzo 1:1, ni malaika watakatifu tu. Sasa soma Mwanzo 1:2.

Fungu hili halikutafsiriwa kwa usahihi na halionyeshi maana ya Kiebrania asili. Biblia toleo la Mfalme James husomeka, “Nayo nchi ilikuwa ukiwa, tena utupu.†Maneno ya msingi matatu yote hayakutafsiriwa kwa usahihi hapa, hivyo kuzuia, na kwa hakika kuficha, maana halisi ya aya.

Neno lililotafsiriwa “ilikuwa†ni hayah. Katika Mwanzo 2:7, neno hili limetafsiriwa kwa usahihi “ikawa,†na katika Mwanzo 9:15, “…kuwa.â€

Maneno kwa ajilia ya “ukiwa, tena utupu†ni tohu na bohu. Yakitafsiriwa kwa usahihi, humaanisha “vurumai, katika mkanganyiko, ukiwa na utupu.†Kwa kifupi, dunia iliyoumbwa kamilifu (fu. 1), “ikawa vurumai na iliyokanganyikiwa†(fu. 2). Tohu na bohu yametafsiriwa kiusahihi katika Yeremia 4:23. Isaya 34:11, miongoni mwa sehemu zingine, inatafsiri usemi huu kama “mkanganyiko na utupu.â€

Angalia Isaya 45:18, inayobainisha namna ambavyo Mungu hakuiumba dunia: “Maana BWANA, aliyeziumba mbingu asema hivi, Yeye ni Mungu; ndiye aliyeiumba dunia na kuifanya; ndiye aliyeifanya imara; hakuiumba ukiwa [tohu kumaanisha vurumai au utupu], aliiumba ili ikaliwe.â€

Kutoka kwenye aya hii, ni wazi kwamba dunia ilikuja kuwa vurumai baada ya Mungu kuiumba—katikati ya matukio yaliyoelezewa katika Mwanzo 1:1 na 1:2. Kwa hivyo fungu la 2 linaelezea kuumbwa-Upya kwa dunia miaka 6,000 iliyopita, na fungu la 1 linaelezea uumbaji wa kwanza wa ulimwengu mzima ambao, kulingana na wanasayansi, ulitokea kiasi cha miaka bilioni 17 iliyopita.

Zaburi 104:30 inasema kwamba Mungu “aufanya upya uso wa nchi.†Zile siku saba za juma la uumbaji ni wakati ambapo Mungu aliikarabati upya dunia iliyokuwa imeharibiwa, kujeruhiwa, kugharikishwa na kisha akaifunika na maji kabisa (Mwa. 1:2). Lakini Matendo 3:19-21 inafunua kwamba ni Kurudi kwa Kristo pekee kutaleta “urejeshaji [kurejesha] wa vitu vyote.â€

Hivyo tunajua kile kilichotokea. Lakini kilitokea jinsi gani? Ni kwa jinsi gani uso wa sayari ulibadilika kutoka kuwa maridadi na kamilifu wakati wa kuumbwa hadi kuwa vurumai, uliokanganyikiwa, ukiwa na utupu? Kwa kuwa Mungu si Mungu wa machafuko (1 Kor. 14:33), tunajua kwamba Hakuiharibu dunia. Basi ni nani au nini kilisababisha hili?

Uasi wa Lusifa

Sasa, tupate historia kiasi. Shetani alitoka wapi? Jinsi gani alitokea kuwa vile alivyo?

Biblia inafunua hoja nyingi muhimu juu ya somo lolote kama mtu atasoma maandiko yote yanayohusiana nalo. Tukiwa na hili kichwani hebu tusome kuhusu Lusifa baada ya kuwa Shetani.

Isaya 14:12-15 inasimulia simulizi isiyo kifani iliyo na viashiria vingi kuhusu mahali alikowahi kuwepo Lusifa, alichofanya na kilichomtokea. Soma kwa makini, ukizingatia semi maalumu zilizotiliwa mkazo: “Jinsi ulivyoanguka kutoka mbinguni, Ewe Lusifa, mwana wa asubuhi! Jinsi ulivyokatwa kabisa hata nchi, Ewe uliyewaangusha mataifa! Nawe ulisema moyoni mwako, Nitapanda mpaka mbinguni, Nitakiinua kiti changu cha enzi juu kuliko nyota za Mungu; Nami nitaketi juu ya mlima wa mkutano, Katika pande za kaskazini. Nitapaa kupita vimo vya mawingu: Nitafanana na Yeye Aliye juu. Lakini utashushwa mpaka kuzimu [“kaburiniâ€â€”mafungu ya 9 na 11], Mpaka pande za mwisho za shimo.â€

Yule aliyeitwa “Lusifa†hawezi kuwa mwanadamu. Mambo aliyoyafanya hayawezi kutendwa na mwanadamu awaye yote. Ni ibilisi pekee anayeweza “kuyaangusha†mataifa yote, na kuweza kusema “angepanda mpaka mbinguni.†Kwa hakika hakuna mtu ambaye angeweza “kukatwa kabisa hata nchi†kwa jinsi ilivyoelezwa hapa. Mwisho, hakuna mtu aliye na kiti cha enzi ambacho kingeweza kuwekwa juu kuliko “nyota za mbinguni.â€

MUNGU anaishi katika upande wa kaskazini wa mbingu au “pande za kaskazini.†Ayubu anaangazia jaribio la Lusifa kutaka kumpindua Mungu mahali pale: “Yeye [Mungu] hutandaza kaskazi juu ya nafasi isiyo na kitu, Na kuutundika ulimwengu pasipo kitu†(26:7). “Nafasi isiyo na kitu†katika “kaskazi†huafikiana na kile ambacho wanajimu wamekiona kuwa ni sehemu isiyo ya kawaida yenye upungufu wa nyota katika eneo hilo la anga za juu. Inakuwa wazi kwamba Shetani alimvamia Mungu katika mwelekeo huo wakati alipotafuta kujiinua kutoka kwenye kiti chake cha enzi ili kukinyakua kiti cha enzi cha Mungu katika “pande za kaskazini.†Hiki ndicho Biblia inakifunua!

Shetani alikuwa amepata mafunzo pale pale katika makao makuu ya SERIKALI ya Mungu itawalayo ulimwengu. Alikua amefundishwa mambo ya msingi ya UTAWALA wa serikali ya Mungu duniani. Mungu alimteua kuwa, na humwita, “mfalme†juu ya huu utawala wa kidunia.

Ezekieli 28:12-17 huenda sambamba na hutilia mkazo Isaya 14, na ni muhimu ikasomwa pia. Kifungu hiki kinaelezea mmoja ambaye baadhi ya “wasomi†hudai alikuwa mwanadamu “mfalme wa Tiro.†Usomaji wa makini huonyesha hili haliwezekani—na ni upuzi.

Fungu hili huongelea juu ya mmoja ambaye “hutia muhuri kipimo, umejaa hekima, na ukamilifu wa uzuri,†ambaye pia “alikuwa ndani ya Edeni, bustani ya Mungu.†Hakuna mwanadamu aliyewahi kuwa mkamilifu, huyu alikuwa ni ibilisi—joka—aliyemdanganya Hawa pale bustanini. Fungu la 13 husema, “katika siku ya kuumbwa kwako,†na Shetani ni kiumbe aliyeumbwa. Fungu la 14 humwita “kerubi afunikaye.†(Kutoka 25:17-20 huelezea “makerubi wawili waaminifu waliobaki wa[lio]funika†kiti cha enzi cha Mungu katika hema ya Agano la Kale. Mabawa yao hufunika “kiti cha rehema.â€) Hakuna mfalme wa kidunia anayelingana na maelezo haya.

Sehemu ya mwisho ya Ezekieli 28:14 inasema kwamba “mfalme†huyu alikuwa “katika mlima wa Mungu†na “alitembea…kati ya mawe ya moto.†Hii huelezea eneo linalozunguka kiti cha enzi cha Mungu! Fungu la 15 hutamka, “uovu [uvunjaji wa sheria] ulipoonekana ndani yako†na fungu la 16 linaurejelea kama “dhambi.â€

Fungu la 16 pia linaelezea kerubi huyu kama aliyekuwa “ametolewa…nje ya†mbingu. Mungu pia alisema “angemwangamiza†(Kiebrania: fukuzia mbali) Lusifa kutoka mbinguni. Fungu la 17 hufunua kwamba “moyo wake uliinuka kwa sababu ya uzuri [wake]†na kwamba “hekima yake iliharibiwa… kwa sababu ya mwangaza [wake].†Fungu linamalizikia kwa Mungu “kumtupa chini hata nchi,†mahali ambapo wafalme wa dunia “wangemtazama.â€

Lusifa alikuwa kiumbe mwenye akili sana—“malaika wa nuru,†kama walivyo “watumishi wake†(2 Kor. 11:13-15). Jina Lusifa lina maana ya “mwenye kuleta nuru.†Kiumbe huyu aliyekuwa mkamilifu hapo awali alileta nuru ing’arayo kwa wote waliokuwa wakimzunguka. Lakini aliasi na kutenda dhambi—na hivyo kuwa “mkuu wa giza.†Uasi wake ukamgeuza kuwa kiumbe aliyepinda, aliyepotoka. Hali akiwa mwenye akili nyingi, kwa hakika amekuwa malaika kichaa aliyeanguka, asiyejua tena kutofautisha jema na baya!

Mwanzoni Mungu aliumba makerubi watatu: Lusifa (aliyegeuka kuwa Shetani), Mikaeli na Gabrieli. Kila mmoja alitawala theluthi ya mamia ya mamilioni ya malaika (Ufu. 5:11). Lusifa na theluthi yake walitawala ulimwengu uliokuwa kabla ya Adamu. Yeye, pamoja na malaika zake, waliasi serikali ya Mungu, na leo anawaongoza malaika hawa walioanguka, au mapepo, kama mungu wa dunia hii.

Alitupwa Duniani Pamoja na Malaika Zake Wote

Ufunuo 12 husema juu ya Shetani na pepo wake wabaya wakiwa “walitupwa katika nchi†(fu. 13). Kwa hakika, sura hii imepachikwa katikati ya kitabu cha Ufunuo, na ni muhtasari mfupi wa historia kamili ya Kanisa la Agano Jipya, ikiongelea matukio makubwa ya miaka 2,000 iliyopita.

Fungu la 3 pale linamwelezea Shetani kama “joka†aliye “kokota theluthi ya nyota za mbinguni na kuziangusha katika nchi†(fu. 4). Kumbuka kwamba “nyota†hizi zilikuwa ni theluthi ya malaika wote ambao waliokuwa chini ya Lusifa kabla hajaasi.

2 Petro 2:4 hutoa kiashiria kingine juu ya huku “kutupwa chini†kwa Shetani na malaika zake “aliowakokota pamoja†naye. Angalia: “Mungu hakuwaachilia malaika waliokosa [Shetani hakuwa malaika pekee aliyeasi], bali aliwatupa shimoni.†(Neno la Kigiriki hapa ni tartaros na linamaanisha aidha “gerezani†ama “kizuiziniâ€â€”hii ni dunia yenyewe.) Pepo hawa wabaya pamoja na Shetani “wanalindwa hata ije hukumu,†wakiisha “kutiwa…katika vifungo vya giza.†Hii inafunua kwamba Mungu aliwatia katika gereza hili la giza pepo wengine wengi walioanguka waungane na “mkuu wa giza.â€

Petro alirekodi kwamba “malaika…waliotenda dhambi.†Hii ina maana gani hasa? Kumbuka fasili ya Mungu ya dhambi. “Kwa kuwa dhambi ni uasi wa sharia†(1 Yohana 3:4). Walivunja Sheria ya Mungu kwa njia kadhaa.

Yuda 6-7 inaelezea uasi wao—dhambi yao—kwa njia hii: “Na malaika wasioilinda enzi

yao wenyewe, lakini wakayaacha makao yao yaliyowahusu, amewaweka katika vifungo vya milele chini ya giza kwa hukumu ya siku ile kuu. Kama vile Sodoma na Gomora na miji iliyokuwa kando-kando, waliofuata uasherati kwa jinsi moja na hawa, wakaenda kufuata mambo ya mwili yasiyo ya asili, imewekwa kuwa dalili, wakiadhibiwa katika moto wa milele.â€

Baada ya kutenda dhambi, hulka ya malaika ilibadilika. Tabia yao haikuwa kamilifu tena—ya haki. Wakawa wameanguka kiroho, na kujawa na mawazo na mtazamo mbaya, na wakapoteza sifa ya kuwa watawala wa kudumu katika Mpango wa Mungu. Mungu anawafananisha na miji ya Sodoma na Gomora iliyokengeuka, iliyoharibika sana kiasi kwamba Hakuwa na budi kuiangamiza. Wakazi wa miji hii hawakufaa tena kwa Mpango wa Mungu—wasiofuzu kwa ajili ya, na wakapoteza sifa ya nafasi zote za uongozi na mamlaka, waliharibika mno kiasi cha kutoruhusiwa kuendelea kuishi.

Ufunuo 12:7-9 inaeleza, kwa undani, lini Shetani na pepo wake wabaya watatupwa hata nchi kwa mara ya mwisho wasiweze tena kuingia mbinguni. Mafungu ya 12-14 yanaonyesha kwamba mwitikio wa ibilisi ni hasira kuu. Wakati huu wa kutisha unakuja kwa ulimwengu mzima! Lakini huku kutupwa chini kwa mara ya mwisho tena kusichanganywe na kile tulichokwisha kusoma.

Shetani alipuuzia hatari kwamba mitazamo isiyo sahihi inapoingia, baada ya muda, inaweka mizizi na kukua. Hatimaye husambaa na kujaza tabia ya yule anayeruhusu mitazamo hiyo kuingia. Kama muda wa kutosha utapita, mitazamo hii itaenea kwa watu wengine, mpaka tabia yao pia iwe imeharibika. Hali hii imeitwa kanuni ya “samaki mmoja akioza.†Kama samaki mmoja aliyeoza ndani ya chombo asipoondolewa, baada ya muda uozo utaenea na kuozesha samaki wengine.

Kitabu cha Ufunuo humtambulisha Shetani kama “mharabu.†Huharibu hatua kwa hatua, huozesha, huangamiza na hukengeusha kila kitu anachokigusa. Kwa upande mwingine, Mungu ni MUUMBAJI—MJENZI! Huunda, hukuza, hurejesha, hujenga na huboresha kila kitu anachokigusa. Hii kwa hakika ndiyo tofauti kubwa kati ya Mungu wa mbinguni na “mungu wa dunia hii†(2 Kor. 4:4).

Mmoja HUJENGA—mwingine HUHARIBU!

Kile Mungu Alichoona

Mungu aliona kwamba uumbaji Wake mkuu, Lusifa, alikuwa ameasi na kujikosesha sifa kama mtawala wa dunia. Ingawa alisikitishwa, Mungu hakushangazwa. Alielewa kikamilifu juu ya uwezekano wa uasi wa Lusifa kabla haujatokea. Alikuwa ameshapanga mbele, akitambua jambo hili lingemaanisha nini.

Sasa Mungu alitambua kuwa Yeye na Kristo ndio Viumbe pekee wasioweza na kamwe hawataweza tenda dhambi. Alikusudia, kwa njia ya Mwanawe, kupanua Familia Yake kwa kutengeneza tabia kamilifu katika wanadamu.

Lakini alijua kwamba Hata-anza kwa kumtengeneza mwanadamu mwenye umbo la roho—na asiyekufa—kama malaika. Alilazimika kuhakikisha kwamba hakutakuwa na viumbe wengine wasiokufa ambao watageuka, katika uasi, na kuwa wadanganyifu na waharabu.

Mpango Wake kwa ajili ya mwanadamu ungetilia maanani kwamba wale ambao watapewa fursa ya kujenga tabia Yake wangepewa uhuru wa kuchagua. Wangeweza kuasi na kutenda dhambi kama njia yao ya maisha waliyochagua. Mungu alielewa kuwa daima huu ungekuwa uwezekano kwa viumbe vyote vyenye uhuru wa maamuzi. Lakini kama wataasi, alilazimika kuondolea mbali uwezekano wa wao kuishi milele, kama Shetani na mapepo yake, katika hali ya maumivu na huzuni ya kudumu, wakiisambaza kwa wale walio karibu nao.

Mungu alilazimika kuyafikiria haya yote katika mpango wake wa kupanua Familia Yake ya kiungu zaidi ya Yeye na Neno—Kristo. Hangeweza kuwa na mmoja, kama memba wa familia Yake aliye na uweza halisi wa Mungu, aasi na kucharuka katika ulimwengu mzima. Hivyo akamtengeneza mwanadamu wa nyama—wa mavumbi ya ardhi. Alikusudia kutekeleza kusudi la kushangaza—la UWEZEKANO WA KUSTAAJABISHA!—ambao uko nje ya ufahamu wa akili za juu kabisa za kibinadamu kuweza kung’amua wao wenyewe!

Mpango wa Kuweka Mbadala wa Shetani

Shetani alidhihirisha kwamba hataweza kutawaliwa na Mungu. Kwa hivyo, mrithi wa kiti chake alipaswa kufuzu ili kuchukua mahali pake, wakati serikali ya Shetani ikiendelea kuwepo duniani. Mwovu bado alikuwepo ofisini—akibaki kuwa “mfalme wa uwezo wa anga†(Efe. 2:2) na “mungu wa ulimwengu huu†(2 Kor. 4:4).

Kwa hakika, Mungu alielewa kwamba Shetani, kama mdanganyifu (Ufu. 12:9), angefanya kila lililo katika uwezo wake kupinga kusudi la mpango mkubwa wa Mungu kwa kuharibu uumbaji Wake mpya—mwanadamu.

Kwa kuelewa kwamba mwanadamu angekuwa na uhuru wa kufanya maamuzi, Mungu alipaswa kupanga na kuamua, pamoja na “Neno,†kwamba huyu Kiumbe mwingine wapekee katika Uungu [Neno] lazima “afanyike mwili wa nyama†(Yohana 1:14) na kuja duniani. Kusudi la hili ni ili kuwa Mwokozi wa wote ambao wangetenda dhambi (Rum. 3:23) na ambao wangehitaji kukombolewa kutoka kwa adhabu ya mauti ya milele (Rum. 6:23).

Mungu alielewa kwamba Angeweza kumfufua Kristo kutoka kaburini baada ya Yeye kulipa adhabu ya kifo kwa ajili ya wanadamu wote. Hivi vilikuwa vipengele vya muhimu vya mpango ambavyo Mungu alivifikiria kwa undani sana. Tutaona kwamba sehemu ya Mpango Wake ilikuwa lazima kujumuisha kutia ndani ya mtu kiasi kidogo cha asili Yake mwenyewe, kwa njia ya kutungwa kwa Roho Yake Takatifu katika akili za wote ambao wangetubu na kugeukia njia Yake.

Roho Takatifu ya Mungu inayo na huakisi tabia kamilifu ambayo ni Yake na ya Kristo, na Mpango Wake wa ajabu ungemruhusu Mungu, ambaye ni Roho, kuweka kiasi kidogo cha tabia yake mwenyewe katika wanadamu, ambao wameumbwa kwa sura na mfano Wake katika mwili. Tutajifunza katika Sura ya Tano ni jinsi gani hasa Roho Takatifu huingia na kutenda kazi ndani ya akili ya mwanadamu.

Kile Alichokabiliana Nacho Kristo

Ni mara tu baada ya Kristo kubatizwa na Yohana Mbatizaji (Marko 1:9-11), Aliingia katika mapambano yasiyo ya kawaida, vita vya muda mrefu na Shetani.

Kuyapinga kwa mafanikio majaribu ya ibilisi ulikuwa ndio ufunguo wa Kristo kushinda dhambi na kufuzu kuchukua mahali pake na kumwondoa wakati wa kusimamishwa kwa ufalme wa Mungu. Mathayo 4 ina maelezo: “Kisha Yesu alipandishwa na Roho…ajaribiwe na Ibilisi†(fu. 1). Kwa njia ya kumtamanisha, mwovu alimtegea chambo Kristo, kwa njia mbalimbali. Chukua muda usome maelezo hayo. Mwishoni mwa majaribio kadhaa ya Shetani ili kuuvunja utashi wa Kristo, maelezo yanafikia kilele.

Angalia kwamba baada ya kuahidiwa kupewa falme zote za ulimwengu na Shetani, Kristo alimkemea (fu. 10) na akamwamuru aondoke. Jaribu likafika mwisho na ibilisi akaondoka. Kristo akawa amefanikiwa kumpinga—na kufuzu!

Shika hili. Yesu Kristo alifaulu jaribio halisi! Aliushinda ulimwengu, mwili Wake na ibilisi katika kushinda dhambi na kufuzu kulipa kwa ajili ya dhambi za ulimwengu.

Kusudi la Mungu Lazima Litimie Kabla Ufalme Wake Haujaweza Kufika

Ingawa Kristo alifaulu [fuzu] kumwondoa Shetani zaidi ya miaka 2,000 iliyopita, ziko sababu kadhaa za kukawia muda mrefu kuusimamisha ufalme wa Mungu.

Kwa kuwa Mpango wa Mungu unachukua miaka 7,000, na siku ya sita ndio inakaribia kumalizika, na ile ya saba-“siku†ya miaka elfu-moja ya Mpango wa Mungu sasa itafuata muda mfupi ujao, basi hivi karibuni Shetani atafungwa (Ufu. 20:2). Lakini hii haiwezi kutokea kabla miaka elfu sita ya kwanza haijakamilika.

Narudia tena, mwanadamu amepewa miaka 6,000 kujaribu njia zake mwenyewe, serikali, dini, falsafa, mifumo ya maadili, aina za elimu—na mbinu za kujaribu kutatua matatizo makubwa ya ulimwengu. Chini ya ushawishi wa Shetani, ametenda dhambi—uasi kwa amri za Mungu—kwa wakati huu wote. Kisha amejaribu kutibu athari mbaya badala ya kutibu chanzo—kuvunja sheria za kiroho za Mungu. Watu wanajifunza masomo magumu. Walio wengi, ambao kamwe hawajajua ukweli wa Mungu wa thamani, wanapaswa kujifunza kwamba suluhu zao hazifui dafu!

Akiisha kushinda dhambi, Kristo alifaulu kuchukua mahali (Math. 4:1-11; Luka 4:1-13) pa “mungu wa ulimwengu huu.†Alithibitisha kwamba hivi karibuni mwovu hataweza tena kudanganya (Ufu. 12:9) na kuwakanganya wanadamu (1 Kor. 14:33). Akiwa bado hajafungwa, Shetani anafanya kila kitu katika uwezo wake kuuzima Mpango wa Mungu. Watumishi wake waliodanganywa (2 Kor. 11:13-15) hufundisha, kwa hakika, kwamba Mungu ameshindwa kuuokoa ulimwengu. Lakini, ni ruhusa ya Mungu pekee inamfanya Shetani aendelee kuwa na ushawishi juu ya “ulimwengu mwovu wa leo†(Gal. 1:4; Yohana 5:19). Tambua kwamba Mungu hapotezi aina ya pambano kuu la“mchezo wa miereka†ambalo ana mamlaka kamili juu yake. Anaelewa barabara nini anakifanya, na uzuri wa mpango Wake unaweza kujulikana. Hakuna Mungu wa kweli anayeweza kuhukumu ubinadamu bila kutoa fursa ya wokovu kwa WOTE!

Ziko sababu nyingine kwa ajili ya kuchelewa Kurudi kwa Kristo. Kwanza alitakiwa kuwaita na kuwafunza wanafunzi wa awali wawe mitume—wawe msingi wa Kanisa (Efe. 2:20) na kuipeleka injili kwa ulimwengu. Kisha, katika kipindi chote cha Agano Jipya, Alihitaji kufunza baadhi ya wengine wa timu ya utawala watakaotawala pamoja Naye.

Kristo hakusimamisha ufalme Wake mara moja, kwa sababu ilimpasa kupaa mbinguni kuwa Kuhani Mkuu wa wale ambao Mungu anawaita. Wakristo wanapatanishwa na Mungu kwa kifo cha Kristo, lakini wanaokolewa kwa MAISHA Yake (Rum. 5:10)—Ufufuo Wake. Pia, akiwa bado mwanadamu, Kristo hangeweza kujitawaza Mwenyewe kama mbadala wa Shetani. Danieli alionyesha kwamba alipaswa kurudi mbinguni (pia Luka 19) kuvikwa TAJI na uwezo na utukufu kabla ya Yeye kurudi.

Ni Nini Kusudi la Mungu Kwa ajili ya Mwanadamu?

Watu wengi hawana wazo kabisa KWA NINI walizaliwa. Haya ni maarifa yanayofunuliwa kwa roho, yasiyofahamika kwa wale ambao Mungu hajawaita kuuelewa ukweli Wake (Yohana 6:44, 65).

Katika sura inayofuata, tutachunguza zaidi tofauti kati ya wanadamu na wanyama na kwamba Mungu anatenda kazi katika akili za wale Anaowaita kuliendea KUSUDI Lake LA KUSTAAJABISHA!

Sura ya Nne – Mpango wa Mungu Kwa Ajili ya Kupanua Familia Yake Takatifu

Fikiri kwa muda. Kipi chaweza kuwa cha muhimu zaidi kuelewa kuliko kusudi la maisha yako?

Wakanamungu hukataa kujua. Wale wasiokubali kwamba Mungu yuko kwa hakika hawawezi kukubali kwamba ana Mpango Mkuu.

Wabeuzi hudhihaki juu ya uwezekano wa kujua. Wanaona mkanganyiko na kutokukubaliana kwa kiasi kikubwa juu ya swali hili na kuhitimisha kwamba kamwe haliwezi kujibika.

Wanasayansi hawawezi kugundua maarifa haya kwa njia ya uchunguzi wa kimaabara. Wanajimu, wanamikrobiolojia na wengine walio wakweli hukubali kwamba Mungu yupo, lakini hiki pekee hakiwezi kufunua Mpango Wake kwa ajili ya mwanadamu.

Wanafalsafa hawawezi kuutambua kwa njia ya kutafakari au mijadala. Majibu yanayofunuliwa kwa namna ya Mungu hayawezi kupatikana kwa karne za kutafakari maswali.

Waelimishaji hawawezi kufundisha kile ambacho wao wenyewe kamwe hawakufundishwa. Wale ambao hufundisha kutoka kwa vitabu vilivyoandikwa na watu wengine hawawezi kufundisha kile ambacho hakimo ndani ya vitabu hivyo.

Wanajimu hung’ara kwa ujanja na hila ambazo hazifunui chochote cha thamani. Je, kuna yeyote anayefikiri kwa makini kwamba “wafanya biashara†kama hawa (wale wanaouza ubashiri kama ufahamu wa kweli), wakidhaniwa huwasiliana na “wafu†na “ulimwengu wa roho†(kwa hakika roho za mapepo), wanashikilia maana ya maisha?

Wanateolojia hutoa nadharia zilizobuniwa-kibinadamu na bandia. Dini zote hudai kuwa na majibu kwa maswali ya maisha, lakini mawazo yao hufifia kama vibadala rahisi—ubunifu feki tupu—wakati ukweli wa kustaajabisha wa Mpango wa Mungu unapoeleweka kikamilifu.

Watu wengi wanaishi maisha yao yote bila ya fununu kwamba kwa nini wako hapa. Wanaenda bila mwelekeo wowote, hawajali kuhusu majibu ya maswali makuu ya maisha—kwa nini maisha na kwa nini kifo? Wengine hufurahia kushiriki midahalo juu ya maana ya maisha, lakini kamwe hawafikii kwenye majibu sahihi. Wengine huhitimisha kwamba mwanadamu ni zaidi kidogo kupita uzao wa mageuko—upofu, bahati bubu!

Kilele cha Uumbaji wa Mungu

Ikiwa umesoma maandiko yangu mengi, unajua kwamba Biblia ni Kitabu cha Mungu cha kuwaadibisha wanadamu. Ndicho chanzo cha maarifa yaliyofunuliwa na ufahamu ambao mwanadamu hawezi kuugundua mwenyewe. Kinafafanua maswali muhimu zaidi ya maisha. Kina MAJIBU!

Kwa mara nyingine, Biblia inaanza na kitabu cha Mwanzo, maana yake “mianzo.†Chimbuko la kitu ni mwanzo wake—jinsi kilivyoanza. Kitabu cha Mwanzo hufafanua jinsi Mungu alivyoanzisha Mpango Wake kwa ajili ya mwanadamu.

Sura ya 1, fungu la 25 linafunua kwamba wanyama waliumbwa kwa njia tofauti na kwamba kila mmoja aliumbwa kwa “jinsi yake.†Angalia inasema kwamba, “Mungu akafanya mnyama wa mwitu kwa jinsi zake, na mnyama wa kufugwa kwa jinsi zake, na kila kitu kitambaacho juu ya nchi kwa jinsi yake...â€

Farasi wanafanana na farasi. Mbwa wanafanana na mbwa. Ng’ombe wanafanana na ng’ombe. Ndege wanafanana na ndege. Hakuna yeyote kati ya hawa—na hakuna kitu kingine chochote—kimefanywa na kutengenezwa katika sura na mfano wa Mungu. Ndivyo anavyosema Mungu, aliyevuvia maelezo haya katika Neno Lake!

Wanadamu siyo sehemu ya jinsi ya wanyama. Hawana mfano wa “mnyama wa nchi†awaye yote. Kama sehemu ya jinsi ya Mungu, mwanadamu aliumbwa ili kuingia katika uhusiano na Muumba wake ambao wanyama kamwe hawawezi kuufikia.

Ni muhimu mno kuelewa kitu kuhusu Mungu ni NANI na NINI. Mwanzo 1 inafunua maarifa ya muhimu sana. Kwa mara nyingine, Yule anayeongea pale alitumia wingi badala ya umoja. Kumbuka fungu la 26: “Na tufanye [zaidi ya mmoja] mtu kwa sura YETU, kwa mfano WETU.†Fungu hili l linarekodi juu ya FAMILIA ya Mungu ikiongea na kuumba. Mungu ni FAMILIA moja—kwa sasa inajumuisha Nafsi mbili.

Fundisho la kipagani la Utatu Mtakatifu hufundisha kwamba Mungu ni Nafsi tatu katika Kiumbe mmoja. Hii inaficha ule ukweli wa muhimu sana kwamba Elohim ni FAMILIA iliyo na Nafsi zaidi ya moja. Katika vigezo vya uhusiano wake na familia ya kibinadamu, umuhimu wa maarifa haya hauwezi kutiwa chumvi.

Kusudi Kuu Lafunuliwa!

Wanamageuko wamezuiwa—wakiwa wamenaswa kabisa—ndani ya mipaka ya nadharia yao. Hawaoni sababu yoyote kubwa ya kuzaliwa kwa mwanadamu kuliko kitoto cha mbwa au twiga. Ikiwa, kama wanavyosema, wanadamu ni daraja la juu tu la wanyama, na ni matokeo ya mageuko yasiyo na kichwa wala miguu, haiwezekani kwa wao hapo hapo waamini katika KUSUDI lililoamuriwa na Mungu lipitalo ufahamu kwa ajili ya maisha ya mwanadamu. Misimamo hii miwili inakinzana. Hakuna yeyote anayeweza kuikubali yote!

Ingawa mara nyingi mwanamageuko ana akili nyingi, utegemezi wake kwa ufahamu wa kibinadamu, ukiambatana na kukataa maarifa yaliyofunuliwa, humwacha akiwa hawezi kabisa kujua kusudi kuu la Mungu kwa ajili ya mwanadamu. Kwa hakika amejifungia mwenyewe nje ya ufahamu wa kweli!

Kitabu hiki kimeandikwa kwa ajili ya wale ambao watazingatia kile ambacho Mungu anafunua, sio kwa wale ambao hawaoni haja. Mungu ANAFUNUA kwamba mwanadamu ana kusudi la kustaajabisha ambalo liko nje kabisa ya fikra za mwandamu. Baada ya kusikia ufafanuzi wa Mungu, wewe utakuwa mwamuzi kama inaleta maana zaidi kuliko kile kitolewacho na wanamageuko na Ukristo wa kidesturi.

Aliumbwa Bila Kuwa Mkamilifu

Mtunga Zaburi aliandika “…kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha†(139:14). Lakini uliumbwa bila kuwa mkamilifu.

Mwanzo 1 imerekodi maelezo ya kuumbwa kwa mwanadamu KIMWILI. Adamu aliumbwa kiasi kwamba alifanana—alionekana kama—Mungu katika umbile la mwili na sura. Ingawa alikuwa mkamilifu kimwili, Adamu aliachwa akiwa hajakamilika katika roho. Kijenzi muhimu kabisa cha rohoni kilikuwa kinakosekana.

Angalia Mwanzo 2:7: “…Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.†Mtu amefanywa kutoka kwa maada [mata] inayoonekana—nyama. Wakati hajaundwa kwa Roho, kama Mungu, ametengenezwa—fanyizwa—katika “sura na mfano†wa Mungu.

Adamu alikuwa wa mwili. Alivuta na kutoa hewa, na alihitaji chakula na maji. Bila mojawapo ya hivi, hangeweza kuishi.

Ingawa Adamu alifanyizwa katika umbo na sura ya Mungu, kulikuwa na tofauti ya wazi—na kubwa—kati yake na Mungu. Adamu alifanyizwa kwa mavumbi. Alikuwa nyama (Mw. 2:7). Kwa kuwa Mungu ni Roho, Amefanyizwa—Tengenezwa—kwa Roho.

“Adamu†Wawili Hufunua Kusudi Kuu

Kuna uwiano mkubwa baina ya Adamu na Kristo, ambaye alikuwa Mungu wa Agano la Kale (Yohana 1:1, 14; 1 Kor. 10:4). Unatoa kiashiria kingine kwa kusudi la Mungu. Paulo anafanya ulinganifu huu kwa njia hii: “Ndivyo ilivyoandikwa, Mtu wa kwanza, Adamu, akawa nafsi iliyo hai; Adamu wa mwisho [Kristo] ni roho yenye kuhuisha. Lakini hautangulii ule wa roho, bali ule wa asili; baadaye [kwenye Ufufuo] huja ule wa roho. Mtu wa kwanza [Adamu] atoka katika nchi, ni wa udongo. Mtu wa pili [Kristo] atoka mbinguni. Kama alivyo yeye wa udongo, ndivyo walivyo walio wa udongo; na kama alivyo yeye wa mbinguni, ndivyo walivyo [kwa Ufufuo] walio wa mbinguni. Na kama tulivyoichukua [waongofu, wanaoongozwa na Roho] sura yake yule wa udongo [fanyizwa kwa nyama], kadhalika tutaichukua sura yake yeye aliye wa mbinguni [iliyofanyizwa kwa roho]†(1 Kor. 15:45-49).

Kauli ya Paulo iliyovuviwa huanza kwa kurejelea Mwanzo 2:7. Angalia usemi ulioko hapo “Ndivyo ilivyoandikwa…†Huu ni uthibitisho wa Agano Jipya kwa maelezo ya kitabu cha Mwanzo! Paulo alijua kwamba Adamu “aliumbwa†na Mungu, kwamba jambo hili lilitokea. Aliamini maelezo ya Agano la Kale.

Lengo la Mkristo ni kupokea mwili wa Roho katika Ufufuo—ili “kuchukua sura yake yeye aliye wa mbinguni.†Kama vile Mungu alivyoumba wanyama—tembo, mbwa, paka, farasi, n.k.—kuzaliana kwa jinsi zao, Yeye (Elohim) alimuumba mwanadamu kwa jinsi ya Mungu.

Elewa pointi hii. Mungu alikusudia kuanza uumbaji Wake wa kiroho na Adamu—na wanadamu. Mchakato huu haujawahi kamwe kuhusisha wanyama. Sasa lazima tuelewe kwa nini.

Akili ya Mwanadmu dhidi ya Silika ya Mnyama

Wanyama wana silika. Hakuna mwanamageuko aliyeweza kufafanua kwa mafanikio kwa nini hii iko hivi au jinsi gani hata inawezekana.

Kwa nini nyuki wanarudi kwenye mzinga wao siku baada ya siku, kizazi baada ya kizazi, wakitengeneza asali kwa njia ile ile waliyoitumia miaka 1,000 iliyopita, isipokuwa walisanifiwa kufanya hivyo?

Kwa nini ndege wanajua kuruka kuelekea kusini, tena katika muda mwafaka? Kisha, ni jinsi gani wengi wanajua kurudi kila mwaka kwenye mti ule ule katika Amerika ya Kati au Amerika ya Kusini—na kisha huruka kurudi kaskazini, ndani ya ratiba? Silika!

Kwa jinsi gani dubu wote “wanajua†kula chakula cha kutosha kuweza kustahimili ubumbwaaji kwa kipindi cha majira yote ya baridi kali—na ni kwa jinsi gani dubu wote hata hujua kubumbwaa, isipokuwa hali hii imejengwa katika tabia zao—kisilika?

Kwa nini wazaliwa wa ng’ombe na wa farasi husimama kitambo kidogo tu baada ya kuzaliwa? Ni kitu kilichopangiliwa ndani yao—kwa njia ya silika.

Kwa nini mbwa mwitu huwinda kwa njia ile ile—kwenye makundi—na hula vitu vile vile?

Kwa nini karibu kila ndege ana mtindo wake tofauti wa kutengeneza kiota?

Kuna wakati jaribio lilifanywa kwa ndege aina ya mnana. Vizazi vitano vilivyofuatana vilinyimwa vifaa vya kujengea viota. Kizazi cha tano kikapewa vifaa lakini kilikuwa hakijawahi kamwe kuona kiota. Papo hapo kiliendelea kutengeneza viota vilivyoonekana sawa kabisa kama viota vyote vya ndege mnana wengine.

Ingawa uwezo wa silika hii ni wa kushangaza kama ulivyo, hudumazwa na uwezo na nguvu za akili za mwanadamu. Wanadamu wana uwezo wa kupata maarifa. Wanaweza kufika mwezini na kuunda kompyuta zenye uwezo wa juu. Wanaweza kuchora ramani za nyumba zenye urefu wa viwanja sita vya mpira wa soka na kugundua siri za atomu. Wanyama hawana uwezo kama huo.

Watu hawapati kujua kisilika kila kitu wanachohitaji kukijua ili kuendesha maisha yao kwa mafanikio. Ni lazima wapate maarifa zaidi kadri wanavyoendelea kuwa watu wazima na kadri hali inavyowalazimu.

Maarifa yote huangukia katika makundi mawili: (1) maarifa ya asili juu ya jinsi ya kutenda kazi na maada [mata] na vitu vya asili, na (2) maarifa ya kiroho yaliyo-muhimu kwa watu kuendeleza uhusiano binafsi na Mungu na wanadamu wenzao. Maarifa yote ni ama ya asili au ya roho.

Maarifa ya asili hupatikana kwa njia ya milango mitano ya fahamu—kuona, kusikia, kunusa, kugusa na kuonja. Watu wanaelewa kwamba ni lazima WAPATE maarifa fulani na kuongezea mengine katika maisha yao yote. Milango ya fahamu huwawezesha kuendelea kuongeza zaidi maarifa ya asili.

Aliumbwa ili Apate Maarifa

Mungu aliwapa Adamu na Hawa “utawala†juu ya dunia (Mwa. 1:26). Hii ilimaanisha kwamba mwanadamu angeweza na angehitaji kujifunza na kutengeneza—kuzalisha—maarifa mengi kadri ambavyo angeitiisha sayari.

Mungu aliwasanifu wanadamu wenye akili ambazo zingeweza kuumba, kuunda, kufikiri, kuangalia kwa makini na kufanya majaribio. Kupitia uwezo huu wa asili katika kufikiri, maarifa ya asili yangeweza kufanyizwa. Jambo hili lilikuwa jema na sahihi, kadri ambavyo lingetumiwa ndani ya mfumo ambao Mungu aliukusudia.

Tatizo la Adamu na Hawa lilikuwa kufikiri kwamba kila aina ya maarifa muhimu kwa ajili ya wokovu wangeweza kuyapata wao wenyewe, kwa kufanya majaribio. Walipoenda-kombo tu kutoka kwa NJIA ya Mungu aliyoikusudia, hawakuwa na tumaini la kufikia kikomo cha safari ambacho alikuwa amekikusudia kwa ajili yao—na wala mwanadamu, aliyefuata uchaguzi wao. Tangu hapo Adamu na Hawa walipokubali upande wa makosa kama MAHALI PAO PA KUANZIA—kwamba wangeweza kufikiri kila kitu wao wenyewe—walikuwa wanaenda kushindwa!

Mkusanyiko wa maarifa mengi kwa miaka maelfu haujabadilisha, na kamwe hauwezi kubadili, ukweli kwamba mwanadamu anauendea mwisho mbaya.

Maarifa Yaliyofunuliwa

Kila aina ya kifaa cha kisasa au cha kitaalamu huja na kitabu cha maelezo ya namna ya kukitumia. Bila hiki, mmiliki angeona kwamba kifaa hakina matumizi yoyote. Hangeweza kujua namna ya kukitumia kwa usahihi. Wala hangeweza kukikarabati [ripea] au kukiweka katika hali nzuri wakati wote.

Hapo nyuma tulifafanua kwamba Mungu alitoa Kitabu cha Maadibisho—Biblia—ambacho kina maarifa nyeti YALIYOFUNULIWA, ambayo hayangeweza kufikiwa. Tofauti na mifumo ya kisasa ya elimu, kinafundisha jinsi ya kuishi, si tu jinsi ya kujipatia kipato [mapato]. Kinafafanua historia, unabii, maarifa muhimu ya maandiko na maelfu ya mambo mengine na kanuni zinazotawala kila nyanja ya maisha.

Sasa elewa. Biblia haikukusudiwa kubeba maarifa YOTE, ni yale tu yaliyo muhimu kwa ajili ya wokovu—maarifa ambayo mwanadamu hangeweza kuyagundua kwa akili za kibinadamu, ufanyaji wa majaribio, uchambuzi na kwa kuchunguza kwa macho. Biblia haikukusudiwa kumfundisha mwanadamu jinsi ya kusanifu maajabu ya uhandisi, darubini zinazoweza kuchunguza pembezoni mwa ulimwengu au kompyuta ambazo zinaweza kufanya trilioni za mahesabu kwa sekunde.

Wanadamu walipewa uwezo wa kufikiri na kusanifu haya na mavumbuzi mengine mengi ya kitaalamu ambayo ni vigumu kuyaeleza. Elimu katika maarifa ya asili ni muhimu.

Hii hapa ndiyo sababu. Idadi kubwa ya wakazi wa dunia wanaishi katika umaskini mkubwa, magonjwa, uchafu, udhalili na ujinga. Wamekosa elimu iliyo ya msingi kabisa ambayo mataifa “yenye mali†yaliyoendelea wanaifurahia. Kwa hivyo, elimu ya msingi inaweza kupelekea uboreshaji wa hali ya mambo na maendeleo kwa ajili ya ustaarabu.

Lakini kwa hakika miaka 6,000 ya taabu, majonzi na kila aina ya uovu, ubaya na huzuni ambavyo ubinadamu umepitia unatosha kuuambia ulimwengu kwamba unapaswa kusikiza kwa makini Kitabu cha Maadibisho ya maarifa ya roho yaliyofunuliwa ambacho ulimwengu umekipuuza. Bado, mwanadamu anaendelea kukataa UFUNUO WA ROHO kutoka kwa Mungu.

Hata hivyo, akiwa amekatwa kutoka mkondo na njia sahihi ya sheria ya sababu na athari inayoeleweka kwa namna ya roho na kutoka sheria ya Mungu iliyofunuliwa, mwanadamu bado ana nguvu za mwili, akili za kibinadamu, ambazo, kwa masikitiko, zimeelekea kwenye silaha za maangamizi na ughaidi, ukatili, utumwa, ukandamizaji, uchafuzi wa mazingira, jinai, mkanganyiko wa kidini, na mengine mengi zaidi.

Hivyo, taabu na huzuni za mwanadamu huzidi kuwa ngumu na kuongezeka kila kukicha.

Lakini kumbuka, mchakato wa Mungu wa UUMBAJI WA KIROHO bado unaendelea. Haujakamilika!

Zao la Kazi ya Mungu

Hebu tuendelee kuchunguza picha kubwa ya KUSUDI la Mungu.

Wewe si wa kwanza kushughulishwa na Mpango mzima wa Mungu—au kushangaa kwa nini unaishi. Ayubu aliuliza swali hili hili: “Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena?†(14:14).

Mungu alimvuvia kujibu swali lake mwenyewe: “Mimi nitangoja siku zote za muda wangu ulioamuliwa, Hata badiliko langu linifikilie. Wewe utaniita, nami nitakujibu; Utakuwa na tamaa kwa kazi ya mikono Yako†(fu. 14-15).

Ayubu alikiri kwamba alikuwa “KAZI ya mikono ya Mungu.†Alijua Mungu “alitamani†kusudi fulani ambalo lilihusisha mchakato unaotenda kazi ndani yake. Alielewa kwamba siku moja Mungu “angemwita†kutoka kaburini, na kwamba “angejibu,†hivyo kutimiza kusudi lake.

Haya ni maarifa ya muhimu ambayo yangeweza kufunuliwa na Mungu pekee. Bila hivyo Ayubu hangeweza kuyafahamu.

Mungu yuko kazini ndani ya wale ambao amewaita. Ana-unda, finyanga, na kujenga tabia Yake hasa ndani yao. Sasa angalia kile Isaya alirekodi: “Lakini sasa, Ee BWANA, Wewe u Baba yetu; sisi tu UDONGO, Nawe u MFINYANZI wetu; sisi sote tu KAZI YA MIKONO YAKO†(64:8).

Cha kuhuzunisha, wengi hawatamruhusu Mungu kutenda kazi nao. Wanapinga KUSUDI Lake. Wanafikiri wanaelewa vizuri zaidi kuliko Mungu Mwenyezi aliyewatengeneza. Wengi wanakataa kuambiwa nini cha kufanya na kuwa udongo katika mikono ya Mungu. Hili ndilo lilikuwa tatizo la Adamu.

Isaya pia aliandika, “Ole wake ashindanaye na Muumba wake! Kigae kimoja katika vigae vya dunia! Je! Udongo umwambie yeye aufinyangaye; Unafanya nini? Au KAZI Yako [Mungu], Hana mikono?†(45:9).

Watu wengi hawana habari kabisa kwamba Mungu anatenda kazi sasa ndani ya wanadamu Aliowaita—au nini anachokifanya anapowaita. Kwa mara nyingine, haya ni maarifa yanayofunuliwa kwa namna ya roho, yasiyoweza kufikiwa na wale ambao Mungu hajawaita kuelewa ukweli Wake (Yohana 6:44, 65; 17:17).

Mungu anatenda kazi sasa katika akili za wale wachache tu walio na Roho Yake Takatifu ndani yao (Matendo 2:38). Wanadamu hawazaliwi wakiwa na tabia ya Mungu. Na, tena, Mungu hawezi kuiweka mara moja ndani yao. Tabia ni lazima ikuzwe.

Mkristo wa kweli hukua katika ufahamu na “[kueni] katika neema, na katika kumjua [maarifa]†(2 Pet. 3:18). Maisha yake yote huvumilia ili kushinda, kwa sababu yuko mafunzoni kwa ajili ya kusudi kuu. Wale wanaoitwa huelewa kwamba “…mwenye KUVUMILIA hata mwisho, ndiye ATAKAYEOKOKA†(Math. 24:13).

Kujifunza Biblia na kuomba kwa bidii ni sehemu ya ratiba ya Mkristo ya kila siku. Yeye anayeitwa ameipata “lulu ya thamani kubwa†na amedhamiria kujenga TABIA YA KIROHO na HULKA ya Mungu. Japokuwa hakuna lolote kati ya haya litampatia wokovu, ni kiini cha tabia yake ambacho huamua thawabu yake.

Paulo alielewa jinsi Mungu anavyotenda kazi ndani ya Wakristo. Alitambua kwamba wokovu (Rum. 6:23), na hata imani ya kuupokea, ni karama za bure. Haviwezi kuchumwa. Lakini hii haina maana kwamba Mungu hatendi kazi sasa (akitaka matendo mema) ndani ya wanadamu, kadri ANAVYOZALIANA YEYE MWENYEWE.

Zingatia: “Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu. MAANA TU KAZI YAKE, tuliumbwa katika Kristo Yesu, tutende MATENDO MEMA, ambayo tokea awali Mungu aliyatengeneza ili TUENENDE NAYO†(Efe. 2:8-10).

Je, umeuelewa usemi ambao Paulo aliutumia—“tu kazi Yake� Kipi chaweza kuwa wazi? Mungu ana kusudi linalotenda kazi ndani ya kila mtu!

Fungu hilo liliendelea kwa kusema kwamba Wakristo lazima “waenende†katika “matendo memaâ€. Mtazamo wa uongo wa “amini tu katika Yesu†huvuruga Kusudi Kuu la Mungu la kuwatengeneza watu kupitia KAZI YAKE makini kama alivyo mfinyanzi na udongo.

Wokovu, ingawa ni kwa “neema…kwa njia ya imani,†hujumuisha matendo mema. Hii humaanisha kuwa wokovu ni mchakato na si kitu ambacho hutokea mara moja panapo “kuutoa moyo wako kwa Yesu.â€

Angalia kitu kingine alichoandika Paulo juu ya mchakato huu unaotokea ndani ya wale ambao Mungu anawaita: “na mfanywe wapya katika roho ya nia zenu; mkavae UTU MPYA, ulioumbwa kwa namna ya Mungu katika haki na utakatifu wa kweli†(Efe. 4:23-24). 2 Wakorintho 5:17 huliweka jambo hili namna hii: “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya…â€

Wale ambao Mungu anatenda kazi nao kwa hakika ni UUMBAJI MPYA!

Yule anayemtumikia Mungu anabadilishwa katika nia yake. Anasalimisha utashi wake na anatafuta kubadilishana na utashi wa Mungu katika mambo yote. Anatafuta kumpendeza Mungu—siyo nafsi yake mwenyewe!

Tumezaliwa ili Tujenge Tabia

Kila mtu ambaye Mungu anamwita hupewa uchaguzi ule ule ambao Adamu na Hawa walikabiliana nao—kujiachilia kwa Mungu na serikali Yake au kujiachilia kwa Shetani na hulka yake.

Mungu ni Baba. Anaye mtoto mmoja aliye-Roho, lakini baadaye atakuwa na wana wengine wengi zaidi (Rum. 8:19). Anazaliana mwenyewe kwa kujenga tabia Yake ndani ya wanadamu waliojiachilia, waliopondeka, waliotungwa-kwa Roho. Kama vile baba wa kibinadamu wanavyotunga watoto wao kimwili, kadhalika Mungu hutunga watoto Wake kwa namna ya roho.

Kama ilivyo kwa watoto kukua na kufanana na wazazi wao wa kimwili, kadhalika wana wa Mungu taratibu huchukua mfano wa Mzazi wao, katika tabia ya utakatifu, na ya haki—“tabia ya uungu†(2 Pet. 1:4). Petro aliwaelezea Wakristo kama “washirika wa TABIA YA UUNGUâ€â€”tabia ya Mungu. Iko tabia ya kimwili ya kuumbwa, tabia ya mwanadamu na HULKA ya MUNGU. Mungu anaitengeneza upya tabia ya mwanadamu iliyoharibika, ya mwilini hata ikawe ya ajabu, ya utukufu, kamilifu, takatifu, TABIA YA KIROHO—TABIA Yake ya UUNGU!

Tabia ni kuelewa—kujua—jema kati ya baya na KUTENDA lililo jema badala ya lililo baya! Mungu hufunua lililo jema, lakini ni kupitia nguvu ya uchaguzi huru, kuamua KUTENDA lililo jema, ndivyo tabia ya haki inavyojengwa.

Tabia ni kuchagua njia sahihi katika hali ya kujua, dhidi ya upinzani. Siyo njia rahisi. Ni kuogelea dhidi ya mkondo, badala ya kuserereka kizembe katika uelekeo wa mkondo unakotiririka. Ni kujenga upendo, furaha, amani, uvumilivu, ukarimu, utu wema, imani, upole, kiasi (kujizuia), hekima, maarifa, ufahamu, unyenyekevu na zaidi. Jambo hili huchukua muda, kwa sababu tabia hujengwa kupitia uzoefu.

Wanyama hawatengenezi tabia yoyote kati ya hizi.

Mungu ana tabia kamilifu katika nyanja zote. Yeye ni upendo (1 Yohana 4:8, 16). Pendo ni utimilifu wa sheria (Rum. 13:10; 1 Yohana 5:3), ambao unahitaji kujiachilia kwa Mungu. Ni kushirikiana, kuvutiwa kuwajali wengine, kuwafanya wa kwanza—mbele ya matakwa binafsi.

Hulka ya Shetani ni ubinafsi, kuangalia mambo yake na kujali tu lililo bora kwa nafsi yake mwenyewe na namna ya kupata zaidi kwa ajili yake mwenyewe. Hii ndiyo fikra aliyoipandikiza ndani ya Adamu na Hawa walipokula matunda ya mti waliokatazwa.

Je unaona kwamba, ingawa Mungu alimfanya mwanadamu kimwili katika umbo na sura Yake mwenyewe, haishii pale?

Uliumbwa ili UWE KAMA MUNGU—kujenga tabia kamilifu, takatifu, ya haki. Mungu anazaliana Mwenyewe ndani ya wanadamu. Kama vile wewe ulivyo mtoto wa wazazi, na huenda una watoto wako mwenyewe, Mungu ni Mzazi wako. Tena, kama vile unavyofanana na wazazi wako, na watoto wako wanafanana na wewe, Mungu anakutaka ufanane Naye—katika tabia ya rohoni! Katika maisha haya, Mungu huanza kuwatengeneza upya kiroho na kuwaunda upya wale Anaowaita. Kusudi Lake ni kujenga tabia Yake ndani yao.

Hivyo basi, Mungu anazaliana Mwenyewe ndani ya wale waliopokea Roho Yake Takatifu. Anaumba watoto ambao wataonekana na KUWA vile Yeye alivyo! Kujenga tabia ya Mungu hasa ndiyo sababu ya kuwepo kwako—ndiyo sababu ulizaliwa! Lakini yako mengi zaidi ya kufahamu.

Huko nyuma tumeeleza kwamba Mungu ametenga miaka 7,000—siku millenia saba—kukamilisha Mpango Wake “hapa chini.â€

Tumekaribia mwisho wa siku ya sita iliyofafanuliwa ambayo alitengewa mwanadamu chini ya Shetani. Kristo atarejea hivi karibuni kusimamisha serikali ya Mungu na sheria Yake kamilifu ya rohoni duniani. Shetani atafungwa (Ufu. 20:2) asiweze tena kuuzamisha ulimwengu huu kwenye uovu na uasi dhidi ya maarifa ya Mungu yaliyofunuliwa.

Baada ya Kristo kurudi, na Shetani kufungwa (Ufu. 20:2), ni wachache tu watakaomkataa Mungu, wasikubali kumtii. Watategemea akili za kibinadamu na kukataa kipengele cha Roho ya Mungu kinachokosekana, ambacho kingewaongoza kwenye uzima wa milele. Watakataa kujenga haki katika maisha yao na kuchagua kubaki haba—wasiokamilishwa—katika kujengeka na kusudi. Lakini mengi zaidi kuhusu wakati huu yatajadiliwa baadaye. Kwanza, lazima tuone kipengele kingine katika mchakato wa ujenzi wa tabia.

Lakini Haki ya Nani?

Ni muhimu mno—kwa hakika muhimu sana!—kuelewa kwamba Wakristo hukua kwa njia ya kuunganishwa kwa Kristo.

Mara nyingi Biblia huongelea juu ya “Kristo ndani yetu†(Gal. 2:20; 4:19; Kol. 1:27; Efe. 3:17; 2 Kor. 13:5). Mkristo hafanyi kazi za kujenga tabia. Yesu Kristo atendaye ndani yake huzifanya. Elewa. Baba huongoza mchakato huu kadri kila mtu anavyobaki na uhusiano Naye kwa njia ya Roho ya Kristo (na Mungu) ndani yake.

Weka jambo hili wazi. Hakuna kitu chochote ambacho unafanya, wewe na kwa juhudi zako mwenyewe, kinachozalisha matendo ya haki. Warumi 10 huwaonya wale wasioelewa jukumu la Mungu katika kujenga tabia, matendo mema na haki: “Kwa maana, wakiwa hawaijui haki ya MUNGU, na wakitaka kuithibitisha haki yao WENYEWE, hawakujitia chini ya haki ya Mungu†(fu. 3).

Ni kupoteza nguvu bure kujenga tabia yako mwenyewe, matendo yako mweyewe ya haki. Hayakupi chochote cha Mungu. Ukuaji wowote kiroho hutoka Kwake! Lakini unapaswa kufanya sehemu yako katika kujiachilia kwa Mungu.

Paulo aliandika, “Maana sisi tu wafanya kazi pamoja na Mungu; ninyi ni SHAMBA LA MUNGU, ni JENGO LA MUNGU†(1 Kor. 3:9). Huu ni ufahamu wa pekee. Mungu anajenga Familia. Yeye ni Mkulima. Wakristo wa kweli ni zao la “ukulima†Wake—“kazi†Yake.

MUNGU, anajenga Kanisa Lake, si mwanadamu yeyote. Kristo alisema, katika Mathayo 16:18, “nitalijenga kanisa Langu.†Si ajabu Paulo aliandika, “ninyi ni jengo la Mungu.†Ndiyo, Mungu anajenga kitu maalumu ndani ya wale anaowaita, vile vile kama anavyojenga Kanisa Lake kwa ujumla.

Bila shaka, kila jengo lililo imara lina msingi wa uhakika. Huu hulisaidia kubaki limesimama. Katika 1 Wakorintho 3:11, Paulo anaongeza, “Maana msingi mwingine hakuna mtu awezaye kuuweka, isipokuwa ni ule uliokwisha kuwekwa, yaani, Yesu Kristo.â€

Maisha yako lazima yaje kujengwa juu ya msingi imara wa KRISTO usiotingishika—na Yeye akitenda kazi ndani yako!

Ufufuo Unaokuja

Kama tulivyoona, wengi wanaojidai kuwa Wakristo wanaamini kwamba “wamezaliwa mara ya pili†katika maisha haya. Daima, wanaamini hili hutokea kufuatia “kumpokea Yesu.†Hiki sicho kile Biblia inachofundisha.

Tuliona kwamba Paulo alisema, “…nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika. Angalieni, nawaambia ninyi siri†(1 Kor. 15:50-51). Maarifa haya hakika ni siri kwa wengi.

Wakati nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu, roho inaweza! Kwa sababu Kristo hakutaka kuacha mwanya wa kutoelewa, alifananisha roho na upepo katika Yohana 3:3-8. Kama upepo, roho haionekani. Haiwezi kuonekana. Ni pale kwenye ufufuo ndipo Wakristo wote wa kweli wanabadilishwa kutoka nyama kuwa roho na KUZALIWA MARA YA PILI, kama tulivyoona!

Kile Utakachofanana Nacho

Kwa kuwa wanadamu wameumbwa kwa “sura†na “mfano†wa Mungu,†mchakato huu hautakamilika—na hauwezi—kukamilika mpaka Ufufuo, wakati ambapo hatutakuwa tena wa “nyama na damu.â€

Kisha Yohana anaongeza, “Kila mtu aliyezaliwa na Mungu hatendi dhambi, kwa sababu uzao wake wakaa ndani yake; wala hawezi kutenda dhambi kwa sababu amezaliwa kutokana na Mungu†(fu. 9). Siku moja tutakuwa na sura ile ile ya Kristo. Wakati huo, tutazaliwa kutokana na Mungu. Lakini Warumi 8:16 inasema kwamba sisi ni “watoto†wa Mungu sasa na warithi pamoja na Kristo sasa.

Kumbuka tuliona kwamba Daudi na Yohana walielewa kwamba, KAMA Ayubu, “wataamka†kwenye ufufuo na kuonekana vile vile kama alivyo Mungu, katika sura, umbo na tabia—na wakiwa wamefanyizwa kwa roho!

Hivyo basi—hebu nirudie tena hili—Mungu anazaliana Mwenyewe ndani ya wanadamu ambao wamepokea Roho Yake Takatifu. Anaumba watoto watakaoonekana na kuwa kama vile Yeye alivyo!

Paulo anakuza kile ambacho Yohana na Daudi walirejelea waliposema kwamba Wakristo watakuwa “kama Yeyeâ€â€”na katika “mfano†Wake. Angalia: “Kwa maana sisi, wenyeji [uraia] wetu uko mbinguni; kutoka huko [Kristo anakuja hapa, si kinyume chake] tena tunamtazamia Mwokozi, Bwana Yesu Kristo; atakayeubadili mwili wetu wa unyonge, upate KUFANANA NA MWILI WAKE WA UTUKUFU, kwa uweza ule ambao kwa huo Aweza hata kuvitiisha vitu vyote viwe chini Yake†(Fil. 3:20-21).

Haya ni maarifa ya kushangaza. Hakuna cha kulinganishwa nayo! Lakini hebu tuyaweke hata wazi zaidi.

Yafuatayo ni maelezo ya moja kwa moja ya Yesu Kristo, kama Alivyo sasa katika utukufu kamili. Yatafakari, ukitambua kwamba NAWE utaonekana—na kuwa—kama Yeye: “Kichwa Chake na nywele Zake zilikuwa nyeupe kama sufu nyeupe, kama theluji; na macho Yake kama mwali wa moto; na miguu Yake kama shaba iliyosuguliwa sana, kana kwamba imesafishwa katika tanuru; na sauti Yake kama sauti ya maji mengi. Naye alikuwa na nyota saba katika mkono Wake wa kuume; na upanga mkali, wenye makali kuwili, ukitoka katika kinywa Chake; na uso Wake kama jua liking'aa kwa nguvu zake (Ufu. 1:14-16).

Kitu hiki cha kushangaza kinachofunuliwa na maelezo haya kuhusu mstakabali wako siyo mawazo yangu binafsi. Ni kile ambacho Biblia yako inafunua! Hiki ndicho Paulo alichomaanisha aliposema, “Na kama tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua sura yake yeye aliye wa mbinguni†(1 Kor. 15:49). Ingawa tumeumbwa kimwili na tuko na sura ya Mungu sasa, baadaye tutakuwa Roho, na kuichukua “SURA yake yeye aliye wa MBINGUNI.â€

Kamata hiki. Roho ya Mungu iliyo ndani yetu itaturuhusu kuamka katika ufufuo. Angalia Warumi 8:11: “Lakini, ikiwa Roho Yake Yeye aliyemfufua Yesu katika wafu inakaa ndani yenu, Yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, KWA Roho Yake inayekaa ndani yenu†(pia 1 Kor. 15 na 1 Thes. 4:13-18). Kristo aliinuliwa (alifufuliwa) kurudi kwenye nafasi Yake kando ya Baba. Alikuwa amekamilisha jukumu Lake la kuwa Mwokozi.

Sasa, elewa pointi hii! Ni Roho ile ile, ikaayo ndani yetu tangu wakati wa kutungwa, itakayotufufua (wale wote waliotungwa na Mungu) kuungana na Mungu katika ufalme Wake.

Kama vile kitoto kipya-kilichotungwa kinavyokua ndani ya tumbo la mama yake, vivyo hivyo Mkristo lazima akue kikamilifu kabla hajatoka tumboni. Wakristo wanapaswa KUKUA katika kipindi cha maisha haya. Ili waweze kupewa nguvu za uungu na mamlaka baadaye, kama “warithi pamoja na Kristo†(Rum. 8:17), ni lazima wafuzu, kwa kujenga tabia ya Mungu iliyo takatifu, ya haki katika maisha yao sasa!

Wajibu wa Mateso

Mapema, kitabu hiki kiliongea juu ya mateso makali, huzuni na matatizo yasiyotatulika ya ulimwengu uliotengwa kutoka kwa Mungu. Hivi karibuni rehema Yake itafupisha hali hii, kuifikisha mwisho milele. Muda aliotengewa mwanadamu chini ya Shetani hivi karibuni utaisha, na wanadamu wote watafundishwa kwa nini walizaliwa.

Lakini kwa nini mateso makali kama haya yamekuwa ya lazima—na kwa muda mrefu? Yamesimamia kusudi gani katika Mpango Mkuu wa Mungu?

Kubwa! Tunasoma kwamba Kristo kama “Kiongozi mkuu wa wokovu wetu,†alifanywa “MKAMILIFU KWA NJIA YA MATESO.†Ni muhimu kuelewa kwa nini Kristo alitakiwa kuteseka.

Waebrania 5:8-9 inafafanua kwa wazi: “na, ingawa ni Mwana, ALIJIFUNZA KUTII kwa mateso hayo Yaliyompata; Naye alipokwisha kukamilishwa, Akawa sababu ya wokovu wa milele kwa watu wote wanaomtii.â€

Ni fungu lenye umuhimu mkubwa kiasi gani kulishika. Kuteseka huamsha utaratibu wa kujifunza kiroho ili utende kazi. Watu wanapoteseka—wanapokutana na maafa—WANAJIFUNZA (Mhu. 7:14)! Wanapata uzoefu—wanajifunza masomo ya muhimu. Jambo hili ni la muhimu sana katika mchakato wa kujenga tabia—kutimiza jukumu la kuwepo kwao!

Ingawa hakuwa na dhambi, hata Kristo alijifunza kupitia mateso. Hii ilimruhusu kuwa “Kiongozi mkuu†wa wokovu wa wana wengi ambao Mungu ataongeza katika Familia Yake.

Je, unaweza kuona sasa kwa nini ulimwengu lazima uteseke? Je sasa unaweza kuelewa vizuri zaidi kwamba ni kwa kupitia magumu, uzoefu wa maumivu ndipo hatimaye watu wataelewa masomo makubwa ya maisha? (Jambo hili litachunguzwa kwa undani zaidi katika Sura ya Sita.)

Bila shaka, somo kubwa zaidi kuliko yote ni kwamba wanadamu lazima watambue hawawezi kupata chochote—fanikisha CHOCHOTE!—bila Mungu. Wanahitaji mno MAARIFA YA KIROHO YALIYOFUNULIWA, ili kwamba wapate kuja katika mwafaka na Mpango mkuu wa Mungu wa kuzaliana Mwenyewe!

Paulo aliwaandikia Wafilipi kwamba yeye (Paulo) alitaka kumjua Kristo “… na ushirika wa MATESO YAKE,†ili kwamba “… nipate kwa njia yo yote kuifikia kiyama ya wafu†(3:10-11). Hii ndiyo sababu aliwaambia Waefeso, “… kuwaangaza watu wote wajue habari za madaraka ya siri hiyo [inayohusisha hitaji la kuteseka na kuvumilia magumu kwa lengo la kujifunza], ambayo tangu zamani zote ilisitirika katika Mungu aliyeviumba vitu vyote kwa Yesu Kristo; kwa kadiri ya KUSUDI la milele ALILOLIKUSUDIA katika Kristo Yesu Bwana wetu†(3:9, 11).

Mpango wa Mungu kwa hakika ni siri kwa ulimwengu huu. Lakini KUSUDI Lake halijabadilika tangu mwanzo wa ulimwengu.

Sasa unaelewa zaidi jinsi ambavyo UNAWEZA kuwa sehemu yake!

Sura ya Tano – Kijenzi Kisichoonekana Kinachowaunganisha Wanadamu Kwa Roho ya Kufanywa Wana

Sayansi ya sasa inaendelea kuuletea ustaarabu maarifa mapya. Kila ugunduzi [uvumbuzi] muhimu wa kisayansi—kila kipande kipya cha maarifa—hupokewa kwa msisimko na kusifiwa duniani kote.

Fikiri juu ya yale yote ambayo kwa sehemu kubwa sayansi imeupatia ubinadamu. Imewaweka watu mwezini na kuunda silaha za maangamizi. Imevunja kificho cha nasaba ya DNA na kuunganisha viumbe mbalimbali. Imejifunza mengi juu ya ukubwa na asili ya kushangaza ya ulimwengu—anga za juu—na kugundua vitu vya ajabu juu ya vipande vidogo vya kiatomu katika aina tofauti tofauti za atomu—anga za ndani. Imefanya ugunduzi [uvumbuzi] mwingi wa kitabibu na kufanikisha mambo ya kushangaza ya kihandisi.

Eneo na uwezekano wa sayansi huonekana kutokuwa na ukomo. Wengi wanaamini kwamba, kadri muda unavyokwenda, ugunduzi [uvumbuzi] wa kisayansi utatatua mengi au yote kati ya matatizo ya mwanadamu. Lakini sayansi ina mpaka katika njia moja muhimu sana inayohusiana na wewe. Kuna ugunduzi [uvumbuzi] ambao kamwe haitaufanya—na kamwe haiwezi—juu ya umbile la fikra za mwanadamu!

Fikra zako zina upana ambazo haziwezi kufahamika au kugunduliwa kwa mchakato au jaribio lolote linalofahamika kwenye sayansi. Dini za ulimwengu huu zimeukosa. Wanateolojia wake ama hawaufundishi wala kuutambua. Hawajatilia maanani kabisa kijenzi hiki cha upeo wa juu—UFUNGUO huu mmoja mkuu—kinachofungua tofauti kubwa sana kati ya wanadamu na wanyama. Ni kwa kufahamu UFUNGUO huu uliofunuliwa pekee ndipo unaweza kujifunza kusudi la kuwepo kwako!

Fikra za Mwanadamu za Kushangaza

Angalia kazi zote za kushangaza za asili—duniani na katika mbingu zote. Nelibini ya kazi ya mikono ya Mungu ambayo inaweza kuonekana na macho ya mwanadamu ni ya kuduwaza.

Fikiria sayari, nyota na galaksi. Kila moja ni ushangao wa aina yake. Kisha fikiria juu ya kila aina ya mimea inayopatikana juu ya dunia. Kuna mamilioni ya tofauti za rangi, umbile, ukubwa, utendaji na uzuri. Mng’ao wa sanifu zake mbalimbali na makusudi ni vya kushangaza! Sasa fikiria juu ya mamilioni ya aina tofauti za wanyama na wadudu. Ni za kushangaza na kusisimua kama ulivyo ulimwengu wa mimea, pamoja na tofauti za makusudi, mwonekano na tabia.

Lakini miongoni mwa uumbaji huu hakuna unaoshindana na uchangamano na uwezekano ambao karibu hauna ukomo wa fikra zako. Ingawa vitu vilivyoelezewa hapo juu ni vya kusisimua, kushangaza, vizuri, hakuna hata kimoja kinachoshangaza kuliko FIKRA ZA MWANADAMU. Hakika hiki ndicho kilele cha viumbe hai vyote. Hakuna kitu kingine katika uumbaji wa Mungu ambacho hata kinaweza kukaribia. Kitu gani kingine ambacho kinaweza kupanga, kufikiri au hata kuumba sehemu ndogo ya kiwango cha kufanana?

Hebu fikiria juu ya vitu vingi kiasi gani akili ya mwanadamu inaweza kusanifu na kutengeneza: Nyumba, simu, magari moshi, magari, ndege, maroketi, kompyuta, mashine nukushi na zana zingine zenye teknolojia ya juu ambavyo kiutendaji havina mpaka katika uchangamano na matumizi yake. Kitu pekee ambacho fikra za mwanadamu haiwezi kusanifu na kujenga ni YENYEWE!

Nani Alitengeneza Fikra Zako?

Mtunga Zaburi aliposema, “…kwa kuwa nimeumbwa Kwa jinsi ya ajabu ya kutisha†(139:14), hii ni kweli zaidi kuhusu ubongo wako—FIKRA ZA MWANADAMU!

Muumbaji wa fikra zako alituma pamoja nazo, habari muhimu, inayofafanua asili, usanifu na kusudi la uumbaji huu mkubwa kuliko uumbaji wote. Anatambulisha ufunguo uliofichwa—kipimo kinachokosekana!—kwa matumizi sahihi na stahiki ya fikra, unaoifungua njia ya amani, furaha, wingi na mafanikio kwa wote.

Lakini habari hii karibu imepuuzwa na watu wote, iliwasilishwa isivyo, isiyoeleweka na iliyokataliwa! Matokeo yake, matatizo, taabu na machungu ya ustaarabu yanaongezeka pasipo kuwa na suluhu inayoonekana na hali ikiendelea kuwa mbaya.

Simama na ufikiri! Tumia mantiki rahisi.

Je Mungu angeweza kuumba Uhandisi Wake wa kushangaza—fikra zako—na kuzipeleka bila Kitabu cha Kuadibisha kinachoeleza jinsi ya kuzitumia? Bila shaka hapana!

Ajabu Kitabu hiki kikubwa kimebaki kuwa siri kwa wengi sana—pamoja na wachache ambao hata hudai kukielewa. Wengi huishi maisha yao yote wakisumbuka juu ya kile ambacho WATU wanafikiri na kusema. Wachache hujishughulisha na kile MUNGU anafikiri na kusema. Kuwa mwaminifu na ujichunguze mwenyewe. Je unapata mitazamo yako kutokana na watu? Au unatafuta kwa mpangilio na kukubali Neno la Mungu lililo dhahiri kama mwongozo wa maisha yako?

Andiko lifuatalo linafafanua kwa nini hata fikra za upeo wa juu haziwezi kabisa kujifunza ufahamu fulani, isipokuwa uwe umefunuliwa kwazo. Angalia: “Wakati ule Yesu akajibu, akasema, Nakushukuru, Baba, Bwana wa mbingu na nchi, kwa kuwa mambo haya Uliwaficha wenye hekima na akili, ukawafunulia watoto WACHANGA†(Math. 11:25). Watu wa fikara nyingi sana wa ulimwengu hawawezi kutambua mambo ambayo Mungu aliyafunua katika Neno Lake! Kwa hakika YAMEFICHWA kutoka kwao.

Lazima tukubali kwa hiari kuchunguza Neno la Mungu kwa ajili ya kile Anachokifunua juu ya fikra zako. Namna ya kufikiri kwako itafunguliwa kwa ufahamu mpya wa kushangaza juu ya kwa nini ulizaliwa—na mustakabali na uwezekano wako wa kushangaza. Hata hivyo, lazima tuanzie mwanzoni.

Kijenzi Kisichokuwa cha Kimwili?

Wengi hudhani kwamba vijenzi vya fikra za mwanadamu ni vya kimwili tu. Je, hii ni kweli? Wengine wanaamini kuwa kila mtu ana nafsi isiyokufa. Je, hii ni kweli? Biblia inasemaje? Je, inakubaliana na hoja yoyote kati ya hizi? Au Neno la Mungu linafundisha jambo tofauti kabisa—jambo ambalo halitiliwi maanani na dini zote, na wala haliwezi kugunduliwa kwa mbinu zote za sayansi?

Kwanza, lazima tufikirie tofauti kati ya FIKRA za mwanadamu na UBONGO wa mnyama. Kuna hoja ambazo sayansi hutuambia juu ya sifa linganifu za hivi viwili. Wote wanaelewa kwamba kwa namna fulani ubongo wa mnyama unatofautiana kabisa na fikra za mwanadamu. Lakini kwa namna gani? Jinsi gani vinatofautiana?

Kwa mfano, baadhi ya viumbe kama sokwe na pomboo, wana ubongo ambao unakaribia kuwa sawa na wa wanadamu katika ukubwa na uzito. Baadhi ya wanyama wakubwa, kama nyangumi na tembo, wana ubongo mkubwa kuliko wa mwanadamu. Lakini akili zao ni ndogo, wana uwezo mdogo sana wa kuumba na hawawezi kuelewa wazo lolote gumu.

Sayansi haijaweza kufafanua—kueleza kwa ukamilifu—tofauti kubwa kati ya ubongo wa mwanadamu na ubongo wa wanyama. Ingawa mwanadamu ana ubongo ambao unaweza kuwa changamani zaidi kidogo kuliko wanyama wenye ubongo wenye ukubwa karibu sawa, tofauti katika uwezo ni kubwa sana. Kwa hakika hakuna ulinganifu.

Wanyama hutenda karibu mambo yote kwa SILIKA. Wanafanya chochote wanachotenda bila kufikiri, tena tangu kuzaliwa. Kwa mfano, karibu muda ule ule baada ya kuzaliwa, ndama anajua nini cha kufanya—jinsi ya kusimama na kutembea, na wapi pa kupata maziwa. Watoto wa wanadamu wanahitaji muda mrefu hata kusimama wima kwa msaada, na lazima wafundishwe kutenda karibu kila kitu.

Wakiwa na fikra, wanadamu wamepewa mikono ili kwamba waweze kutengeneza. Wakiwa na ubongo tu, wanyama hutenda kwa silika na wana nyayo, makucha na kwato. Hali hii huwafanya wasiweze kujenga kitu changamani kama luninga—achilia mbali eropleni aina ya jeti au roketi za kusafiria kwenda anga za mbali—hata kama fikra zingewaongoza. Wanyama pia hawawezi kupata maarifa zaidi ya uwezo mdogo wa kuitikia vichochezi fulani.

Wanadamu wana uwezo wa kupata maarifa, kufikia hitimisho, kukusanya na kuchambua hoja, kufanya maamuzi—na kujenga tabia. Hii ndiyo tafauti moja, kubwa kabisa, kati [baina] ya watu na wanyama.

Wanyama kwa kiwango kikubwa wana mpaka kwa sababu Mungu ameweka ndani yao kwa njia ya silika, kila kitu wanachohitaji kutenda kwa ufanisi katika mazingira yao.

Kwa upande mwingine, watu hawapati kujua kila kitu cha lazima ili kutenda kwa ufanisi katika maisha kwa silika. Ni lazima waendelee kupata maarifa zaidi katika maisha yao yote ili waweze kutatua changamoto mpya na matakwa yanayoelekezwa kwao.

Jambo hili linawezeshwa na kijenzi cha fikra, kisichoonekana, kisichofahamika. Asingekuwa na kijenzi hiki kisichoonekana, kisicho cha-kimwili, mwanadamu angekuwa tu mnyama mwingine bubu!

Roho Ndani ya Mtu

Hebu sasa tujenge fundisho la msingi la Biblia. Biblia imerekodi, “Lakini imo roho ndani ya mwanadamu, Na pumzi za Mwenyezi huwapa akili†(Ayubu 32:8). Hii ni kauli dhahiri. Hapa, Mungu anafunua kwamba watu wana aina ya roho, inayoitwa “roho ndani ya mtu.†Kuielewa kikamilifu roho hii kunahitaji uchunguzi wa maandiko mengine yanayaoielezea.

Lakini kabla ya kuangalia kwa ndani ukweli wa jambo hili—kabla ya kutafuta kuona nini Biblia inasema juu ya roho hii ya kibinadamu—ni lazima tuelewe na kukubali kile Biblia isichokisema.

Kufanya hivi, ni lazima tuchunguze imani potofu iliyo maarufu—jambo la KUBUNI!—linalofundishwa na kuaminiwa na mamilioni wasiohesabika juu ya somo hili.

Siyo Nafsi Isiyokufa

Wengi husoma fungu kama hili na kuhitimisha kwamba linazungumzia juu ya nafsi isiyokufa. Lakini ndivyo hivyo? Hivi usemi “roho ndani ya mtu†ni sawa na “nafsi isiyokufa†iliyojengwa kwa roho?

Watu wengi hawaelewi uhusiano kati ya watu wenye mwili na nafsi. Wanadhani kwamba wanadamu huzaliwa na nafsi isiyokufa. Imani maarufu ni kwamba, panapo kifo, nafsi za watenda dhambi huenda jehanamu milele na zile za wenye haki huenda mbinguni milele, kwa kuwa roho zote hudhaniwa kuwa hazifi. Je, hiki ndicho Biblia inafundisha?

Tuliona kwamba Warumi 6:23 inasema kwamba “mshahara wa dhambi ni mauti,†siyo maisha katika jahannamu. Je, Biblia kwa namna fulani pia inafundisha kwamba watu wana nafsi zisizokufa? Inasema juu ya “nafsi,†lakini kwa muktadha upi?

Biblia hakika inafundisha kwamba kuna mwunganisho kati ya watu na nafsi. Mwanzo 2:7 inasema, “BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu AKAWA nafsi hai.â€

Fungu hili halisemi kwamba watu wana nafsi, lakini wao ni nafsi. Adamu AKAWA nafsi—hakupewa nafsi. Kisha, karibu hapo hapo, Mungu alimwonya, “BWANA Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula, walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo UTAKUFA [si mwili wako tu] hakika†(fu. 16-17).

Yanapowekwa pamoja, mafungu haya matatu yanafunua kwamba watu ni nafsi na kwamba nafsi inaweza kufa!

Ezekieli anathibitisha maelezo ya kitabu cha Mwanzo. Mara mbili alivuviwa kuandika, “Nafsi itendayo dhambi, itakufa†(18:4, 20). Kifo ni kutokuwepo kwa uhai. Ni kukatishwa—kukoma—kwa maisha. Kifo si maisha katika eneo lingine. Si kuyahama “maisha haya†kuyaendea “maisha mengineâ€â€”“maisha yajayo.â€

Hatimaye, juu ya somo ama nafsi inaweza kufa, angalia hiki katika Mathayo 10:28: “Msiwaogope wauuao mwili, wasiweze kuiua nafsi; afadhali mwogopeni Yule [Mungu] awezaye kuangamiza mwili na nafsi pia katika jahannamu.â€

Biblia inasema kwamba nafsi zinaweza KUANGAMIZWA! Kulingana na fungu hili, zinaweza kuangamizwa vile vile kama miili inavyoweza. Wote tunatambua kwamba miili hatimaye hufa na kwamba, baada ya hapo, huoza na “huangamizwa†kabisa kwa sababu ya mchakato wa asili wa kuharibika. Fungu hili linafafanua kwamba Mungu hufanya uangamizaji wa nafsi KATIKA JAHANNAMU! Miili inaweza kufa kwa njia nyingi. Lakini nafsi huangamizwa katika jahannamu na Mungu. (Somo hili litachunguzwa kwa undani zaidi katika sura ya Kumi.)

Roho ya Mwanadamu

Sasa umejiandaa kugundua kitu ambacho karibu HAKUNA MTU anayekielewa. Ingawa mwanadamu amejengwa kwa nyama, ana kijenzi kisicho-mwili, roho ndani ya mtu, ambayo inaweza kujulikana tu kwa kile ambacho Mungu amefunua katika Neno Lake Takatifu.

Kwa sababu mtu amefanyizwa kwa maada ya mwili—nyama—Mungu, aliye wa Roho, alihitaji kuwa na njia ya Yeye (Roho) kuweza kutenda na kuwasiliana na mwanadamu (nyama). Baadaye, tutaelewa zaidi juu ya mwunganisho muhimu wa roho kati ya Mungu na wanadamu, na jinsi unavyotenda kazi hasa.

Angalia hii: “Ufunuo wa neno la Bwana juu ya Israeli. Haya ndiyo asemayo BWANA, azitandaye mbingu, auwekaye msingi wa dunia, aiumbaye roho ya mwanadamu ndani yake†(Zak. 12:1). Ni Mungu anayeumba, anayesanifu na “anaunda†roho ya mtu ndani ya kila mwanadamu.

Fungu lifuatalo hufafanua kwamba watu wote wana roho hii: “Bwana, Mungu wa roho za wenye mwili wote, na aweke mtu juu ya mkutano†(Hes. 27:16). Yeye Anayeumba roho zote ndani ya watu Anajiita Mwenyewe Mungu wa roho hizi.

Viumbe vyote vyenye mwili hatimaye hufa. Hii inatokea kwa watu na wanyama. Zingatia. “Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo pumzi moja; wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama; kwa maana yote ni ubatili. Wote huendea mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini hurudi tena. Ni nani ajuaye kama roho ya binadamu huenda juu, na kama roho ya mnyama huenda chini?†(Mhu. 3:10-21).

Sulemani hasemi kwamba kuna roho ndani ya wanyama, badala yake anauliza swali lisilohitaji jibu, “Ni nani ajuaye… roho ya mnyama huenda chini…?†Mafungu mengi yanafunua kwamba kuna roho ndani ya wanadamu, lakini wanadamu hawajui juu ya ukweli huu na ule kama wanyama pia wana aina ya “nafsi†au roho. Fungu hili linaonyesha kwamba hapa haiongelei juu ya pumuzi tu, ni kitu tofauti dhahiri. Lakini wanyama hawana roho kama hiyo.

Maarifa ya Kustaajabisha

Sasa hebu angalia fungu hili la kustaajabisha. Paulo katika Agano Jipya aliandika, “Maana ni nani katika binadamu ayajuaye mambo ya binadamu ila roho ya binadamu iliyo ndani yake? Vivyo hivyo na mambo ya Mungu hakuna ayafahamuye ila Roho ya Mungu†(1 Kor. 2:11).

Usijaribu “kufasiri†fungu hili. Liache lijifasiri lenyewe. Likubali kwa kile linachosema. Aya hii inatambulisha aina MBILI tofauti za roho—“Roho ya Mungu†na “roho ya mwanadamu.†Hizi siyo kitu kimoja. Kila moja hutimiza jukumu tofauti katika upataji maarifa, na fungu hili linatambulisha ni jinsi gani.

Maarifa ya mwanadamu (“mambo ya mwanadamuâ€) hupatikana kwa sababu Mungu amewapa wanadamu roho—roho ndani ya mtu. Kauli ya Paulo iliyovuviwa pia huweka wazi kwamba maarifa (“mambo ya Munguâ€) yanaweza kupatikana tu kwa kuwepo kwa Roho ya Mungu. Hata maarifa haya haya—kwamba roho mbili hizi zipo na jinsi zinavyotenda kazi—yenyewe tu hakika inashangaza! Lifikirie hili kwa namna hii. Kwa hakika hakuna mtu mwenye maarifa juu ya JINSI ambavyo MAARIFA yawe ya kimwili au ya kiroho yanavyopatikana!

Kumbuka kauli dhahiri, “Lakini imo roho ndani ya mwanadamu, Na pumzi za Mwenyezi huwapa akili.†Hii hurudia hasa kile ambacho Paulo alikisema. Anaitambulisha roho hii, huku akitofautisha ufahamu wa kiroho (au maarifa) kama kitu ambacho kinatoka kwa Mungu—“Mwenyeziâ€â€”kwa njia ya “uvuvio†Wake. Jambo hili hutokea kwa njia ya uwepo wa Roho ya Mungu katika fikra zilizoongoka.

Wanyama hawana roho iliyo ndani ya mwanadamu. Ubongo wa mnyama uko tofauti na fikra za mwanadamu. Wanadamu wanapewa roho hii toka kutungwa mimba, ikiwawezesha, kupata na kuhifadhi maarifa kwa kutumia milango mitano ya fahamu. Kumbuka, bila kuwepo kijenzi hiki cha roho kisichoonekana, mwanadamu angekuwa tu mnyama mwingine bubu. Lakini amepewa nguvu ya kupata, kuhifadhi na kutumia maarifa kwa makusudi ya aina zote.

Wanadamu wote waliumbwa na Mungu kupokea aina mbili tofauti za roho. Moja inayokuja wakati wa kutungwa mimba, na nyingine inakuja kwa njia tofauti kabisa—kutubu na kubatizwa. Bila kuwa na Roho ya Mungu, watu kwa urahisi tu hawako kamili. Uwepo wao hubakia tu kwa kile ambacho wanaweza kupata wao wenyewe bila msaada wa Mungu. Hivyo, kiasi kikubwa cha maarifa ya kiroho hubaki bila kufikiwa. Ingawa uwezo wa mwanadamu kupata maarifa ya kimwili ni ng’ambo ya ule wa mnyama, wanadamu hawawezi kuufikia ufahamu huu mwingine wa ajabu.

Hebu tujifunze zaidi juu ya jinsi Roho ya Mungu inavyotenda kazi na roho ya mwanadamu katika fikra zilizoongoka. Mithali 20:27 hutoa ufahamu wa muhimu: “Pumzi [Roho] ya mwanadamu ni taa ya BWANA; Hupeleleza yote yaliyomo ndani yake.†Lifikirie fungu hili katika njia ifuatayo: Mungu anaweza kutenda kazi ndani ya ubongo wa kimwili—kuwasiliana na kuuvuvia—kwa njia ya, au kwa kutumia, kijenzi kisicho cha ki-mwili cha roho iliyo ndani ya mwanadamu.

Mungu Huwasiliana Kupitia Roho ya Mwanadamu

Zingatia mfano mmoja wa jinsi Mungu anavyotenda kazi kupitia roho ya mwanadamu. Hueleza kanuni ya muhimu. Mpangilio unahusisha Mfalme Koreshi wa Uajemi. Mungu alimtaka arudi Yerusalemu na kujenga hekalu la pili kuchukua mahali pa hekalu la Sulemani, ambalo lilikuwa limeharibiwa. Angalia: “Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la BWANA alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, BWANA akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia†(Ezra 1:1).

Mungu aliwasiliana na Koreshi kupitia (“kuiamushaâ€) roho yake. Hufanya vivyo hivyo leo. Sasa chunguza andiko lifuatalo. Linaongeza mtazamo mpya kwenye fungu tulilokwisha kulisoma kuhusu roho iliyo ndani ya mwanadamu na jinsi inavyotenda kazi.

Roho ya Mungu Hutenda Kazi pamoja na Roho ya Mwanadamu

Katika fikra zilizoongoka, Roho ya Mungu na roho iliyo ndani ya mwanadamu hukaa.

Zinatenda kazi pamoja, kila moja na nyingine [kwa umoja]: “Roho yenyewe hushuhudia PAMOJA NA roho zetu, ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu†(Rum. 8:16).

Kwa kweli huu ni ufahamu wa kushangaza. Mtu aliyeongoka ni tofauti na wanyama katika njia MBILI tofauti.

Lakini kwanza tambua kwamba sayansi kamwe haikuweza kujifunza kile ambacho umemaliza kukisoma!

Sasa zingatia pointi ya nyongeza. Kutoka muda ule hapo tu unapoongoka, umekwisha-nunuliwa kwa damu ya Kristo, Mungu anaimiliki roho yako: “maana mlinunuliwa kwa thamani. Sasa basi, mtukuzeni Mungu katika mwili wenu, na katika roho yenu ambavyo ni vya Mungu†(1 Kor. 6:20). Mungu ana umiliki halisi wa roho yako—na panapo uongofu inakuwa ya Kwake ili kutenda kazi nayo.

Ni muhimu kuuelewa mchakato wa kujenga tabia unaoendelea ndani ya fikra zilizoongoka na jinsi unavyohusisha roho ya mwanadamu. Angalia: “Asiye mwepesi wa hasira ni mwema kuliko shujaa; Na mtu aitawalaye roho yake kuliko mtu atekaye mji†(Mith. 16:32).

Kujizuia—kiasi—limeorodheshwa kama tunda la Roho ya Mungu katika Wagalatia 5:23. Chukua muda ulisome. Yanapowekwa pamoja, mafungu haya yanaonyesha kwamba ni kupitia Roho ya Mungu pekee ikitenda kazi pamoja na roho iliyo ndani ya mwanadamu ndipo kiasi kinaweza kujengwa!

Mungu Huhifadhi Roho Iliyo Ndani ya Mwanadamu

Mwishoni mwa maisha ya mtu aliyeongoka, Mungu hurudisha roho ya mwanadamu kwake Mwenyewe. Ndani yake, Amehifadhi kumbukumbu kamili, kwa undani ya kila kitu kinachohusu maisha ya mtu huyo. Hii ni kauli wazi ya maandiko. Angalia: “Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo†(1 The. 5:23).

Roho, nafsi na mwili huwakilisha vyote ambavyo alikuwa mtu. Ubinadamu, uzoefu, maarifa yaliyokusanywa na tabia ya kila mwanadamu inaakisiwa ndani ya roho ya mwanadamu—roho iliyo ndani ya mwanadamu.

Hii ndiyo sababu roho iliyo ndani ya mwanadamu humrudia Mungu panapo kifo: “Nayo mavumbi kuirudia nchi kama yalivyokuwa, Nayo roho kumrudia Mungu aliyeitoa†(Mhu. 12:7). Hivyo basi, kwenye kifo, roho ya mwanadamu humrudia Mungu, aliyeiunda na kuiweka katika fikra.

Kumbuka Mhubiri 3:21: “Ni nani ajuaye kama roho ya binadamu huenda juu, na kama roho ya mnyama huenda chini?†Sasa unajua kile ambacho wachache wengine wanajua—kwamba roho iliyo ndani ya mwanadamu hakika hurudi kwa Mungu.

Shemasi Stefano alielewa. Wakati alipokuwa akipigwa mawe hadi kifo kwa sababu ya kutoa hubiri kali lililowachongea wasikilizaji wake, Biblia inaandika, “Wakampiga kwa mawe Stefano, naye akiomba, akisema, Bwana Yesu, pokea roho yangu. Akapiga magoti, akalia kwa sauti kuu, Bwana, usiwahesabie dhambi hii. Akiisha kusema haya akalala†(Matendo 7:59-60). Hiyo ni sahihi! Stefano alikufa (“alilalaâ€) akijua kwamba Mungu angeipokea roho yake na itaungana naye, tutajifunza, kwenye ufufuo.

Sasa tuko tayari kwa ajili ya andiko la mwisho kabla ya kuendelea. Ni jiwe la pembeni ambalo linafafanua “uhifadhi†wa roho zote za wanadamu na mahali halisi Mungu anapoziweka. Elewa hili: “Bali ninyi mmeufikilia mlima Sayuni, na mji wa Mungu aliye hai, Yerusalemu wa mbinguni, na majeshi ya malaika elfu nyingi, mkutano mkuu na kanisa la wazaliwa wa kwanza walioandikwa mbinguni, na Mungu mwamuzi wa watu wote, na roho za watu wenye haki waliokamilika†(Ebr. 12:22-23). Hii ni aya ya ajabu. Mungu wa “roho zote†(na wa “watu wenye haki waliokamilikaâ€) huziweka pamoja Naye, mpaka ufufuo.

Ni mbinguni—Yerusalemu wa mbinguni—mahali ambapo roho za watakatifu wote wa Mungu tangu Uumbaji zimewekwa—zimehifadhiwa kamili—zikisubiri “kuja kwa Bwana wetu Yesu Kristo†(1 Thes. 5:23).

Roho ya Shetani ya Uasi

Kabla ya kuendelea, tunahitaji angalau kidogo kutaja aina nyingine ya roho. Paulo aliliandikia Kanisa la Waefeso kuhusu nguvu ya ibilisi na ushawishi wake kwa ulimwengu: “ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa UWEZO wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi†(2:2).

Kando na Roho ya Mungu na roho iliyo ndani ya mwanadamu, inapasa ieleweke kwamba ibilisi ni roho. Yeye ni sehemu ya milki ya roho za malaika, ikijumuisha malaika waaminifu na mashetani (malaika walioanguka).

Angalia kwamba fungu la 2 linasema “ROHO ya Shetani…hutenda kazi ndani ya wana wa kuasi.†Ibilisi ni roho na ana UWEZO, kupitia roho yake, kuwashawishi wanadamu kuelekea uasi! Katika Sura ya Tisa, tutajifunza kwa undani zaidi jinsi Shetani, kupitia roho yake, hutuma hali za kukasirika, hisia na mitazamo ya kikatili katika fikra za watu, vikileta uasi. Ibilisi ana nguvu nyingi za USHAWISHI, zikimwezesha kupeleka mawazo ya udanganyifu, hasira, kiburi, chuki, tamaa, wivu, uchungu na mengine, moja kwa moja katika mawazo ya watu!

Shetani, kama mungu wa ulimwengu huu, amewapotosha walio wengi wa wanaodhaniwa kuwa Wakristo hata kukataa kusudi kubwa la Mungu, linalohusisha utii Kwake—ili kwamba waweze kumfuata Kristo wa uongo asiye na masharti, anayeabudiwa kwa wingi sana na kuaminiwa leo, kwenye wokovu wa uongo.

Picha Kubwa

Hebu sasa tuiangalie picha kubwa. Kwa kuwa sasa tunaelewa zaidi kuhusu roho ya mwanadamu, lazima tuendelee kuchunguza mpango mzima wa Mungu kwa ufupi. Lazima tuangalie zaidi kile Anachokifanya na ubinadamu.

Kumbuka, wanadamu wana uwezo wa kupata maarifa. Wanyama hawana uwezo huu. Na Mungu amepangilia ndani ya wanyama, kupitia silika, kila kitu wanachohitaji ili kuishi kwa ufanisi kwenye mazingira yao. Hakuna “roho ya mnyama†ikizipa fikra nguvu.

Wanadamu hupokea roho ndani ya mwanadamu tangu kutungwa mimba. Huwawezesha, kupitia matumizi ya milango mitano ya fahamu, kupata na kuhifadhi maarifa.

Kwa mara nyingine tena, watu hawapati kujua kila kitu wanachohitaji kujua ili kutenda kwa ufanisi katika maisha yao yote kwa silika. Ni lazima waendelee kupata maarifa zaidi kadri wanavyokua kuelekea utu-uzima na kadri mahitaji yanavyowakabili. Wanyama hawana hitaji kama hilo.

Tumekwisha kujadili kwamba maarifa yote yaliyopo huangukia ama kwenye maarifa ya kawaida (namna ya kutumia maada na vitu vinavyoonekana [dhahiri])—au maarifa ya kiroho (yale ambayo ni muhimu kwa watu kutengeneza uhusiano binafsi baina ya Mungu na mwanadamu, na kupata wokovu).

Watu wote wanatambua kuwa kukusanya maarifa yafaayo kutumika ni mchakato wa maisha yote unaoendelea siku zote za maisha yao. Roho iliyo ndani ya mwanadamu inawezesha hili!

Lakini ni muhimu kutambua kwamba roho ya mwanadamu siyo mwanadamu mwenyewe—iko ndani ya mwanadamu. Kuna tofauti kubwa! Roho hii haina nguvu za fikra yenyewe. Vivyo hivyo ubongo. Ubongo husikia kupitia masikio na huona kupitia macho. Roho ya mwanadamu haifanyi mambo haya yenyewe. Ubongo hufikiria—huku roho ikiupatia uwezo wa akili. Kumbuka, roho iko ndani ya mwanadamu, ikiipatia milango mitano ya fahamu za kimwili uwezo wa kutenda kazi na ubongo kwa ajili ya uchambuzi na utambuzi wa maana na uelewa. Kama umeme/sitima kwa kompyuta, roho hutia nguvu fikra kuchakata habari iliyopokelewa kupitia milango mitano ya fahamu.

Maarifa yote hupatikana kwa kujifunza. Vitoto vichanga huzaliwa bila maarifa YOYOTE—fikra zao ni kama karatasi nyeupe zikisubiri kuandikwa kitu juu yake. Katika mchakato wa ukuaji, lazima wajifunze kutenda kila jambo. Kutenda kama mtu mzima kunahitaji maarifa mengi ya kawaida. Bila shaka, watu wazima wanatambua kwamba hakuna mtu anayeweza kufanikiwa katika maisha pasipokuwa na kiwango fulani cha maarifa.

Lakini hapa kuna tatizo kubwa. Maarifa ya kawaida ambayo mwanadamu ameyapata hayajamtosha kuweza kutatua matatizo mengi makubwa yanayotesa mataifa ulimwenguni. Kwa mfano, hawezi kabisa kujifunza namna ya kuwa na furaha au kuleta wingi wa mali na amani. Na hakuna yeyote aliyegundua jinsi ya kumaliza vita, umasikini na magonjwa ulimwenguni.

Kwa nini? Ubinadamu unakosa kijenzi kingine muhimu!

Kiunganishi Kinachokosekana

Baada ya Mungu kuwaumba Adamu na Hawa, aliweka mbele yao uchaguzi muhimu kuliko wote—uamuzi wa muhimu sana kuchagua njia moja kati ya mbili. Angalia: “BWANA Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai. BWANA Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya. BWANA Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya†(Mwa. 2:7-9).

Mwanzo 3:1-8 inabeba maelezo ya uamuzi wa kihistoria wa Adamu na Hawa. Walimsikiliza nyoka na wakachagua mti usiofaa! Hii ilibeba madhara makubwa zaidi ya kile ambacho wengi wangeweza kuota kwa sababu, kwa kutochagua MTI WA UZIMA, Adamu na Hawa walijikata kabisa kutoka kwa Roho ya Mungu. Waliachwa bila kukamilika, pungufu, wasioweza kupokea ufahamu au kutengeneza mawazo ya KIROHO. Walijitenga wenyewe kutoka kwa KIUNGANISHI muhimu sana KINACHOKOSEKANA kwa ufahamu wa kiroho wa kusudi la Mungu, njia inayoongoza kwenye kujenga-tabia na majibu sahihi kwa matatizo ya mwanadamu!

Hiki hapa ndicho kilichotokea baadaye: “Bwana Mungu akasema, Basi, huyu mtu amekuwa kama mmoja Wetu, kwa kujua mema na mabaya; na sasa asije akanyosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala, akaishi milele; kwa hiyo BWANA Mungu akamtoa katika bustani ya Edeni, ailime ardhi ambayo katika hiyo alitwaliwa. Basi akamfukuza huyo mtu, akaweka Makerubi, upande wa mashariki wa bustani ya Edeni, na upanga wa moto uliogeuka huko na huko, kuilinda njia ya mti wa uzima†(fu. 22-24).

Mungu aliwanyima Adamu na Hawa njia ya kufika mbele Yake na kwa Roho Yake. Ingawa hili halikuwa kusudi Lake, lilikuwa ni matokeo ya uchaguzi wao.

Mungu alikusudia toka mwanzo kuwapa Adamu na Hawa Roho Yake. Ingeungana na roho iliyo ndani ya mwanadamu kutengeneza maisha mapya ya roho yaliyotungwa ndani ya kila mmoja wao—na ndani ya wanadamu wote watakaofuata.

Adamu alipewa zaidi ya ubongo—alipokea FIKRA, iliyo na ROHO YA MWANADAMU. Alikuwa na uwezo wa kuchagua—kujiamulia mwenyewe hatima yake. Hakulazimishwa kufuata, au kuongozwa bila habari kwenye, njia yoyote iliyopangwa. Hakuwa amepangiliwa au kuzuiliwa kwenye kuwaza kisilika, kama walivyokuwa wanyama wasioongea.

Adamu alipoukataa Mti wa Uzima, alikataa fursa ya kupokea Roho ya Mungu. Hiki ndicho kingefungua fikra zake kuujua Mpango wa Mungu—kwamba kwa nini alikuwa ameumbwa. Tuliona kwamba uamuzi wake ulisababisha yeye na mke wake, Hawa, kutupwa nje ya Bustani. Lakini uamuzi wao wa pamoja ulibeba madhara makubwa kwa wanadamu wote walitokana na wao—ambao sasa hawakuwa na uwezekano wa kuufikia Mti wa Uzima.

Pamoja na uamuzi huu, si tu kwamba Adamu alijitenga mwenyewe na wanadamu wote wasimfikie Mungu, bali pia alikataa fursa kwa ajili ya uzima wa milele—“kuishi milele†(Mwa. 3:22).

Elewa nini maana ya hili! Wanadamu HAWAJAKAMILISHWA—ni wapungufu! Maarifa yote yanayoingia ndani ya fikra zao yamejikita tu kwenye mambo yanayoonekana na vitu. Kwa dhambi yake kubwa ya kumkataa Mungu na Mti wa Uzima, Adamu alikataliwa na Mungu na kutupwa nje ya Bustani, na ubinadamu ulitupwa nje pamoja naye—sasa ukiwa umekatwa kabisa kutoka kwa Mungu mpaka Kristo Atakaporejea!

Kwa hakika huu ni ufahamu wa kushangaza—usiojulikana kwa wengi isipokuwa wachache tu leo. Na haukuwahi kujulikana mpaka karne ya ishirini!

Baadhi ya Wachache Hawatasalimu Amri Kamwe

Kusudi la Mungu kamwe halijabadilika. Anatamani kutoa uzima wa milele kwa wote watakaofaulu kuupata. Sasa, karibu kila mmoja anajua juu ya fungu lifuatalo: “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele†(Yohana 3:16).

Cha kusikitisha, hata hivyo, aya hii maarufu ni zaidi kidogo ya mchuuko usio na maana yoyote ya kweli kwa mamia ya mamilioni. Lakini umeona kwamba kuna kusudi la kushangaza ambalo Mungu analitekeleza ndani ya wale aliowaita. Kumbuka kwamba sisi tu udongo na Mungu ni mfinyanzi na sisi kama “kazi ya mikono (Yake)†(Isa. 64:8). Lakini Paulo alifahamu ni jinsi gani Mungu anatenda ndani ya Wakristo. Pia aligundua kwamba wokovu (Rumi. 6:23), na hata imani ya kuupokea, vyote ni karama za bure.

Hivi haviwezi kuchumwa. Lakini hii haina maana kwamba Mungu hatendi kwa dhahiri (na anataka matendo mema) kwa wanadamu, kadri Anavyozaliana Mwenyewe.

Wengi hawatamruhusu Mungu kutenda kazi pamoja nao. Baadhi hata watamkataa Mungu kabisa, wakikataa Kumtii—wakikataa kumruhusu atende kazi pamoja nao kama udongo. Watatumainia fikra zao wenyewe na kukikataa kiunganishi kinachokosekana cha Roho ya Mungu, ambacho kingewaongoza kwenye uzima wa milele. Watachagua kubaki wapungufu—wasiokamilishwa katika kusudi na tabia.

Mafungu yanayofuata yanaelezea mwisho wao. Malaki 4:3 inasema, “Nanyi mtawakanyaga waovu; maana watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu; katika siku ile niifanyayo, asema Bwana wa majeshi.†Waovu wataharibiwa milele. Mathayo 10:28 ilithibitisha hili wazi. Pia angalia Obadia 16: “Kwa maana kama vile mlivyokunywa juu ya mlima Wangu mtakatifu, ndivyo mataifa yote watakavyokunywa daima; naam, watakunywa na kubabaika, nao watakuwa kana kwamba hawakuwepo kamwe.

Ole kwa wale ambao wanakataa ahadi ya Mungu kufuzu kwa ajili ya ufalme wa Mungu!

Katika Sura ya Kristo

Paulo aliandika juu ya wale ambao Mungu anatenda kazi ndani yao, “Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na MFANO WA MWANA WAKE, ili Yeye awe mzaliwa wa kwanza miongoni mwa ndugu wengi†(Rumi. 8:29). Kama ilivyofafanuliwa, Mungu anapanua Familia Yake, akiongeza wana zaidi. Kristo alikuwa wa kwanza na wengine wote lazima wafanane na sura Yake—kwa tabia na mfano Wake.

Mungu anatengeneza “ndugu†zaidi katika Familia ambamo WOTE watakuwa na tabia moja na wakiwa wa roho.

Kujua kwamba Mungu na Kristo waliwatengeneza wanadamu katika “sura na mfano†wao inathibitisha kwa nini Agano Jipya linaongelea juu ya “kufananishwa na mfano wa Mwana Wake.†Maandiko ya Agano la Kale na Jipya yanaenda pamoja—yako pamoja kwa usawa mkamilifu katika kufunua kusudi la Mungu.

Mungu kamwe hajatenda kazi ndani ya wanyama. Wanapungukiwa katika maadili na kitengo cha kiroho. Wametengenezwa kwa ajili ya huduma na kufurahisha wanadamu na mazingira. Lakini hawawezi kupata maarifa mapya na kamwe hawajaahidiwa uzima wa milele. Wao sio sehemu ya Mpango wa Mungu wa kutengeneza tabia na kuzaliana Yeye Mwenyewe. Kamwe Mungu hajatenda ndani au kupitia wanyama kufikia kusudi lolote la kiroho. Yuko kazini ndani ya wanadamu waliotungwa, wakiongozwa na Roho.

Kuzaliana kwa mwanadamu kunawakilisha mtindo ule ule ambao Mungu Mwenyewe anautumia. Familia ya mwanadamu ni KIELELEZO cha Familia ambayo Mungu anaijenga. Ufunuo 19:7-9 inaonyesha kwamba ndoa kati ya wanaume na wanawake inaonyesha picha ya ndoa kati ya Kristo na bibi harusi Wake, itakayofungwa wakati wa Kurudi Kwake. Jambo hili litafafanuliwa zaidi katika Sura ya Saba.

Tumejifunza Biblia inafundisha kwamba Mungu ana Mpango ulioelezwa kwa ukamilifu ukihusisha kuzaliwa halisi katika ufalme Wake kwa ajili ya wale wote aliowaita. Na kuzaliwa mara ya pili hakutokei katika maisha haya. Hatuwezi kuwa sehemu ya Ndoa ya Kristo katika maisha haya, lakini tunaweza kujizoeza kusudi kuu la Mungu—kufanya zoezi!—kupitia NDOA za wanadamu na FAMILIA.

Fahamu tena! Kila mwaadamu ana uwezekano unaoduwaza, akiwa na uwezo mbali sana na wanyama, unaozidi hata wa malaika watakatifu wa Mungu. Angalia tena: “Amefanyika bora kupita malaika, kwa kadiri jina alilolirithi lilivyo tukufu kuliko lao. Kwa maana alimwambia malaika yupi wakati wo wote, Ndiwe Mwanangu, Mimi leo nimekuzaa? Na tena, Mimi nitakuwa kwake Baba, Na Yeye atakuwa Kwangu Mwana?†(Ebr. 1:4-5).

Kubadilishwa kwenye Ufufuo

Maada yote ni ya kawaida. Umetengenezwa kwa maada—wewe ni wa kawaida, wa mavumbi ya nchi. Hakuna chochote cha kudumu kuhusu nyama yako. Pasipokuwa na chakula, maji na hewa, hata kwa muda mfupi utakufa. Vivyo hivyo, hakuna atakayepata uzima wa milele bila kuwa na Roho Takatifu ikitenda kazi ndani yake. Bila kuwa na Roho hii ikisaidia kumbadilisha mtu, kumpa uzima wa milele, hakuna aliye na tumaini! Bila kuwa na mawasiliano na Mungu, Roho Yake na Kusudi Lake, vikiwezesha utambuzi wa kiroho, wale wote walio katika ulimwengu wa Shetani watayaacha maisha yao ya kimwili na kufa, bila ya chochote kufuatia. Lakini Mungu anatenda kazi na wachache sasa!

Awali tulimnukuu Ayubu. Alifahamu kuwa Roho ya Mungu ilitenda kazi na roho yake kumpatia ufahamu. Alikuwa anaelewa Mpango na kusudi la Mungu vilikuwa vikitenda kazi maishani mwake. Tuliona kwamba aliuliza, “Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena? Mimi nitangoja siku zote za vita vyangu, Hata BADILIKO langu linifikilie. Wewe utaniita, nami nitakujibu; Utakuwa na tamaa ya kazi ya mikono Yako†(14:14-15). Ayubu alijua kwamba ufufuo ulikuwa unamngojea—wakati “atakapobadilishwa.†Wakati huu alipaswa, “kungoja†kaburini mpaka Mungu atakapomwita.

Ayubu alikuwa na Roho ya Mungu na alifahamu lini na jinsi gani Mungu atamfufua na kumbadilisha. Alitambua kwamba itakuwa Roho ile ya Mungu iliyo ndani yake itakayowezesha badiliko lake. Mapema, tuliona kwamba, katika Warumi 8, Paulo alikuwa ameandika, “Lakini, ikiwa Roho Yake Yeye aliyemfufua Yesu katika wafu anakaa ndani yenu, Yeye aliyemfufua Kristo Yesu katika wafu ataihuisha na miili yenu iliyo katika hali ya kufa, kwa Roho Yake inayokaa ndani yenu†(fu. 11).

Paulo pia aliandika kwa Wakorintho juu ya badiliko linalokuja kwenye ufufuo, wakati wote watakapoamka kutoka usingizini wakiwa na mwili mpya wa roho. Huko nyuma, tuliona sehemu ya aya hii. Hii hapa ni sehemu yake iliyobaki: “Na kama tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua sura yake yeye aliye wa mbinguni. Ndugu zangu, nisemayo ni haya, ya kuwa nyama na damu haziwezi KUURITHI ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika. Angalieni, nawaambia ninyi SIRI; HATUTALALA sote, lakini sote TUTABADILIKA, kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho; maana parapanda italia, na wafu watafufuliwa, wasiwe na uharibifu, nasi tutabadilika. Maana sharti huu uharibikao uvae kutokuharibika, nao huu wa kufa uvae kutokufa†(1 Kor. 15:49-53).

Aya hii inaongelea juu ya siri ambayo Paulo alipaswa kufafanua. Kwa hakika ni siri kwa ulimwengu kwamba badiliko hili la kuwa-roho linakuja kutokea kwenye ufufuo wa wafu wakati Kristo atakaporudi. Wengi wanadhani kwamba wana nafsi isiyokufa inayoenda mbinguni wakati wa kifo. Bado, wachache huonekana kuuliza au kujali jinsi gani mtu anavyoweza kubadilika kutoka kuwa “wakufa†hadi kuwa “wa kutokufa†(fu. 53-54), wakati wa ufufuo, kama tayari ana nafsi isiyokufa!

Lakini tabia ya Mungu itakuwa imekamilika katika wale “Anaowahuisha†kwenye ufufuo, akiwaacha wasiweze kutenda dhambi tena (1 Yohana 3:9).

Ujira Wake Pamoja Naye

Kristo atakaporudi, ataleta ujira wa kila mmoja wa ndugu wa kiume na wa kike wote ambao ndani yao Yeye na Baba wametenda kazi. Watakuwa wamefaulu kupata utukufu mkuu: “Kwa sababu Mwana wa Adamu atakuja katika utukufu wa Baba Yake pamoja na malaika Zake; ndipo ATAKAPOMLIPA KILA MTU KWA KADIRI YA MATENDO YAKE†(Math. 16:27).

Elewa hili! Kazi zako katika maisha haya zina uhusiano wa moja kwa moja na ujira wako katika maisha yajayo. Ujira huo unahusisha UTAWALA. Sehemu ya awali ya utawala huo itakuwa miaka 1,000. Watawala hukaa juu ya viti vya enzi: “Kisha nikaona VITI VYA ENZI, wakaketi juu yake, nao wakapewa hukumu; nami nikaona roho zao waliokatwa vichwa kwa ajili ya ushuhuda wa Yesu, na kwa ajili ya neno la Mungu, na hao wasiomsujudia yule mnyama, wala sanamu yake, wala hawakuipokea ile chapa katika vipaji vya nyuso zao, wala katika mikono yao; nao wakawa hai, WAKATAWALA pamoja na Kristo miaka elfu. Hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu. HUO NDIO UFUFUO WA KWANZA (Ufu. 20:4-5).

Lakini Mpango wa Mungu hautaishia na wale tu waliojumuishwa katika Ufufuo wa Kwanza. Mungu anakusudia kuwapa wanadamu wote fursa ya kupokea Roho Yake, kujenga tabia Yake—kutimilika na kufikia UKAMILIFU!

Tukiendelea katika Ufunuo, Yohana aliongelea juu ya kuendelea kwa Mpango wa Mungu hata wakati ambapo wanadamu wote watapokea fursa kwa ajili ya wokovu. Kipindi hiki kinaitwa “Hukumu ya Kiti cha Enzi Kikuu Cheupe†na inaelezewa kwa jinsi hii: “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na Yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso Wake, na mahali pao hapakuonekana. Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa katika mambo hayo yaliyoandikwa katika vile vitabu, sawasawa na matendo yao. Bahari ikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake; na Mauti na Kuzimu zikawatoa wafu waliokuwamo ndani yake. Wakahukumiwa kila mtu kwa kadiri ya matendo yake†(20:11-13).

Lakini wale wa Kanisa la Mungu—Kanisa moja ambalo Kristo aliahidi kulijenga (Math. 16:18)—wanafundishwa na kuongozwa sasa katika kweli zote na njia za Mungu. “Kundi hili dogo†linawalisha na kuwaandaa wale ambao watatawala pamoja na Kristo. Paulo aliwaandikia Waefeso akielezea wajibu wa watumishi wa kweli wa Kristo: “kwa…kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo†(4:12-13).

Kuungana Tena na Roho ya Mwanadamu

Roho iliyo ndani ya mwanadamu haibadilishi wala haifufui mtu. Hii huja kutoka kwa Roho ya Mungu kwanza ikitenda kazi katika fikra. Tumeona kwamba, katika ufufuo, roho iliyo ndani ya mwanadamu ITAUNGANA na Roho Takatifu. Tutakuwa vile vile, isipokuwa tu tutakuwa wa roho na hivyo hatutakuwa na asili ya mwanadamu au mivuto ya mwili.

Fikiria juu ya roho iliyo ndani ya mwanadamu kwa njia hii: Ni kama kanda ya kaseti ya kila kitu tulichowahi kujifunza au kutenda—na ndio kielezo cha fikra kwa ajili ya mwili wetu wa roho unaokuja, ikibeba kumbukumbu, tabia na uzoefu wa kila mwanadamu. Kwa mantiki hiyo, kama kanda yoyote ya kaseti, inaweza “kurudishwa nyuma.†Bado, haiwezi kuwa na au kutoa maisha, au kutenda yenyewe, kwa sababu ni lazima iunganishwe na ubongo halisi—au fikra za kiroho kwenye ufufuo.

Kama mtu anayefanya kazi na kompyuta, kadhalika roho iliyo ndani ya mwanadamu hutenda kazi pamoja na ubongo kuunda FIKRA ZA MWANADAMU zinazoshangaza!

Sayansi kamwe haitagundua maarifa haya. Kile ulichojifunza katika sura hii hakifahamiki karibu na mtu yeyote. Lakini sasa unajua!

Kuna mlipuko wa maarifa kuliko wakati wowote. Lakini jambo hili linatokea katikati ya mateso, huzuni, kutoridhika, dhuluma, vita na kukanganyikiwa kwa mwanadamu kunakozidi kuliko wakati wowote. Kwa nini kuna mmomonyoko wa maadili kiasi hiki sambamba na maendeleo ya vitu yanayotisha? Pamoja na uwepo wa silaha za maangamizi zinazotishia uwepo wa mwanadamu hasa, tunauliza: Kwa nini? Na tuelekee wapi kutoka hapa?

Sura ya Sita – Kwa Nini Ubinadamu Hauwezi Kamwe Kutatua Matatizo Yake

Ulimwengu umejaa matatizo—magonjwa, uchafu, umaskini, ujinga, mkanganyiko wa kidini, vita, ughaidi, jinai, dhuluma, njaa, kukosa maadili, utumwa, ugandamizaji, migogoro ya kisiasa na mengine mengi. Kwa nini? Kadiri muda unavyoendelea matatizo yanazidi, si kupungua. Kwa nini? Pia, matatizo yaliyopo yanaendelea kuwa mabaya zaidi kwa jumla badala ya hali kuwa nzuri. Kwa nini? Kwa nini, katika kila hatua, mwanadamu amevuruga na kuharibu juhudi zote za kutatua matatizo yake yaliyo kwa-kweli makubwa sana?

Kwa wakati huo huo, mtu mmoja mmoja, amezidi kutokuwa na uwezo wa kushughulikia na kushinda matatizo yake binafsi. Kama ilivyo kwa ulimwengu katika ujumla wake, kila wakati unaopita unawakuta watu mmoja mmoja na familia wakizama katika bahari kubwa ya kuporomoka kimaadili na shida zinazoonekana kutokuwa na majawabu. Wengi zaidi na zaidi wanaonekana kutoweza kabisa kutawala maisha yao.

Ndio, kwa nini?

Wanadamu wamefanya ugunduzi mwingi wa kiteknolojia unaoshangaza, lakini hawawezi kutengeneza majibu ya matatizo yao. Wanadamu wamethibiti nguvu za kompyuta kuwasaidia kuchambua kiasi kikubwa cha habari, lakini watu hawawezi kutatua kwa usahihi matatizo yao binafsi. Wanasayansi wamegundua mengi kuhusu ukubwa, uzuri na usahihi wa ulimwengu, lakini hawawezi kugundua njia ya amani. Wanajimu wanaweza kutafuta na kuona galaksi mpya, nzuri kote ulimwenguni, lakini hawawezi kupata njia ya kuhifadhi uzuri na fahari ya dunia. Wanasayansi pia wamesambaratisha nguvu za atomu, lakini hawana uwezo wa kuainisha majibu kwa maswali makuu ya maisha. Wakufunzi wamefundisha wengi jinsi ya kujipatia kipato, lakini si jinsi ya kuishi.

Mwanahistoria na mwandishi anayejulikana sana wa mambo ya kiutawala Peggy Noonan anafupisha hali changamani, iliyovurugika ambayo imekuwa historia ya mwanadamu: “Katika utepe mrefu wa historia, maisha yameendelea kutawaliwa na dosari na vurugu, yakijawa na njaa, vitisho, vita na magonjwa. Lazima tulifikiri tungekuwa na hali nzuri kwa sababu mwanadamu amekuwa bora. Lakini kwa hakika mwanadamu hawi “bora,†au siyo? Mwanadamu ni mwanadamu. Hulka ya mwanadamu ni hulka ya mwanadamu; utashi wa kuharibu unaenda sambamba na utashi wa kujenga na kutengeneza na kuboresha†(“Zama ya Amerika Isiyo na Uhakika,†Knight Ridder, Nov. 9, 2001).

Nani angeweza kukataa?

Hali ya Sasa—na Ijayo

Fikiria baadhi ya hali za kutisha duniani leo. Kama matukio yatabaki bila kushughulikiwa, yanabashiriwa kuwa mabaya zaidi ifikapo mwaka 2050—ikiwa mwanadamu ataishi kufikia huko! Takwimu zifuatazo zinatoka kwenye ripoti ya Umoja wa Mataifa kuhusu “Hali ya Idadi ya Watuâ€, miaka ya 2001 na 2007. Hizi ni ripoti kamili ambazo zinamfanya msomaji afikiri.

Idadi ya watu duniani (bilioni 6.7) imeongezeka zaidi ya mara tatu katika kipindi cha miaka sabini iliyopita. Imeongezeka zaidi ya mara mbili tangu mwaka 1960 na inabashiriwa kufikia bilioni 9.34 ifikapo mwaka 2050. Nchi arobaini-na-tisa maskini zaidi, zilizoduni kimaendeleo kwa hakika zitaongezeka mara tatu na kufikia watu karibu bilioni mbili. Kuongezeka kwa idadi ya watu duniani kwa jinsi hii kutaleta matatizo makubwa.

Ni asilimia 2.5 tu ya maji duniani ndio yaliyo safi. Kati ya haya ni asilimia 20 tu (au asilimia 0.5) yanafikiwa ama ardhini au juu ya ardhi. Idadi ya watu walioko sasa inatumia asilimia 54 ya maji haya. Kufikia mwaka 2025, matumizi ya maji yanatarajiwa kuongezeka kufikia asilimia 50 katika nchi zinazoendelea, na asilimia 18 katika maeneo mengine. Kulingana na ukuaji wa dunia kwa ongezeko la watu milioni 75 kwa mwaka inahitaji kiasi cha maji sawa sawa na yale ya Mto mkuu Rhine. Pia, nchi zinazoendelea humwaga kati ya asilimia 90 na 95 ya maji yao machafu yasiyosafishwa na asilimia 70 ya maji ya viwandani yasiyosafishwa kwenye maji yaliyo juu ya ardhi. Ongezeko la watu linamaanisha kwamba tatizo hili litazidi kuwa baya zaidi. Kwa kuongezea, mvua ya tindikali na mtiririko wa kemikali kutokana na mbolea na viuatilifu vinatosha kuharibu ubora wa maji, na kuyafanya yasifae kutumika kwa kiwango kikubwa.

Ongezeko la idadi ya watu linaendelea kuzidi kiwango cha uzalishaji wa chakula. Kuna watu milioni 850 walio na utapiamlo wa kudumu, na bilioni 2 wasio na “uhakika wa kupata chakula.†Ni aina 15 tu ya mazao hutoa asilimia 90 ya chakula cha ulimwengu, bado inakadiriwa kwamba aina tofauti sitini elfu za mimea zinaweza kutoweka ifikapo 2025 tu! Kufikia mwaka huo, idadi ya wakazi wa dunia inayotarajiwa kuwa bilioni 8 (namba za kukadiria hubadilika) bila shaka watahitaji mara mbili ya mahitaji ya chakula ya wakati huu, ikienda sambamba na usambazaji ulioboreshwa, ili kuondoa tatizo la njaa kabisa. Lakini ni wataalamu wachache wanaoona hili likiwezekana hata kwa kiwango cha chini.

Kila siku, watu 160,000 wanahamia mijini kutoka mashambani. Hili linatokea kwa haraka zaidi katika nchi zisizoendelea. Jambo hili husababisha matatizo makubwa: usafi, msongamano, upatikanaji wa huduma za kisasa za afya na uwezo wa shule kumudu ongezeko la wanafunzi.

Zaidi ya nusu ya magonjwa yote duniani yanahusiana na suala la usafi. Kila mwaka, uchafuzi wa hewa huua karibu watu milioni 3 katika nchi zinazoendelea pekee, huku hali duni ya usafi ikiua wengine milioni 12. Aina mbali mbali za uchafu wa majumbani (moshi, vinyesi, mkaa wa kupikia na kupasha joto, n.k) huathiri watu bilioni 2.5 kwa mwaka na kuua milioni 2.4. Mabadiliko ya hali ya hewa yanabadili maeneo hatarishi kwa magonjwa yanayoenezwa na wadudu. Magonjwa mapya hatari zaidi yanatokea au yanarudi. Na bakteria wengi wamethibitika kuwa sugu kwa dawa kwa sababu ya matumizi yanayozidi kiwango ya viua vijasumu.

Baadhi ya matatizo yanayobashiriwa kutokea hivi karibuni ni pamoja na: Udogo na kuendelea kupungua kwa ardhi inayofaa kwa kilimo, uharibifu wa misitu, mipangomiji, kupungua kwa mashamba ya familia, uharibifu wa ardhi, uhaba na uchafuzi wa maji, matatizo ya umwagiliaji, taka, kupotea kwa aina za mazao, kuongezeka kwa makali na mfululizo wa hali mbaya ya hewa, inayosababisha mafuriko na uharibifu wa mazao ya msimu, na uzalishaji wa hewa ya ukaa na mabadiliko ya tabia ya nchi. Wakati huo huo, kulingana na tovuti ya Uhifadhi wa Hali Asili, karibu hekari 1.6 za misitumvua—ijulikanayo kama “mapafu ya ulimwengu†kwa sababu ya kutoa hewa nyingi sana ya oksijeni—inapotea kwa ukataji wa magogo kila sekunde!

Kwa jumla, matatizo haya yanaashiria janga lisiloelezeka, na hata maangamizi, kwa ubinadamu usiokuwa tayari kuyatatua na matatizo mengine mengi.

Wakati ulimwengu ukiteseka kutokana na “wingi wa habari,†hakuna lolote kati ya ongezeko hili la maarifa linaloshughulikia hasa matatizo sugu, changamani yanayoongezeka. Pamoja na uwezo wake wote kiakili wa kuunda vitu, mwanadamu hawezi kutatua matatizo muhimu—yanayotishia uwepo wake juu ya dunia anayoiharibu hatua kwa hatua.

Wakufunzi wamelaghai vizazi kuamini uongo wa nadharia ya mabadiliko. Hii imesababisha mamilioni wasiohesabika kuamini kwamba mwanadamu anaendelea kubadilika kuelekea hali nzuri na ya juu ya uwepo wake. Angalia kila mahali na utaona matunda ya uongo huu mkuu. Mwanadamu habadiliki kwenda juu—anadidimia kwenda chini, kuelekea hali mpya za chini za kujiendekeza, kushuka kimaadili na maovu.

KWA NINI?

Miti Miwili

Ni jinsi gani ustaarabu uliingia katika hali ya kukanganyikiwa, mgawanyiko, vita, mashindano na mabishano yaliyomo duniani kote leo? Amri ya mwanzo ya Mungu kwa Adamu ilikuwa, “Walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika†(Mwa. 2:17).

Katika sura inayofuata (3:6), Hawa, na Adamu akifuata, waliasi na kula matunda ya mti huu usio sahihi. Angalia kwamba mti huu uliwakilisha maarifa ambayo yalikuwa “mema na mabaya.†Kwa maneno mengine, mti ule haukuwa mbaya kabisa—ulijumuisha mchanganyiko wa maarifa ya kweli na uongo! Ndivyo ilivyo kwa makanisa ya ulimwengu huu. Baadhi yana kiwango kidogo cha “maarifa†ya mafundisho ya kweli (“memaâ€) yaliyochanganyika na “maarifa†ya mafundisho ya uongo (“mabayaâ€). Lakini Mungu daima amewaambia watumishi Wake wa kweli kutochanganya ukweli na uongo. Alimwonya Adamu kwamba kula mti usio sahihi matokeo yangekuwa ni kifo. Ikawa hivyo.

Onyo ni lile lile kwetu leo!

Nilipokuwa nikijifunza ukweli kwa mara ya kwanza mwaka 1966, mtu aliyenifundisha alitumia ulinganishi ambao kamwe sikuwahi kuufikiria kabla—lakini kamwe sijausahau tangu wakati huo: Fikiria juu ya keki tamu iliyotiwa kemikali ya sumu kama aseniki, risini au sumu kali ya kusisimua neva, ingawa haina kitu zaidi ya viambata vizuri vya afya. Kuila keki hii daima matokeo ni kifo!

Viambata vizuri havingeweza kutosha kuishinda sumu iliyofichwa ndani ya keki. Vivyo hivyo, Kanisa la Mungu halichanganyi na haliwezi kuchanganya ukweli na makosa. Kama ilivyo kwa keki, matokeo kwa wale wanaochanganya ni ya kufisha!

Sheria Kuu Isiyoonekana!

Kila mmoja anaifahamu sheria ya nguvu ya uvutano. Wote wanatambua kuwa kama wangeivunja sheira hii, ingeweza “kuwavunjaâ€. Kama mtu kwa bahati mbaya atadondosha tofali juu ya mguu wake, matokeo yaweza kuwa mifupa iliyovunjika. Kama mruka angani ataruka kutoka kwenye ndege, na mwavuli ukashindwa kufunguka, matokeo ni kifo cha hakika. Hii ni rahisi kuelewa.

Ifuatayo ni baadhi ya mifano ambayo ni dhahiri kidogo tu, lakini ni halisi. Kama mtu ni mgonjwa mara kwa mara, ni wazi kwamba sheria za afya (chakula sahihi, mazoezi ya kutosha au usingizi wa kutosha, n.k.) zinavunjwa. Afya mbaya ina sababu moja au zaidi. Kama ndoa itaishia kupeana talaka, inaweza pia kuwa ni kwa sababu moja au zaidi: kukosekana mawasiliano, matatizo ya kifedha, kifo cha mtoto, matatizo ya unyumba, huzuni mahala pa kazi, n.k. Kama mtu atakamatwa kwa kuendesha akiwa amelewa, ni rahisi kuiona sababu.

Ingawa wengi hawatambui sababu na athari kama SHERIA kuu inayotawala karibu kila tendo maishani, angalau wanafahamu kiujumla kwamba ni kanuni inayotenda kazi katika nyakati fulani.

Lakini kila aina ya athari inaweza kufuatiliwa hadi kwenye sababu moja au zaidi. Mimba zisizotarajiwa au haramu, makosa ya jinai, matumizi ya madawa ya kulevya, kufilisika, na athari zingine maelfu, zote zinaweza kuunganishwa kwenye sababu maalumu. Tengeneza orodha yako mwenyewe. Unaweza kuona kwamba karibu haina mwisho.

Biblia toleo la King James inafundisha, “…laana isiyo na sababu haimpigi mtu.†Tafsiri zingine mbili za fungu hili ni “…laana “isiyostahili†haitafikia lengo lake†(Biblia ya Yerusalemu), na “…laana isiyo na msingi kamwe haitimii†(Moffatt). Andiko hili linasema kwamba kila gumu linabeba sababu—kuna SABABU kwa ajili ya kila ATHARI!

Kwa nini mwanadamu haoni sheria hii ikitenda kazi anapouangalia ulimwengu katika ujumla wake? Kwa nini ni kwamba hakuna anayetafuta sababu ya matatizo ya maisha na maovu? Kwa nini wakufunzi hawafundishi kanuni hizi kuu kuliko zote? Kadiri unavyoangalia ulimwengu unaokuzunguka, unashughulishwa nao? Je unashangaa KWA NINI umejawa na shida, huzuni na kutoridhika? Na kwa nini hata dini ya Kikristo imepuuza uhusiano huu muhimu baina ya sababu na athari?

Sababu ya matatizo yote ya ulimwengu ilianza katika Bustani ya Edeni. Kama inavyotamkika kirahisi kama ilivyo, ni kweli. Ulimwengu umepoteza uwezo wa kuona uamuzi uliofanywa na Adamu na Hawa. Walichagua kutokula matunda ya Mti wa Uzima, badala yake walichagua kula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Ulishawahi kujiuliza nini kingetokea kama wawili hao wangechagua Mti wa Uzima? Fikiri jinsi ambavyo kufanya hivyo kungekuwa kumebadili ulimwengu wote! Kila kitu kingekuwa tofauti.

Kusingekuwepo majeshi, vita, kifo, uteketezaji au uhamishaji wa watu. Kusingekuwepo njaa au kukosa chakula kwa sababu kungekuwa na chakula tele kwa ajili ya kila mmoja. Kusingekuwepo madaktari, kwa sababu hakungekuwa na magonjwa. Mahospitali yote na vituo vya afya visingekuwepo kamwe. Wala magereza, jela, majaji, mahakama na majeshi ya polisi yaliyopo kwa ajili ya kuadhibu wavunja sheria.

Furaha, ustawi, mafanikio na amani vingepatikana ulimwenguni kote. Watu wote wangekaa kwa maelewano—majirani, familia, mtu mmoja mmoja na mataifa. Unaweza kufikiri ulimwengu kama huo?

Wakati Adamu na Hawa walipofanya uchaguzi usio sahihi, ilituathiri wewe na mimi moja kwa moja! Walileta athari zisizosemeka juu ya ubinadamu, kwa sasabu ya SABABU yao moja isiyo sahihi—na jambo hili halikuwahi kueleweka kabla ya karne ya 20.

Hebu tuchunguze zaidi ukweli juu ya KWA NINI ulimwengu unasumbuliwa na matatizo yasiyoisha.

Nia ya Mwili

Kabla ya kuendelea, hebu tuchunguze sababu kubwa ya kwa nini kuvunja sheria ya sababu na athari imeupiga ulimwengu kwa matatizo yasiyotatulika.

Paulo anarekodi kauli ya ajabu: “Kwa kuwa ile nia ya mwili ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii†(Rum. 8:7). Tafsiri zingine hutumia msemo mkali “ni ADUI wa Mungu†badala ya “ni uadui juu ya Mungu.â€

Kwa wale watakaoiamini, aya hii pekee hutoa mwanga wa kushangaza juu ya utendaji wa asili—“mwiliâ€â€”fikra za kila mwanadamu. Zikiwa zimetengwa na Mungu, fikra za asili ni adui wa Mungu—zinamchukia. Fikiria juu ya hili! Jiulize mwenyewe ikiwa mtumishi yeyote wa kanisa, mtu wa dini au mwanateolojia ameshawahi kukuelezea jambo hili.

HAPANA! Viongozi wa kidini wa ulimwengu huu kamwe hawarejelei jambo hili. Ama hupuuza ufahamu huu kabisa au hawatambui athari zake kwa mwanadamu katika ujumla wake!

Fungu hili linasema wazi kwamba fikra asili hazitaki, na hata zinachukia, kujiachilia kwa Mungu na kutii Sheria Yake. Ingawa watu wengi wanadai kwamba “wanampenda Mungu,†ukweli ni kwamba fikra zao zinadharau njia Yake na kwa kweli zinakataa kunyenyekea Kwake—kwa mamlaka Yake juu ya maisha yao.

Ndiyo maana Yeremia aliandika, “Ee BWANA, najua ya kuwa njia ya mwanadamu haimo katika nafsi yake; kuelekeza hatua zake si katika uwezo wa mwanadamu anayetembea†(10:23). Hii ni kauli nyingine ya ajabu. Wanapokabiliwa na matatizo au maamuzi muhimu, kwa urahisi tu wanadamu HAWAJUI WAFANYE NINI! Hawana namna ni kwa jinsi gani watashughulikia kwa usahihi na kutatua changamoto, shida na matatizo wanayokutana nayo katika maisha yao binafsi.

Jinsi gani basi wataweza kutatua matatizo changamani zaidi yanayoughubika ustaarabu leo? Hawawezi. Suluhu zilizotokana na kufikiri kibinadamu mara nyingi huzalisha matatizo zaidi. Tutajifunza kwa nini iko hivyo.

Kupapasa Amani

Hakuna kitu kinachoweza kufahamika au kukamilishwa bila maarifa sahihi. Hata jambo rahisi kama kubadilisha gurudumu la gari huhitaji “kujua jinsi ya kufanya.†Bila ya maarifa sahihi, mwanadamu hubaki asiye na uwezo kabisa—bila msaada kabisa—mbele ya matatizo yake. Kwa sababu mwanadamu amekataa chanzo cha maarifa sahihi, amezungukwa na taabu za kutisha.

Fikiria tatizo moja la ulimwengu ambalo limeshindikana kutatuliwa na suluhu zote zilizobuniwa kibinadamu katika historia yote iliyorekodiwa: Kuipata amani. Mwanadamu amejizuilia mwenyewe asipate maarifa ambayo yangefanya hili liwezekane. Wewe angalia tu vichwa vya habari vya magazeti ya kila siku. Vita inaonekana kuikamata sayari katika kila sehemu ya ulimwengu.

Hii ni kwa sababu serikali za wanadamu kwa urahisi tu haziwezi kitu. Hazijaweza kamwe kufanikiwa katika kupata suluhu za kudumu kwa matatizo ya ustaarabu. Wanapungukiwa na maarifa ya lazima yanayohitajika ili kuyatatua. Hawana majibu kwa maswali makuu ya mwanadamu. Mwanadamu hawezi, yeye mwenyewe, kufahamu njia ya kuifikia amani—au, kwa mantiki hiyo, njia ya kupata wingi, furaha, afya na ustawi. Wapiga bongo wakubwa, viongozi, wakufunzi na wanasayansi wameshindwa kabisa katika jitihada zao za kuleta amani duniani. Mungu hajaufunulia ubinadamu, katika ujumla wake, jinsi ya kupata suluhisho la vita.

Si ajabu basi kwamba Mungu alimvuvia nabii Hosea kurekodi, “Watu Wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa: kwa kuwa umeyakataa maarifa, Mimi Nami nitakukataa wewe†(4:6)? Mwanadamu angeweza kujua, kufahamu na kuyafikia maariafa yaliyo muhimu zaidi kuhusu jinsi ya kuishi, lakini alichagua kuyakataa. Matokeo yake, Mungu alimkataa—AKAKATA MAWASILIANO KABISA—mwanadamu asimfikie. Na hii inawakata kabisa wanadamu wasifikie suluhu sahihi kwa matatizo walio nayo yenye kutisha, yanayozidi kuwa mabaya.

Uzima au Mauti?

Uwepo wako kibinadamu kwa hakika ni suala la uzima au mauti. Yesu alisema “…Nalikuja ili wawe na UZIMA, kisha wawe nao tele†(Yohana 10:10). Bado, Paulo aliandika, “wote wametenda dhambi†(Rum. 3:23) na “mshahara wa dhambi ni MAUTI†(Rum. 6:23). Kumbuka, wanadamu hawana nafsi, wao ni nafsi (Mwa.2:7).

Mwanadamu kwa asili hauendei uzima wa milele, badala yake anayaendea MAUTI!

Wanadamu wanaishi kadiri ya miaka 70 hadi 80, na chini zaidi katika sehemu zingine za ulimwengu. Wachache hufanikiwa kuishi miaka zaidi ya hapa, lakini hatimaye wote hufa. Ingawa, kamwe halikuwa kusudi la Mungu toka awali kwamba iwe hivyo. Mungu anataka tupitie uzoefu wa maisha kwa milele yote.

Mungu anakusudia kwamba wanadamu wote hatimaye wapokee Roho Yake Takatifu. Anaitaka hatimaye iziingie fikra zote. Hebu tujifunze zaidi ni jukumu gani hiki kijenzi cha roho cha PILI hutenda katika mchakato, na jinsi kinavyofanya kazi na roho iliyo ndani ya mwanadamu, iliyoelezewa katika Sura ya Tano. Kwanza pitia tena kile Paulo aliandika: “Roho [Roho Takatifu] yenyewe hushuhudia pamoja na roho zetu [roho iliyo ndani ya mwanadamu], ya kuwa sisi tu watoto wa Mungu; na kama tu watoto, basi, tu warithi; warithi wa Mungu, warithio pamoja na Kristo (Rum. 8:16-17).

Tuliona roho mbili zimeelezewa hapa. Je uliona kwamba Roho ya Mungu hutenda kazi “pamoja†na roho za wanadamu kuufikia wokovu kama “warithio pamoja na Kristo� Ni Roho hii hii ambayo Adamu aliahidiwa na angeipokea kama angekula matunda ya Mti wa Uzima!

Katika 1 Wakorintho 2, Paulo pia alikuwa amesema, “Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho ya Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyajua, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya roho†(fu. 14). Hili ni fungu muhimu muno. Ni rahisi tu kwamba haiwezekani kwa wanadamu bila Roho ya Mungu kufahamu maarifa ya kiroho—ufahamu wa kiroho. Mambo kama hayo yataonekana “upumbavu†kwa fikra ambazo haziwezi “kutambua kwa jinsi ya roho.†Haijalishi mtu ni mwenye akili au kipaji cha namna gani, bila Roho ya Mungu, inaweza kusemwa kwamba wana KIWANGO CHA AKILI ya kiroho cha SIFURI! Hakuna lolote kati ya matatizo yaliyo ya kawaida kwa watu mmoja mmoja au mataifa yanaweza kushughulikiwa kikamilifu na kutatuliwa bila kuhusika kwa Roho Takatifu ikitenda kazi katika fikra.

Hata kujaribu kuwaambia watu kwamba wanapungukiwa kijenzi hiki cha kiroho ni zoezi lisilo na mafanikio, kama Mungu hafungui fikra zao (Yohana 6:44, 65). Itaonekana upumbavu kwao, kwa sababu hata habari hii “inatambulikana kwa jinsi ya roho.†Na kadri mtu anavyokuwa mwenye akili na kujitumainia mwenyewe, pengine ndivyo itakavyoonekana upumbavu zaidi kwake kuambiwa kwamba fikra zake hazijakamilika.

Kama Adamu angekula matunda ya Mti wa Uzima, angepokea Roho ya Mungu. Angejifunza njia ya upendo—njia ya “kutoaâ€â€”badala ya njia ya “kupokea,†inayofuatwa na ulimwengu huu. Kumbuka, Biblia inafundisha kwamba “pendo ndilo utimilifu wa sheria†(Rum. 13:10), na kwamba “pendo…limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Takatifu†(Rum. 5:5).

Warumi 8:6 inasema: “Kwa kuwa nia ya mwili [asili] ni mauti; bali nia ya roho ni UZIMA na AMANI.†Kama Adamu angepokea Roho ya Mungu, angepokea uzima moja kwa moja ndani yake. Angekuwa “mrithi†pamoja na Kristo kama vile alivyo Mkristo yeyote wa kweli leo. Pia angeijua njia ya amani.

Kwa kweli mambo haya yote ni nyeti sana, maarifa yasiyo ya kawaida—yasiyojulikana kwa wote isipokuwa kwa wachache waliotawanyika juu ya dunia hivi sasa. Kwa urahisi tu ni kwamba hayakuwahi kujulikana mpaka wakati wetu!

Nani Anashikilia Utawala Juu ya Dunia?

Hebu kwa muda huu turudi kwenye bustani. Kwa hakika Shetani alikuwa akingoja pale kwa ajili ya “mtoto†Adamu na Hawa. Waliumbwa siku ya sita ya juma, Ijumaa, wakapumuzika Sabato, Jumamosi, na huenda walishawishiwa na Shetani (Mwa. 3:1-6) siku ya Jumapili—wakiwa na umri wa siku mbili

Bila shaka hakuna mtoto mwenye umri wa siku-mbili anayejua jinsi ya kutambua kati ya jema na baya. Adamu na Hawa mara ile walifikiri walikuwa wamekua vyakutosha kufanya maamuzi yao wenyewe. Kama ilivyo kwa watoto wengi leo, maarusi hawa walichagua kutomsikiliza Mzazi wao, Mungu. Badala yake, waliamini uongo wa Shetani kwamba “hakika wasingekufa.†Na, akiwa amefarakanishwa na Mungu kwa dhambi (Isa. 59:1-2; Yer. 5:25), mwanadamu ameamini uongo wa mungu wa ulimwengu huu tangu Uumbaji. Chini ya mvuto wa Shetani, mwanadamu ametenda dhambi na uasi kwa amri za Mungu kwa muda huu wote. Kisha amejaribu kutibu na kusahihisha athari zote mbaya badala ya kutibu sababu yenyewe—uvunjaji wa amri za Mungu. Hivyo, Mungu anavumilia akimwacha mwanadamu ajifunze masomo machungu. Walio wengi sana, ambao kamwe hawajajua ukweli wa thamani wa Mungu, wanapaswa kujifunza kwamba njia zao wenyewe hazifai kitu!

Makanisa ya Ulimwengu Yamedanganywa

Mungu anazaliana Mwenyewe kwa kuweka kiasi kidogo sana CHA YEYE MWENYEWE ndani ya kila mtu Anayemtunga. Kupitia toba na ubatizo, mtu hupokea karama ya Roho Takatifu (Matendo 2:38), baada ya kuwa ameitwa na Mungu kurithi ahadi ya wokovu (fu. 39).

Petro, anayeongea katika Matendo 2:16-17, alimrejelea nabii Yoeli aliyetabiri juu ya wakati ambapo Mungu “angemimina Roho [Yake] juu ya wote wenye mwili†(2:28). Hiyo ilianza na kuzaliwa kwa Kanisa la Agano Jipya kwenye siku ya Pentekoste katika mwaka 31 BK.

Makanisa ya ulimwengu huu hayafahamu chochote kuhusu njia ya kweli kuufikia wokovu. Hata hawatambui wokovu wa kweli ni nini. Ni Kanisa pekee ambalo Kristo analiongoza (Efe. 1:22-23; Kol. 1:18) ndilo linafahamu pointi hizi. Yesu hakuja kuukoa ulimwengu sasa. Kamwe hajawahi kuwa kwenye “kampeni ya kuokoa-roho†kama wengi walivyochukulia.

Ukristo bandia wa ulimwengu huu umepofushwa usione ukweli na mpango wa Mungu. Badala ya kumtii Mungu, mamilioni wamedanganywa katika kukubali mawazo na mapokeo ya wanadamu. Yesu alisema, “Nao Waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu, Ninyi mwaiacha amri ya Mungu, na kuyashika MAPOKEO ya wanadamu†(Marko 7:7-8).

Tumeona kwamba hulka ya mwanadamu ni uadui dhidi ya Mungu. Inauchukia ukweli, sheria, serikali na njia ya Mungu. Haitaki kutawaliwa na yeyote au kitu chochote. Inataka uhuru kufuata njia yake yenyewe—inaamini mawazo yake yenyewe, desturi na mapokeo—bila kuingiliwa na Mungu.

Kama mtu yeyote ana shauku katika kumtii Mungu, ni kwa sababu tu “amevutwa†(Yohana 6:44) na Roho ya Mungu na kuitwa (Math. 22:14) kuufahamu ukweli Wake wa ajabu. Macho yake yamefunguka kwa uwezekano wake wa kushangaza. Matokeo yake, anataka kuishi njia tofauti kabisa ya maisha.

Hukumu iko juu ya Kanisa sasa, si juu ya ulimwengu. Petro aliliandikia Kanisa, “Kwa maana wakati umefika wa hukumu kuanza katika nyumba ya Mungu [Kanisa]†(1 Pet. 4:17). Hatimaye, ulimwengu wote utajifunza ukweli (Isa. 11:9), pamoja na mataifa yote yakiufikilia mpango wa wokovu. Lakini wakati huo haujafika bado kwa wanadamu kwa kiwango kikubwa. Fokasi ya mpango wa Mungu wa upatanisho, msamaha wa dhambi, kushinda, kuendelea kujenga tabia na kupokea karama ya uzima wa milele umelenga juu ya Kanisa pekee katika zama hii!

Wale walioitwa wakati huu lazima wamshinde ibilisi, mivuto ya ulimwengu huu na mwili wao, kama vile Kristo alivyoshinda, ili wafaulu kuwa sehemu ya ufalme wa Mungu unaokuja hivi karibuni—ili waweze kutawala pamoja na Kristo. Tulisoma hapo awali kwamba watatawala pamoja na Kristo juu ya kiti Chake cha enzi (katika Yerusalemu), wakati huo ndipo atakapowaita watu wote kupokea fursa ya wokovu—wakati Shetani atakapokuwa ameondolewa kutoka kwenye kiti chake cha enzi duniani na kutupwa ndani ya shimo la kuzimu “atakapofungwa…kwa miaka elfu moja†(Ufu. 20:2-3).

Wale watakaoitwa baadaye—kipindi cha mileniamu au kipindi cha hukumu kwa ajili ya mabilioni wote waliopata kuishi—hawatahitaji kumshinda ibilisi wala mivuto ya ulimwengu wake. Hakuna shaka, ni wachache sana miongoni mwa hawa watamwasi Mungu na kukataa wokovu. Bila shaka, wachache watachagua hili, na tuliona kuwa wataharibiwa katika ziwa la moto liyeyushalo (2 Pet. 3:10-12). Watageuzwa kuwa majivu (Mal. 4:3) kwa sababu Mungu wa haki na rehema, kwa hakika “atawaondoa kutoka shida zao kihalisi.†Biblia huelezea tukio hili kama “mauti ya pili†(Ufu. 20:6), kwa sababu wanadamu wote “wamewekewa†kufa mara moja kwa kuwa ndio matokeo ya dhambi ya Adamu (Ebr. 9:27; Mwa. 2:17).

Mpango wa Mungu Ulifunuliwa Kupitia Siku Takatifu

Mungu alipanga mbinu ambayo kwa hiyo watu Wake kamwe wasingesahau au wakose kuuelewa ukweli wa Mpango Wake Mkuu wa kuuokoa ubinadamu. Akianza na Waisraeli wa zamani, Aliamuru kwamba SIKUKUU SABA, au Sabato za mwaka, zitunzwe kila mwaka kama simulizi ya kusudi hili kwa ujumla.

Sikukuu ya kwanza, inayotambulisha jukumu la Kristo kama Mwokozi na Kuhani Mkuu, ni PASAKA. Hii hutunzwa kila mwaka kukumbuka dhabihu Yake na damu iliyomwagika kwa ajili ya msamaha wa dhambi. Kisha huja sikukuu ya pili, SIKU saba za MIKATE ISIYOTIWA CHACHU, zikionyesha uondoleaji mbali wa dhambi na mchakato wa kushinda.

Inayofuata, sikukuu ya tatu, inaitwa SIKUKUU YA PENTEKOSTE (“Malimbuko†katika Agano la Kale), hutunzwa siku ya hamsini (Pentekoste maana yake hesabu hamsini) baada ya mganda wa kutikiswa unapokuwa umekatwa wakati wa Siku za Mikate Isiyotiwa Chachu. Matendo 2:1 inaonyesha kwamba Kanisa la Agano Jipya lilianza katika siku hii. Kanisa lote la Agano Jipya hadi leo, na wachache kutoka Agano la Kale, kwa pamoja wanakuwa malimbuko ya mpango wa Mungu wa wokovu (Yak. 1:18).

Katika siku za mwanzo za majira ya kipupwe huja sikukuu nne za mwisho, kila moja ikionyesha tukio muhimu linalofuata katika Mpango wa Mungu. SIKUKUU YA TARUMBETA ni sikukuu ya nne, na tukio kitovu inayoliwakilisha ni Kuja kwa Kristo Mara ya Pili. Inayofuata, sikukuu ya tano ni SIKU YA UPATANISHO na inawakilisha kipindi ambapo ulimwengu wote utakuwa “mmoja†pamoja na Mungu na Kristo kwa sababu Shetani atakuwa amefungwa. Na sikukuu ya sita, SIKUKUU YA VIBANDA (pia ikitimiza siku saba), inawakilisha miaka 1,000 ya mwisho ya Mpango wa Mungu, wakati Kristo pamoja na watakatifu waliofufuliwa watatawala juu ya dunia. Ni katika kipindi hiki ambapo Mti wa Uzima utatolewa kwa wote wenye kumtafuta na kumtii Mungu.

Mwisho, sikukuu ya saba ni SIKU KUU YA MWISHO. Inawakilisha Hukumu ya Kiti Kikuu cha Enzi Cheupe, wakati Kitabu cha Uzima (Ufu. 20:12) kitafunguliwa kwa wanadamu wote waliopata kuishi—toka kipindi cha Adamu mpaka sasa, ili kwamba kila mmoja hatimaye apokee fursa kwa ajili ya wokovu.

Wakiwa wamevalia silaha za maarifa haya kwa ufupi, Wakristo si wanaharakati—wa kisiasa, kijamii au kiroho—kama ambavyo wanavyofundishwa wengi wa wanaodai kuwa Wakristo, kisha wanafikiri wanaweza na wanatakiwa “kuutengeneza ulimwengu.†Hawajaribu “kuuleta ufalme†kupitia juhudi za kibinadamu. Wanajua kwamba Mungu pekee ndiye awezaye kuuleta ufalme Wake duniani! Kama wanadamu wangeweza kufanikisha hili, ungekuwa “ufalme wa wanadamu†si ufalme wa Mungu.

Watumishi wa kweli wa Mungu wanaishi na maarifa ya jinsi ambavyo injili ya kweli ya ufalme wa Mungu hueleza kinagaubaga njia itakayopelekea amani ya ulimwengu, furaha, afya na ustawi wa kila kitu. Wanafahamu kwamba ufalme wa Mungu unakuja kutatua matatizo YOTE ya ulimwengu yaliyo magumu sana.

Wakristo wa kweli wanajua kile kinachoujia ustaarabu—ikijumuisha habari mbaya ndani ya kipindi-kifupi na HABARI NJEMA za kipindi-kirefu. Wanafahamu unabii na hawachukui mambo mikononi mwao wenyewe, hivyo kutafuta kuzima kusudi la Mungu, ambalo ni kumwonyesha mwanadamu kwamba hawezi kabisa kujitawala mwenyewe au kutatua matatizo yake bila Roho Takatifu!

Hatari ya Kujikomesha Itafupishwa

Wasiwasi na mashaka vinaongezeka ulimwenguni kote. Wengi zaidi sasa wanauliza, “Nini kinatokea? Kila kitu kinaelekea wapi?†Matatizo yatazidi kuwa makubwa sana kiasi kwamba tutafikia kile kipindi kilichoelezwa katika Mathayo 24:21-22. Katika sura hii, Kristo alikuwa anaelezea hali za mambo muda mfupi kabla ya Kurudi Kwake aliposema: “Kwa kuwa wakati huo kutakuwapo DHIKI KUBWA, ambayo haijatokea namna yake tangu mwanzo wa ulimwengu hata sasa, wala haitakuwapo kamwe. Na kama siku hizo zisingalifupizwa, asingeokoka mtu ye yote [baki hai]; lakini kwa ajili ya wateule zitafupizwa siku hizo.â€

Ni kwa jinsi gani hasa mwanadamu anavuruga juhudi zake kutatua matatizo yake? Ni kwa kiwango kikubwa sana, kiasi kwamba bila uingiliaji kati wa Mungu Mwenyezi katika mambo ya wanadamu, uhai wote wa wanadamu duniani ungeweza kufutika hivi karibuni—futiliwa mbali! Uchafu, upungufu wa chakula na maji, magonjwa na matumizi ya silaha za maangamizi yangewapelekea wanadamu kujikomesha. Kwa rehema, Mungu hataruhusu matukio kufikia huko. Kusudi lake kuu na mpango unatendeka vile vile kama ulivyopangwa na kwa wakati kuelekea mwisho wenye furaha na amani—kusuluhisha taabu zote za mwanadamu!

Lakini, kwa wakati huu, fokasi ya Mungu ya msingi ni juu ya Kanisa Lake—Kanisa la kweli—juu ya wale Aliowaita na kuwaunganisha na Roho Yake Takatifu na maarifa maalumu.

Sura ya Saba – Ni Wapi na Kwa nini Kanisa la Mungu la Kweli

Kumbuka mara nyingine tena ahadi ya Kristo, “Nitalijenga Kanisa Langu†(Math. 16:18). Haijalishi jinsi gani watu wanalifasiri, fungu hili linaongelea juu ya kanisa moja! Kristo aliendelea, “na milango ya kuzimu [kaburi] haitalishinda.†Aliahidi kwamba Kanisa Lake haliwezi kuharibiwa kamwe.

Zaidi ya mifumo ya makanisa 2,000 yanayodai kuwa ya Kikristo “yamejengwa†na watu, nchini Marekani pekee. Kanisa lingine linaanzishwa kila baada ya siku tatu. Makadirio yanaiweka idadi ya wanaodai kuwa Wakristo kufikia bilioni 2. Ingawa mahudhurio kanisani yanaonekana kuongezeka, hayaongezeki kwa kasi kama mkanganyiko ulioko juu ya swali la ni lipi kanisa sahihi.

Ingawa imesemwa, “Hawawezi kukosea wote,†ni sahihi zaidi kusema, “Hawawezi kuwa sahihi wote.†Ikiwa Kristo alijenga Kanisa Lake kama vile Alivyosema, basi linaweza kupatikana mahali fulani duniani leo—na ndilo Kanisa pekee lililo sahihi. Lakini lazima tuulize: Tutalipata vipi—ni kitu gani tutakitafuta—tutalitambua vipi—tutalijuaje iwapo tutaliona?

Mama yangu alinihitaji nisome vitabu vingi nilipokuwa nakua.Nilitumia majira mengi ya kiangazi nikitekeleza agizo lake la kusoma “kitabu kimoja kila juma.†Nilivifurahia vingi kati ya hivyo na ninashukuru kwamba alifanya hivi. Mara moja, au pengine mara mbili au tatu, nilichukua Biblia na kujaribu kuisoma. Lakini sikufika mbali, kwa sababu haikuleta maana kwangu. Kwa urahisi sikuielewa Biblia.

Licha ya kukosa ufahamu huu, nilipofika umri wa miaka kumi-na-sita, nilipewa “kipa imara†katika kanisa nililokuwa nimezaliwa. Ninakumbuka kuhudhuria kwa muda mfupi mbele ya baraza la “mashemasi†kujibu maswali kadhaa rahisi, ambayo siyakumbuki tena. Nakumbuka kuthibitisha kiujumla mambo fulani juu ya dhehebu hili, lakini pia nakumbuka kwamba nilikuwa sijali hata kidogo kama nilikuwa au sikuwa kwenye kanisa sahihi, au kama nilikuwa natimiza fasili ya Biblia ya Mkristo.

Hakuna swali lolote kati ya haya lililonivutia hata kidogo. Niliamini kwa juu juu tu kwamba Mungu yupo, lakini Hakuwa halisi kwangu. Kwa hakika sikuwahi jaribu kujenga uhusiano binafsi na Yeye au kulitafuta Kanisa Lake la kweli. Sikufanya maombi wala kujifunza Neno Lake kwa ajili ya kupata mwongozo au mafundisho na maadibisho. Mambo haya hayakuingia katika fikra zangu mpaka baada ya mwaka mmoja na nusu baadaye, katika mwaka 1966, niliposikia sauti kwenye redio iliyotambulisha kwangu kauli ya Kristo katika Mathayo 16:18. Nilianza kuuliza ni wapi naweza kulipata hili Kanisa la kweli. Mara ile niling’amua kwamba lilipasa kuwepo kwa sababu, kwa kusoma kwa kawaida tu kuanzia wakati huo, nilipata kuifahamu ahadi ya Kristo kwamba si tu kwamba Kanisa lingekuwepo, lakini lisingeweza kuharibiwa.

Mapokeo ya Wanadamu

Kumbuka Kristo alisema, “Nao waniabudu bure, Wakifundisha mafundisho Yaliyo maagizo ya wanadamu†(Math. 15:9). Katika maelezo sambamba ya kauli hii kwenye Marko, Aliendelea, “Vema! Mwaikataa amri ya Mungu mpate kuyashika MAPOKEO YENU†(7:9).

Ukristo wa ulimwengu umejawa na mapokeo. Mojawapo ya mapokeo makubwa zaidi ni mtazamo juu ya Kanisa la Agano Jipya. Wengi wa watumishi wa makanisa, wanateolojia na wanadini hufasili kanisa kwa namna hii: “Wale wote ambao wanaamini hasa katika Yesu Kristo kama Mwokozi wao wanaunda Kanisa la kweli.†Kauli hii mara nyingi hufuatiwa na usemi maarufu, “ziko njia nyingi kwenda mbinguni†au “kuna njukuti nyingi kwenye gurudumu la wokovu.†Japokuwa Biblia haifundishi kwamba mbinguni ni thawabu ya waliookolewa, mantiki ya wazi ya semi hizi ni kwamba watu wanaweza kuamini chochote wanachotaka, au kuwa miongoni mwa kundi lolote wanalochagua, na bado wakabaki kuwa Wakristo. Ijapokuwa watu wanaamini kwa dhati mapokeo ya hisia hizo, kwa unyofu hawako sahihi kabisa!

Utafiti wangu ulinipeleka hadi kwenye UTHIBITISHO thabiti wa ni-wapi lilipokuwa Kanisa ambalo Yesu aliahidi kulijenga. Nilijifunza kwamba Kanisa hili lingeweza kufuatiliwa kwa uangalifu kwa takribani miaka 2,000 ya historia ya Agano Jipya. Hakika nilishtushwa. Sikuamini Biblia ilikuwa wazi kabisa juu ya somo linalowakanganya wengi sana.

Biblia inatamka, “Kwa maana Mungu si Mungu wa machafuko, bali wa amani; vile vile kama ilivyo katika makanisa yote ya watakatifu [muktadha unaonyesha hii inarejelea kwa mikusanyiko yote ya Kanisa la kweli, si mashirika ya wanadamu]†(1 Kor. 14:33).

Kanisa la Mungu (lililoundwa na mikusanyiko mingi ya watakatifu) lilipaswa kuakisi amani—si mkanganyiko. Huhitaji kukanganyikiwa juu ya utambulisho wa Kanisa la kweli. Mungu alimvuvia Paulo kuandika, “jaribuni [thibitisheni] mambo yote; lishikeni lililo jema†(1 Thes. 5:21). Wakati kauli hii inarejelea mambo ya kimaandiko kwa wazi (si juu ya aina ya gari ya kuendesha au nyumba ya kununua), inasema kwamba “Mambo YOTE,†sio “baadhi ya mambo,†ndio lazima YATHIBITISHWE! Hakika Mungu asingezuia kitu chenye uzito mkubwa wa jinsi hii—umuhimu mkubwa wa jinsi hiyo—kama jambo linalohusu mahali linapopatikana Kanisa Lake la kweli. Na asingewaambia watu kwa msisitizo kuthibitisha mambo ambayo hayawezi kuthibitishwa!

Kadri nilivyojifunza mafundisho mengine ya Biblia, ndivyo nilivyojifunza makanisa ya ulimwengu huu hayakuwa sahihi—karibu kwenye KILA KITU! Andiko moja la wazi baada ya lingine lilipingana na kila wazo la mapokeo ya “Kikristo†niliyokuwa nimefundishwa. Nilishangazwa—kwa hakika niliduwazwa—jinsi ilivyokuwa rahisi kupata uthibitisho wa moja kwa moja, uliowazi, usiopingika kiasi kwamba hata mapokeo yaliyo maarufu sana ya madhehebu makubwa hayakujengwa juu ya Biblia—kabisa!

Kila wakati niliposoma fundisho la Biblia—wokovu, ubatizo, Mungu ni nani na nini, injili, mauti na jehanamu, sheria na dhambi, neema, kuzaliwa mara ya pili, Sabato ya Kikristo, asili ya kile kinachodhaniwa kuwa sikukuu za “Kikristoâ€, mahali yalipo leo makabila ya sasa ya Israeli ya kale, mfuatano wa matukio ya unabii yanayotangulia Kurudi kwa Kristo na mengine mengi—niliongeza uthibitisho usiopingika wa kile ambacho Biblia ilifundisha hasa! Nilisisimuka na kuvutiwa sana. Nilipata kujua kwamba makanisa ya ulimwengu huu kwa hakika yalikuwa yamekanganyikiwa juu ya yote haya na pointi zingine za wazi za mafundisho ya Biblia. Nilikuja kutambua kwamba lazima palikuwepo kanisa ambalo liliamini kwa usahihi na kutenda mafundisho yote ya Biblia.

Nilijifunza kwamba Kanisa hili lilikuwepo, na kwamba uthibitisho unaolitambulisha na kulitenga kutoka kwenye makanisa yote yanayotambuliwa, ya Ukristo wa kawaida haukuwa tofauti na uthibitisho wa fundisho lolote lingine la kibiblia. Pia nilijifunza kwamba upana wa uthibitisho—ujazo mwingi wa hoja—ulikuwa mkubwa sana, kiasi cha kustaajabisha katika wingi wake.

Kundi Dogo, Linaloteswa

Alipokuwa anaongea na wanafunzi Wake juu ya umuhimu wa kuutafuta ufalme wa Mungu, Kristo alisema, “Msiogope, enyi kundi dogo; kwa kuwa Baba yenu ameona vema kuwapa ninyi ule ufalme†(Luka 12:32). Makanisa yaliyo na mamilioni ya watu, achilia mbali idadi ya bilioni mbili, hayawezi kufikiriwa kuwa “kundi dogo†hata kwa upana wa kiasi chochote. Hivyo, Kanisa dogo la Kristo haliwezi kuonekana kwa urahisi.

Kristo alielewa kwamba Kanisa Lake—kundi Lake dogo—lingeudhiwa na kudharauliwa na ulimwengu. Muda mfupi tu kabla ya kusulubishwa Kwake, Alionya, “Likumbukeni lile neno nililowaambia, Mtumwa si mkubwa kuliko bwana wake. Ikiwa waliniudhi mimi, watawaudhi ninyi†(Yohana 15:20). Katika fungu lililotangulia, Yesu aliwakumbusha wanafunzi Wake kwamba “Mimi Naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia.†Kristo aliudhiwa, mpaka kufikia kusulubishwa vibaya baada ya usiku wa mateso makali ya kinyama. Kwa hivyo, Kanisa la kweli hutazamia kuudhiwa pia—na kuchukiwa! Wale walio ndani yake si “wa ulimwengu.†Ulimwengu unalitambua hili na huwachukia kwa ajili hiyo (Rum. 8:7). Kristo alimtumia Paulo kurekodi, “Naam, na wote wapendao kuishi maisha ya utauwa katika Kristo Yesu wataudhiwa†(2 Tim. 3:12). Neno “wote†linamaanisha kile lisemacho!

Fikiria kile ambacho tumemaliza kujadili. Ni makanisa mangapi unayoweza kutaja ambayo ni madogo, yanaudhiwa, si ya ulimwengu huu—na ambayo hata yanachukiwa kwa ajili hiyo? Yafikirie yale unayoyafahamu. Je, kuna lolote linalolingana na maelezo haya?

Hakika siyo mengi!

Umuhimu wa Jina la Kanisa

Makanisa ya ulimwengu yana idadi kubwa sana ya majina tofauti, yaliyopatikana kwa njia mbalimbali. Hii ni pamoja na mafundisho wanayofundisha, majina ya watu walioyaanzisha, aina ya serikali ya kanisa iliyobuniwa-kibinadamu inayofuatwa, mahali yalipo, au upana na ukubwa uliokusudiwa, kama vile – ulimwengu [mahali pote] au katoliki, hili la mwisho likiwa na lengo la kufikiriwa kana kwamba linafunika mahali kote.

Usiku ule wa kusalitiwa Kwake, Kristo aliliombea Kanisa Lake. Hiki hapa ndicho alichosema: “Baba Mtakatifu, kwa JINA LAKO, MWENYEWE uwalinde hao Ulionipa, ili wawe na umoja kama sisi Tulivyo. Nilipokuwapo pamoja nao, Mimi naliwalinda KWA JINA LAKO…Mimi nimewapa neno Lako; na ulimwengu umewachukia; kwa kuwa wao si wa ulimwengu, kama Mimi nisivyo wa ulimwengu. Mimi siombi kwamba Uwatoe katika ulimwengu; bali Uwalinde na yule mwovu. Wao si wa ulimwengu, kama Mimi nisivyo wa ulimwengu. Uwatakase kwa ile kweli; neno Lako ndiyo kweli†(Yohana 17:11-12, 14-17).

Kuna maeneo kumi-na-mawili tofauti ambapo Agano Jipya linarekodi kwamba Kanisa la kweli limelindwa katika Jina la Baba—Mungu. Matano hurejelea kwa Kanisa zima, au mwili wa Kristo, katika ujumla wake. Mengine manne huongelea mkusanyiko mahali maalumu dhahiri, huku yakitumia mtajo ule ule “Kanisa la Mungu.†Hii inaweza kurejelea kwa Kanisa la Mungu huko Uyahudi au Korintho, n.k. Vielelezo vingine vitatu huongelea juu ya kila mkusanyiko katika mahali maalumu ikiunganishwa kwa pamoja. Vielelezo hivi vyote vinatumia usemi “Makanisa ya Mungu†(Matendo 20:28; I Cor. 1:2; 10:32; 11:16, 22; 15:9; 2 Kor. 1:1; Gal. 1:13; I Tim. 3:5, 15; 1 Thes. 2:14; 2 Thes. 1:4).

Katika zama hizi, kwa sababu za ushirika, Kanisa linaweza kutumia jina lingine kielelezo kujitofautisha na “Makanisa ya Mungu†mengine—yale ambayo hujipachika tu jina la Mungu, lakini hayatii amri Zake, hayaamini mafundisho Yake ya kweli au kutenda Kazi Yake. Herbert W. Armstrong, kiongozi wa Kanisa katika karne ya ishirini, alichagua jina Kanisa la Mungu la Ulimwengu Mzima na kabla ya hapo, Redio Kanisa la Mungu. Tumechagua jina Kanisa la Mungu Rejeshwa.

Kama vile madhehebu mbalimbali ya walio wengi yanaweza kuwa na mafundisho machache sahihi yaliyochanganyika na makosa mengi, vivyo hivyo baadhi yanajipachika yenyewe jina la Kanisa la Mungu. Kitabu hiki baaadaye kitaelezea ni kwanini baadhi ya makanisa machache yanaweza hata kuwa na kiasi kikubwa cha ukweli, lakini yanachagua kukubali mafundisho mbalimbali ya uongo. Ni kanisa moja tu juu ya uso wa dunia lililo na jina sahihi na linafundisha mafundisho ya kweli na mengi ya ziada ambayo Biblia inafundisha! Tunasoma jinsi ambavyo Kristo aliomba katika Yohana 17, “Uwatakase kwa ile KWELI; neno Lako ndiyo KWELI.†Kanisa ambalo Kristo analitumia, kulielekeza na kuliongoza limetakaswa—limetengwa [wekwa wakfu]—kwa imani yake ya ukweli dhahiri wa Neno la Mungu!

Tukipitia upya, pamoja na kubeba jina “Kanisa la Mungu,†tumeona pia kwamba Kanisa la Mungu limetoka ulimwenguni, ni dogo na linaudhiwa, hata kiwango cha kuchukiwa nao. Kisha Kanisa hili pia limetengwa kutoka ulimwenguni kwa IMANI na MATENDO yake—ambayo yanakubaliana kikamilifu na ukweli wa Biblia!

Kuunganishwa Kupitia kwa Neno la Mungu

Wanadamu wana fasili zao zinazotofautiana kuhusu nini hasa ni Kanisa, lakini ni fasili ya Biblia pekee—fasili ya Mungu—iliyo muhimu. Jisomee mwenyewe. Paulo alimwandikia mwinjilisti Timotheo, “…upate kujua jinsi iwapasavyo watu kuenenda katika nyumba ya Mungu, iliyo kanisa la Mungu aliye hai, nguzo na msingi wa KWELI†(1 Tim. 3:15). Mwishoni, hakuna fasili nyingine, iliyobuniwa na wanadamu, inakubalika. Fasili hii ya Kanisa la kweli ambalo Kristo alilijenga itatuongoza katika sehemu yote iliyobaki ya sura hii. Kanisa la Mungu linao na linafundisha “ukweli.â€

Tumejadili jinsi makanisa ya ulimwengu huu yalivyo katika mkanganyiko, mgawanyiko kwa kutoafikiana bila kikomo juu ya mafundisho na utendaji. Amosi 3:3 inauliza, “Je! Watu wawili waweza kutembea pamoja, wasipokuwa wamepatana?†Jibu ni HAPANA!

Makanisa ya ulimwengu huu hayatekelezi kanuni ya “mtu hataishi kwa mkate tu, ila kwa kila neno la Mungu†(Luka 4:4), sawasawa kama ilivyoandikwa. Badala yake, kwa kuwa wanafuata mapokeo mengi ya wanadamu yanayotofautiana, kutoafikiana kusiko na mwisho kunawatenganisha, kuwagawa na wanaunda makanisa mengi zaidi na zaidi ya wanadamu. Kwa ujumla “hayatembei pamoja,†kwa sababu “hayakubalianiâ€â€”ama yenyewe kwa yenyewe au na Mungu!

Kanisa la Mungu liko tofauti. Mafungu mengi ya Agano Jipya yanaonyesha kwamba Kanisa ambalo Kristo alijenga limeungana—huku washiriki wake wote na mikusanyiko yote wakitembea pamoja katika mwafaka kamili kila mmoja na mwenzake, na pamoja na Mungu na Kristo.

Pointi ya muhimu, inayodhihirisha umoja wa Kanisa la kweli, inajitokeza katika ombi la Kristo katika Yohana 17, katika usiku wa kusalitiwa Kwake. Aliomba, “Na kwa ajili yao najiweka wakfu mwenyewe, ili na hao watakaswe [watengwe] katika kweli… Wote wawe UMOJA; kama Wewe, Baba, ulivyo ndani Yangu, Nami ndani Yako; hao nao wawe UMOJA ndani Yetu: ili ulimwengu upate kusadiki ya kwamba Wewe ndiwe Uliyenituma. Nami utukufu ule Ulionipa Nimewapa wao; ili wawe UMOJA kama sisi Tulivyo UMOJA: Mimi ndani yao, Nawe ndani Yangu, ili wawe wamekamilika katika UMOJA; ili ulimwengu ujue ya kuwa Ndiwe Uliyenituma, ukawapenda wao kama Ulivyonipenda Mimi†(fu. 19, 21-23).

Hizi ni kauli nzito! Kristo alikusudia kwamba Kanisa Lake liwe limeungana—“mojaâ€â€”si pungufu ya walivyokuwa Yeye na Baba! Hakuna nafasi ya kutokubaliana katika Kanisa ambalo limeungana kiasi hiki. Mafungu haya yanaelezea umoja kamili kwa njia ya ile kweli—umoja ule ule ambao Baba na Kristo wanaufurahia. Ni aina hii ya umoja unaowawezesha Wakristo wa kweli kuwa “ndani†yao—kuwa ndani ya Kristo na Baba (fu. 21).

Hata katika Agano la Kale, Daudi alivuviwa kurekodi, “Tazama, jinsi ilivyo vema, na kupendeza, Ndugu wakae pamoja, kwa UMOJA†(Zab. 133:1).

Sasa lazima tuchunguze aya kadhaa katika Agano Jipya ili tuone kama, kwa hakika, aina hii ya umoja wa ajabu ulikuwa dhahiri baada ya Kanisa la Agano Jipya kuanza kwa kweli. Je, watumishi wa kweli wa Mungu walifundisha na kusimamia aina hii ya upatanifu?

Katika siku ya Pentekoste, wakiwa wamekusanyika katika “moyo mmoja†(Matendo 2:1), Wakati Kanisa la Agano Jipya lilipoanza kuwepo, waongofu 3,000 walibatizwa. Wakawa ule mwanzo kabisa wa Kristo kujenga Kanisa Lake. Maelezo ya kwanza kabisa yaliyotolewa yalikuwa “…Wakawa wakidumu katika FUNDISHO LA MITUME, na KATIKA USHIRIKA†(fu. 42), “…wote walioamini walikuwa pamoja†(fu. 44) na “…siku zote kwa moyo mmoja… na kushiriki chakula chao kwa furaha na kwa moyo mweupe†(fu. 46).

Kutoka kwa mafungu haya tunaona wazi ya kwamba Kanisa ambalo Kristo alijenga lilianza katika umoja—mwafaka!—juu ya mafundisho, na kuwa pamoja. Sasa fungu la 47: “Bwana akalizidisha kanisa kila siku kwa wale ambao yapasa waokolewe.†Katika Kanisa ambalo Yesu Kristo wa kweli huongoza na kuelekeza, Yeye ndiye Yule aliongezaye, akilijenga!

Paulo Alikazia Umoja

Mengi yanaweza kueleweka kwa kuchunguza maelekezo ya Paulo kwa mikusanyiko mbalimbali aliyokuwa akisimamia.

Mkusanyiko wa Wakorintho ulikuwa na matatizo mengi—ikiwa ni pamoja na mgawanyiko wa kuogofya [tisha] na mafarakano. Paulo aliwaonya kwa nguvu kuacha kukubaliana na mafundisho mengine na kukoma kupendelea watendakazi. Angalia: “Basi ndugu, nawasihi…kwamba nyote mnene mamoja; wala pasiwe kwenu faraka, bali mfungamanishwe pamoja kikamilifu katika nia moja na shauri moja. Basi, maana yangu ni hii…kila mtu wa kwenu kusema, Mimi ni wa Paulo, na, Mimi ni wa Apolo, na, Mimi ni wa Kefa [Petro], na, Mimi ni wa Kristo. Je! Kristo amegawanyika?†(1 Kor. 1:10, 12-13).

Usikose kujua kusudi la aya hii. Paulo alivuviwa kueleza, katika njia tano tofauti, jinsi ambavyo watu wa Mungu katika zama zote wangepaswa kuungana na kuwa katika mwafaka. Na mafungu haya hayawezi “kusemwa kuwa yana tafsiri fasiri ya kiroho†kwa udanganyifu wa kufikiri kibinadamu.

Baadaye, katika barua hiyo hiyo kwa Wakorintho, Paulo alirekodi kwamba Kanisa lilikuwa na washiriki wengi (ndugu), bado walikuwa kama sehemu mbalimbali za mwili wa binadamu, katika maana kwamba washiriki hawa walikuwa wameunganishwa. Kwa makini jifunze sura ya 12. Mafungu ya 12 hadi 14 yanasema, “Maana kama vile mwili ni MMOJA, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya mwili ule MMOJA, navyo ni vingi, ni mwili MMOJA: vivyo hivyo na Kristo. Kwa maana katika Roho MOJA sisi sote tulibatizwa kuwa mwili MMOJA…Kwa maana mwili si kiungo kimoja, bali ni vingi.â€

Muktadha unatumia mfano wa mikono, miguu, macho, masikio na mdomo kuonyesha jinsi viungo tofauti vya mwili wa mwanadamu vimeunganishwa ndani ya mtu huyo huyo mmoja. Paulo anaendelea, “Bali Mungu amevitia viungo kila kimoja katika mwili kama alivyotaka. Lakini kama vyote vingekuwa kiungo kimoja, mwili ungekuwa wapi? Lakini sasa viungo ni vingi, ila mwili ni MMOJA†(fu. 18-20).

Mafungu haya pia hayawezi kusemwa kuwa “yana fasiri ya kiroho†kwa kufikiri kibinadamu. Hayaelezei kile kinachodhaniwa kuwa “mwili†wa “kirohoâ€, usiounganishwa, wa watu na mashirika yote yasiyopatana ya unaojiita “Ukristo.†Mguu wowote, jicho au sikio vinapotolewa kutoka kwa mwili wa mwanadamu hufa! Hakuna kiungo kilichokatwa kinachoweza kukaa kwa muda mrefu bila mtiririko wa damu na tishu-unganishi vilivyo muhimu kukiunga kwenye mwili. Mungu aliuumba mwili wa mwanadamu, Hivyo ni wazi anaufahamu mfano ambao aliuvuvia. Tutarudi kwa jambo hili baada ya muda mfupi.

Kwa uthibitisho zaidi wa maana ya mwili, fikiria maandiko mawili zaidi, yaliyoandikwa kwa mikusanyiko miwili tofauti chini ya uongozi wa Paulo.

Angalia maelezo yake kwa mkusanyiko wa Wakolosai: “Naye [Kristo] ndiye kichwa cha mwili, yaani, cha Kanisa†(1:18). Fasili ya Biblia ya mwili wa Kristo ni sawa sawa na ya Kanisa! Paulo aliwaonya Wakolosai wawe “wakiunganishwa pamoja katika upendo, na…uhakika kamili wa ufahamu,†wenye “shina na wenye kujengwa katika Yeye; na muwe imara katika ile imani, kama mlivyofundishwa†(2:2, 7). Hakuna kutoelewa isivyo katika umoja kamili ambao Paulo anauelezea hapa. Ndugu wanatembea “pamoja,†wakiwa na uhakika wa “ufahamu†sahihi “waliofundishwa.â€

Sasa angalia mafundisho yake kwa mkusanyiko wa Waefeso. Akiongelea juu ya mambo ambayo Mungu aliyaweka chini ya mamlaka ya Kristo, Paulo aliandika, “…akamweka [Kristo] awe kichwa juu ya vitu vyote kwa kanisa; ambalo ndilo mwili Wake†(1:22-23). Katika sura ya 4, Paulo aliwaonya Waefeso waweze “kujitahidi kuuhifadhi umoja wa Roho katika kifungo cha amani. Kuna MWILI MMOJA [Kanisa], na Roho MOJA, kama na mlivyoitwa katika tumaini MOJA la wito wenu. Bwana MMOJA, imani MOJA, ubatizo MMOJA. Mungu MMOJA, naye ni Baba†(3-6). Tena, hapatakiwi kuwa na kukanganya umoja na mwafaka huu ambao aya hii inautaka kwa watu wa Mungu. Kumbuka jinsi Kristo alivyoomba kwa ajili ya aina hii ya kuwa mmoja na umoja.

Mafungu machache baadaye, Paulo alielezea umuhimu wa watendakazi waaminifu, daima wakitenda kazi pamoja na kufundisha Kanisa la Kristo. Soma kwa uangalifu [makini] na kuelewa aya ndefu ifuatayo, ambayo ni muhimu: “Naye alitoa wengine kuwa mitume, na wengine kuwa manabii; na wengine kuwa wainjilisti na wengine kuwa wachungaji na waalimu; kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe: hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika kwenye cheo cha kimo cha utimilifu wa Kristo: ili tusiwe tena watoto wachanga, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu; lakini tuishike KWELI katika upendo na kukua hata tumfikie Yeye katika yote, Yeye aliye Kichwa, Kristo: katika Yeye mwili wote ukiungamanishwa na kushikanishwa kwa msaada wa kila kiungo, kwa kadiri ya utendaji wa kila sehemu moja moja, huukuza mwili upate kujijenga wenyewe katika upendo†(fu. 11-16).

Kanisa ni Mwili wa Kristo na, akiwa Kichwa chake, Analitawala, kuliongoza na kulijenga, akiliongeza kila siku. Mafungu haya yanalielezea kwamba LIMEUNGAMANISHWA katika ukweli wa mafundisho na upendo. Katika usemi baada ya usemi, aya hii inathibitisha kuwa Kanisa lote (“mwili woteâ€na “kila sehemu yakeâ€) lazima liwe linatembea pamoja katika mwafaka mkamilifu wa mafundisho ya kweli chini ya mamlaka ya Kristo. Na Yeye hutenda kazi kupitia kwa watumishi Wake wa kweli ili kulitunza Kanisa lisichukuliwe na “kila upepo wa mafundisho [mengine].â€

Sasa fikiria onyo la Paulo kwa mkusanyiko wa Wafilipi: “… mnasimama imara katika roho MOJA, kwa moyo MMOJA mkiishindania imani ya injili; wala hamwaogopi adui zenu†(1:27-28). Na, “ijalizeni furaha yangu, ili mwe na nia moja, wenye mapenzi mamoja, wenye upatano MMOJA, mkinia MAMOJA†(2:2). Aya hizi zinafundisha kuwa umoja kamili katika kanisa ndilo sharti pekee linalokubalika kwa Mungu!

Mkusanyiko wa eneo la Warumi ulikuwa na matatizo kuhusu mafundisho ya uongo yaliyokuwa yanaingia Kanisani. Angalia jinsi Paulo alivyowaagiza kushughulikia hii: “Ndugu zangu, nawasihi, waangalieni [chukulia maanani] wale wafanyao FITINA na mambo ya kukwaza kinyume cha mafundisho mliyojifunza; MKAJIEPUSHE NAO. Kwa sababu walio hivyo…kwa maneno laini na ya kujipendekeza waidanganya mioyo ya watu wanyofu†(16:17-18).

Kuulinda Umoja

Hii ni lugha nzito. Lakini inathibitisha jinsi ilivyo muhimu kwa Mungu kwamba watu Wake wasipotee kutoka kwa ukweli na kufuata mafundisho na mapokeo yaliyobuniwa na wanadamu.

Petro pia alifundisha hitaji muhimu sana la muungano kwa Kanisa na umoja. Aliandika, “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu†(1 Pet. 2:9). Semi nne katika fungu hili ziko katika umoja—zikimaanisha moja, siyo kadhaa, kwa kila neno lililorejelewa. Kwa mfano, kama taifa limegawanyika katika mataifa kadhaa, hakuna mtu ambaye angelifikiria kuwa ni taifa moja—yangekuwa mataifa mengi, siyo taifa “mojaâ€. Vivyo hivyo ni kweli kwa Kanisa la Mungu.

Liko moja tu!

Pia, Kristo Mwenyewe alifundisha hili juu ya suala la umoja kwa Kanisa: “Kila ufalme ukifitinika juu ya nafsi yake, hufanyika ukiwa; tena mji au nyumba yo yote ikifitinika juu ya nafsi yake, haitasimama [baki]†(Math. 12:25). Kumbuka kwamba Paulo aliuliza katika 1 Wakorintho 1:13, “Je! Kristo amegawanyika?†Hili ndilo jibu la KRISTO. Agizo lake hata linashangaza zaidi pale msomaji anapofikiria kwamba anauelezea ufalme wa Shetani katika maelezo haya! Yesu alifundisha kwamba hata ibilisi ni makini kiasi cha kujua kwamba ufalme wake hauwezi kugawanyika na ukabaki! Bila shaka Mungu mkuu wa mbinguni na Yesu Kristo angalau wana akili kama Shetani aliye mwovu. Bila shaka, wao ni wenye hekima isiyo na kikomo! Wote wanafahamu kwamba Kanisa lao pia haliwezi kuwa limegawanyika na litarajie kudumu (“kusimamaâ€).

Maonyo kwa Kanisa

Baada ya mitume wa kwanza kufariki, lile kanisa kubwa la uongo la ulimwengu wote liliingia ulingoni na kwa kiasi kikubwa kuliharibu Kanisa linaloonekana. Kwa sababu ya mateso, mara nyingi yakijumuisha vitisho, vifungo, mateso na kifo, watu wengi walikubali kushindwa na wakauacha ukweli wa Njia ya Mungu na kwa hiyo kutoka kwa Kanisa la kweli. Mara nyingi kipindi hiki kinaitwa “Karne Iliyopotea.†Bado, kama vile Kristo alivyoahidi, Kanisa Lake daima limedumu. Halijawahi kupotea au kuharibiwa—ingawa kwa hakika limebaki kuwa “kundi dogo†ambalo limetunza Neno Lake, na Kanisa ambalo siku zote limelindwa katika jina la Mungu.

Petro alionya, “Lakini kuliondokea manabii wa uongo katika wale watu, kama vile kwenu kutakavyokuwako waalimu wa uongo, watakaoingiza kwa werevu uzushi wa kupoteza, wakimkana hata Bwana aliyewanunua, wakijiletea uharibifu usiokawia. Na wengi watafuata ufisadi wao; na kwa hao njia ya kweli itatukanwa. Na katika kutamani watajipatia faida kwenu kwa maneno yaliyotungwa†(2 Pet. 2:1-3).

Kabla ya kifo chake, Paulo aliwaonya wazi wazi wazee wa Waefeso kuelewa kile ambacho kingetokea baada ya kuondoka kwake. Angalia: “Jitunzeni nafsi zenu, na lile kundi lote nalo, ambalo Roho Takatifu imewaweka ninyi kuwa waangalizi ndani yake, mpate kulilisha Kanisa lake Mungu… Najua mimi ya kuwa baada ya kuondoka kwangu mbwa-mwitu wakali wataingia kwenu, wasilihurumie kundi; tena katika ninyi wenyewe watainuka watu wakisema mapotovu, wawavute hao wanafunzi wawaandamie wao†(Matendo 20:28-30). Historia imerekodi kwamba hiki ndicho kilichotokea hasa wakati wa (na baada ya) Karne Iliyopotea.

Tunasoma kwamba Kristo aliahidi kwamba wakati viongozi wa uongo, aliowarejelea kwenye Yohana 10 kama “wevi na wanyang’anyi,†wanapoweza kuingia Kanisani, “kondoo wanaisikia SAUTI Yake [Kristo]: na Huwaita kondoo Wake kwa majina yao, na huwapeleka nje.†Sauti Yake imefasiliwa wazi katika Maandiko kama “kweli†(Yohana 18:37).

Aliendelea mbele katika Yohana 10 kuongeza, “Naye awatoapo nje kondoo Wake wote, Huwatangulia; na wale kondoo humfuata, kwa maana waijua SAUTI Yake. Mgeni hawatamfuata kabisa, bali watamkimbia; kwa maana hawazijui sauti za wageni†(fu. 3-5). Kristo anaendelea kwa kuelezea watumishi fulani: “Yule hukimbia kwa kuwa ni mtu wa mshahara; wala mambo ya kondoo si kitu kwake†(fu. 13). Ahadi hii ya pekee inaonyesha kwamba kamwe Kristo hatawaacha kondoo Wake na daima atawalinda wale wanaosikia sauti Yake na kwa hiari wanamfuata wanapokuwa katika hatari ya mafundisho ya uongo!

Kanisa la Mungu halifanyi maafikiano juu ya hata moja ya mafundisho Yake ya kweli. Kama vile Kristo alivyotabiri, ni dogo, linalochukiwa na kuteswa “kundi dogo†ambalo Mungu amelilinda katika jina Lake. Linatenda Kazi ya Mungu—likipeleka injili ya kweli ya ufalme wa Mungu kwa ulimwengu kabla zama hii haijaisha. Matunda yake ni ishara ya mibaraka ya Mungu. Linakua na lina washiriki waliotawanyika katika nchi mbalimbali duniani kote. Ukweli kwamba unasoma kitabu hiki ina maana kwamba umekutana nalo—sawa kama mimi nilivyobahatika kukutana na Kanisa la kweli na kujifunza ukweli katika mwaka 1966 kwa mara ya kwanza.

Kanisa ni Mwili Uliopangika

Mungu anawataka watoto Wake walielewe kusudi Lake. Ametoa analojia [kifanani] ya msingi ambayo ni rahisi kueleweka. Analinganisha Kanisa Lake moja—Kanisa Lake la kweli—na mwili wa mwanadamu. Tumemaliza kusoma kwamba “Maana kama vile MWILI NI MMOJA, nao una viungo vingi, na viungo vyote vya MWILI ule MMOJA, navyo ni vingi, ni MWILI MMOJA; vivyo hivyo na Kristo. Kwa maana katika Roho moja sisi sote tulibatizwa kuwa MWILI MMOJA...†(1 Kor. 12:12-13).

Wakolosai 1:18 na Waefeso 1:22-23 yalifunua kwamba “mwili†unamaanisha Kanisa.

Liko Kanisa moja tu na, kama ulivyo mwili wa mwanadamu, viungo vyote vimeungana. Kichwa, macho, masikio, vidole vya mikono, vidole vya miguu, mikono na miguu ni tofauti lakini ni-viungo vilivyoungana vya mwili wa mwanadamu.

Angalia, tena, kile ambacho Paulo aliongeza katika sura ya 12: “Basi NINYI mmekuwa mwili wa Kristo, na viungo kila kimoja peke yake. Na Mungu ameweka wengine katika Kanisa, wa kwanza mitume, wa pili manabii, wa tatu waalimu…†(fu. 27-28). Kanisa limepangika, limeundwa—lina SERIKALI ya Mungu!

Kiwango cha Mungu Ndoa na Familia—Kanisa

Katika Agano Jipya lote, Mungu amejitanabaisha Mwenyewe kama Baba mwenye “watoto†wengi—wale walio wa Kanisa Lake. Wakati wote Kristo aliirejelea Nafsi ile nyingine katika Uungu kama “Baba.†Alielewa kwamba Alikuwa “Mwana.†Sasa kwa kuwa Kristo, si mwanadamu tena (Rum. 1:1, 3), amefufuliwa kutoka kwa wafu, Amefanyika Mwana wa Mungu (fu. 4; Ebr. 1:8). Soma kwa uangalifu [makini] Warumi 1:1-4 uone kwamba kwa hakika, Kristo alikuwa mzao wa Daudi—mwanadamu wa nyama—kupitia mama Yake.

Kristo alikuwa na mama aliye mwanadamu, Mariamu. Ana Baba aliye Roho. (Kwa hakika, Yusufu hakuwa baba Yake hasa.)

Fikiria kwa kitambo! Mungu alikuwa mzazi wa kiume wa Kristo katika tumbo la mwanamke aliye mwanadamu. Hii si kauli ya kawaida kueleweka. Pata maana yake hasa: Namna ya Mungu (Baba) huzaa kama ilivyo kwa namna zingine. Mungu alichagua bikra mwanadamu (yeye aliyeumbwa katika “sura na mfano Wakeâ€) kumzaa Mwanae. Wala, kwa namna yoyote hii haikuwa “kinyume,†kwa sababu Mungu alikuwa hazaliani nje ya namna Yake. Kumbuka, Mungu aliamuru kwamba wanyama na binadamu wote—viumbe vyote vyenye uhai—vizaliane kwa “namna yake†(Mwa. 1:25). Uzaaji wa Baba (roho) wa Kristo ndani ya mwanadamu (mwenye mwili) hukataa ufafanuzi wa aina nyingine.

Baada ya kifo Chake na Kufufuka, na kurudi kuwa nafsi Roho, Kristo alifanyika “mzaliwa wa kwanza (Mwana) kutoka kwa wafu†(Kol. 1:18). Alipata kuzaliwa mara ya pili katika Familia ya Mungu—kwa ule Ufufuo. Warumi 1:4 inasema kwamba Kristo alikuwa “Mwana wa Mungu…kwa ule ufufuo kutoka kwa wafu.†Hiki ndicho kilimfanya Kristo kuwa Mwana. Na inawakilisha jinsi wanadamu wanavyookolewa.

Mafungu mengi yanaonyesha kwamba Kristo ni Mungu. Ni Mwana wa kiungu, mwanakaya [memba] wa Familia ya kiungu ya Mungu. Waebrania 1:8 inaliweka jambo hili wazi. Hapo, Baba anamrejelea Mwanae—Kristo—kama Mungu. Angalia: “Kiti chako cha enzi, Mungu [Kristo], ni cha milele na milele.†Elewa mafungu haya. Kristo ni Mwana aliyezaliwa kwa ufufuo kutoka kwa wafu.

Hebu tuunganishe ufahamu huu moja kwa moja kwa Kanisa.

Kristo Kuoa Kanisa

Hatima ya mwisho ya Kanisa ni nini? Nini hasa kinatokea mara baada ya ufufuo wa wafu? Jibu linaduwaza. Lakini kwanza lazima tufasili ni akina nani na nini hasa walio memba wa Kanisa.

Rudi kwa Warumi 8 na sasa soma fungu la 9: “Lakini ikiwa Roho ya Mungu inakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho, kama ndivyo kwamba Roho ya Mungu inakaa ndani yenu. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho ya Kristo, huyo si Wake.†Kuwa Mkristo, ni lazima mtu awe na Roho ya Mungu. Ni rahisi hivyo tu.

Kumbuka kwamba 1 Wakorintho 12:13 inafunua kwamba memba wote wa Kanisa “wanabatizwa katika mwili mmoja.†Kubatizwa inamaanisha kuzamishwa, kuwekwa ndani ya. Kwa hiyo, Mkristo anawekwa ndani ya Kanisa la Mungu kwa kupokea Roho Takatifu. Roho hii humfanya awe mwana aliyetungwa. Wale wasio na Roho ya Mungu, bila kujali kanisa au dhehebu walimo, hao “si Wake.â€

Tumekwisha kuona kwamba wale wote waliotungwa kwa Roho wanakuwa “warithi†wa wokovu (Rum. 8:17).

Lakini yako maarifa mengine muhimu ya kufahamu. Yanaungana moja kwa moja na kusudi la ndoa na familia ya mwanadamu. Namna ambavyo mwanamume anavyompenda, na kutenda kazi na kumwongoza mke wake inakusudiwa kuwa mfano wa uongozi wa Kristo juu ya Kanisa Lake. Agano Jipya kwa hakika linatambulisha Kanisa kama BIBI HARUSI mtarajiwa. Mafungu mengi yanafunua hili.

Kwanza, angalia mfanano ufutao baina ya Kristo na Kanisa Lake, na wanadamu waume na wake zao: “Kwa maana mume ni kichwa cha mkewe, kama Kristo naye ni kichwa cha Kanisa…Apate kujiletea Kanisa tukufu, lisilo na ila wala kunyanzi wala lo lote kama hayo; bali liwe takatifu lisilo na mawaa†(Efe. 5:23, 27).

Biblia inafunua kwamba uhusiano wa MUME aliyeongoka na mke wake ni mfano wa uhusiano wa KRISTO kwa Kanisa! Kristo anatenda kazi pamoja na Kanisa Lake namna ile ambayo waume wanapaswa kutenda kazi pamoja na wake zao. Anakusudia “kujiletea [Kanisa] Mwenyewe,†katika sherehe ya ndoa, wakati, madoa yote, makunyanzi na mawaa yakiwa yameondoka. Lakini sherehe hii ya ndoa itafikiwa tu na wale wanaojifunza masomo ya maisha haya—wale wanaopata uzoefu kupitia mateso na kujenga tabia sasa!

Baada ya Kristo kurudi na kusimamisha tena serikali ya Mungu (Ufu. 19:11-16), Anakuwa Mtawala na Kiongozi mkuu juu ya mataifa yote duniani, pamoja na Kanisa Lake. Angalia: “Malaika wa saba akapiga baragumu; pakawa na sauti kuu katika mbingu, zikisema, Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo Wake; Naye atamiliki hata milele na milele†(Ufu. 11:15).

Lakini hii siyo yote. Mara ile, hapo Anaporudi, hiki ndicho Kristo anachokifanya: “Nikasikia sauti kama sauti ya makutano mengi…ikisema, Haleluya; kwa kuwa Bwana Mungu wetu, Mwenyezi, amemiliki. Na tufurahi, tukashangilie, tukampe utukufu Wake; kwa kuwa ARUSI ya Mwana-Kondoo imekuja, na MKEWE amejiweka tayari. Naye amepewa kuvikwa kitani nzuri, ing'arayo, safi; kwa maana kitani nzuri hiyo ni matendo ya haki ya watakatifu. Naye akaniambia, Andika, Heri walioalikwa KARAMU YA ARUSI ya Mwana-Kondoo…†(Ufu. 19:6-9).

Bila shaka, Mwanakondoo wa Mungu wakati wote amekuwa ni Yesu Kristo (Yohana 1:29, 36; Ufu. 5:6).

Sasa elewa kikamilifu maarifa haya ya kustaajabisha: Kristo ni Mungu. Yeye ni wa “namna ya Mungu.†Kama ilivyo kwamba Mungu na Kristo wasingeweza kuzaliana nje ya namna yao wenyewe (Mwa. 1:24-26), sawa kama ilivyo kwa mnyama yeyote asivyoweza kuzaliana na mnyama wa namna nyingine, kadhalika Kristo asingeweza kuoa nje ya Namna ya Mungu.

Wakati wa Kurudi Kwake, katika moja ya matukio ya kustaajabisha sana katika historia yote, Kristo ATAOA KANISA LAKE! Huu ni ukweli dhahiri kutoka Neno la Mungu—na umekwisha kuuona!

Kristo Alioa Israeli ya Kale

Makubaliano ya Agano la Kale kati ya Kristo na Israeli ya kale kwa hakika yalikuwa ni makubaliano ya ndoa, au agano.

Katika Yeremia 3:14, Mungu aliwaambia Israeli, “maana Mimi ni mume wenu.†Japokuwa baadaye Alimtaliki (3:8) kwa sababu ya kutokuwa mwaminifu, ndoa ilibaki mpaka kifo cha Kristo.

Ndoa ya Kristo na talaka kutoka kwa, Isareli ya kale ilifuata sheria ya Agano la Kale—ona Ezekieli 16:38 na Kumbukumbu la Torati 24:1.

Sasa fahamu tena kwamba Israeli ya kale kwa hakika ilikuwa ndilo Kanisa la Agano la Kale. Mahali pengi kwenye Agano la Kale hulirejelea kama “kusanyiko la Israeli.†Matendo 7:38 huirejelea Israeli kama “kanisa jangwani.†Majina haya yana maana ile ile. Neno “kanisa,†katika Matendo 7:38, na “kanisa,†lililoelezewa katika Mathayo 16:18, ni neno lile lile katika Kigiriki.

Agano Jipya liko tofauti, katika mantiki kwamba linahusisha ahadi za kiroho, zenye kuhusiana na NEEMA, sio MBARI tu. Pamoja na hayo, Mataifa (wale wa mbari zingine) waliruhusiwa kuwa sehemu ya Israeli ya kale, lakini tu kwa sharti kwamba walitunza sheria, amri na hukumu zilizotawala nchi.

Kanisa—Israeli ya Kiroho

Ndoa zote hufika mwisho pale mmoja wa wanandoa anapokufa. Kwa suala la Israeli ya Kale, ndoa yake ilikwisha—haikuwepo tena—kwa sababu Kristo kupitia dhabihu Yake, alikufa. Baada ya Kufufuka Kwake, Kristo sasa alikuwa huru—anayestahili—kuoa upya.

Kanisa la Agano Jipya leo bado ni Israeli—isipokuwa Yeye ni wa kiroho, si wa kimwili, kiasili. Vile vile hafungwi kwenye mbari fulani ya watu.

Hiki hapa ni kile ambacho Paulo aliliandikia kusanyiko la Waefeso, ambalo karibu lote lilikuwa la watu wa Mataifa: “Kwa ajili ya hayo kumbukeni ya kwamba zamani ninyi, mlio watu wa Mataifa kwa jinsi ya mwili…kwamba zamani zile mlikuwa hamna Kristo, mmefarakana na jamii ya Israeli…Lakini sasa, katika Kristo Yesu, ninyi mliokuwa mbali hapo kwanza mmekuwa karibu kwa damu yake Kristo…sasa ninyi si wageni wala wapitaji, bali ninyi ni WENYEJI pamoja na watakatifu, watu wa NYUMBANI MWAKE MUNGU (2:11-13, 19).

Dhabihu ya Kristo ilikuwa kwa ajili ya ulimwengu wote (Yohana 3:16). Hii inajumuisha Mataifa, ambao ndio wengi mno, watu wenye idadi kubwa duniani. Waisraeli wengi wa kimwili, kwa wakati huu, na pamoja na ulimwengu, wamekatwa kutoka kwa Mungu kwa sababu ya dhambi. Bado hawajajumuishwa kwenye Israeli ya kiroho—Kanisa.

Wagalatia ambao walikuwa watu wa Mataifa pia walielewa kwamba walikuwa wamejumuishwa katika Israeli ya kiroho. Angalia: “Na kama ninyi ni wa Kristo, basi, mmekuwa [Wagalatia ambao ni wa Mataifa] uzao wa Ibrahimu [Israeli], na WARITHI sawasawa na ahadi†(3:29). Wagalatia walikuwa sehemu ya Israeli ya kiroho kwa neema, sio mbari. Warumi 11, hasa mafungu ya 25-26, yanafafanua hili kwa undani zaidi.

Tumeona kwamba Kanisa lote (wale wote walioongoka katika kipindi cha miaka 6,000) litaolewa na Kristo wakati wa Kurudi Kwake na kusimamishwa kwa ufalme wa Mungu. Mathayo 22 inaonyesha hili: “Ufalme wa mbinguni [ufalme wa Mungu] umefanana na mfalme mmoja aliyemfanyia mwanawe ARUSI. Mungu ni “Mfalme†na Kristo ndiye “Mwana†katika mfano huu.

Mathayo 25 pia inaelezea arusi hii inayokuja: “Ndipo ufalme wa mbinguni [wa Mungu] utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki BWANA ARUSI…usiku wa manane, pakawa na kelele, Haya, BWANA ARUSI yuaja; tokeni mwende kumlaki…Na hao walipokuwa wakienda kununua, BWANA ARUSI akaja, nao waliokuwa tayari wakaingia pamoja naye ARUSINI; na mlango ukafungwa†(fu. 1, 6, 10).

Mlango “ulifungwa†kwa sababu wengine watafungiwa nje! Watakuwepo wengi leo ambao watasikitishwa vibaya kwa sababu ujinga wao kuhusu Mpango wa Mungu utawazuia (baadhi kwa kitambo, wengine kwa wakati wote) wasiwe sehemu ya bibi arusi.

Hali ya ndoa katika ulimwengu huu iko katika mkanganyiko. Wengi huchagua kuishi pamoja kabla ya ndoa, au wanaikataa moja kwa moja taasisi hii iliyobarikiwa na Mungu. Wengine wanafuata ndoa za jinsia moja, au “mitindo mbadala ya maisha.†Wote hawa hushindwa kuona kusudi kuu la ndoa linalofunuliwa kwa jinsi ya Mungu—lile ambalo ndoa inakusudiwa kuwa taswira yake!

Bila shaka, hakuna yeyote ANAYEKATAA maana kuu ya wakati wote na kusudi kuu la ndoa ataruhusiwa kuwa sehemu ya bibi arusi anayeolewa na Kristo. Hiyo ingemdhihaki Mungu na kuuzawadia uasi!

Kristo Alijenga Kanisa Lake

Mungu analiita Kanisa Lake, Bibi Arusi Wake ajaye, “jengo†ambalo “limefungamanishwa pamoja†(Efe. 2:21). Kwa hakika Kristo “anajenga jengo†lenye kujumuisha “mawe yaliyo hai [yanaishi]†(1 Pet. 2:5). Zaburi 127:1 inasema, “Bwana asipoijenga nyumba waijengao wafanya kazi bure. Bwana asipoulinda mji Yeye aulindaye akesha bure.†(Tuliona kwamba 1 Timotheo 3:15 inaliita Kanisa la Mungu “nyumba ya Mungu.â€) Kristo anaendeleza ujenzi Wake wa Kanisa leo hii, na umekutana nalo.

Tuliona kwamba Kanisa la kweli limeainishwa kama mfano wa Yerusalemu na kama Mama wa ndugu wote walio ndani ya Kanisa (Gal. 4:26; Ebr. 12:22-23). Kama alivyo Mama yeyote, huwatunza na huwalisha watoto wake. Tumeona kwamba Kanisa la kweli limefananishwa na bibi arusi aliyetabiriwa kuolewa na Kristo wakati wa Kurudi Kwake (Ufu. 19:7-9). Ameelezewa kama, wakati huo, akiwa “amejiweka tayari†kwa ajili ya tukio hili la kushangaza na lenye utukufu!

Je utakuwa yule anayejitahidi “kujiweka tayari�

Hatimaye, hatujaelezea maana halisi ya neno la Kigiriki lililotafsiriwa “Kanisa†katika Agano Jipya. Hii inahitaji ufafanuzi. Wengi wamedhani kuwa inamaanisha jengo au taasisi, wakati halimaanishi lolote kati ya haya. Neno “kanisa†ni ekklesia, ikimaanisha “mwito kutoka,†hasa ikiwa mkusanyiko wa kidini. Wakristo kwa hakika wameitwa watoke kwa ulimwengu huu—njia zake—tamaduni zake—kawaida zake—mapokeo yake—maarifa yake ya uongo—na kuingia ndani ya Kanisa la kweli, na ushirika pamoja na Mungu na Kristo (1 Yohana 1:3). Chukua muda kuonja ufahamu huu wa kushangaza.

Mungu ananguruma hivi kwa watu wote kila mahali: “Kwa hiyo, TOKENI kati yao, Mkatengwe nao…Nami nitawakaribisha. Nitakuwa Baba kwenu, Nanyi mtakuwa Kwangu wanangu wa kiume na wa kike, asema Bwana Mwenyezi†(2 Kor. 6:17-18).

Na-iwezekane Mungu akusaidie utoke katika Babeli ya ulimwengu huu (Ufu. 18:4), ili uweze KUFUZU kutawala pamoja na Kristo aliye hai, mwenye uweza wote katika ulimwengu mpya wa kushangaza, mkamilifu unaokuja!

Wachache wanachagua kutoka katika ulimwengu. Wako radhi [tayari] kumtafuta Mungu kwa mioyo yao yote. Hawa ndio wale wanaoitwa na Mungu kwa wakati huu. Hebu tuelewe.

Je Wengi Wamepotea?

Wengi wa wanaojidai kuwa Wakristo wamefundishwa kwamba Mungu anajaribu kuuokoa ulimwengu sasa. Namna hii ya kufikiri huwekwa hivi: Mungu na ibilisi wako vitani juu ya hatima ya mwanadamu. Hii inatazamwa kama pambano kuu kati ya wema na uovu—Mungu na Shetani. Tuliona kwamba Ufunuo 12:9 inasema Shetani ameudanganya ulimwengu wote—na picha ya jinsi ambavyo hatimaye Mungu atawaokoa wanadamu wote ndio udanganyifu wake mkuu. Kwa hakika, picha hii inamfaa Shetani kwa sababu angependa kuona ulimwengu ukifikiri kwamba yeye ana nguvu zaidi kuliko Mungu.

Hebu tuliweke hili kwa njia nyingine: Je leo ndio fursa pekee kwa wanadamu wote kuuchagua au kuukataa Ukristo? Je watu wote lazima “waamue sasa†kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi? Je hiki ndicho Biblia inachofundisha? Jibu ni HAPANA ya msisitizo! Kama ingekuwa ndiyo, basi Mungu anashindwa vibaya katika pambano Lake na ibilisi kwa ajili ya kuamua hatima ya wanadamu wote. Kwa maneno mengine, Mungu “anawaita†wanadamu wote, lakini wengi HAWAITIKI!

Fikiria! Katika mwaka 1920, wakati baba yangu alipozaliwa, kulikuwa na watu kama bilioni 2 duniani. Sasa idadi ya watu inakaribia bilioni 6.7—na wengi wanaongezeka kila siku. Takriban watu bilioni 2.2, au sehemu-ya-tatu, wanaamini—kwa namna moja au nyingine—katika jina la Yesu Kristo. Hii inawakilisha jumla ya zaidi ya aina 2,000 za mifumo tofauti ya wanaojiita Wakristo. Takriban sehemu-ya-tatu nyingine ya wanadamu wamesikia juu ya Kristo lakini hawajamkubali na wala hawadai kumfuata. Mwisho, sehemu-ya-tatu iliyobaki ya watu wote duniani hawajui chochote kuhusu Kristo. Wengi wanapatikana India, Afrika, Japani, China na sehemu za Amerika ya Kusini na Kusini-mashariki mwa Asia hawajawahi hata kusikia habari Zake. Je hawa wamehukumiwa kupotea, bila kupata fursa ya kufahamu kile walichokosa au kwa nini—bila kuwa na fursa ya “kuitwa�

Biblia inapoongelea juu ya jina la Kristo, inasema wazi, “Wala hakuna wokovu katika mwingine awaye yote, kwa maana hapana jina jingine chini ya mbingu walilopewa wanadamu litupasalo sisi kuokolewa kwalo†(Matendo 4:12). Zaidi, Warumi 10:13 inasema kwamba ni lazima watu waliitie jina hili ili waokolewe. Fahamu! Ni wazi kwamba wale wote ambao hawakujisalimisha kwa Mungu wa Biblia na kumkubali Yesu Kristo kama mwokozi wao hakika hawaokolewi! Mabilioni wasiohesabika wamekufa katika hali hii. Wengi wamedhani kwamba njia nyingine mbadala kwa hawa ni kwamba waliukosa wokovu na kwamba toka zamani Mungu alishapanga jambo hili kwa walio wengi miongoni mwa waliopata kuishi.

Wengi Hawaitwi

Tena, ikiwa vita ni “ongoa roho kwa ajili ya Kristo,†karibu kwa msisimuko mkubwa kama wengi wa wahubiri wa Kikristo wanavyonadi, basi ibilisi ni mwenye nguvu zaidi, na ana ufanisi zaidi, katika jitihada zake kuliko Mungu. Huu ndio uwezekano mwingine pekee—isipokuwa kama kuna namna ya tatu ambayo imebeba umati mkubwa wa watu. Lakini lazima iwe ni aina ambayo haijatambuliwa. Ipo!—Mungu hawaiti halaiki ya wanadamu leo.

Ukweli ni kwamba Mungu kwa uangalifu anaita idadi teule kutoka kwa halaiki ya waliodanganywa ili waelewe Mpango Wake na mafundisho ya kweli ya Biblia. Lakini tumeona Anaita wachache waliochaguliwa!

Fasili yenyewe ya nini Kanisa la Agano Jipya inalazimisha uchunguzi wa somo la “kuitwa.†Sura hii—na kitabu—isingekamilika bila kuangalia kwa karibu maana ya “kuitwa.â€

Wengi kwa kawaida hushangaa kama wanaitwa na Mungu. Mtu atajuaje? Je hisia zinatosha kwa suala muhimu sana kama hili? Mwito ni nini? Neno la Mungu linasemaje? Unahitaji kujua.

Kuitwa na Kuchaguliwa na Mungu

Biblia inaongea wazi juu ya wale walioitwa na Mungu. Angalia kile ambacho Paulo aliwaambia ndugu wa Thesalonike: “Yeye [Mungu] ni mwaminifu ambaye awaita ninyi…†(1 Thes. 5:24). Kama onyo kwa mkusanyiko wa Wagalatia, waliokuwa wanapoteza ufahamu wa injili ya kweli, alisema hivi: “Nastaajabu kwa kuwa mnamwacha upesi hivi Yeye aliyewaita katika neema ya Kristo, na kugeukia injili ya namna nyingine†(1:6), na baaaye akaongeza, “Kushawishi huku hakukutoka kwake Yeye anayewaita ninyi†(5:7-8). Kwa mkusanyiko wa Wakorintho aliandika, “Maana, ndugu zangu, angalieni mwito wenu, ya kwamba si wengi wenye hekima ya mwilini, si wengi wenye nguvu, si wengi wenye cheo walioitwa†(1 Kor. 1:26).

Kristo mwenyewe aliongea katika matukio mengi kuhusu mwito wa Wakristo. Inawezekana unaifahamu kauli Yake, “Kwa maana waitwao ni wengi, bali wateule ni wachache,†inayopatikana katika Mathayo 22:14 na 20:16. Baadaye, akiongeza maana kwa sehemu ya pili ya usemi huu, Alitoa maelezo yafuatayo kwa wanafunzi Wake: “Si ninyi mlionichagua Mimi, bali ni Mimi niliyewachagua ninyi†(Yohana 15:16), na kisha “Bali mimi naliwachagua katika ulimwengu, kwa sababu hiyo ulimwengu huwachukia†(fu. 19).

Zinapowekwa pamoja, aya hizi zinafafanua kwamba Mungu anaita watu wachache—kwa hakika wachache sana—kutoka ulimwenguni kwa kusudi Lake kuu. Wale wanaoitikia wito Wake kisha “huchaguliwa,†wakaendelea hadi kutubu, kubatizwa na kuongoka.

Vipi Kuhusu Wewe?

Kadri muda unavyoenda, wengi hujikuta wakijifunza mambo ambayo kamwe hawakuwahi kuyasikia kabla. Wanagundua kwamba kuna ufahamu sahihi (wa kweli) wa mafundisho ya Biblia, na kuna ufahamu ambao sio sahihi. Wanakuja kutambua kwamba wamekutanishwa na ufahamu usio wa kawaida, usiojulikana na wote wanaowazunguka. Wanaona kwamba Biblia inaleta maana—kwamba si ngumu kueleweka kama walivyokuwa wakifikiri awali. Halafu, wanapoona haja ya kutenda kulingana na yale wanayojifunza inaongezeka, wengi hujiuliza, “Je Ninaitwa na Mungu?â€

Wakati mwingine swali hili huchukua muundo wa “Je ninapitia ‘uongofu’?†au “Je nitafute kubatizwa?†au hata “Je nimekutana na Kanisa la Mungu la kweli?†Kwa kiwango cha juu, wengi hawana uhakika juu ya jinsi ya kujibu maswali haya ya msingi, na wengi hawana wazo la aina yoyote ile kuhusu jinsi ya kuyatatua kwa usahihi.

Hebu tuweke dhahiri, kutoka katika Neno la Mungu, jinsi ya kujua kama Mungu anakuita. Inaweza kufanywa rahisi, bila kuwa na uwezekano wa kutofahamu. Ikumbukwe kwamba, swali hili ni moja ya maswali muhimu utakayopata kukumbana nayo. Kufahamu vyema jibu lake ni suala lenye UMUHIMU MKUBWA kwa maisha yako!

Nilianza kujifunza kwa mara ya kwanza ukweli wa Mungu nilipokuwa na umri wa miaka 17. Kabla Mungu hajaniita, sikuwahi kujua hata moja ya mafundisho ya kweli ya Biblia. Mchakato wa kuitwa kwangu ulianza pale niliposikia sauti ya mtu aliyeitwa Herbert W. Armstrong, ikitangaza kutoka Pasedena, Kalifonia. Hii ilikuwa mwaka 1966, na mara hiyo ikawa wazi kwangu kwamba nilikuwa nasikia mambo kutoka kwa mtu huyu ambayo KAMWE sikuwahi kuyasikia kabla—tena na UTHIBITISHO dhahiri wa maandiko kuyaunga mkono. Nakumbuka kushangazwa jinsi Biblia ilivyoanza kuwa wazi—na jinsi ilivyoleta msisimko kuisoma. Kabla ya hapo—kipindi chote nilichohudhuria dhehebu langu la ujana lililojulikana, lililoheshimiwa sana—wakati wote nilikuwa nimeiona Biblia isiyo na tija na ngumu kueleweka.

Watu wa zama zote na tamaduni hujaribu kupata ufumbuzi wa “mwito†ni nini hasa. Wengi huuhafifisha mpaka kuwa zaidi kidogo ya hisia inayowajia, wanayodhani kwamba imetoka kwa Mungu. Mamilioni ulimwenguni wanahisi “wameitwaâ€â€”wakati mwingine kwa “kanisa,†au kwenye “huduma,†au “kazi za umisionari,†na wakati mwingine kufanya kazi na watoto, na bado inaweza kuwa kufanya kazi katika fani ya udaktari au hata kwenye jeshi. Wakiwa hawajui yale ambayo Mungu anasema, wengi sana wamebaki kutegemea hisia, wakidhani kwamba maisha yao—na njia wanazochagua—yamevuviwa kwa mpango wa Mungu. Wanadhania “uvuvio†huu ni kuitwa na Mungu. Inasikitisha, wengi kamwe hawajifunzi kwamba “miito†hii haihusiani kabisa na kumfuata Mungu wa kweli wa Biblia.

Mwito wa kweli kutoka kwa Mungu ni zaidi sana ya hisia fulani ambayo kwa fikra za kibinadamu hufurahia kuhitimisha kuwa “imetoka kwa Munguâ€!

Kufasili Mwito wa Kweli

Katika Injili ya Yohana, tuliona Yesu alisema, “Hakuna mtu awezaye kuja Kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka….†(6:44). Mafungu kumi-na-tisa baadaye, Alirudia kwa wasikilizaji Wake, “Kwa sababu hiyo nimewaambia ya kwamba hakuna mtu awezaye kuja Kwangu isipokuwa amejaliwa na Baba Yangu†(fu. 65). Katika fungu linalofuata, Yohana anarekodi kwamba “Kwa ajili ya hayo wengi miongoni mwa wanafunzi Wake wakarejea nyuma, wasiandamane Naye tena.â€

Wengi wa waliosikia kauli za Kristo kwa kweli hawakuelewa kwamba yapasa Mungu “awavute†watu na kwamba mwito ni kitu ambacho “wanapewa.†Ingawa wengi leo wanaonekana kuelewa kwamba kwa mtindo fulani ni lazima waitwe, hawatafuti kufahamu—kutoka kwenye Biblia!—jinsi ya kujua bila ya shaka kwamba ni Mungu anayeita—anavuta—akiwapatia—wao chochote kile wanachopaswa kukipokea.

Hebu tuangalie maandiko machache yanayodhihirisha wazi ni nini kile Wakristo “wanapewa†pale wanapoitwa. Ni lazima tumalize kabisa mkanganyiko wowote.

Katika Mathayo, wanafunzi wa Kristo waliuliza, “Kwa nini wasema nao [makutano waliomsikiliza] kwa mifano?†(13:10). Jibu lake ni muhtasari wa jinsi gani na kwa kutumia nini Mungu huita: “Akajibu, akawaambia, Ninyi mmejaliwa kuzijua siri za ufalme wa mbinguni [au ufalme wa Mungu], bali wao hawakujaliwa†(fu. 11). Mafungu kadhaa yanayofuata yanakuza kile alichomaanisha, akifafanua jinsi gani walio wengi duniani wanaweza kusikia kweli za Mungu (“siri za ufalmeâ€) wasizielewe. Kwa kuwa walio wengi mno miongoni mwa wanadamu hawavutwi na nguvu ya Roho ya Mungu, hawajapewa uwezo wa kutambua Neno la Mungu.

Hii inahusikaje na wewe? Jibu hufafanua moja kwa moja jinsi ya kujua ikiwa Mungu anakuita: Mwito, kwa lugha rahisi, ni kuelewa kweli za Mungu unapoziona, kuzisoma au kuzisikia.

Jiulize mwenyewe: “Ninaelewa mafundisho ya Biblia na kweli ninapozisikia? Je maandiko juu ya injili ya ufalme wa Mungu; mpango wa wokovu na kusudi la kuwepo kwa mwanadamu; kilele, cha matukio yaliyotabiriwa yanayokuja hivi karibuni; Ujumbe wa Mungu wa onyo kwa watu Wake; Sheria Yake—ikiwa ni pamoja na amri ya Sabato—Siku Takatifu; kutoa zaka; wanyama safi na wasio safi; Kanisa moja la kweli; na mafundisho mengine mengi yanaleta maana kwangu?â€

Unaposoma au kusikia mambo haya katika vitabu kama hiki, je yana maana yoyote kwako? Unayaelewa? Je yako DHAHIRI katika ufahamu wako? Je, unayaona kama MAARIFA MAALUMU ambayo wengine hawana? Unajaribiwa kutoamini kwamba unaweza kuonyeshwa mambo ambayo wengi hawana habari nayo?

Kama majibu kwa maswali haya ni “ndiyo†basi Mungu anakuita—“anakuvutaâ€â€”wewe! Siri za ufalme wa Mungu zinatolewa KWAKO!

Kuwajibika kwa Maarifa Yaliyotolewa

Watoto wanazaliwa wakiwa hawajui chochote. Hawajui hata yale ya msingi kabisa juu ya jema na baya. Yapasa wafundishwe karibu kila kitu. Vivyo hivyo, ulimwengu haujui mambo ya Mungu—jema kiroho kutoka kwa baya kiroho. Lakini kuwa na maarifa ya mambo haya huja wajibu wa kuyatendea kazi.

Aya mbili za Biblia hudhihirisha kwamba Mungu huwahesabia watu wajibu kwa kile wanachoelewa. Angalia Yakobo 4:17: “Basi yeye AJUAYE KUTENDA MEMA, wala hayatendi, kwake huyo ni dhambi.†Sasa soma Waebrania 10:26: “Maana, kama tukifanya dhambi kusudi baada ya kuupokea UJUZI WA ILE KWELI, haibaki tena dhabihu kwa ajili ya dhambi.â€

Hebu tuelewe. Kila wakati unapojifunza zaidi juu ya ukweli wa Mungu (lile lililo “jemaâ€), na inaleta maana kwako—angalau unapata uelewa wa jumla—unapewa maarifa ya kiroho yasiyo ya kawaida ambayo kwayo Mungu anakuhesabia wajibu. Umeona katika sura iliyopita kwa nini wengine ambao hawavutwi na Roho ya Mungu hawana nafasi—yoyote!—kuelewa kile wanachosoma. Lakini ni lazima ujiulize ikiwa unaelewa kile unachojifunza.

Kufahamu—kuelewa maana ya—maarifa ni kitovu cha mchakato wa kuitwa. Zaidi, kwa kuona kwamba unapewa maarifa ya pekee inafanya kuelewa jinsi Mungu anavyoita mtu liwe jambo nyeti kuliko wengi zaidi walivyoamini. Tambua kwamba Mungu atamwita kila mtu mara moja tu. Kwa hiyo, unawajibika sasa kwa maarifa ambayo unapewa. Kama mtu hafanyii kazi kile anachojifunza, Mungu atauondoa ufahamu huo (Rum. 2:13; Zab. 111:10), na mtu kama huyo yuko katika hali mbaya kiroho.

Uhuru Mkuu

Kweli ya Mungu inasisimua sana kuifahamu. Ndiyo njia pekee ya kuyaendea mambo ya ajabu, yaliyo mema katika maisha—mambo ambayo Mungu anataka uyapate. Vile vile ndiyo njia pekee kuuendea uhuru mkubwa zaidi ambao unaweza kupatikana! Kristo aliwaambia Wayahudi fulani waliodai kumwamini: “Ninyi mkikaa katika neno Langu [kweli – Yohana 17:17], mmekuwa wanafunzi Wangu kweli kweli; tena mtaifahamu kweli, nayo HIYO KWELI ITAWAWEKA HURU†(Yohana 8:31-32). Ni lazima uwe tayari [radhi] “kuendelea†katika kujifunza Neno la Mungu, kujifunza zaidi kweli Yake, ambayo Kristo anafafanua “itakuweka huru†kutoka ulimwengu uliokatwa kutoka kwa Mungu na kutekwa mateka na Shetani. Hata huu ufahamu ni maarifa ya thamani kuu.

Washirika wenzako ulimwenguni huenda hawaelewi lolote katika mambo haya. Vivyo hivyo hata jirani zako. Bila ya Mungu kuwaita, hawana namna ya kufurahia sasa kile ambacho umepewa WEWE—kama unaelewa na unatendea kazi kweli ya Mungu.

Vile vile ni muhimu kwamba uthibitishe katika fikra yako mambo unayojifunza. Lazima ujikute ukitaka KUTHIBITISHA mafundisho ya Mungu. Paulo pia aliwaambia Wathesalonike “JARIBUNI [THIBITISHENI] mambo yote; lishikeni lililo jema†(1 The. 5:21). Kama unajua Mungu anakuita, chukua muda kuthibitisha kwamba Yuko. Kisha thibitisha kwamba Biblia kweli ni Neno Lake lililovuviwa kwa ajili ya mwanadamu.

Hatimaye, thibitisha utambulisho wa Kanisa la Mungu. Ondoa shaka yote, ukiondoa uwezekano wowote wa mkanganyiko. Tuliona yako makanisa mengi bandia—mengi “yenye-kufanana†kiroho ulimwenguni. Usidanganywe na lolote kati ya hayo. Kwa kuwa Kristo aliahidi, “Nitalijenga Kanisa Langu,†dhamiria kujua hakika kama umekutana nalo.

Wakati ukithibitisha mambo haya, omba kwa bidii juu ya kile unachojifunza. Unapokuwa na shaka juu ya jambo lolote, kumbuka kwamba Kristo alifundisha, “ombeni, nanyi mtapewa, tafuteni, nanyi mtaona; bisheni, nanyi mtafunguliwa†(Math. 7:7).

Yohana 14:17 inafafanua jinsi gani wale wanaokuja kwenye uongofu wanaanza kuona kwamba wanaweza kuona wazi mambo ya Mungu. Angalia kile Kristo alisema alipokuwa akiongea na wanafunzi Wake juu ya Roho Takatifu ambayo wangeipokea baada ya muda mfupi: “ndiyo Roho ya kweli; [ambayo] ulimwengu hauwezi kuipokea, kwa kuwa hau[i]oni wala hau[i]tambui; bali ninyi mwa[i]tambua, maana [i]nakaa kwenu, nayo itakuwa ndani yenu.â€

Mahali hapa, wanafunzi walikuwa kama walivyo wengi leo—pengine kama wewe, pia. Walikuwa wanaona kweli nyingi za kiroho kwa sehemu, lakini bado hawakuweza kuelewa kikamilifu umuhimu mkubwa wa kujifunza Mpango wa Mungu na njia Yake ya maisha. Kupitia Roho Takatifu ikitenda kazi pamoja nao, Mungu alikuwa anafunua mambo fulani ambayo wangeelewa tu katika kiwango kikubwa mara itakapokuwa ndani yao, kuanzia kwenye kuongoka. Hatimaye, kuelewa kikamilifu mambo yote ya Mungu—siri zote za ufalme wa Mungu—ni lazima mtu atungwe kwa Roho Takatifu. Hii hutokea wakati inapoingia moja kwa moja katika fikra! Kukosa kubatizwa na kutopokea Roho ya Mungu iliyo muhimu mno, haiwezekani kabisa kwa mtu yeyote kuelewa hata kweli moja ya kibiblia!

Kumbuka. Shetani ni MDANGANYIFU MKUU. Amezalisha mifumo mingi ya dini za uongo duniani kote. Anapotosha kweli kwa njia zisizo kikomo, na mchakato wa Mungu wa kuita haukubakizwa.

Kuwa na uhakika kama unaitwa kwa wakati huu. Lazima uamue kama unaelewa kweli za kitabu hiki—kama unapewa fursa yako ya wokovu sasa!

Kuelewa Uongofu

Kuitwa kutoka ulimwenguni—Babeli—moja kwa moja huongoza kwenye somo la uongofu—UONGOFU HALISI!

Uongofu wa kweli ni nini? Je ni kule tu “kumkiri Kristo kama Bwana na Mwokozi� Vipi na ni lini mtu anaongoka? Je ni ghafla mara moja? Au ni mchakato wa polepole, unaodumu maisha yote?

Wengi sana hupambana na matatizo, udhaifu na dhambi. Je Mungu anatarajia ushindi—kukua? Hii ina maana gani? Inafanyikaje? Roho Takatifu inatimiza jukumu gani? Na vipi kuhusu imani na toba?

Wengi hudhani kwamba lazima wawe wakamilifu. Wengine wanahukumu njia ya Mungu kwa mienendo ya Wakristo. Je mtu anaweza kutenda dhambi na kubaki kuwa Mkristo? Vipi kuhusu msamaha?

Mamilioni wanatafuta majibu kwa maswali haya, lakini wanaridhika kukaa katika uongofu wa uongo. Katika sura inayofuata, somo la uongofu wa Kikristo hatimaye linafanywa dhahiri!

Sura ya Nane – Uongofu wa Kweli ni Nini?

Ni lini mtu anaongoka? Nimewajua wengi walioushuku uongofu wao kwa sababu walikuwa hawajafundishwa maana ya uongofu wa kweli. Wakiwa katika mashambulizi—katika mbano—walikosa uhakika wa kujua kwamba wangeweza kutatua matatizo yao kwa ufanisi. Hawakuwa na uhakika kwamba walikuwa hata na nguvu za kuyashinda.

Kwa kuwa ibilisi—mtunzi wa machafuko (1 Kor. 14:33)—anaudanganya ulimwengu wote, vile vile anatafuta kuwakanganya wanaojidai kuwa Wakristo kuhusu somo hili la muhimu sana. Kwa kweli, kwa sababu mambo mengi sana yako hatarini katika uelewa huu, anaweka vizuizi vyote. Kitu anachokichukia sana ni pale hata mtu mmoja anapomgeukia Mungu.

Wachache sana wanauliza, “hivi Mkristo halisi ni nini?†Je ni yule “anayehudhuria kanisaniâ€â€”“anayemkiri Yesuâ€â€”“anayemjua Kristoâ€â€”ambaye “amebatizwaâ€? Je kuna fungu moja ambalo tunaweza kuligeukia linalotoa fasili ya Biblia ya Mkristo halisi—linalomaliza mkanganyiko wote?

Kumbuka, Paulo aliandika, “Kwa kuwa wote wanaoongozwa na Roho ya Mungu, hao ndio wana wa Mungu†(Rum. 8:14). Mkristo, basi, ni yule aliye na Roho Takatifu ikimuongoza. Lakini je, kuwa na Roho ya Mungu ni muhimu kabisa ili kuwa Mkristo? Kufikia mahali hapa, katika muktadha, Paulo alikuwa ameshasema, “Lakini ikiwa Roho ya Mungu inakaa ndani yenu, ninyi hamwufuati mwili; bali mwaifuata roho. Lakini mtu awaye yote asipokuwa na Roho ya Kristo, huyo si Wake (fu. 9)!

Maneno mazito! Ama mtu ana Roho ya Mungu, na ni Mkristo, au hanayo na sio Mkristo—yeye “si Wake.†Wale wote ambao wameongoka kwa kweli wanayo Roho Takatifu ndani yao.

Lakini hii ina maana gani? Je kupokea Roho ya Mungu ndicho kitu pekee kilichopo kwa Ukristo na uongofu—au kuna zaidi?

Kupokea Nguvu

Kristo aliwafundisha mitume kwa siku arobaini baada ya Ufufuo Wake (Matendo 1:3). Aliwaagiza kungoja Yerusalemu mpaka wapokee ile Roho Takatifu siku kumi baadaye, katika siku ya Sikukuu ya Pentekoste. Wanafunzi walimwuliza Yesu kama alikuwa Anakaribia kusimamisha ufalme Wake duniani. Muda mfupi kabla ya kupaa mbinguni, Alisema, “Si kazi yenu kujua nyakati wala majira…Lakini mtapokea NGUVU, ikiisha kuwajilia juu yenu Roho Takatifu†(fu. 7-8). Haya yalikuwa maneno Yake ya mwisho kabla hajatoweka.

Kama vile mitume walivyongoja kwa ajili ya nguvu kupitia Roho Takatifu, watu wengi leo hii wanangoja namna fulani ya nguvu za ziada pale wanapoongoka. Mwambie kijana kwamba atapewa funguo za gari la familia na atakuwa hana ugumu kuelewa kwamba yuko karibu kupokea nguvu halisi. Nilipokabidhiwa funguo za gari ya baba yangu kwa mara ya kwanza, nilielewa kikamilifu maana yake. Hakuna tofauti na yule anayeelekea kuwa Mkristo akingoja kupokea Roho ya Mungu wakati wa toba na ubatizo.

Paulo alimwandikia Timotheo, “Maana Mungu hakutupa roho ya woga, bali ya nguvu na ya upendo na ya akili timamu†(2 Tim. 1:7). Kwa kuwa Wakristo wana Roho ya Mungu, nguvu halisi kabisa imekuja maishani mwao. Kwa hakika, fungu hili pia linasema kwamba Mkristo anadhihirisha upendo—au maisha ya kutoa—na kwamba mwenendo wake unaakisi akili timamu.

Ukweli kwamba Roho ya Mungu inatia hali ya akili timamu ni uthibitisho kwamba Mungu anawataka Wakristo kufahamu mwito wao—uongofu wao—KUSUDI la Mungu kwao. Mungu anawataka watu Wake kuwa timamu katika njia sahihi. Kwa hakika, hii lazima ijumuishe kufahamu vipengele vyote vya msingi vya uongofu wa kweli.

Roho Takatifu Inatolewa Lini?

Jinsi gani hasa mtu anapokea Roho ya Mungu? Na anawezaje kujua bila shaka kwamba tayari imetolewa? Kwa kuwa kipindi hiki kinahusisha uongofu, ni katika pointi ipi ambapo yule anayetegemea kuwa Mkristo atakuwa na uhakika kwamba Mungu ametoa Roho Yake? Kwa kuwa kutokuwa na Roho ya Mungu kunamfanya mtu asiwe Mkristo wa kweli, hakika Mungu asingewaacha watumishi Wake katika shaka juu ya ama wanayo—hasa lini wanaipokea—na jinsi gani!

Kitabu cha Matendo kinasema, “Petro akawaambia, Tubuni mkabatizwe kila mmoja kwa jina Lake Yesu Kristo, mpate ondoleo la dhambi zenu, nanyi mtapokea kipawa cha Roho Takatifu†(2:38).

Kupokea Roho ya Mungu kunakuja pale kunapokuwa na toba halisi na ubatizo sahihi. Pamoja na hii pia huja ondoleo la dhambi, au msamaha. Hivyo kuna kipindi maalumu wakati uongofu unapoanza. Kuna wakati maalumu ambapo Roho Takatifu inaingia katika fikra na mtu anakuwa Mkristo wa kweli—na Mungu anakuwa ametunga mwana mpya. Hata hivyo, kuna mengi zaidi ya kufahamu.

Lazima tuulize, je wokovu sasa umekamilika ndani ya Mkristo? Je sasa “ameokoka� Je mwana mpya wa Mungu aliyetungwa amekuwa mkamilifu ghafla, asiyeweza kamwe kutenda dhambi au kukosea, kwa sababu anadhani sasa ameokoka?

Uongofu halisi wa Kikristo ni mchakato wa POLEPOLE wa kukua na kushinda—wa kubadilika na kuendelea. Lakini kwa jinsi gani? Na mwishoni mwa mchakato, Mkristo “aliyekamilika†anafananaje? Na hii inahusika vipi na lengo la Mkristo—pamoja na kile anachokishindania kama thawabu yake ya mwisho ya yeye kuwa Mkristo?

Kusudi la Mungu Kwa Ajili Ya Wakristo

Tumeona kwamba, katika huduma Yake, Kristo alitangaza injili ya ufalme wa Mungu—na kwamba kilichofichwa katika ujumbe huu ni ufahamu juu ya UWEZEKANO WA KUSTAAJABISHA kwa ajili ya yule anayejisalimisha kweli kweli kwa Mungu. Kokote kule Kristo alikokwenda, Aliongea juu ya ufalme unaokuja—au SERIKALI—ya Mungu. Wakati mifano Yake mingi ilijengwa kwenye ujumbe huu, wachache walioisikia walielewa maana yake. Na alipoongea mifano hii, wakati wote Alijumuisha jinsi gani Wakristo wa kweli walikuwa wakifuzu kuwa sehemu ya serikali hiyo!

Mathayo 13 imebeba nusu dazeni ya mifano ya “ufalmeâ€. Sura hii inaanza na mfano wa “Mpanzi na Mbegu,†ukionyesha mtu akirusha mbegu katika maeneo na aina tofauti tofauti za udongo. Katika maeneo mengine, mfano ulieleza jinsi ambavyo mbegu ilikua na kustawi katika maisha ya yule aliyeipokea. Katika maeneo mengine, ama zilikufa haraka baada ya kuanza kukua, au hazikuweka mizizi kabisa. Wengine waliopokea mbegu walikua katika tabia mara “thelathini, sitini au miamoja†njiani kuelekea kwenye ufalme.

Huu unafuatwa na mfano wa “Ngano na Magugu.†Mfano huu unaelezea “tunda†linaloonekana katika maisha ya Wakristo kabla ya wakati ule ambapo Mungu anawakusanya “ghalani†Mwake. Tunda, jema au baya, linawakilisha ukuaji wa Mkristo, au kukosekana ukuaji. Ghala ni mfano wa ule ufalme.

Mfano wa tatu unauonyesha ufalme ukianza kama “punje ndogo ya haradali†inayokua na kuwa mti mkubwa. Huu unafuatwa na mfano wa chachu, ukionyesha ufalme wa Mungu kama chachu ikienea hadi kujaza unga uliokandwa (dunia, na mataifa yote) ambamo imo. Wa tano unaulinganisha ufalme wa Mungu na “hazina iliyofichwa†iliyopatikana kwenye shamba. Aliyeiona anauza vyote alivyo navyo ili kulinunua shamba hili.

Mfano wa sita unaueleza ufalme kama “lulu ya thamani kuu,†ambayo mtu anainunua baada ya kuuza vyote alivyo navyo ili kupata kiasi cha pesa kinachotosha kwa ajili ya kuinunua. Mfano wa saba na wa mwisho kwenye sura hii unaelezea ufalme kama “juya†linalokusanya kila aina ya samaki. Samaki “wazuri†wanatunzwa—“wabaya†wanatupwa. Yesu anafafanua kwamba samaki wazuri ni wale wanaoingia katika ufalme. Wabaya wanawakilisha wale wanaochomwa (fu. 50) na kuharibiwa katika “tanuru la moto†(ziwa la moto).

Katika kila moja ya mifano hii, ujumbe ni ule ule. Baadhi (si wote!) wana nia ya kulipa gharama ya kuwa Mkristo. Wana nia ya kukua kwa namna ya roho na kujenga tabia ili waweze baadaye kurithi ile thawabu ya milele ya kuzaliwa kama (sio kutungwa tu tena) Wana wa Mungu—katika ile FAMILIA YA MUNGU—wakitawala pamoja Naye katika ufalme wa Mungu.

Kuna mifano mingine mingi ya Agano Jipya. Ufundishaji mwingi wa Kristo ulikuwa ni kwa njia ya kutumia hadithi juu ya vitu vya kawaida vinavyojulikana sana. Ilikusudiwa kubeba masomo ya kina juu ya wito wa Mkristo, kwa wale ambao fikra zao zimefunguliwa na Mungu kuuelewa.

Kumbuka maneno ya Kristo, “Hakuna mtu awezaye kuja Kwangu, asipovutwa na Baba aliyenipeleka†(Yohana 6:44, 65). Inapasa irudiwe kwa msisitizo kwamba hatua ya kwanza kuelekea uongofu ni mwito. Bila huo, ni rahisi tu kwamba huwezi kufahamu kweli ya Mungu, inawezekana tu kwa njia ya nguvu ya Roho Takatifu ikitenda kazi pamoja nawe. Hivyo, mchakato wa kufikia uongofu wa kweli wa Kikristo huanza na mwito au kuvutwa na Baba.

Mifano ya talanta, dinari, sherehe ya harusi, wanawali kumi, kondoo na mbuzi, kadhi dhalimu, mtini, kondoo aliyepotea, shilingi iliyopotea, mwana mpotevu, wakili asiyemwaminifu, Lazaro na mtu tajiri, Msamaria mwema na mingine, yote yanahusisha au kuonyesha Mkristo akiingia ufalme ujao, au Familia tawala, ya Mungu wakati wa Kuja kwa Kristo Mara ya Pili. Nafasi ingeweza kuchukuliwa kuchunguza kwa karibu kila mfano na kuthibitisha hili. Ingawa mingine ni mifupi sana, na mingine mirefu, kusudi la mifano mingi ya Kristo kwa hakika ni lile lile. Kwa wale wanaofuata maagizo ya Petro “kukua katika neema, na katika…maarifa†(2 Pet. 3:18), utawala katika serikali ya Mungu chini ya Kristo unaweza kupatikana.

Ufalme wa Mungu Unaokuja

Katika Hubiri la Mlimani, Kristo alisema “Bali utafuteni kwanza ufalme wa Mungu, na haki Yake†(Math. 6:33). Mkristo wakati wote lazima ajitahidi kufikia malengo haya mawili yasiyotenganishika. Angalia kwamba KIPAUMBELE chake ni kutafuta ufalme wa Mungu. Lakini pia lazima ajenge haki Yake (ya Mungu)—tabia Yake ya kiungu. Sehemu kubwa ya hubiri hili ni msisitizo juu ya UJENZI WA TABIA kwa njia ya utii kwa Sheria ya Mungu.

Yohana alirekodi maneno ya Kristo: “Nyumbani mwa Baba yangu mna makao mengi [maofisi]…Naenda kuwaandalia mahali. Basi Mimi Nikienda na kuwaandalia mahali, Nitakuja tena Niwakaribishe Kwangu; ili Nilipo Mimi, nanyi mwepo†(14:2-3).

Hii inahitaji uchunguzi.

Kwanza, kuna “maofisi†mengi katika “nyumba†ya Mungu (ufalme). Pili, Kristo anaandaa vyeo hivi kabla “Hajaja tena.†Tatu, Wakristo hawaendi kule Aliko ili kuwa pamoja Naye—mbinguni au mahali pengine popote—kwa sababu Yesu alisema, “Nitakuja tena.†(Mpaka sasa unaona kwamba mbinguni kamwe haijawahi kuwa thawabu ya waliookoka.) Mkristo ameahidiwa urithi wa utawala juu ya dunia (Mat. 5:5).

Sura moja baadaye (15:1-2), Kristo anaendelea, “Mimi ndimi Mzabibu wa kweli…kila tawi ndani Yangu lisilozaa matunda Huliondoa; na kila tawi lizaalo matunda Hulisafisha, ili lizidi kuzaa matunda.†Katika fungu la 5, Anasema tena, “huzaa sana matunda,†na katika fungu la 8, “Hivyo hutukuzwa Baba Yangu, kwa vile mzaavyo sana matunda.†Hatimaye, Anasema, “ni Mimi niliyewachagua ninyi… mwende mkazae matunda†(fu. 16).

Hili ni muhimu sana! Mkristo anapaswa kuzaa matunda maishani mwake! Fungu la 8 linaenda mbele kufafanua kwamba kwa kufanya hivi, “nanyi mtakuwa wanafunzi wangu.†Kristo anakutambua kama mmoja wa wanafunzi Wake (na wana wa Mungu waliotungwa) kwa ama unazaa matunda katika maisha haya au sio!

Tumejifunza kwamba kitabu cha Ufunuo kinarekodi mahali kadhaa ambapo Kristo, kupitia Yohana, anaahidi ufalme kwa wale wanaoshinda. Hebu tupitie upya: “Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo Yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa, naye atawachunga kwa fimbo ya chuma†(2:26-27), na “Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja Nami katika kiti Changu cha enzi†(3:21).

Yanapowekwa pamoja na Ufunuo 5:10, ni wazi kwamba watakatifu waliofufuliwa wanakuwa “wafalme na makuhani†ambao “wanatawala duniani†pamoja na Kristo, lakini tu kama ni washindi katika maisha haya.

Maarifa haya kweli ni ya pekee—na ya thamani. Ulimwengu haujui juu ya ufalme wa Mungu unaokuja. Aliye “mungu wa ulimwengu huu†amefanikiwa kabisa kuwadanganya wanadamu wasioshuku bila kujua.

Lakini Wakristo wanatambua kwamba wako katika mafunzo ya kila siku kwa ajili ya UTAWALA. Sio vipofu tena kwa kusudi la Mungu. Kwa hiyo, ni muhimu sana kwamba wafahamu “kanuni za mafunzo†yao.

Imani na Toba

Tumefafanua kwamba Mungu anatoa Roho Yake wakati wa ubatizo, ambao unatokea baada ya toba. Lakini jinsi gani toba inatimizwa? Je ni kwamba mtu anatangaza, kwa kudai kirahisi, “nimetubu� Je hii ndio yote kwa jambo hili? Jibu ni HAPANA kwa msisitizo! Siyo rahisi kiasi hicho.

Toba ni KARAMA kutoka kwa Mungu kama vile ulivyo mwito wa awali wa mtu. Inapoongelea juu ya watu wa Mataifa wakiijilia toba, Matendo 11:18 inasema, “Basi, Mungu amewajalia hata mataifa nao toba liletalo uzima.

2 Timotheo 2:25 inaongelea juu ya wakati ambapo “Mungu...awape...kutubu na kuijua kweli.†Hatimaye, Warumi 2:4 inafafanua kwamba ni “wema†wa Mungu ambao “unaongoza kwenye toba.†Watu “hawaiendelezi†toba kwa kusudi la kumtaka Mungu awape Roho Yake Takatifu (Matendo 2:38).

Watu lazima wamtafute Mungu na waombe kwa ajili ya karama ya toba. Siyo kitu cha moja kwa moja na haitakiwi kitazamwe kwa jinsi hiyo. Lakini Mungu hutoa toba kwa wale wote wanaoitafuta kwa mioyo yao yote, kama Daudi alivyofanya katika Zaburi 51. (Pengine chukua muda kusoma zaburi hii yote, inayovutia, inayofumbua macho.)

Lakini mtu anatubu nini hasa? Kumbuka kwamba Biblia inasema, “wote wametenda dhambi†(Rum. 3:23). Dhambi ni nini?

Kwa mara nyingine, 1 Yohana 3:4 inasema, “Dhambi ni uvunjaji wa sheria.†Hii inarejelea Sheria ya Mungu, kumbuka, nia ya kawaida, ya fikra za mwili inaichukia Sheria ya Mungu (Rum. 8:7). Kwa asili watu hawamtii Mungu. Hulka ya mwanadamu inaasi—inavunja—Sheria ya Mungu, na inafanya hivyo kwa kawaida! (Tutajifunza mengi zaidi juu ya hulka ya mwanadamu katika sura inayofuata.) Mkristo anatunza Sheria Yake. Haisikii tu au kuongea juu yake: “Kwa sababu sio wale waisikiao sheria walio wenye haki mbele za Mungu, bali ni wale waitendao sheria watakaohesabiwa haki†(Rum. 2:13).

Kwa hiyo, Mungu atatoa tu Roho Yake kwa yule ambaye amemtwaa—yule ambaye yuko radhi kumtii Yeye (Matendo 5:32).

Ulimwengu unaionyesha Sheria ya Mungu kama katili [kali] na mzigo. Lakini Yohana aliandika, “Kwa maana huku ndiko kumpenda Mungu, kwamba TUZISHIKE AMRI ZAKE; wala amri Zake si nzito†(1 Yohana 5:3). (Pia Warumi 13:10.) Sheria ya Mungu ni takatifu, njema na ya rohoni (Rum. 7:12, 14) na ni kwa njia ya Roho ya Mungu ndipo mtu yeyote anaweza kumtii Mungu na kwa njia hiyo kutekeleza upendo kwa Mungu. Warumi 5:5 inasema, “pendo la Mungu limekwisha kumiminwa katika mioyo yetu na Roho Takatifu tuliyopewa sisi.â€

Moyo uliotubu umegeuka kutoka njia zake wenyewe. Unataka kumfuata Mungu. Umejisalimisha kwa Mungu—umejisalimisha kwa serikali Yake, mamlaka Yake katika maisha yake. Fikra kama hizo zinajitahidi kumwiga Yesu Kristo na kuzaa “matunda ya Roho.†Kumbuka, Kristo aliongea juu ya “kuzaa sana matunda.†Baadaye alimvuvia Paulo KUORODHESHA “matunda ya Rohoâ€â€”upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi (kujizuia)—katika Wagalatia 5:22-23. Haya huwa dhahiri katika mwenendo wa yule anayeongozwa na Roho—aliyeongoka­—mtu.

Fikra zilizotubu zimegeuka kutoka njia ya maisha ya ubinafsi ya “kupokeaâ€, hadi kwa njia ya “kutoa.†Mwelekeo wote wa kufikiri wa Mkristo unakuwa umegeuzwa—UMEBADILISHWA kabisa—kwenda njia mpya kabisa ya kuyatazama maisha.

Mkristo anaishi kwa imani (Ebr. 10:38; Hab. 2:4). Lakini imani ya Kristo (Ufu. 14:12), sio imani ya kibinadamu, ndio inayofanya iwezekane kwa mtu kumtii Mungu. Hata hivyo, lazima mtu adhihirishe imani ya awali kwamba Kristo amemsamehe wakati wa ubatizo (Matendo 2:38). Ni katika kipindi hiki ambapo rekodi ya zamani ya mwenendo wa Mkristo inafutwa—safishwa kabisa. Imekuwa safi kama theluji—imesafishwa kwa damu ya Yesu Kristo (Efe. 1:7; Kol. 1:14). Hatimaye nafasi ya imani hii ya awali ya kibinadamu inachukuliwa na imani ya KRISTO ndani ya mtu ambaye sasa ameongoka (Rum. 1:17). Tumeona kwamba imani ni mojawapo ya matunda ya Roho ya Mungu, ambayo imeingia katika fikra za Mkristo wakati wa kutungwa—wakati wa uongofu na ubatizo.

Usielewe vibaya! Humdai Mungu Roho Yake kwa sababu umedhihirisha imani na umetubu. Ni karama (Matendo 2:28), kama ilivyo toba yenyewe. Roho Takatifu si kitu ambacho unaweza kuchuma kwa matendo yako, vivyo hivyo kama wokovu usivyoweza kuchumwa kwa matendo (Efe. 2:8-9).

Biblia inafundisha kwamba “toba ni kwa Mungu†na kwamba “imani ni kwa…Kristo†(Matendo 20:21). Uongofu ni jambo la mtu binafsi baina ya Baba na Kristo, na kila mtu. Kama Mungu anakuita kweli, fanya imara mwito wako (2 Pet. 1:10). Ni wa thamani sana!

Hii ndiyo njia pekee ya kuiendea karama ya kushangaza unayopewa!

Uongofu Wa Kweli Wafafanuliwa

Nguvu ambayo inakuja pamoja na Roho ya Mungu inamsaidia mtu kukua na kushinda. Nguvu hii ni Kristo anayeishi maisha Yake ndani ya Mkristo, kihalisia. Bila ya msaada Wake, mwongofu huyu mpya hafiki popote—haraka! Kristo aliposema, “zaeni sana matunda†(Yohana 15:5), aliifuatia kauli hii na “Maana pasipo Mimi ninyi hamwezi kufanya neno lolote.†Nguvu za kibinadamu—uwezo wa kibinadamu—unamsaidia mtu kushinda kwenye maeneo ya kimwili tu. Matatizo ya kiroho hayawezi kushindwa kwa juhudi za kimwili, kiakili au kihisia.

Kumbuka kwamba Kristo ndiye Mzabibu na sisi ni matawi. Matawi lazima yawe yameunganishwa kwenye Mzabibu, na hii inatokea kwa njia ya Roho ya Mungu ikitenda kazi katika fikra.

Alipokuwa akiongelea hili, Kristo alisema, “mito ya maji yaliyo hai itatoka ndani yake. (Na neno hilo alilisema katika habari ya Roho, ambayo wale wamwaminio watapokea…)†(Yohana 7:38-39). Kadri inavyotenda matendo mema, Roho ya Mungu hutiririka na kutoka “nje ya†Mkristo. Kwa hiyo, ni lazima kuijaliza tena, la sivyo itamalizika na kupotea kabisa. Hii ndiyo sababu Kristo alisema, “Basi, ikiwa ninyi…mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Takatifu hao wamwombao?†(Luka 11:13). Kwa kawaida watu wa Mungu huomba, katika sala, kuongezewa zaidi Roho Takatifu.

Paulo aliandika, “Nayaweza mambo yote katika Yeye [Kristo] anitiaye nguvu†(Fil. 4:13), na “ndugu zangu, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu ZAKE†(Efe. 6:10). Kristo pia alisema, “kwa Mungu yote yawezekana†(Math. 19:26). Hata Yesu alikiri kwamba, akiwa katika mwili, “hakuweza kwa [Yeye] mwenyewe kufanya neno lolote†(Yohana 5:30). Ukiwa na Roho ya Mungu ikitenda kazi na kuongezeka ndani yako, hii inaweza kuwa kweli kwako!

Lakini uongofu wa kweli wenye kina hautokei usiku mmoja. Paulo aliwaandikia Wakorintho kwamba walikuwa “watoto katika Kristo†(1 Kor. 3:1). Alielezea jinsi ambavyo walihitaji “maziwa,†badala ya “nyama,†kwa ajili ya chakula. Mkristo mpya kabisa ni kama mtoto mchanga. Kwa kulinganisha, kwanza anajifunza kukaa, kisha kutambaa, kabla ya kutembea (na hata hapo, mwanzoni, kwa hatua za kuyumbayumba za kitoto). Baadaye tu ndipo hatimaye anajifunza kukimbia (kwa namna ya roho).

Paulo alielewa hili. Alilinganisha uongofu na mashindano ya mbio (1 Kor. 9:24). Kwa hakika, ingawa si papo kwa hapo, mkimbiaji hatimaye lazima aongeze kasi, kwa sababu Paulo alisema, “pigeni mbio namna hiyo, ili mpate [shinda].â€

Namna hiyo ndiyo njia ya maisha ya Mkristo. Pole pole, kwa ukuaji wa kuendelea, kupitia mazoezi ya kila siku, yakizaa maendeleo katika maisha ya yule anayemwiga Kristo. Mkristo mpya kwa uaminifu anajitahidi, kutoka moyoni, kuwa tofauti—kugeuka na kwenda hiyo njia nyingine—NJIA YA MUNGU—maisha yake yote yaliyosalia!

Si Njia Rahisi

Lakini je njia ya Mkristo ni rahisi? Je kuwa kama Kristo katika tabia ni sawa na mithali ya “matembezi mepesi [rahisi]� Kwa hakika ni hapana!

Hebu turejee kwenye Hubiri la Mlimani ili kupata jibu la Kristo mwenyewe. Alisema, “Ingieni kwa kupitia mlango ulio mwembamba [ngumu]; maana mlango ni mpana, na njia ni pana iendayo upotevuni, nao ni wengi waingiao kwa mlango huo. Bali mlango ni mwembamba, na njia imesonga iendayo uzimani, nao waionao ni wachache†(Mat. 7:13-14). Wakati wote imekuwa ni wale wachache sana tu wanaohiari kulipa gharama ili kuishi njia hii ngumu ya maisha.

Kumbuka, Wakristo “hukimbia.†Kukimbia huhitaji nguvu—ni KAZI NGUMU! Wakimbiaji huchoka baada ya kutumia nguvu nyingi. Waangalie watu katika mashindano ya mbio ndefu wanapokaribia mstari wa kumalizia. Wanakuwa wamechoka, wameishiwa—wamepigika! Kukimbia sio rahisi. Na wakati mwingine, kama mshiriki wa mbio za nyika au marathoni, mkimbiaji analazimika kupita milima na mabonde, juu ya ardhi iliyobomoka.

Paulo mwenyewe alisema, “nakaza mwendo, niifikilie mede ya thawabu ya mwito mkuu wa Mungu katika Kristo Yesu†(Fil. 3:14). Kabla ya hili, alisema kwamba alikuwa amejifunza “kuyasahau yaliyo nyuma†na “kuyachuchumilia yaliyo mbele†kufikia lengo kuu lililokuwa mbele yake (fu. 13). Kama mkimbiaji amejitahidi kukimbia mbio ndefu, mwishoni anakuwa amekwisha kabisa. Bado, kama akikata tamaa, hana nafasi ya kushinda, na mazoezi yake yote na juhudi katika kujiandaa kwa ajili ya ushindi vitakuwa vimepotea bure! Hivyo, bila kujali mkimbiaji atakuwa amechoka kiasi gani, anakumbuka, “kwa Mungu mambo yote yanawezekana.â€

Paulo pia aliuongelea Ukristo kama “mashindano ya miereka†(Efe. 6:12). Mtu yeyote aliyeshindana miereka anajua ni jambo gumu—kufikia hata kusikia kichefuchefu na kutapika. Vile vile aliulinganisha na vita. Angalia 1 Timotheo 6:12: “Piga vita vile vizuri vya imani; shika uzima ule wa milele.†Pia, 2 Kor. 10:4 inasema, “Maana silaha za vita vyetu si za mwili, bali zina uwezo katika Mungu hata kuangusha ngome [Kigiriki: nyumba zenye maboma].â€

Hakuna kitu chochote chema au rahisi kuhusu vita. Ni hatari na kawaida husababisha majeruhi wengi—wengine hujeruhiwa, wengine huuawa. Hii ndiyo sababu Paulo anawaonya Wakristo “kupigana vita VIZURI†(1 Tim. 1:18). Kristo anaitwa “Kiongozi mkuu wa wokovu wetu†katika Waebrania 2:10. Askari asiyekuwa na uzoefu au yule ambaye hajafunzwa anaweza kuwa majeruhi wa vita kwa urahisi kama hatajisalimisha kwa wenye mamlaka na kufuata amri za mkuu wa kikosi!

Kuwapinga Maadui Watatu

Wakristo wako vitani kwenye mistari ya mbele mitatu tofauti. Ni lazima wawe macho—bila kupuuzia uwezekano wa hatari kutoka kwa yeyote kati ya maadui hao WATATU ambao wanakabiliana nao wakati wote. Inahitaji unyenyekevu kwa Mkristo kukiri, kwake mwenyewe na kwa Mungu, kwamba yeyote kati ya maadui hawa ana uwezo wa kumlemea.

Hebu tuwaangalie kwa ufupi.

Waefeso 6 inaendelea kuelezea aina sita za silaha ambazo Wakristo huzitumia katika vita vya kiroho. Soma kwa uangalifu mafungu ya 12-17. Yana onyo zito, tusisahau kwamba tunashindana miereka dhidi ya “pepo wabaya katika sehemu zilizoinuka.â€

Kwanza, ibilisi na malaika zake walioanguka wanataka kumshinda na kumharibu kila mtu aliye katika mchakato wa kufanyika mwana wa Mungu. Kama umekwisha kutungwa na Mungu, wewe ni mwana wa Mungu, unayebeba uwezekano mkubwa mno kwa ajili ya utawala. Ibilisi anachukia matazamio kwamba unaweza kupokea kile ambacho yeye hajaahidiwa—kuwa memba katika Familia ya Mungu. Anangoja mafichoni, “kama simba akitafuta mtu ammeze†(1 Pet. 5:8). Lakini hawezi kumshinda yule “anayekesha†na wale “wanaompinga†(fu. 9)! Mkristo ni lazima aendelee kutambua na kupinga mitazamo ya Kishetani inayonyatia kwenye fikra zake.

Pili, 1 Yohana 5:19 inasema, “dunia yote inakaa katika uovu.†Hilo ndilo shitaka rasmi zito la mwanadamu. Bado hilo lipo hapo katika Biblia yako! Mkristo pia lazima apinge mivuto ya ulimwengu huu, pamoja na mng'ao wake wote, misisimko, uvutivu na majaribu. Tumeona kwamba huu si ulimwengu wa Mungu wa kweli. Mungu wa ulimwengu huu ameufanya ulimwengu kama anavyotaka uwe. Mungu wa kweli si Mungu wa mkanganyiko [machafuko], ujinga na shida ambazo zimepenya na kuenea katika tamaduni na jamii za ulimwengu wa Shetani.

Yako majaribu mengi, vishawishi, mitego na mashimo ambamo mtumishi wa Mungu anaweza kuangukia humo kwa urahisi kama hayuko karibu na Mungu na kuishi kwa kila neno la Biblia (Mat. 4:4; Luka 4:4). Paulo aliwaagiza Wazee wa Efeso kwamba “Neno la Mungu…laweza kuwajenga na kuwapa urithi [wokovu—uzima wa milele]†(Matendo 20:32). Lisome kila siku!

Tatu, kujifunza Neno la Mungu kutakusaidia ushinde mivuto ya mwili wako. Baada ya Paulo kusema, “Kwa kuwa nia ya mwili ni mauti; bali nia ya roho ni uzima na amani,†aliongeza, “Wale waufuatao mwili hawawezi kumpendeza Mungu†(Rum. 8:6, 8). Mkristo bado ameumbwa kwa mwili, lakini hayuko tena “katika mwiliâ€, kwa sababu ana Roho ya Mungu ikimwongoza.

Ikiachwa bila uangalizi, hulka ya mwanadamu inajumuisha ubatili, wivu, tamaa, uchoyo, husuda, sonona, chuki, hasira, kiburi, uasi, upumbavu, ukaidi, uongo na uadui dhidi ya Mungu. Yule anayetembea katika njia ya Mungu anajitahidi kujizuia na kujifunga mwenyewe popote pale Neno la Mungu linapoagiza. Na anajitahidi kujizoeza katika mambo yote ambayo Mungu anamuagiza. Wakati Mungu anapotoa maagizo kufanya jambo fulani, anajitahidi kulifanya! Wakati Mungu anapotoa maagizo kutofanya jambo fulani, anajitahidi kutolifanya!

Ingawa kujifunza kufuata mtindo huu wakati wote inachukua maisha yote, ujenzi wa tabia ya Mungu ndilo kusudi ambalo kwa hilo kila mwanadamu alizaliwa. Kazi yake ni “kuvaa†tabia ya Mungu na Kristo, na “kuvua†mivuto ya kimwili ya hulka ya mwanadamu (Kol. 3:8-13). Japokuwa jambo hili si rahisi, thawabu ni kuu.

Ni kwa njia ya maombi ya kila siku, kujifunza Biblia, kutafakari na pia kufunga kwa muda fulani (kutokula wala kunywa maji kwa kipindi fulani), ndipo mtoto wa Mungu ataweza kuwashinda wale maadui watatu ambao wanamvizia kila siku ya maisha yake! Kwa hiyo, anza mara moja kuwa katika maombi ya kila siku, kujifunza Biblia, kutafakari na kufunga. Vitendea kazi [vifaa] hivi vinne vya makuzi ya Mkristo vitatenda kazi kwa karibu na kitendea kazi cha tano kitakachokuja baadaye—kuitumia Roho ya Mungu itakayokuwa ndani yako.

Pambano la Paulo

Biblia imejaa visa vya watumishi wakuu wa Mungu wakipigana ili kushinda dhambi. Karibu katika kila kisa, walilazimika kujifunza masomo magumu na wakati mwingine yanayoumiza sana. Wanapochunguzwa kwa ujumla, Musa, Nuhu, Daudi, Samweli, Petro na wengine wengi wanaonekana kuwa walipambana na kila aina ya tatizo linalojulikana kwa mwanadamu.

Paulo anawakilisha mfano wa pekee wa jinsi mmoja wa watumishi wakuu wa Mungu alivyopambana ili kushinda dhambi. Mwishoni mwa maisha yake, aliweza kusema kwamba alikuwa “amepiga vita vizuri,†na alikuwa “amemaliza mwendo wake†akijua kwamba “taji†ilimgoja. Lakini hii haikutokea bila kushindana miereka, kukaza mwendo, kukimbia, kushindana na kupigana vita dhidi ya hulka ya mwanadamu.

Soma kwa uangalifu [makini] Warumi 7:14-23. Itakufundisha na kukutia moyo kwamba hauko peke yako njiani kuelekea kumshinda Shetani, jamii na nafsi—ambavyo vyote hutuelekeza kutenda DHAMBI!

Paulo alisema, “Kwa maana twajua ya kuwa torati asili yake ni ya rohoni; bali mimi ni mtu wa mwilini [wa mwili, aliyeumbwa kwa nyama], nimeuzwa chini ya dhambi. Maana sijui nifanyalo, kwa sababu lile nilipendalo, silitendi; bali lile nilichukialo ndilo ninalolitenda†(fu. 14-15). Aliendelea, “kwa kuwa kutaka nataka, bali kutenda lililo jema sipati. Kwa maana lile jema nilipendalo [kulifanya], silitendi; bali lile baya nisilolipenda [kulifanya] ndilo nilitendalo†(fu. 18-19).

Inaonekana kana kwamba kila kitu alichokifanya Paulo au kile ambacho hakutaka kukifanya, hulka yake ya mwanadamu, mwili wake, ulimsababisha kutenda kinyume chake hasa! Kwa nini?

Mungu alimvuvia kurekodi jibu kwa ajili yetu: “Basi nimeona sheria hii, ya kuwa kwangu mimi nitakaye [kujaribu] kutenda lililo jema, lipo lililo baya. Lakini…naona sheria iliyo mbali, inapiga vita na ile sheria ya akili zangu, na kunifanya mateka ya ile sheria ya dhambi iliyo katika viungo vyangu†(fu. 21, 23).

Paulo aliendelea kuongeza kwamba ni kwa njia ya nguvu ya Nia ya Kristo ndani yake ndipo aliweza kushinda na kupata ushindi wa mwisho katika kutunza Sheria ya Mungu, badala ya kuitii ile “sheria†halisi ya dhambi. Ni kwa njia hii pekee ambapo baadaye Paulo alisema kwamba alikuwa “amepiga vita vizuri†na alikuwa “amemaliza mwendo wake†hadi ushindi.

Usifanye kosa. Ukristo ni vita! Lakini ni vita ambayo Mkristo anatarajia KUSHINDA!—kadri anavyoendelea kuwa karibu na Mungu ili kupata nguvu kwa ajili ya kushinda.

Mungu anatazama kusudi la moyo wako. Ni utashi wako wa ujumla na motisha ambavyo ni vya muhimu Kwake. Anataka kujua kama, baada ya kutenda dhambi, unasikitika kwa hilo na wakati wote unadhamiria kujitahidi kutenda vizuri zaidi. Anatambua majaribu yanayotuzinga tena vizuri zaidi kuliko sisi. Anaangalia kuona kama tutakuwa watulivu na macho kadri tunavyong’oa dhambi kutoka maishani mwetu—na kama tutaendelea kukaza mwendo mbele!

Kuweka Lengo

Kama ukweli unakuwa wazi—DHAHIRI kabisa—kwako, weka lengo la toba, ubatizo, na upokeaji wa Roho Takatifu ya Mungu—mwanzo wa UONGOFU WA KWELI!

Wakati unajiandaa kwa ajili ya kuongoka, fokasi katika kuchunguza tabia na mitazamo yote mibaya unayoweza kuiona. Kuna mabadiliko halisi ya nje ambayo unaweza kuyafanya kabla ya ubatizo. Fahamu. Uongofu unahusu kubadilika, kukua, kushinda—na kukuza tabia ya Mungu.

Chukua kila hatua kwa uangalifu. Fuata muda uliosahihi kwako. Lakini, usijicheleweshe bila ulazima, eti tu kwa sababu hujaomba kwa bidii au mara nyingi kwa ajili ya “karama†ya toba (2 Tim. 2:25; Matendo 11:18). Uwe mwangalifu usije ukafuata utaratibu wa ulimwengu, kuangukia katika kusubiri kwa hisia za kimwujiza kwamba “sasa ndio wakati.â€

Katika kipindi hiki, tumia muda kusoma maandiko yangu yote yanayohusu imani, uongofu, ubatizo, uwezekano wako wa kibinadamu, na uthibitisho wa uwepo wa Mungu, wa Neno Lake na wa Kanisa Lake.

Mengi—kwa hakika kila kitu—ni pata potea kwa ajili yako kama Mungu anakuita sasa!

Tabia Kamilifu ya Mungu

Mungu mkuu, mwenye nguvu zote, aliyeziumba mbingu na nchi, pia alikuumba wewe. Ulimwengu unaoonekana uliumbwa kuakisi utukufu wa Mungu, na kuwa zawadi nzuri kwa ajili ya mwanadamu kuona na kufurahia.

Uliumbwa kwa ajili ya kusudi kuu lisilo na kikomo. Uliumbwa ili kuwa kama Mungu katika kila nyanja ya maisha yako. Kumbuka, Mungu anazaliana Mwenyewe ndani ya watu—KUJENGA TABIA YA KIROHO ndani yao!

Ni mara chache sasa watu hata wanaongelea juu ya, au kujihusisha wenyewe na, ukuzaji wa tabia—uliojulikana kama “wema.†Inaonekana kwamba wachache sana leo wanafahamu juu ya hili. Ni kwa njia ya Neno la Mungu lililofunuliwa pekee ambapo fasili sahihi ya tabia inaelezwa na kueleweka.

Uliona kwamba tabia ni kufahamu—kujua—jema kutoka baya na kutenda lile lililo jema badala ya lile lililo baya! Kumbuka, Mungu anafunua lile lililo jema—JINSI YA KUISHI. Lakini tabia ya haki inajengwa kwa njia ya nguvu ya uamuzi huru—kuamua KUTENDA lililo jema. Tabia huchagua kutenda lile lililo jema badala ya kuchagua kutenda lile lililo baya. Haijishughulishi yenyewe na kitu gani WENGINE wanasema au kutenda. Inajishughulisha na kile tu ambacho MUNGU anasema kitendwe!

Mungu ni upendo. Upendo ni utimilifu wa sheria. Ni kitendo cha kuwajali wengine kinachotoka na kububujika, kuwatanguliza wengine—kabla ya matakwa binafsi.

Daima jikumbushe wewe mwenyewe kwamba kujenga tabia halisi ya Mungu ndiyo sababu ya wewe kuzaliwa!

Paulo alisema kwamba Roho ya Mungu inaakisi “akili timamu†(2 Tim. 1:7). Hata katika kiwango cha kibinadamu, ni watu wachache leo hii walio hata na “maarifa mengi ya kawaidaâ€. Inaonekana vigumu kuliko wakati wowote kubaki sawasawa na imara, kadri mashinikizo na shida zinapowazonga watu zinawasababisha kutenda vitu vingi ambavyo siyo timamu, vya kigeni na vya ajabu zaidi. Roho ya Mungu itakuongoza kwenye njia timamu za kufikiri zilizo imara, thabiti (Fil. 4:8). Itakusaidia kuona mambo yanayotendeka kukuzunguka, na kuyachukulia kwa namna ya kimungu. Itautua ufahamu wako na kukuongoza kufanya maamuzi ya hekima, sahihi na timamu katika maisha yako ya kila siku.

Jishughulishe! Jisukume kukua na kushinda. Usitegemee kwamba itakuwa rahisi, kama “kuanguka kutoka kwenye gogo la mti.†Ongezeka katika maarifa. Mara ukiongoka, tambua kwamba “umechaguliwa kuwa askari†na ni lazima wakati mwingine “kuvumilia taabu,†kama Paulo alivyomwandikia Timotheo (2 Tim. 2:3-4). Kuvunja mazoea yako yote ya zamani kutachukua muda. Hata hivyo, mazoea hayo umeyatenda—na, kwa namna fulani, hata uliyafanya vizuri zaidi—kwa maisha yote. Tabia zako zimekuwa sehemu yako. Zimekuwa “hulka ya pili.†Kwa hali yoyote, kumbuka kwamba tabia hizo siyo ile “tabia ya uungu†(2 Pet. 1:4)—na ni mbali sana nayo—inayoingia pamoja na kupokea Roho ya Mungu wakati wa ubatizo na uongofu.

Kama wewe ni mtu mzima, ilikuchukua miaka kumi na tano hadi ishirini kurefuka hadi kimo fulani. Ukristo hauna tofauti! Huo ni muda mrefu. Na huenda ilihusisha “maumivu mengi ya ukuaji.†Huenda ulianguka na ukajichuna goti au ulitoka damu puani mara nyingi kabla ya kufikia utu uzima. Ukristo hauna tofauti! Usikatishwe tamaa na ukaacha kukua, kama mtoto asivyotakiwa kukata tamaa na “kuacha maisha†kwa sababu tu atakuwa ameanguka chini au amejichuna goti. Mtoto wako anapoanguka, unamwambia asimame, kwa sababu ni sehemu ya maisha. Ukristo hauna tofauti!

Watoto wadogo siku zote wanataka kukua haraka zaidi kuliko ratiba ya maisha inavyoruhusu. Ingawa utoto ni wakati wa ajabu kwa namna nyingi, inaonekana kwamba wengi wa vijana hawawezi kusubiri kufikia utu uzima. Ukristo hauna tofauti! Lakini Ukristo kamili, utu uzima unakuja tu baada ya muda mrefu wa KUFANYIA MAZOEZI njia sahihi ya maisha.

Lakini Inakuwaje Mtu Akitenda Dhambi?

Tumethibitisha kwamba wanadamu wote wanatenda dhambi. Je Mkristo mpya aliyetungwa ategemee hili kuendelea baada ya ubatizo? Je ukamilifu unafikiwa kwa usiku mmoja kwa namna fulani ya “kukiri imani†au kwa kitendo cha toba na ubatizo?

Haiko hivyo! Kuna aya moja ndefu ya maandiko ambayo inasaidia sana kwenye somo la msamaha na mambo mengine yanayohusiana na hilo.

Mafungu yafuatayo yana maagizo mengi—lakini tu baada ya kuyasoma yote kwanza. Angalia: “…na ushirika wetu ni pamoja na Baba, na pamoja na Mwana Wake Yesu Kristo…ili furaha yetu itimizwe. Na hii ndiyo habari...kwamba Mungu ni nuru, wala giza lo lote hamna ndani Yake. Kama tukisema ya kwamba twashirikiana naye, tena tukienenda gizani, twasema uongo, wala hatuifanyi iliyo kweli; bali kama tukienenda nuruni, kama Yeye alivyo katika nuru, twashirikiana sisi kwa sisi, na damu Yake Yesu, Mwana Wake, yatusafisha dhambi yote. Kama tukisema kwamba hatuna dhambi, twajidanganya wenyewe, wala kweli haimo mwetu. Kama tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote. Kama tukisema kwamba hatukutenda dhambi, twamfanya Yeye kuwa mwongo wala neno Lake halimo mwetu. Watoto wangu wadogo, nawaandikia haya ili kwamba msitende dhambi. Na kama mtu akitenda dhambi tunaye Mwombezi kwa Baba, Yesu Kristo mwenye haki, naye ndiye kipatanisho kwa dhambi zetu†(1 Yohana 1:3-2:2).

Hapa kuna maagizo mengi ya muhimu. Fungua Biblia yako na hebu tuchunguze fungu baada ya fungu.

Fungu la 3: Yohana, mtume hai wa mwisho katika Biblia, akiongea kwa niaba ya mitume wote (“sisiâ€), anaeleza kwamba ushirika wa kweli wa Mkristo uko katika uwanda wa kiroho pamoja na Kristo na Baba. Ni kwa kupitia Hao tu kwamba Wakristo wanaweza kuwa na ushirika halisi wa kweli pamoja na kila mmoja, ndani ya Kanisa la Mungu.

Fungu la 4: Kusudi la Yohana lilikuwa ni kuwaonyesha watu chanzo cha furaha halisi, kamili ya kudumu.

Fungu la 5: Mungu wa kweli anawakilisha nuru—Yeye “ni nuruâ€â€”na hakuna chochote cha giza juu ya kile Anachokifanya au namna Alivyo. Mtu anayefanya ushirika na Mungu wa kweli wa Biblia huwa-anataka kuja kwenye nuru na kutoka kwenye giza lote la ulimwengu huu.

Fungu la 6: Hili ndilo fungu la kwanza la mafungu sita linaloanza na neno “ikiwa.†Matumizi ya neno hili mara zote huonyesha hali—katika suala hili, hali zile zinazohusisha uhuru wa maamuzi. Watu wengi wanadai “kumjua†Mungu, kufanya ushirika pamoja Naye, lakini hawamjui wala hawatendi KWELI Yake katika maisha yao. Anasema hii inawafanya wawe waongo dhahiri (2:4).

Fungu la 7: Damu ya Kristo inaendelea kusafisha dhambi zote—ila, makosa, udhaifu na mawaa—za mtu anayejitahidi kutembea katika kweli ya Mungu—na katika kufanya ushirika na Wakristo wengine wa kweli. Ingawa kwa kawaida hawakusudii, Wakristo huteleza na wanapaswa kurudi tena kwenye mstari.

Fungu la 8: Fungu hili ni la muhimu sana. Wakristo wanapaswa kukiri kwamba wanatenda dhambi. Umekuwa uzoefu wangu kwamba kujidanganya (Yer. 17:9) ni sababu moja kubwa sana inayowafanya watu wengi wasikue na kushinda kama inavyotakiwa. Kujidanganya mwenyewe—kujiambia uongo mwenyewe—bado ni uongo.

Na hakuna nafasi kwa ajili ya ile kweli kukaa ndani ya mtu kama huyo!

Fungu 9-10: Fungu la 9 haliongelei juu ya mtu ambaye hajaongoka, mwenye kufuata nia ya mwili. Kwa yule anayekiri na kutubu dhambi zake, mafungu haya yanajithibitisha yenyewe. Yesu Kristo yuko pale kumwosha—KUMSAFISHA!—Mkristo wa kweli wakati anapokuwa ametanga mbali kutoka kwenye nuru ya kuishi kwa Neno la Mungu na Sheria kwa kitambo. Mkristo lazima ajifunze kushinda. Kama ilivyo kujifunza kupiga kinanda au kuchora picha nzuri, hili halitokei kwa usiku mmoja.

Sura ya 2, mafungu 1-2: Yohana anatumia neno la upendo, “Watoto wangu wadogo,†kwa sababu hivyo ndivyo Mungu anavyowaangalia watoto Wake wakiume na wakike waliotungwa. Sisi wote ni watoto wadogo machoni Pake. Anajua Anahitaji kutuangalia kama wazazi wa kibinadamu wanavyowaangalia watoto wao wachanga. Ingawa ni kusudi la Mungu kwamba tusitende dhambi, tunapotenda dhambi, Kristo anasimama mbele ya Baba kama “Wakili†wetu. Kama Kuhani wetu Mkuu (Ebr. 4:14-16), Yesu kihalisia “anawaunga mkono†ndugu na dada Zake wadogo mbele ya Baba. Anajua ina maana gani kupambana na dhambi na kushinda, na anaahidi nguvu na msamaha kwa wale wanaokiri kwamba wanahitaji mambo yote mawili.

Mafungu manne yanayofuata katika 1 Yohana 2 yanamwelezea Mkristo mtiifu kama yule anayetunza Sheria ya Mungu na anajitahidi kutembea na kuishi maisha yale yale ambayo Yesu aliishi (fu. 6). Ni yule “anayetunza neno Lake (la Mungu),†akijitahidi kutolegeza masharti. Muda wote anatafuta kutenda kilicho sahihi.

Unapojikwaa, na wakati mwingine kuanguka chini, kumbuka maneno ya Daudi katika Zaburi 37:23-24: “Hatua za mtu zaimarishwa na BWANA…Ajapojikwaa hataanguka chini, BWANA humshika mkono na kumtegemeza.†Kama mzazi anyanyuavyo au amtegemezavyo mtoto, vivyo hivyo mara kwa mara Mungu huwanyanyua na “kuwashika†watoto Wake. Hebu ahadi hii ya Mungu ikutie moyo unapojisikia kukata tamaa kwa sababu umepungua katika mwenendo wa Mkristo.

Vipi Kuhusu Kifo?

Kumbuka, lengo la Mkristo ni kuwa kama Kristo na Baba—kuwa mkamilifu kama Mungu alivyo mkamilifu (Mat. 5:48). Vipi kama mtu anakufa kabla ya ukamilifu haujafikiwa? Je mtu huyo alishindwa? Je mtu anapotea kwa sababu hakufika kuwa mkamilifu kabisa katika maisha haya?

Hakuna mwanadamu ambaye atakuja kuwa mkamilifu kabisa akiwa angali katika mwili. Anatakiwa aendelee wakati wote kutafuta kuwa—kujitahidi kuwa—kama Kristo katika maisha yake yote.

Ukamilifu ni lengo ambalo linabeba njia ya maisha ambayo ni ya kutawala kila wazo la mtu, tendo na neno. Mungu anaangalia moyo, dhamira ya mtu anayejisalimisha Kwake. Alimradi anaendelea kukua kwa namna ya roho na kushinda—na anaongozwa na Roho Takatifu—anabaki kuwa mwongofu, mwana wa Mungu aliyetungwa. Kifo hakibadilishi kitu chochote, kwani Mungu ndiye anayetawala maisha ya Mkristo. Wakati Mkristo anapokufa, anakuwa “amelala tu katika Kristo.†Anasubiri ufufuo wa watakatifu wote na kuingia ufalme wa Mungu (1 Kor. 15:50-55; 1 Thes. 4:13-18).

Dhambi Isiyosamehewa

Wengi sana wana wasiwasi kwamba huenda wametenda “dhambi isiyosamehewa.†Nimewashauri makumi ya watu waliokuwa wamejawa na hofu na wasiwasi kwa sababu walikuwa wanahisi, au hata wakati mwingine walidhani “hakika,†kwamba walikuwa na hatia ya dhambi hii isiyosamehewa. Baada ya kushauriana nao, wakati wote ilikuwa wazi kwamba walikuwa bado. Lakini mara nyingi ilichukua mashauri mengi na ufafanuzi kuwathibitishia kwamba walikuwa hawajatenda dhambi isiyosamehewa.

Mara nyingi ilinilazimu kufafanua kwamba kitendo chenyewe cha kujishughulisha/kujali ni ushahidi kwamba mtu hajaenda mbali kiasi cha kupata hatia ya dhambi hii. Dhambi isiyosamehewa inahusisha makusudi, kudhamiria, dhambi iliyofikiriwa kabla ikijengwa juu ya uamuzi wa wazi na wa mwisho kutenda aina yoyote ya dhambi na kubaki ndani yake. Kigezo—kiini—mtazamo ni wa makusudi. Ndiyo, wengi hutenda dhambi kwa kuridhia—lakini hiyo ni tofauti na kutenda dhambi kwa makusudi.

Kila wakati watu wanapotenda dhambi, kwa hakika wanakuwa wako radhi kutenda kile walichotenda. Lakini kwa kawaida walizidiwa na aina fulani ya jaribu au hali ya mambo iliyowaruhusu kuteleza. Muda mfupi baada ya hapo walisikitika sana kwa ajili ya kile walichotenda. Ingawa hii haipunguzi uzito wa ubaya wa dhambi, kama mtu anasikitikia matendo yake na anataka kubadilika—anataka kutubu na kusamehewa—na hii inaambatana na uamuzi wa kutenda vyema wakati mwingine, basi yuko mbali na kuwa ametenda dhambi isiyosamehewa.

Mungu ni wa rehema na hata ana shauku ya kukusamehe—wakati unapotubu kutoka moyoni! Anasema kwamba Anakuhitaji wewe, na wale wote ambao Anawaita, kufanikiwa (2 Pet. 3:9; 1 Tim. 2:4). Wakati Shetani anajaribu watu, akitazamia waanguke, Mungu kwa nyakati fulani anawapima watumishi Wake, akitaraji—hata akitegemea—wapate kushinda. Kumbuka, Mungu hataki kabisa yeyote ashindwe!

Hivyo, kama unajali kwamba huenda umetenda dhambi isiyosamehewa, basi bado unajishughulisha na, kwa hiyo, hujaitenda! Kama hujamwacha Kristo, kwa kutaka, kwa makusudi, basi hujatenda dhambi isiyosamehewa! Ikiwa umekubali kushindwa na jaribu, na umevunja moja au zaidi ya sheria za Mungu, kubali na ukiri kwa Mungu. Bado unaweza kutubu, kubadilika na kuendelea mbele katika njia kuelekea kwenye uzima wa milele katika ufalme wa Mungu!

Usikate tamaa! Usiondoke! Mfalme Sulemani aliandika, “Ukizimia siku ya taabu, Nguvu zako ni chache†(Mit. 24:10), na “Kwa maana mwenye haki huanguka mara saba [hapa, neno la Kiebrania humaanisha nyingi] akaondoka tena; Bali wasio haki hukwazwa na mabaya†(fu. 16). Usije “ukarudi nyuma†(Ebr. 10:38-39).

Mara mbili, Kristo alisema, “Lakini mwenye kuvumilia hata mwisho, ndiye atakayeokoka†(Math. 24:13; 10:22). Mkristo haokolewi moja kwa moja wakati wa ubatizo na toba. Ukianguka chini, simama—mtafute Mungu, tubu na usonge mbele! Mungu ataendelea kukushika kama unaendelea KUVUMILIA!

Kumjua Mpinzani Wako

Wengi wanaelewa kile ambacho kawaida kinaitwa hulka ya mwanadamu. Biblia ina mengi ya kusema juu yake. Yule ambaye atakwenda kushinda majaribu na dhambi lazima afahamu kwamba anatakiwa kushughulikia na kuishinda hulka ya mwanadamu ili kufanikiwa!

Lakini HULKA YA MWANADAMU ni nini? Kwa nini ipo? Ilitoka wapi? Je Mungu aliiumba? Kwa nini ina ubinafsi sana na ovu? Wachache wameelewa somo hili. Baada ya hapa, tutajifunza ukweli wa kwa nini watu hufikiri na kutenda kama wanavyofanya.

Sura ya Tisa – Asili ya Hulka ya Mwanadamu

Masumbufu na maovu ya mwanadamu yametabiriwa kuongezeka zaidi katika zama hizi. Vurugu za kutisha, ugaidi na vita vinaongezeka kadiri hulka jeuri ya mwanadamu inavyozidi kutotawalika. Baada ya ufyatuaji risasi uliotokea shuleni hivi karibuni na kuacha wengi wakiwa wamechinjwa, mzazi mmoja alitamka, “siuelewi tena ulimwengu huu.â€

Unaweza kuuelewa ulimwengu huu na sababu ya masumbufu yake. Kuifahamu hulka ya mwanadamu ndio ufunguo.

Binadamu wote wanayo hulka ya mwanadamu. Ubinafsi, uozo, vurugu na maovu ya kutisha yanayochipuka kutokana na hulka ya mwanadamu vimeupiga ulimwengu kwa maelfu ya miaka. Kumbuka kwamba Yohana alisema, “Ulimwengu wote umo katika uovu†(1 Yohana 5:19). Sababu ya hali hii inatokana moja kwa moja na hulka ovu ya mwanadamu.

Kila “mtaalamu†ana mapendekezo tofauti kuhusu ni nini hulka ya mwanadamu na huwa inatoka wapi. Hata hivyo, hakuna anayefahamu majibu kwa maswali haya au kwa swali la kwa nini hulka ya mwanadamu ipo. Hii ni kwa sababu wanakikataa CHANZO kinachopelekea kufahamu majibu kwa maswali yote makuu ya maisha.

Zingatia kweli kinzani! Fikiri juu ya vitu vya kushangaza ambavyo FIKRA za mwanadamu zinaweza kutengeneza. Kama tulivyoeleza, ustadi na uvumbuzi wake kwa hakika havina kikomo. Hata hivyo haviwezi kutatua matatizo ya msingi kabisa ya maisha—umasikini, ujinga, uovu, uhalifu, vita na taabu.

Matatizo haya yote—na mengi zaidi—ni matokeo ya hulka ya mwanadamu isiyodhibitika!

Hakuna “Hulka Boraâ€

Wanateolojia na wanadini wengi wanafundisha kwamba wanadamu wote wamejaliwa “hulka bora†iliyojificha ndani, ikisubiri “kufunguliwa†na kutumiwa. Jambo hili siyo kweli. Biblia haisemi kitu kama hicho! Hata hivyo, mamilioni wanakubaliana nacho.

Fundisho hili linatokana na fundisho la kipagani la muda mrefu la utengano wa mwili na nafsi. Linasema kwamba wanadamu wote wana nafsi ya asili, iliyo safi iliyofungiwa ndani ya mwili mwovu ulio kama gereza hadi wakati wa kufa, ambapo nafsi huwekwa huru. Wazo hili ni jaribio la kufafanua asili ya hulka ya mwanadamu bila kuchunguza ukweli wa kile ambacho Mungu anasema.

Hakuna “Dhambi ya Asiliâ€

Mamilioni zaidi wanaamini fundisho lisilo la kibiblia la “dhambi ya asili.†Ingawa ni kweli Adamu na Hawa walitenda dhambi, Biblia haifundishi chochote kuhusu “dhambi†yoyote “ya asili†waliyoitenda, inayorithishwa, kizazi hata kizazi, kwa kila mtu. Neno lenyewe halipatikani popote katika maandiko na ni la kubuni—hadithi ya kufikirika!—ya wanadamu.

Kumbuka Warumi 3:23 ilisema, “Kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.†Kila mwanadamu ametenda dhambi kwa namna yake mwenyewe! Wote wanahusika na wana hatia kwa ajili ya dhambi zao wenyewe—siyo zile za Adamu na Hawa au mtu mwingine!

Dhambi ya Adamu na Hawa ilileta madhara yafuatayo: (1) Ilimfungia kabisa mwanadamu Mti wa Uzima na (2) ilileta adhabu ya kifo juu ya wanadamu wote (Mwa. 2:17; Ebr. 9:27; Rum. 6:23).

Kile Kristo Alichofundisha

Katika Marko 7, Kristo aliwahutubia wale ambao walifikiri wangekuwa “wamenajisika†kwa uchafu ambao wangeweza kuumeza kupitia kula chakula bila kunawa mikono. Mafarisayo walifika mbali, kunawa mikono yao mara kwa mara kuzuia “kunajisika,†na wakamwuliza Kristo kwanini wanafunzi Wake hawakufanya kama wao. Kwa hakika, Kristo alijua kwamba kumeza uchafu kidogo kwa bahati mbaya kutokana na kutonawa mikono hakumfanyi mtu yeyote kuwa najisi kwa namna ya roho.

Jibu Lake lilifafanua kile ambacho HUWATIA wanadamu unajisi: “Akasema, Kimtokacho mtu ndicho kimtiacho unajisi. Kwa maana ndani ya mioyo ya watu hutoka mawazo mabaya, uasherati, wivi, uuaji, uzinzi, tamaa mbaya, ukorofi, hila, ufisadi, kijicho, matukano, kiburi, upumbavu. Haya yote yaliyo maovu yatoka ndani, nayo yamtia mtu unajisi†(fu. 20-23).

Kwanza, kubali kwamba Kristo alitoa kauli—na kwamba lazima iwe ya kweli! Kauli hii, yenyewe, ni ufunuo wa kushangaza. Lakini tuliona kwamba Yeremia aliongeza zaidi: “MOYO huwa mdanganyifu kuliko vitu vyote, una ugonjwa wa kufisha; nani awezaye kuujua?†(Yer. 17:9). Kwa hakika, wengi hawafahamu hili kuhusu wao wenyewe, ingawa mara nyingi huliona haraka kwa wengine. Zaidi, tuliona kwamba Paulo, chini ya uvuvio wa Mungu, alirekodi, “Kwa kuwa ile nia ya mwili [asili] ni uadui juu ya Mungu, kwa maana haitii sheria ya Mungu, wala haiwezi kuitii†(Rum. 8:7).

Kwa kweli hizi ni kauli za kushangaza kuhusu fikra za kila mwanadamu. Lakini ni kwa jinsi gani mbubujiko huu wa mawazo mabaya, unaotoka ndani ya watu wote, ulikuja kuwepo kwa mara ya kwanza? Ulifikaje pale?

Je Mungu hupenyeza hulka ya mwanadamu ndani ya vitoto vichanga wakati wa kuzaliwa? Inawezekana Mungu wa upendo, mwenye hekima zote, mwenye uweza wote awachukue watoto wachanga wasio na hatia na kuwageuza kuwa waovu wa kutisha toka wakati wanapozaliwa? Na kama Mungu haweki hulka hii pale, basi huwa inatoka wapi? Tena, asili yake ni nini?

Hulka ya Mwanadamu Ndani ya Adamu Wakati wa Uumbaji?

Hebu tuulize: Je Adamu alipewa hulka ya mwanadamu na Mungu tokea wakati ule alipoumbwa? Mwanzo 1:26-27 inarekodi uumbaji wa mwanadamu uliofanywa na Mungu. Kisha fungu la 28 linasema, “Mungu akawabarikia, Mungu akawaambia, Zaeni, mkaongezeke…â€

Kama Mungu angekuwa amepenyeza uovu, ubinafsi, hulka ya mwanadamu ya dhambi ndani ya Adamu na Hawa wakati ule wa kuumbwa kwao, ingekuwa vigumu kuelezewa kama “kuwabarikiaâ€. Kama ingekuwa hivi, ingekuwa vyema kuelezewa kama “kuwalaaniâ€!

Sasa soma fungu la 31: “Mungu akaona kila kitu alichokifanya, na tazama, ni chema sana.†Fikiri juu ya kile ambacho andiko hili linasema. Kwa maana nyingine, ni kauli inayoduwaza kuhusu hulka ya mwanadamu. Hulka ya mwanadamu siyo “njema sanaâ€â€”ni OVU SANA! Hata hivyo, Mungu aliuita uumbaji Wake “mwema sanaâ€!

Aya moja nyingine ya Agano la Kale inatoa mwanga katika zao la Mungu la mwisho mwishoni mwa juma la Uumbaji. Sulemani aliandika hivi katika Mhubiri 7:29: “… hili tu nimeliona; Mungu amemfanya mwanadamu mnyofu, lakini wamebuni mavumbuzi mengi.†Mungu aliwaumba wanadamu katika hali ya “unyofuâ€, lakini wanadamu (“waoâ€) waligeukia “mavumbuzi†ya hulka ya mwanadamu.

Ikiwa Mungu “aliwabariki†Adamu na Hawa, alisema kwamba kile alichokifanya katika kuwatengeneza kilikuwa “chema sana,†na ki-asili aliwaumba “wanyofu†hivyo udanganyifu (Yer. 17:9), uadui dhidi ya Sheria ya Mungu, chuki, ubinafsi, kiburi, ubatili, tamaa na maovu mengine yote ya hulka ya mwanadamu (Marko 7:20-23) visingeweza kuwepo. Hakuna uthibitisho wa uasi dhidi ya Mungu au Njia Yake katika maelezo haya. Kwa hiyo, inawaelezea Adamu na Hawa kabla ya kukutana na Shetani.

Mrusha Matangazo Mkuu

Paulo aliliandikia Kanisa la Efeso kuhusu maisha ambayo Mungu alikuwa amewaita kutoka kwayo wakati Alipowafunulia ukweli Wake. Sura ya 2, fungu la 2, lililotajwa huko nyuma, huelezea nguvu za ibilisi na ushawishi wake juu ya ulimwengu: “Ambazo mliziendea zamani kwa kuifuata kawaida ya ulimwengu huu, na kwa kumfuata mfalme wa UWEZO wa anga, roho yule atendaye kazi sasa katika wana wa kuasi.â€

Hii ni aya ya kushangaza. Usemi “wana wa kuasi†pia unapatikana katika Waefeso 5:6 na Wakolosai 3:6. Hebu tuchunguze jinsi gani vielelezo hivi vinahusiana na usemi, “mfalme wa uwezo wa anga.â€

Angalia fungu la 2 linasema kwamba “roho ya Shetani…hutenda kazi katika wana wa kuasi.†Je unaliona hili? Unalielewa? Shetani ana uwezo wa kutumia “anga†kurusha matangazo, kwa njia ya roho yake, mtazamo wa uasi! Hupeleka hali za mioyo, hisia na mitazamo ya uadui katika fikra za watu. Haya “hutenda kazi†ndani ya mioyo na fikra za watu yakiwaletea uasi. “Nguvu hii ya anga†humpa ibilisi USHAWISHI mkubwa, ikimwezesha kupeleka mawazo ya mkanganyiko, udanganyifu, hasira, kiburi, chuki, upumbavu, ubatili, wivu, tamaa, uchoyo, husuda, uasi na mengine mengi moja kwa moja kwenye fikra za watu!

Fikiria hili kwa njia hii. Ibilisi anamiliki kituo cha redio kikubwa kuliko vyote, kinachorusha matangazo masaa 24 kwa siku. Tumejifunza kwamba “kituo†hiki chenye nguvu huufikia na kuudanganya ulimwengu wote! Hata hivyo, werevu wake wa kushangaza umekuwa wa kushawishi mno kiasi kwamba amefanikiwa kuwasadikisha wengi kwamba hayuko!

Ibilisi ana nguvu sana kuliko wengi wanavyodhani. Kumbuka, ni yeye tu aliye na nguvu nyingi kuweza kushawishi—kama “mungu†asiye bayana (na Shetani ni mungu wa ulimwengu huu)—anaweza kupofusha na kudanganya kwa kiwango kikubwa kiasi hiki. Matokeo yake, ametengeneza ulimwengu uliojawa na uasi—utovu wa sheria!

Kabla ya ugunduzi wa redio, uwezo wa Shetani kama mrusha matangazo, wa kutisha na mfalme wa nguvu za anga, haukuweza kufahamika kwa urahisi. Lakini sasa unaweza kumtambua!

Sasa tunaweza kuwafahamu vizuri “wana wa kuasi.†Kama vile Wakristo walivyo na Roho Takatifu, watu hawa pia wanavuviwa na kuongozwa na roho—ile ya mungu wa ulimwengu huu. Shetani hurusha roho ya uasi dhidi ya Sheria ya Mungu—uasi—kupitia mitazamo—ndani ya wanadamu. Waefeso 2:2 iko wazi. Lakini ulimwengu uliodanganywa haujui chochote juu ya ufahamu huu!

Kama ukisikiliza redio, kwa kawaida unatafuta kituo kinachocheza kile unachotaka kusikia. Leo, watu “huvinjari†vituo vya redio au runinga. Hatimaye, kitu fulani huwavutia, na husimama na kusikiliza kituo walichochagua. Katika kila hali, vituo huchaguliwa kwa kupenda. Watu wana mamlaka juu ya kile wanachosikia au kukitazama.

Sivyo ilivyo kwa kituo cha Shetani. Ulimwengu—na wewe—hauamui kutuni [fungulia] kwenye matangazo ya ibilisi. Na hakuna yeyote kwa wakati wowote anayeamua kudanganywa. Lakini kila mwanadamu duniani ametuni kwenye mawimbi ya Shetani moja kwa moja! Uovu wake, uadui, uasi, udanganyifu na ubinafsi “viko hewani†wakati wote.

Kwa hiyo, kwa hakika ni HULKA YA SHETANI inayotambuliwa [inayopachikwa] kimakosa kama HULKA YA MWANADAMU. Kusema kweli, mara inapoingizwa kwa watu, hulka ya Shetani inakuwa ya asili kwao. Inakuwa hulka yao—sasa, hulka ya mwanadamu.

Japokuwa huwezi kuiona kama vile usivyoweza kuona mawimbi ya redio au runinga, anga linalokuzunguka kwa hakika limejaa chaji na “kufurika†uwezo na nguvu za matangazo ya Shetani.

Kwa kweli ni muhimu kuona jinsi roho hii inavyotenda kazi ndani ya watu. Ni ufunguo pekee mkuu kufungulia mlango wa kufahamu hasa jinsi Shetani anavyoweza kudanganya na kutawala kwa werevu zaidi ya watu bilioni sita na nusu.

Kumbuka jinsi ambavyo Mungu aliweza kuwasiliana na Silasi kupitia (kwa “kuiamushaâ€) roho yake. Shetani hufanya vivyo hivyo. Kama vile ambavyo Mungu anaweza kumwongoza mwanadamu kwa kusudi jema, roho ya Shetani huwashawishi watu kuelekea chuki, hasira, ubinafsi, vurugu, mashindano, ubatili, wivu, tamaa, uchoyo, uuaji na udanganyifu.

Kwa hakika, wakati Shetani anapoingiza mitazamo yake ndani ya ubinadamu usiotilia shaka, hauna wazo kwamba anafanya hivyo. Ibilisi hatangazi makusudi yake kabla au kuongea kwa sauti ya kusikika.

Mauaji, Uongo na Uharibifu

Kama vile Mungu Baba alivyo na wana, mungu wa ulimwengu huu naye ni baba akiwa na watoto wake! Zingatia uthibitisho huu:

Kwenye tukio moja, Paulo alimwambia mchawi aliyeitwa Bar-yesu, aliyekuwa anajaribu kuzuia mahubiri na huduma ya Paulo. Paulo alimwita mtu huyu moja kwa moja: “Ewe mwenye kujaa hila na uovu wote, mwana wa ibilisi, adui wa haki yote, huachi kuzipotoa njia za Bwana zilizonyoka?†(Matendo 13:10).

Kando na kumtambua kama “mwana wa ibilisi,†Paulo anafundisha kwamba watoto wa ibilisi ni maadui wa “haki yote†na “njia za Mungu.†Hii ndiyo maana ya kuwa mwana wa ibilisi!

Lakini haki ni nini? Zaburi 119:172 inaifasili: “Maana MAAGIZO Yako yote [ya Mungu] NI HAKI.â€

Wana wa Shetani wanachukia, na ni maadui wa, sheria za Mungu—maagizo Yake! Kumbuka, wanatambuliwa kama “wana wa kuasi.â€

Ufunuo 19:11 inamweleza Shetani kama “mharabu.†Neno la Kiebrania lililorejelewa hapa, Abadoni, maana yake ni “Shetani.†Neno la Kiyunani lililotumika pale, “Apolioniâ€, maana yake ni “mharabu.†Ufahamu huu unaweka jukwaa kwa ajili ya andiko linalofuata.

Makabiliano ya kushangaza baina ya Kristo na watu waliodai “kumwamini†yalitokea katika Yohana 8:30-31. Unatakiwa kusoma kisa chote, lakini huu hapa ni muhtasari wake. Wale waliokuwa wamedai kuwa na imani katika Kristo kwa hakika walitafuta kumwua muda mfupi tu baadaye (fu. 37)! Kristo alisema, “Lakini mnatafuta KUNIUA Mimi, kwa sababu neno Langu halimo ndani yenu.â€Aliongezea tena, “Lakini sasa mnatafuta kuniua Mimi, Mtu ambaye nimewaambia iliyo kweli†(fu. 40). Wengi wanasema wanataka kusikia iliyo kweli—lakini siyo kama inamaanisha kuambiwa kwamba wana makosa, hasa kuhusu mawazo yaliyotunzwa kwa upendo mkubwa.

Kisa hiki kinafikia kilele cha kushangaza katika mafungu ya 43-44. Kristo aliwauliza, “Mbona hamyafahamu hayo niyasemayo?†Akajibu swali Lake Mwenyewe na “...kwa sababu ninyi hamwezi kulisikia neno Langu.†Nini hasa kinachoweza kusababisha watu waliosimama kando ya Kristo kushindwa “kusikia neno Lake�

Fungu la 44 linajibu, “Ninyi ni wa baba yenu, ibilisi, na tamaa za baba yenu ndizo mpendazo kuzitenda. Yeye alikuwa mwuaji tangu mwanzo; wala hakusimama katika kweli, kwa kuwa hamna hiyo kweli ndani yake. Asemapo uongo, husema yaliyo yake mwenyewe; kwa sababu yeye ni mwongo, na baba wa huo.†Kristo alisema wazi, “Ninyi si wa Mungu†(fu. 47), na hawa viongozi wa kidini wanaovuviwa na Shetani mara ile wakamshutumu kwamba “ana pepo†(fu. 48)! Wengi wanaodai “kumwamini Kristo†leo hawana tofauti na wale walioelezewa hapa.

Maelezo haya ni kauli nzito, yenye kuelekeza. Jitahidi mwenyewe kuliona hili. Ibilisi ni baba anayeua, kudanganya na kuharibu. Kama mwanzilishi wa mauaji, udanganyifu na uharibifu, husambaza mitazamo hii kwa watoto wake ulimwenguni kote!

Shetani Anashikilia Utawala Juu ya Dunia

Usifanye kosa! Ulimwengu umejawa na watoto wa ibilisi. Imekuja kuonekana kwamba watoto kimsingi ni kama wazazi wao. Kwa hiyo, wana wa Shetani hudanganya, huchukia, huua na huharibu. Utazame ulimwengu. Ni lazima sasa iwe wazi kabisa KWA NINI mkanganyiko, vita, ujinga, umasikini, magonjwa na taabu vimejaa miongoni mwa mataifa. Matunda ya hulka ya mwanadamu—hulka ya Shetani—yako wazi kila mahali waliko wanadamu.

Angalia jinsi ambavyo Paulo alielezea “siku za mwisho†zinazotangulia Kurudi kwa Kristo: “Lakini ufahamu neno hili, ya kuwa siku za mwisho kutakuwako nyakati za hatari [kutisha]. Maana watu watakuwa wenye kujipenda wenyewe, wenye kupenda fedha, wenye kujisifu, wenye kiburi, wenye kutukana, wasiotii wazazi wao, wasio na shukrani, wasio safi, wasiowapenda wa kwao, wasiotaka kufanya suluhu, wasingiziaji, wasiojizuia, wakali, wasiopenda mema, wasaliti, wakaidi, wenye kujivuna, wapendao anasa kuliko kumpenda Mungu; wenye mfano wa utauwa, lakini wakikana NGUVU zake; hao nao ujiepushe nao†(2 Tim. 3:1-5).

Wakati ulimwengu umejawa na dini—una “mfano wa utauwaâ€â€”haufundishi ukweli wala si dini ya Mungu! Unakataa nguvu ya Mungu wa kweli, na ulimwengu unaabudu kiumbe tofauti bila kujua ambaye anatamba mwenyewe kama Mungu wa Biblia.

Katika kurejea, ibilisi pia anaitwa “mungu wa ulimwengu huu,†“mfalme wa ulimwengu huu,†“mfalme wa nguvu za anga,†na mmoja ambaye tuliona “huyadhoofisha mataifa†na “audanganyaye ulimwengu wote.†Haya yote lazima yawe yamebeba maana mpya.

Uchaguzi wa Adamu wa Kihistoria

Lakini jinsi gani ibilisi alipata kumfikia mwanadamu? Kitu gani kilifungua mlango kwa ushawishi wake—kwa matangazo yake?

Ingawa imeelezwa huko nyuma, lakini kwa mtazamo mwingine, kisa kinachojulikana sana bali kinachoeleweka kwa kiwango kidogo sana cha Bustani ya Edeni kinashikilia ufunguo:

“Basi nyoka [Shetani] alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu aliowafanya BWANA Mungu. Akamwambia mwanamke, Ati! Hivi ndivyo alivyosema Mungu, Msile matunda ya miti yote ya bustani? Mwanamke akamwambia nyoka, Matunda ya miti ya bustanini twaweza kula; lakini matunda ya mti ulio katikati ya bustani Mungu amesema, Msiyale wala msiyaguse, msije mkafa. Nyoka akamwambia mwanamke, Hakika hamtakufa, kwa maana Mungu anajua ya kwamba siku mtakayokula matunda ya mti huo, mtafumbuliwa macho, nanyi mtakuwa kama Mungu, mkijua mema na mabaya. Mwanamke alipoona ya kuwa ule mti wafaa kwa chakula, wapendeza macho, nao ni mti wa kutamanika kwa maarifa, basi alitwaa katika matunda yake akala, akampa na mumewe, naye akala. Wakafumbuliwa macho wote wawili wakajijua kuwa wa uchi, wakashona majani ya mtini, wakajifanyia nguo†(Mwa. 3:1-7).

Hata zaidi ya tulivyokwisha kuona, kisa hiki kinawakilisha uamuzi unaoshangaza—na kwa kweli unaofika-mbali. Badala ya kufuata maelekezo ya Mungu, Adamu alichukua matunda ya “mti wa ujuzi wa mema na mabaya.†Alidhani kwamba alijua vizuri zaidi kuliko Mungu. Alijichukulia mwenyewe haki ya kuamua baina ya kile kilicho sahihi [chema] na kile kisicho sahihi [kibaya]. Alifikiri kwamba angeweza kutegemea fahamu zake mwenyewe za kimwili. Kwa njia hii, uamuzi huu “ulifungua macho yake†(fu. 7)—lakini si kwa mambo ya Mungu, ambayo huja tu kwa kupokea Roho ya Mungu (1 Kor. 1:9-10). Bila shaka, haikuwa Roho ya Mungu iliyowaingia Adamu na Hawa muda huu. Bali, roho ya upinzani iliingia kwenye fikra zao kwa mara ya kwanza kabisa. Roho mbaya ya ushawishi wa Shetani iliingizwa katika fikra zao muda huo kama mwonekano wa kwanza kabisa wa “hulka ya mwanadamu.†Hivi ndivyo jinsi “macho yao yalivyofumbuliwa.â€

Uamuzi wa Adamu kwa wakati huo ulifungia fursa yoyote ya kupata maarifa ya kweli ya kiroho kutoka kwa Mungu. Hivyo, ufahamu wake ukabaki na kikomo kwa kile tu ambacho angeweza kujifunza kupitia milango mitano ya fahamu za kimwili—na kumwacha akiwa wazi kupokea matangazo ya Shetani. Hulka ya mwanadamu ikapata kuwepo kwa mara ya kwanza!

Kwa sababu ya uamuzi huu, Adamu akawa amejitenga kabisa yeye mwenyewe na ubinadamu asimfikie Mungu. Huu mti mwingine umekuwa ukielekeza watu na mataifa namna ya kufikiri tangia hapo uamuzi wa Adamu wa kihistoria. Lazima tuelewe hii inamaanisha nini kwa ajili yako na mimi. Kwa dhambi yake ya kumkataa Mungu na Mti wa Uzima, Adamu alikataliwa na Mungu na kufukuzwa kutoka bustanini. Na ubinadamu ulitupwa nje pamoja naye kwenye ulimwengu wa Shetani!

Shetani alimdanganya Hawa, aliyemwongoza Adamu kuingia dhambini pamoja naye. Aliwafanya wakatae—wasiamini!—kile ambacho Mungu alikuwa amewafundisha katika Mwanzo 2:16-17. Udanganyifu wa ibilisi uliwafanya watoto hawa wawili wakubwa kuamini kwamba walikuwa hawahitaji tena kumsikiliza Mzazi wao. Hulka ya mwanadamu ikaingia. Wakiwa wamefukuzwa kutoka bustanini, walilazimika kujitafutia. Wakiwa wameikataa Sheria kamilifu ya Mungu (Rum. 7:12, 14) na utawala—SERIKALI Yake juu ya uumbaji wote—kama viongozi katika maisha yao, na wakiwa wamesalimu amri kwa Shetani na njia yake ya dhambi (2 Tim. 2:25-26), walibaki wenyewe peke yao.

Kwa sababu ya dhambi, hawakuwa tena na uwezo wa kuzifikia baraka za Mungu, uongozi, ulinzi au karama ya Roho Yake Takatifu, ambayo ingekuja kwa kula matunda ya Mti wa Uzima.

Hulka Ya Mwanadamu Hairithiwi

Shika hili! Hulka ya mwanadamu haikutoka kwa Mungu, lakini badala yake moja kwa moja kutoka kwa Shetani ibilisi.

Lakini hulka ya mwanadamu hairithiwi—inapatikana (hasa kwa kujifunza au kujizoeza)! Watoto wa Adamu na vizazi vyote vilivyofuata “hawakuirithisha†wakati wa kutunga mimba. Mzazi anayepoteza jicho, mkono au mguu hazai watoto wenye jicho moja, mkono mmoja au mguu mmoja. Wakati Mungu alipotumia ubavu mmoja wa Adamu kumuumba Hawa, haikuwa na maana kwamba wanaume wote baada ya hapo wanapungukiwa na ubavu mmoja. Biblia inamrejelea mtoto wao Habili kama “Habili mwenye haki.†Uasi wao haukuzuia utii wake.

Adamu na Hawa walikuwa “watoto†wakubwa. Vile vile kama watoto wanaozaliwa leo, walikuwa safi wakati wa kuumbwa kwao (“kuzaliwaâ€) lakini kwa haraka wakawa wazi kwa “tangazo†ambalo hawakuweza kulizuia. Waliumbwa siku ya sita ya juma (Ijumaa), wakapumuzika siku ya Sabato (Jumamosi), na huenda walishawishiwa na Shetani (Mwa. 3:1-6) siku iliyofuata (Jumapili)—katika umri wa siku mbili! Hivyo, tena, Shetani alikuwa anasubiri kwa ajili ya Adamu na Hawa wasioshuku [tilia shaka] na ambao bado walikuwa hawana hatia.

Adamu na Hawa WALICHAGUA kutomsikiliza Mzazi wao, Mungu, lakini badala yake WALICHAGUA kuamini uongo wa Shetani kwamba “hakika wasingekufa.†Kwa kufanya hivyo, walikataa utawala wa serikali ya Mungu katika maisha yao. Tena, kama Adamu angetii maelekezo ya Mungu, angeweza kufuzu kumwondoa Shetani na kurejesha SERIKALI ya Mungu duniani.

Hebu tuchunguze agizo moja la muhimu la Agano Jipya na mfano wa jinsi ambavyo hulka ya mwanadamu inavyopatikana, siyo kurithiwa. Paulo alitoa mwanga muhimu katika onyo lifuatalo alilolitoa kwa Kanisa la Wakorintho: “Maana nawaonea wivu, wivu wa Mungu; kwa kuwa naliwaposea mume mmoja, ili nimletee Kristo bikira safi. Lakini nachelea; kama yule nyoka alivyomdanganya Hawa kwa HILA yake, asije akawaharibu fikra zenu, mkauacha urahisi [wepesi] ulio katika Kristo†(2 Kor. 11:2-3).

Paulo alikuwa akiwaandikia watu walioishi miaka 4,000 baada ya Adamu na Hawa. Alitambua kwamba ibilisi alikuwa yungali hai akitenda kazi. Wakorintho walikuwa watu wazima wenye uwezekano wa kudanganywa (laghaiwa) kwa namna ile ile kama Hawa. Paulo aliwaonya wawe macho kwamba wasirejee kufuata njia za hulka ya mwanadamu. Kama vile ambavyo hulka ya Hawa haikuwa mbaya na yenye uadui kwa Mungu kabla hajadanganywa, vivyo hivyo hulka za Wakorintho waongofu.

Mara ile mtu anapoitwa na kuongoka, akiisha kupokea Roho ya Mungu, ameivua hulka ya mwanadamu ya zamani ya maisha yake yaliyopita. Paulo pia aliongeza katika Waefeso 2:3, “Ambao zamani, sisi sote nasi tulienenda kati yao, katika tamaa za miili yetu, tulipoyatimiza mapenzi ya mwili na ya nia, tukawa KWA TABIA YETU watoto wa hasira kama na hao wengine.†Mafungu haya yanafuata na ni sehemu ya maandiko yanayomtambulisha Shetani kama “mfalme wa nguvu za anga.â€

Ifuatayo ni aya ile ile kutoka kwenye tafsiri ya Phillips ya Agano Jipya. Tafsiri hii kwa usahihi inaelezea jinsi ambavyo watu wote wamepata hulka ya mwanadamu kutoka kwa Shetani. “Mliserereka juu ya kijito cha mawazo ya namna ya kuishi ya ulimwengu huu, na mlimtii MTAWALA WAKE ASIYEONEKANA [Shetani ndiye “mtawala asiyeonekana†wa ulimwengu huu—2 Kor. 4:4—ambaye bado anatenda kazi ndani ya wale wasioitikia kweli ya Mungu]…Sisi sote tuliishi namna hiyo wakati uliopita, na tulifuata hisia na mawazo ya HULKA ZETU MBAYA…kama alivyo mtu mwingine yeyote.â€

Ni kweli jinsi gani! Watu wengi husonga mbele maishani wakifuata hisia (“misisimkoâ€) na mawazo (“mafikaraâ€) vinavyowajia siku kwa siku. Sura yote ya Waefeso 1 ni maelezo ya Paulo kwa ndugu hao kuhusu mwito wao wa awali katika njia ya Mungu ya maisha. Chukua muda ili kuisoma, ikiwezekana utumie tafsiri ya Moffatt. Waefeso walikuwa wametoka katika mfumo wa ulimwengu huu na hawakuwa tena “kwa asili†watoto wa hasira, na walikuwa hawamtii tena “mfalme wa nguvu za anga.†Walikuwa wameshaanza “kuachana†na hulka ya mwanadamu kwa kujisalimisha kwa Mungu badala ya misisimko, mivuto, hisia na mawimbi ya majaribu ya Shetani.

Isingekuwa vyema kwa Mungu kuwaingizia hulka ya mwanadamu watoto wachanga wanaozaliwa, na kisha kuwaweka chini ya “hasira†Yake kwa sababu ya kuwa nayo. Je unaiona pointi hii? Hulka ya mwanadamu inapatikana, pamoja na hulka hii inayopatikana inaongoza kwenye kumwasi Mungu—na HII huwaweka watu chini ya hasira ya Mungu!

Wakristo Walioongoka Hawana Kinga

Hebu turudi kwa Mkristo. Ukweli kwamba mtu ametubu, amebatizwa na kupokea Roho ya Mungu (Matendo 2:38) haitangui au kuzuia moja kwa moja uwezo wa Shetani kushambulia, kujaribu, kutafuta kushawishi, na kuchunguza kwa makini palipo na udhaifu.

Kubali ukweli huu! Umekuwa ukitekeleza njia ya Shetani kwa maisha yako yote. Pengine umekuwa mzuri sana katika njia hii. Niamini, kadri unavyojitahidi kushinda na kupinga mivuto inayotenda kazi ndani yako, utaona kwamba ushawishi wa Shetani, katika sura ya hulka ya mwanadamu, ni, kama tabia zako, kwa kweli “hulka ya pili†kwako—zaidi ya unavyojua sasa! Kushinda haitakuwa rahisi au kutokea usiku mmoja. Ni pambano la maisha yote dhidi ya msimamo na njia ya maisha ambayo Mkristo ameikataa na kugeuka kuiacha.

Kumbuka, ibilisi alionekana katika umbo la nyoka na AKAMSHAWISHI Hawa kwa mafanikio kupitia jaribu (Mwa. 3:1-6). Fungu la kwanza linafunua jinsi anavyojaribu watu kuingia kwenye uasi na dhambi. Inasema, “Basi nyoka alikuwa mwerevu kuliko wanyama wote wa mwitu...†Shetani alimdanganya Hawa kwa kumjaribu na uzuri wa mti ambao matunda yake Mungu alimwambia asiyale.

Jaribu kamwe halitoki kwa Mungu. Yakobo 1:13-15 inasema, “Mtu ajaribiwapo, asiseme, Ninajaribiwa na Mungu; maana Mungu hawezi kujaribiwa na maovu, wala Yeye mwenyewe hamjaribu mtu. Lakini kila mmoja hujaribiwa na tamaa yake mwenyewe huku akivutwa na kudanganywa. Halafu ile tamaa ikiisha kuchukua mimba huzaa dhambi, na ile dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.â€

Jaribu wakati wote huanzia kwa “mjaribu,†akitenda kazi kwenye tamaa za watu. Ibilisi anatambua mahali ambapo hulka ya mwanadamu inaweza kudhuriwa, mahali ambapo watu wanaweza “kudanganywa†ili kwamba “dhambi itungwe.â€

Waefeso 6:11 inaonya dhidi ya “hila za Shetani,†wakati Ufunuo 2:24 inaonya dhidi ya “fumbo za Shetaniâ€! 2 Wakorintho 2:11 inaonya tusiwe “wajinga kwa fikra zake.†Wakristo daima wako macho kwa njama zake.

Yakobo alifundisha, “BASI MTIINI Mungu. Mpingeni Shetani, naye atawakimbia†(4:7).

Kristo Alishinda na Akafuzu Kuchukua Mahali pa Shetani

Kupinga jaribu la ibilisi ndiyo ilikuwa kitovu cha Kristo kushinda dhambi. Hebu tuchunguze kisa hiki, lakini wakati huu kwa kina zaidi.

Kinapatikana katika Mathayo 4, na kinaanza katika fungu la 1: “Kisha Yesu alipandishwa na Roho...ili ajaribiwe na ibilisi.†Ibilisi alimjaribu Kristo mara kwa mara: “Kisha ibilisi akamchukua mpaka mlima mrefu mno, akamwonyesha milki zote za ulimwengu, na fahari yake, Akamwambia, Haya yote nitakupa, ukianguka kunisujudia†(fu. 8-9). Angalia kwamba Kristo alimkemea Shetani (fu. 10) na akanukuu Kumbukumbu la Torati 6:13: “Mche Bwana, Mungu wako; ndiye utakayemtumikia.†Kwenye pointi hii, jaribu la mwisho katika kisa hiki likaisha na ibilisi akaondoka. Kristo alikuwa amepinga kwa mafanikio!

Elewa aya hii muhimu! Kisa hiki kinaelezea kujaribiwa kwa Kristo. Kile ambacho ibilisi alimwahidi kilikusudiwa Kumjaribu. Ikiwa kama Kristo na Shetani wote walijua kwamba milki za ulimwengu huu hazikuwa za ibilisi kutoa, basi jaribu lilikuwa wapi? Ahadi isingekuwa na uzito wowote—ingekuwa tupu—kama mataifa na himaya hazikuwa za ibilisi kutoa.

Kwa Kristo kushinda lile jaribu palilazimika KUWEPO jaribu! Hatimaye, Kristo alifanikiwa mahali ambapo Adamu na Hawa walishindwa. Kristo alifaulu jaribio halisi kabisa! Aliushinda ulimwengu, ibilisi na mwili Wake, katika kuishinda dhambi na kufaulu kulipa fidia (maisha Yake) kwa ajili ya ukombozi wa mwanadamu.

Shika pointi hii muhimu hasa. Ni kwa kumshinda ibilisi pekee ndipo Kristo alipofuzu kurejesha serikali ya Mungu duniani wakati wa Kuja Kwake mara ya Pili!

Baada ya kulipinga jaribu kwa mafanikio katika Mathayo 4, Kristo alianza kuihubiri injili ya ufalme wa Mungu. Kumbuka maelezo ya Marko: “Mwanzo wa injili ya Yesu Kristo, Mwana wa Mungu...Hata baada ya Yohana kutiwa gerezani, Yesu akaenda Galilaya, akiihubiri Injili ya ufalme wa Mungu, akisema, Wakati umetimia, na ufalme wa Mungu umekaribia; tubuni, na kuiamini injili†(1:1, 14-15).

“Wakati ambao ulikuwa umetimia†ulikuwa ni ule wa USHINDI MKUU wa Kristo katika pambano Lake kwa kumshinda Shetani na ulimwengu wake. Ushindi huu kwa hakika ulimuidhinisha Kristo kutangaza kurejea kwa serikali ya Mungu, takribani miaka 2,000 baadaye, chini ya uongozi Wake. Kutawazwa Kwake katika ofisi ya wakati ujao sasa kulikuwa rasmi.

Katika wakati huu, Mungu lazima aite wachache—wachache sana—ili wawekwe tayari kwa ajili ya wakati wa uzinduzi wa serikali ile na kutawala katika ufalme wa Mungu pamoja na Kristo. Wachache hawa lazima pia washinde, kama vile Kristo alivyoshinda, ili kustahili kwa ajili ya utawala—na Shetani anawachukia wale wote wanaofuzu kuchukua mahali pake!

Kushinda Siyo Rahisi

Hebu wakati huu turudi kwenye suala la ujenzi wa tabia kwa njia ya kushinda.

Kama ilivyo kwa msuli wowote mwilini, tabia inajengwa kwa kusukuma dhidi ya upinzani. Kuukabili upinzani huo kwa mafanikio huimarisha msuli (katika hili, fikra). Tumeona mara kwa mara kwamba kujenga tabia inamaanisha kuchagua kutenda lililo jema badala ya kuchagua kutenda lililo baya. Tabia haijishughulishi na kile ambacho watu WENGINE wanasema au kutenda. Inajishughulisha tu na kile ambacho MUNGU anasema kitendwe!

Usisahau kamwe kwamba Mkristo lazima ampinge Shetani, ambaye yuko kazini kila mahali. Lakini si kwa njia ya nguvu za kibinadamu pekee kwamba hili linaweza kufikiwa.

Mapema, tulirejelea hila za Shetani, na Paulo alirekodi, “Hatimaye, ndugu zangu, mzidi kuwa hodari katika Bwana na katika uweza wa nguvu Zake. Vaeni silaha zote za Mungu, mpate kuweza kuzipinga hila za Shetani. Kwa maana kushindana kwetu sisi si juu ya damu na nyama; bali ni juu ya falme na mamlaka, juu ya WAKUU wa giza la ulimwengu huu, juu ya majeshi ya pepo wabaya katika mahali pa juu†(Efe. 6:10-12).

Andiko hili lina mengi ya kuzingatia. Wakristo lazima “washindane†kwa nguvu dhidi ya nguvu za ibilisi na mapepo yake—“pepo wabayaâ€â€”siku kwa siku. Ni lazima wapambane daima dhidi ya hisia za kukwazwa, uadui, husuda, hasira na mitazamo mingine mingi.

Maandiko mengi ya Agano Jipya yanaeleza kiwango ambacho kwacho hulka ya mwanadamu, kama haitadhibitiwa kwa kushinda, ina utawala kamili juu ya kila nyanja ya maisha ya watu. Na matunda ya hulka ya mwanadamu yako dhahiri ulimwenguni kote. Kwa uangalifu zingatia na fikiria juu ya aya pana nne zifuatazo. Tafakari juu ya ushahidi wake katika maisha yako, na tambua kwamba zinawakilisha orodha ya mambo ambayo huenda unahitaji kuyashinda.

Paulo aliwaandikia Wagalatia, “Basi matendo ya mwili ni dhahiri [wazi], ndiyo haya, uasherati, uchafu, ufisadi, ibada ya sanamu, uchawi, uadui, ugomvi, wivu, hasira, fitina, faraka, uzushi, husuda, ulevi, ulafi, na mambo yanayofanana na hayo, katika hayo nawaambia mapema, kama nilivyokwisha kuwaambia, ya kwamba watu watendao mambo ya jinsi hiyo hawataurithi ufalme wa Mungu†(5:19-21).

Kushinda—kutokomeza mitindo hii ya mwenendo na namna ya kufikiri—moja kwa moja kumeungana na wokovu na kutawala katika ufalme wa Mungu!

Sasa zingatia kile Paulo alichowaandikia Warumi: “Na kama walivyokataa kuwa na Mungu katika fahamu zao, Mungu aliwaacha wafuate akili zao zisizofaa [zisizokuwa na maamuzi], wayafanye yasiyowapasa. Wamejawa na udhalimu wa kila namna, uovu na tamaa na ubaya; wamejawa na husuda, na uuaji, na fitina, na hadaa; watu wa nia mbaya, wenye kusengenya, wenye kusingizia, wenye kumchukia Mungu, wenye jeuri, wenye kutakabari, wenye majivuno, wenye kutunga mabaya, wasiowatii wazazi wao, wasio na ufahamu, wenye kuvunja maagano, wasiopenda jamaa zao, wasio na rehema; ambao wakijua sana hukumu ya haki ya Mungu, ya kwamba wayatendao hayo wamestahili mauti, wanatenda hayo, wala si hivyo tu, bali wanakubaliana nao wayatendao†(1:28-32).

Orodha hii nzito ya mitazamo mibaya na mienendo inatoa muhtasari wa hali ya ubinadamu wote.

Paulo pia aliwaandikia Warumi juu ya ulimwengu wote ulio chini ya ushawishi na utawala wa ibilisi. Angalia hii: “HAKUNA mwenye haki hata mmoja. HAKUNA afahamuye; HAKUNA amtafutaye Mungu. WOTE wamepotoka, wameoza wote pia; HAKUNA mtenda mema, la! Hata mmoja. Koo lao ni kaburi wazi, Kwa ndimi zao wametumia hila. Sumu ya fira i chini ya midomo yao. Vinywa vyao vimejaa laana na uchungu. Miguu yao ina mbio kumwaga damu. Uharibifu na mashaka yamo njiani mwao†(3:10-16).

Si ajabu Yohana aliwaamuru Wakristo wa kweli wa zama zote katika njia ifuatayo ya moja kwa moja: “Msiipende dunia, wala mambo yaliyomo katika dunia. Mtu akiipenda dunia, kumpenda Baba hakumo ndani yake. Maana kila kilichomo duniani, yaani, tamaa ya mwili, na tamaa ya macho, na kiburi cha uzima, havitokani na Baba, bali vyatokana na dunia†(1 Yohana 2:15-16).

Misemo mitatu iliyo katika mlazo kimfanano inaenda sawa na kile Hawa alichopenda kuhusu mti wa ujuzi wa mema na mabaya (Mwa. 3:6). Chukua muda kulisoma tena fungu lile. Itakuwa wazi kwa nini Yohana aliandika kama alivyofanya, miaka 4,000 baadaye, kuhusu ulimwengu ambao Adamu na Hawa walichagua na wakasaidia kuujenga bila kukusudia.

Kwa Yeye Ashindaye

Ubinadamu wote umedanganywa kabisa, na unaserereka, bila kujua kusudi la Mungu, ambalo ni kurejesha serikali Yake duniani, hatimaye kutawala mataifa yote. Ni wale wachache mno, wanaoitwa sasa, wanafahamu urejeshaji huu unaokuja.

Wakati wale wote walio wa ulimwengu huu kimsingi wamejikita kwenye kupata vitu na kufurahia anasa, hili siyo lengo—mtazamo—wa yule anayemtafuta Mungu na ni Mkristo wa kweli. Anajitahidi kubaki katika mapatano ya kudumu na kusudi kuu kabisa la Mungu, kwa ajili ya maisha yake.

Ufahamu wa muhimu lazima uingizwe hapa. Unaainisha maandiko ambayo tutajifunza hivi punde.

Biblia inafundisha, katika Ufunuo 2 na 3, kwamba Mungu ametenda kazi na Kanisa Lake kupitia enzi au awamu saba tofauti zinazofuatana. Katika sura hizi mbili, Kristo anaeleza kila awamu. Ukiacha moja, enzi tano za mwanzo zinaelezewa kama zenye kuwa na matatizo maalumu ya kimaandiko na kiroho ambayo hatimaye yalipelekea kuanguka kwazo. Kila wakati hili lilipotokea, Mungu aliinua kiongozi mwingine kusimamisha awamu iliyofuata.

Wakati mitazamo fulani ilitawala kila enzi, fahamu kwamba baadhi ya mitazamo ambayo Kristo anaielezea inapatikana katika enzi zote. Kwa hiyo, ina masomo kwa Kanisa zima kwa namna ya kiujumla. Ingawa tumerejelea aya kadhaa zinazokuja, sasa zinabeba maana mpya. Hebu tuzipitie upya.

Katika ujumbe Wake kwa THIATIRA, enzi ya nne, Kristo anaelekeza, “Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa, naye atawachunga kwa fimbo ya chuma...†(Ufu. 2:26-27). Hii ni picha ya wazi ya kusimamishwa tena serikali ya Mungu juu ya mataifa yote ya dunia. Wakristo watapokea NGUVU HALISI ili KUTAWALA.

Maelekezo kwa LAODIKIA, enzi ya mwisho, yanaongeza ufahamu zaidi: “Yeye ASHINDAYE, nitampa kuketi pamoja Nami katika kiti Changu cha enzi, kama Mimi nilivyoshinda nikaketi pamoja na Baba Yangu katika kiti Chake cha enzi†(3:21).

Fungu moja zaidi katika Ufunuo linatoa muhtasari wa aya mbili zilizopita: “Ukawafanya kuwa WAFALME na MAKUHANI kwa Mungu wetu; nao watamiliki juu ya nchi†(5:10).

Wafalme na makuhani ni waalimu. Wale wote ambao wameitwa na Mungu wako mafunzoni kuwa waalimu katika ufalme wa Mungu. Hii ndiyo sababu utume mkuu wa Kristo kwa Kanisa Lake katika zama zote ni, “Basi, enendeni, mkawafanye mataifa yote kuwa wanafunzi [mkawafundishe]†(Math. 28:19).

Kanisa la Mungu linafanya hivi leo. Sasa unafundishwa ukweli wa ajabu wa Mungu katika kitabu hiki!

Ni watu wachache tu kwa kulinganisha na walioitwa katika Agano la Kale, huku ikiwa wazi kwamba watatu tu—Habili, Henoko na Nuhu—waliitwa kabla ya Gharika. Baada ya Gharika wakaja wazee (Ibrahimu, Isaka na Yakobo) na manabii, akiwepo Daudi na Lutu. Mungu alimtumia kila mmoja wa wanaume hawa kwa kusudi maalumu au utume. Lakini hawa wote walifunzwa na walitakiwa KUMSHINDA Shetani, majaribu ya ulimwengu wake na mivuto ya mwili. Kama ilivyokuwa kwa watumishi hawa wakuu, Wakristo WANASHINDA matatizo yao, udhaifu, dhambi na mitazamo mibaya, badala ya hayo kuwashinda na kuwazidi nguvu. Wanavumilia hata hali iweje!

Kristo alisema, “Ulimwenguni mnayo dhiki; lakini jipeni moyo; MIMI NIMEUSHINDA ULIMWENGU†(Yohana 16:33). Kristo alikuwa ameshinda ulimwengu na mungu wake. Kumbuka kwamba alisema, “KAMA MIMI NILIVYOSHINDA nikaketi pamoja na Baba Yangu katika kiti Chake cha enzi.†Ni lazima usikose pointi hii. Ni KUSHINDA kwa Kristo kulikomstahilisha Yeye kutawala. Kama vile Alivyostahili kuchukua mahali pa Shetani, vivyo hivyo na sisi lazima tustahili!

Uwezo mkuu kama huo wa kutawala usingeweza kutolewa kwa watu ambao hawajajiandaa—ambao HAWAJASTAHILI kuutumia kwa usahihi. Mungu hayuko tayari kutoa MAMLAKA makubwa kwa watu ambao wanaweza kuasi na kugeukia njia za Shetani. Anajua kwamba Hawezi kamwe kuwa na “Lusifa mwingine-aliyegeuka-Shetani†asababishe uharibifu na machafuko, wakati huu akiwa na baadhi ya nguvu za Mungu mwenyewe. Tumeona kwamba haitawezekana kwa yeyote katika serikali ya Mungu itawalayo kutenda dhambi (1 Yohana 3:9).

Shetani Kufungwa

Wakati Kristo atakaporudi, Shetani, kama kiongozi aliyeondoshwa madarakani juu ya dunia, ataondolewa. Hakuna kiongozi anayeweza kuchukua madaraka ya kiongozi aliyeshindwa, na kumruhusu mtu huyo kubaki katika nafasi ya kutawala pamoja naye. Kiongozi aliyepoteza sifa angeweza kula njama na kudhoofisha yale yote ambayo kiongozi mpya anapanga na kuyatekeleza. Kwa kuwa serikali zote za wanadamu zinaelewa hili, bila shaka, Mungu pia anafahamu. Anajua kwamba Shetani lazima aondolowe kutoka nafasi yake ya ushawishi.

Angalia: “Kisha nikaona malaika akishuka kutoka mbinguni, mwenye ufunguo wa kuzimu, na mnyororo mkubwa mkononi mwake. Akamshika yule joka, yule nyoka wa zamani, ambaye ni Ibilisi na Shetani, akamfunga miaka elfu; akamtupa katika kuzimu, akamfunga, akatia muhuri juu yake, asipate kuwadanganya mataifa tena, hata ile miaka elfu itimie; na baada ya hayo yapasa afunguliwe muda mchache†(Ufu. 20:1-3).

Fungu hili lina ufahamu nyeti kuhusu mpango wa baadaye wa Mungu kwa ajili ya ubinadamu wote. Hivi karibuni, Shetani atafungwa (atatiwa gerezani) na kufanywa asiweze kuwadanganya wakaazi wote wa dunia. Majaribu ya ulimwengu huu na hulka ya mwanadamu, vilivyosababishwa na Shetani, vitatoweka—japokuwa bado kutakuwepo na mivuto ya mwili ambayo wote watatakiwa kuishinda (Rum. 7:18, 21-23).

Wakati Shetani atakapokuwa amefungwa, amani itaanza “kupatikana†ulimwenguni kote kihalisia. Watakatifu watakuwa wanatawala pamoja na Kristo kutokea Yerusalemu—akiwa amekwisha kurejesha serikali ya Mungu katika ufalme Wake, ikisimamiwa na Familia ya Mungu. Sheria ya Mungu iliyo “takatifu, ya haki, kamilifu na ya rohoni†(Rum. 7:12-14) itatekelezwa miongoni mwa mataifa yote.

Lakini kufungwa jela kwa Shetani kutadumu miaka 1,000, na kisha ataonekana tena kwa muda mfupi. Sasa soma: “Na hiyo miaka elfu itakapokwisha, Shetani atafunguliwa, atoke kifungoni mwake; naye atatoka kuwadanganya mataifa walio katika pembe nne za nchi, Gogu na Magogu, kuwakusanya kwa vita, ambao hesabu yao ni kama mchanga wa bahari†(Ufu. 20:7-8).

Fahamu! Ulimwengu utakuwa umejua amani kwa miaka 1,000, wakiwa hawajaachwa wazi kwa matangazo ya Shetani. Lakini kufunguliwa kwake kunaleta urejeaji wa mara moja wa hulka ya mwanadamu.

Shetani ni roho asiyeonekana, ikimaanisha kwamba anaweza kufanya uwepo wake usijulikane. Kwa hiyo, hata pamoja na maonyo ya kabla hajaonekana yaliyoendelea wakati wa miaka 1,000, wengi watapuuzia hatari itokanayo na matangazo ya Shetani na itawashinda. Angalia uingiaji wake tena “anawadanganya mataifaâ€â€”TENA! Ufunuo 20:9 inaelezea hawa mamilioni wanaodanganywa upya wanajaribu kuvamia Yerusalemu na watakatifu wote walio ndani yake. Vurugu, uadui, hasira na chuki vya hulka ya mwanadamu vitakuwa vimeingia tena: “Wakapanda juu ya upana wa nchi, wakaizingira kambi ya watakatifu, na mji huo uliopendwa [Yerusalemu]. Moto ukashuka kutoka mbinguni, ukawala.â€

Wale wanaochagua njia ya Shetani, ama kwa kujua au kwa kukosa uangalifu sababu ya uzembe, hatimaye watafikilia mwisho wa kutisha.

Hukumu ya Kiti Kikuu cha Enzi Cheupe

Fungu la 10 linaelezea Shetani “akitupwa katika ziwa la moto†na kwa mara nyingine tena akinyang’anywa uwezekano wowote wa kuingiza hulka yake na kuwadangaya mataifa. Mafungu 11-13 yanaeleza kipindi cha ajabu baada ya miaka elfu moja—Hukumu ya Kiti Kikuu cha Enzi Cheupe—wakati ambapo wote waliopata kuishi tangu wakati wa Adamu hadi Kuja kwa Kristo Mara ya Pili watapewa fursa kwa ajili ya wokovu. Hatimaye wengi watapokea wokovu—uzima wa milele—kwa sababu ushawishi wa Shetani utakuwa umeondolewa kutoka duniani usirudi tena. Hawatahitajika kushinda ushawishi wake au mivuto na ulaghai wa ulimwengu wake.

Kristo Anairejesha Serikali ya Mungu

Wakati Kristo atakaporudi duniani Atavikwa taji kama Mfalme wa wafalme na Bwana wa mabwana (Ufu. 19:16). Wakati huo, Atafungulia uzima wa milele na wokovu kwa ulimwengu mzima, ambao sasa ungali umetengwa na Mungu, uliopofushwa na unaoongozwa na hulka ya Shetani.

Watu wa mataifa yote wataketi mbele ya Kristo. Baadhi watakuwa wamestahili kutawala na wengine watakuwa wameshindwa. Angalia: “Hapo atakapokuja Mwana wa Adamu katika utukufu Wake, na malaika watakatifu wote pamoja Naye, ndipo atakapoketi katika kiti cha utukufu Wake; na mataifa yote watakusanyika mbele Zake; Naye atawabagua kama vile mchungaji abaguavyo kondoo na mbuzi; Atawaweka kondoo mkono Wake wa kuume, na mbuzi mkono Wake wa kushoto. Kisha Mfalme atawaambia wale walioko mkono Wake wa kuume, Njoni, mliobarikiwa na Baba Yangu, URITHINI UFALME mliowekewa [wale wote ambao wameshinda] tayari tangu kuumbwa ulimwengu†(Math. 25:31-34).

UFALME WA MUNGU utarejeshwa duniani hivi karibuni, na wale wote ambao wamejiandaa “wataurithi ufalme.†Ni wale washindi tu, wale waliojisalimisha kwa Mungu na kumpinga Shetani kwa mafanikio katika maisha yao yote, watakuwa na sehemu katika wakati huu ujao wenye utukufu: “Yeye ASHINDAYE atarithi vitu vyote, Nami nitakuwa Mungu wake, naye atakuwa Mwanangu. Bali waoga, na wasioamini, na wachukizao, na wauaji, na wazinzi, na wachawi, na hao waabuduo sanamu, na waongo wote, sehemu yao ni katika lile ziwa liwakalo moto na kiberiti. Hii ndiyo mauti ya pili†(Ufu. 21:7-8).

Je utakuwa mtu yule ANAYERITHI VITU VYOTE?

Hili linatambulisha swali la zama zote la “Je kuna maisha baada ya kifo?â€â€”na, kama ndivyo, yanakuja lini?

Sura ya Kumi – Nini Hutokea Baada ya Kifo?

Je! Maisha haya ndiyo yote yaliyopo? Dini nyingi zinadai kujua kile ambacho hutokea wakati wa kifo. Hata hivyo hazikubaliani. Kwa nini kuna mkanganyiko kama huo kuhusu kile kinachotokea BAADA YA MAISHA? Kwa nini iwe fumbo hivyo—kutoafikiana hivyo?

Swali hili la maisha baada ya kifo limemtatiza mwanadamu katika vizazi vyote. Kumbuka, miaka maelfu iliyopita, Ayubu aliuliza, “Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena?†(14:14). Swali hili linabaki hata leo.

Wengi wanaojidai kuwa Wakristo wanaamini kwamba wana nafsi isiyokufa. Wamefundishwa kwamba wafu ama huenda mbinguni au jahannamu. Viongozi wengi wa dini, wainjilisti na watu wa dini huongea kwa uhuru “wakati sisi sote tutakapofika mbinguni.†Wanatangaza kuwa hili ni fundisho la Biblia. Lakini je! Ni kweli?

Ni lazima tusidhani. Kumbuka mara nyingine tena, Yesu alisema, “Nao waniabudu BURE, Wakifundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu†(Marko 7:7-8). Wanadamu wana dhana zao wenyewe, zilizojengwa kwenye imani za Biblia zisizohakikishwa siku zote. Ikiwa Biblia ni Neno la Mungu, ni lazima tuchunguze kile inachosema hasa, si kile watu wanachodai inasema. Uwe tayari kuweka kando desturi zilizozoeleka na mahali pake uweke Andiko lililo wazi.

Kisha uwe tayari kumwamini Mungu, siyo watu.

Kabla ya kujibu swali “Je! Kuna maisha baada ya kifo?,†hebu tuchunguze kile kinachotokea wakati uleule wa kufa. Wakati Ayubu alipouliza, “atakuwa hai tena?â€, alimaanisha nini “tenaâ€? Ikiwa wafu wako hai daima kwa njia yoyote, wanawezaje kuwa hai TENA?

Ni lazima tuelewe!

Mshahara wa Dhambi

Kama una kazi, unapokea cheki [hundi] ya malipo kwa muda uliopangwa. Zinawakilisha mshahara unaolipwa kwa kazi iliyofanyika. Vipi kuhusu Mungu? Je Naye hulipa mshahara? Warumi 6:23 ilisema, “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu.†Hapa uzima wa milele unatofautishwa na KIFO—KUANGAMIA! Mshahara wa dhambi ni mauti, siyo maisha. Tutaona kwamba ufahamu huu haukubaliani na mateso ya milele katika jahannamu.

Hakuna fumbo kuhusu maana ya mshahara ambao mwajiri humlipa mwajiriwa kwa kazi yake. Kwanini pawe na mkanganyiko juu ya maana ya mshahara ambao Mungu humlipa mwenye dhambi kwa kazi yake? Humlipa mtu mwovu cheki [hundi] ya malipo ya mauti—siyo maisha katika mahali pa mateso. Biblia inasema kile inachomaanisha na inamaanisha kile inachosema.

Hebu turudi kwenye Yohana 3:16 na tuliangalie tena katika muktadha mwingine! Cha kusikitisha, fungu hili linalojulikana na kunukuliwa kwa wingi sana halieleweki karibu na kila mtu. Angalia: “Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata Akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.†Mamilioni hunukuu fungu hili lakini hupuuzia moja ya pointi yake iliyo wazi kabisa.

Lisome tena. Angalia kwamba linatoa taswira ile ile ya Warumi 6:23! Wakati huu, uzima wa milele umetofautishwa na KUANGAMIA—MAUTI.

Neno la Kigiriki lililotafsiriwa kupotea ni apollumi na linamaanisha, “kuharibu kikamilifu, kufa, poteza, potea.†Hakuna shaka juu ya kile maneno haya yanachomaanisha. Vitu “viharibikavyo haraka†kama vile matunda na mboga mboga, ni vile ambavyo vinaoza—mpaka “vinaharibika kikamilifu†au “kupotea.†Hili siyo gumu kuelewa wakati tunapoongelea juu ya kitu kingine kando ya mwanadamu. Wale wanaopokea wokovu wameahidiwa kwamba “hawatapotea†bali “wawe na uzima wa mileleâ€! Ikiwa jahannamu ni mahali pa mateso ya milele, basi watu wanaoteseka pale wana UZIMA wa milele. Lakini fungu linasema, “wasipotee,†siyo “wasipate uzima wa milele katika maumivu makali.â€

Ni jinsi gani neno potea linahusiana na fundisho maarufu kuhusu jahannamu? Kwa nini Mungu alimvuvia Yohana kutumia neno hili kama hiki sicho hasa Alichokusududia?

Nafsi Huharibiwa

Wazo la jahannamu inayowaka daima halitenganishiki na wazo kwamba wanadamu wote wana nafsi zisizokufa. Je hiki ndicho Mungu anachosema? Jibu ni HAPANA kwa msisitizo!

Ni muhimu kurejea upya kwa kitambo kidogo kama kutoa utangulizi kwa ufahamu wa muhimu. Mwanzo 2:7 ilionyesha kwamba mwanadamu ni nafsi na hana nafsi. Mungu aliwaambia Adamu na Hawa “wangekufa†ikiwa watakula matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya. Ezekieli alisema (mara mbili) kwamba “nafsi itendayo dhambi, itakufa.†Mathayo alisema kwamba Mungu anaweza kuharibu mwili na nafsi katika jahannamu (10:28).

Tuliona kile ambacho nabii Malaki aliandika kuhusu hali ya mwisho ya waovu walioharibiwa katika jahannamu: “Kwa maana, angalieni, siku ile inakuja, inawaka kama tanuru; na watu wote wenye kiburi, nao wote watendao uovu, watakuwa makapi; na siku ile inayokuja itawateketeza, asema BWANA wa majeshi; hata haitawaachia shina wala tawi. Lakini kwenu ninyi mnaolicha Jina Langu, Jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mbawa zake; nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama ndama wa mazizini. Nanyi mtawakanyaga waovu; maana watakuwa majivu chini ya nyayo za miguu yenu; katika siku ile niifanyayo, asema BWANA wa majeshi†(4:1-3). Obadia 16 inaongezea zaidi na hii “...nao watakuwa kana kwamba hawakuwepo kamwe.â€

Wafu watakuwa “wamekufa na kutoweka†kikamilifu kiasi kwamba itakuwa kana kwamba hawakuwepo kamwe. Hakika, kama walikuwa wanaungua katika jahannamu milele, na wengine mamilioni walioko mbinguni wakishuhudia hili, ingekuwa vigumu fungu hili kutumika.

Je! Wafu Wana Ufahamu?

Ni vipi kuhusu wakati uleule wa kifo? Je! Nini hasa hutokea pale mtu anapokufa?

Fikra za mwanadamu zinatofautishwa na ubongo wa wanyama kwa kuwa zina mawazo yenye akili. Kwa kudhania, ikiwa wafu hawajafa, bali wangali hai kabisa, basi lazima wawe na uwezo wa kuwa na mawazo yenye akili kwa namna fulani. Ni lazima angalau wawe na ufahamu wa mazingira yao. Hebu tuchunguze mfuatano [mfululizo] wa maandiko.

Kwanza, angalia Zaburi 146:3-4: “Msiwatumainie...binadamu ambaye...Pumzi yake hutoka, huurudia udongo wake, Siku hiyo mawazo yake yapotea.†Wakati watu wanapokufa, mawazo yao hukoma mara moja—“katika siku hiyo.†Hivyo ndivyo Biblia yako inavyosema.

Fungu hili pia halipatani na wazo kwamba wafu ama wako hai mbinguni au wanateseka katika mahali pa mateso makali wakijua kinachoendelea. Tungeweza kudhani kwamba, ikiwa walikuwa wanafurahia wokovu, bila shaka wangejua kuwa wanafurahi! Tungeweza pia kudhani kwamba kama walikuwa wanateseka, wangejua kwamba wanateseka. Je! Ingewezekana kwamba wanaoteseka sana kwa namna fulani wasiwe na habari kwamba wanateseka?

Jiulize mwenyewe: Nini ingekuwa pointi ya kuteseka kwao, au ya kufurahia kwao wokovu, ikiwa wasingeweza kujua habari yake? Mauti (kwa hakika maisha!) katika jahannamu ingebidi iwe kana kwamba walikuwa wamezimia—wasiwe na habari kabisa ya kinachoendelea mahali walipo—wakati mfumo wao wa neva za fahamu unahisi maumivu makali ya kuungua. Jambo hili lingetendekaje?

Tumia kifanani kifuatacho. Kabla mtu hajafanyiwa upasuaji mkubwa, analazwa usingizi [anatiwa nusukaputi]—inamfanya asiwe na ufahamu—ili kwamba asije akasikia maumivu. Madaktari wa tiba wanaelewa hili—kwa nini wanateolojia na watu wa dini hawaelewi? Kwa nini wanakataa maelezo ya wazi ya Biblia?

Baadhi wanapuuza ujumbe wa maandiko kwa hiari. Wanadai kwamba ni yale mawazo ya “ufu†pekee ambayo hupotea, kwa madai kwamba wafu huondoka katika wigo wa kidunia na kupata uzoefu wa aina mpya ya “mawazo,†yasiyo ya kawaida, yaliyotofauti. Kwa hakika, hii ni dhihaka, na Biblia haisemi hili, lakini tunapaswa angalau kulichunguza wazo hili.

Hebu sasa tuangalie fungu ambalo liko moja kwa moja zaidi: “kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lo lote...†(Mhu. 9:5).

Msomaji mkweli hawezi kuelewa isivyo fungu hili! Lolote inamaanisha lolote!

Sulemani pia alirekodi, “Kwa maana linalowatukia wanadamu linawatukia wanyama; jambo moja lawatukia; anavyokufa huyu ndivyo anavyokufa huyu; naam, wote wanayo pumzi moja; wala mwanadamu hana kitu cha kumpita mnyama...Wote huenda mahali pamoja; wote hutoka katika mavumbi; na hata mavumbini wote hurudi tena†(Mhu. 3:19-20).

Sasa angalia Zaburi 115:17: “Sio wafu wamsifuo BWANA, Wala wowote washukao kwenye kimya.†Mauti inamaanisha “kimya.†Bila shaka hii haikubaliani na wazo maarufu la mamilioni ya wafu wakiomboleza na kupiga mayowe kwa uchungu—au mara moja wanapokea uzima wa milele mbinguni au mahali pengine popote pamoja na mamilioni ya wengine wakidhaniwa kufanya mazungumzo, kuimba, kupiga vinubi na kumsifu Mungu. Hakuna mandhari kati ya hizi inayoweza kuelezewa kama KIMYA!

Zaburi 6:5 inafafanua zaidi kwamba wafu hawana kumbukumbu ya ufahamu. Angalia: “Maana mautini hapana kumbukumbu Lako: Katika kuzimu ni nani atakayekushukuru?†Je mtu yeyote anaweza kupendekeza kwa nguvu kwamba wafu, wanaoteseka jahannamu, wangeweza kupitia uzoefu wa kawaida wa kumbukumbu za kibinadamu, lakini wasiwe na habari ya Mungu—wasiwe na uwezo wa “kumkumbuka†Yeye? Je! Mungu angewaweka watu katika “jahannamu†na kisha kuwaacha pale wateseke, daima wakishangaa jinsi gani ilikuwa hata wakawepo pale—alikuwa NANI aliyewaweka pale—kwa sababu hawana “kumbukumbu†ya kitu chochote kinachohusiana na MUNGU? Tungeweza kuuliza: Lakini ni wangapi hata wanaelewa aya hii?

Tukitumia swali lile lile kwa wale ambao walipokea wokovu inakuwa dhihaka zaidi. Je inawezekana kwa namna fulani watu “wakazunguka mbingu siku nzima†na wasiwe na habari kwamba walikuwa mbele ya uwepo wa Mungu au ya hata Yeye alikuwa nani?

Hapana! Wakati watu wanapokufa, WAMEKUFA!

Mpaka hapo, hatujaelezea kila kitu kuhusu uzima na mauti, lakini tunajua kwamba uzima wa mbele hautokei mara moja wakati wa kufa! Tumethibisha kwamba wakati mtu anapokufa, amekufa! Lakini nini hutokea baadaye?

Ufufuo wa Wafu

Kanuni ya kwanza ya kujifunza Biblia ni kuiacha Biblia ifasiri Biblia wakati wote. Uweke ukweli ilio nao katika wepesi na uwazi—na ukosefu wa kina na upumbavu wa siku zote—mawazo ya wanadamu vitaanguka kama nyumba iliyojengwa kwa karata [kadi].

Hapa kuna sababu za wafu kutokuwa na maarifa au kumbukumbu ya Mungu.

Yesu alisema, “Msistaajabie maneno hayo; kwa maana saa yaja, ambayo WATU WOTE waliomo makaburini wataisikia sauti Yake. Nao watatoka; wale waliofanya mema kwa ufufuo wa uzima, na wale waliotenda mabaya kwa ufufuo wa hukumu†(Yohana 5:28-29).

Kristo alifahamu kwamba wengi wangeona hili linastaajabisha. Hii ndiyo sababu Aliwaambia wanafunzi “Kutostaajabu juu ya hiliâ€â€”Alifahamu kwamba watu wengi wangestaajabu kufikiri kwamba kila mtu aliyepata kuishi sasa yuko “kaburini,†akingoja ufufuo! Wewe nawe pia usistaajabu maneno ya Kristo. Yakubali! Alisema kwamba “wote†wako makaburini, siyo “baadhiâ€.

Hakuna mawazo ya ufahamu na hakuna kumbukumbu ya Mungu baada ya kufa kwa sababu kila mmoja ambaye amekufa sasa anangoja moja ya ufufuo aliorejelea Kristo. Watu wote watafufuliwa, ama wapate uzima wa milele au kuhukumiwa. Hiki ndicho Neno la Mungu linachosema.

Si ajabu Daudi alisema, “Bali mimi nitautazama uso wako katika haki, Nitashibishwa, wakati NITAKAPOAMKA, nikiwa na sura Yako†(Zab. 17:15). Alifahamu kwamba ufufuo ulikuwa ni kuamshwa kuyarudia maisha.

Tuliona kwamba, kama Daudi, Ayubu pia alitazama mbele hadi kwenye ufufuo wa uzima. Lakini wakati huu angalia mafungu yanayozunguka swali lake la mwanzoni lililorejelewa: “Laiti ungenificha kuzimuni, Ukanilinda kwa siri, hata ghadhabu zako zitakapopita [Siku ya Bwana inayokuja, au Siku ya Ghadhabu ya Mungu], Na kuniandikia muda ulioamriwa, na kunikumbuka! Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena? Mimi nitangoja siku zote za vita vyangu, Hata badiliko langu linifikilie. Wewe utaita, nami nitakujibu†(14:13-15).

Ayubu hakumwomba Mungu kwamba angeuficha mwili wake tu kuzimuni. Alimwomba Mungu “unifiche…unitunze…uniandikie…unikumbuke.†Pia alitambua kwamba Mungu angemtunza “kwa siri.†Jiulize mwenyewe hii inapatana vipi na kuwa mbinguni au jahannamu. Kama ni hivyo, Mungu angekuwa na uwezo mdogo sana wa kutunza siri na sehemu ya fungu iliyobaki isingeleta maana. Na kwanini Mungu angehitaji “kumkumbuka†Ayubu kama alikuwa amepangiwa kwenda mbinguni moja kwa moja baada ya kufa? Wote (Mungu na Ayubu) walijua angesubiri ufufuo kwa maelfu ya miaka.

Sasa angalia swali la Ayubu—“Mtu akifa, je! Atakuwa hai tena?†Kama Ayubu alikuwa anakwenda kuendelea kuwa hai wakati wa kufa, jinsi gani angeweza “kuwa hai tena� Ayubu alijua kwamba atakuwa “anangoja...kaburini†kwa ajili ya ufufuo panapo “wakati ulioamuriwa,†wakati “atakapobadilishwa.†Alijua kwamba kuwa hai tena ilikuwa sawa na kuzaliwa mara ya pili.

Lakini ilimaanisha nini kwamba atabadilishwa?

Tuliona kwamba Paulo aliandika juu ya “badiliko†linalowasubiri Wakristo wote wa kweli. Soma tena 1 Wakorintho 15:51-52, 54: “Angalieni, nawaambia ninyi siri; hatutalala sote, lakini sote tutabadilika, kwa dakika moja, kufumba na kufumbua, wakati wa parapanda ya mwisho...wafu watafufuliwa...na huu wa kufa utakapovaa kutokufa, HAPO NDIPO [bado] litakapokuwa lile neno lililoandikwa, MAUTI imemezwa kwa kushinda.†Ninarudia, hakika ni kama siri kabisa kwa ulimwengu ya kwamba kunakuja kuamushwa na badiliko wakati wa ufufuo.

Na tena, lazima pia tuulize, jinsi gani mtu atakwenda kutoka “kufa†hadi “kutokufa†kama tayari ana nafsi isiyokufa? Wazo hili pia ni siri [fumbo]—lakini, kinyume na siri za Mungu, hii ni moja ya siri zilizosanifiwa na wanadamu ambazo haziwezi kufahamika au kufumbuliwa, kwa sababu hazileti maana.

Je unaona mantiki ya kipumbavu ya wanadamu pale wanapopuuzia maandiko yaliyo dhahiri?

Kama vile Ayubu alivyofahamu kwamba “angebadilishwa,†na Daudi alifahamu kwamba “angeamka,†Paulo alifahamu kwamba Wakristo “watabadilishwaâ€â€”wataamka kutoka “usingiziniâ€â€”mara ufufuo utakapokuja. Kwenye ufufuo, watu wataamka kihalisi kutoka mautini.

Jiulize mwenyewe: Jinsi gani watu wanaweza kufufuliwa kama tayari wako hai kama nafsi zisizokufa? Ni wafu peke yao, kama alivyokuwa Kristo wanahitaji kurudishwa kuwa hai, kutoka kaburini. Hilo ndilo kusudi la ufufuo. Usidanganywe na walaghai wasemao, “Ufufuo unahusisha mwili tu, kwa kuwa nafsi imesalia kuwa haiâ€! Umeshaona maandiko mengi yakikanusha uwongo huo.

Panapo uchunguzi wa msingi, mawazo ya watu wenye akili mara nyingi yamefunuliwa kama upumbavu wa wazi. Watu walitunga dhana maarufu ya jahannamu kama njia ya kuwaogofya watu wafuate dini za uongo walizokuwa wametengeneza. Mungu wa kweli asingeweza kuwakaanga watu milele yote—bila kuwaruhusu kuteketea, kufikisha mwisho mateso yao kwa rehema. Hiki ndicho dubwana [jitu la kutisha] lingefanya. Lakini hatimaye, miungu ya uongo, iliyobuniwa na wanadamu “itatenda†na “kufundisha†chochote ambacho wanadamu “walioisanifu†wameiamulia.

Mabilioni wameishi na kufa bila hata kujua jina la Yesu Kristo na bila ya kuwa na fursa kwa ajili ya wokovu. Ikiwa wasiookolewa huenda moja kwa moja jehannamu, wakati wanapokufa, basi zaidi ya nusu ya watu waliopata kuishi wangali hai pale!

Kwa kuwa hakuna mwanadamu aliyewahi kurudi kutoka kwa wafu ili kutoa taarifa ya kwanza—kwa hakika, simulizi za kijinga na ubunifu katika magazeti madogo yenye picha na vichekesho zimejaa—ama ni lazima tuchague kuamini mawazo ya wanadamu au tuchunguze maandiko kwa ajili ya kile ambacho Mungu anafunua kuhusu mada hii.

Aina Tatu za Ufufuo

Kumbuka kwamba “wote walio makaburini†hatimaye watafufuliwa. Hakika, Biblia inafundisha kwamba mpango wa Mungu unajumuisha aina TATU za ufufuo zinazojitegemea. Ufunuo 20 inaelezea kila moja. Tumekwisha kuelezea ufufuo wa KWANZA. Fungu la 4 hufafanua kwamba watakatifu watatawala duniani pamoja na Kristo kwa miaka 1,000 baada ya Shetani kufungwa (fu. 1-2). Tutaelezea zaidi ufufuo wa kwanza baadaye, lakini fungu la 5 linafafanua kwamba “hao wafu waliosalia hawakuwa hai, hata itimie ile miaka elfu.â€

Mwishoni mwa miaka 1,000 utakuja ufufuo wa PILI. Huu utajumuisha mabilioni ya watu, kutoka wakati wa Adamu, ambao hawakupata kamwe fursa ya kuijua kweli. Sasa endelea katika Ufunuo 20 pamoja na kile tulichosoma mwanzoni: “Kisha nikaona kiti cha enzi, kikubwa, cheupe, na Yeye aketiye juu yake; ambaye nchi na mbingu zikakimbia uso wake, na mahali pao hapakuonekana. Nikawaona wafu, wakubwa kwa wadogo, wamesimama mbele ya hicho kiti cha enzi; na vitabu vikafunguliwa; na kitabu kingine kikafunguliwa, ambacho ni cha uzima; na hao wafu wakahukumiwa...sawasawa na matendo yao†(fu. 11-12).

Kitabu cha Ezekieli kina sura ya ajabu inayoelezea, katika njozi, bonde la mifupa mikavu. Karibu kila mtoto wa shule ya Jumapili huimba kuhusu mifupa iliyoelezewa katika njozi hii, bali pasipokuwa na ufahamu. Chukua muda usome sura ya 37 katika ukamilifu wake. Inaonyesha kwa picha mamilioni waliokuwa sehemu ya taifa la kimwili la Israeli ya kale na Israeli ya sasa (makabila yote 12, siyo Wayahudi peke yao) wakipewa fursa kwa ajili ya wokovu wa kiroho ambayo Mungu kamwe hakuwapa katika Agano la Kale.

Fungu la 11 linawaelezea kama “wasio na tumaini.†Ezekieli aliagizwa kuliambia lundo hili kubwa sana la mifupa mikavu. Angalia: “Basi...MUNGU asema hivi; Tazama, nitafunua makaburi yenu, na kuwapandisha kutoka katika makaburi yenu, Enyi watu Wangu, nami nitawaingizeni katika nchi ya Israeli†(fu. 12). Hapa, mamilioni wanaelezewa kama wakifufuliwa kutoka “makaburini†mwao. Ni wazi kwamba ufufuo ambao fungu hili linauelezea ni wa kimwili, kurudi kwenye uwepo wa nyama na damu, Angalia kile kinachotokea baada ya hapo.

Ezekieli aliendelea kuiambia mifupa: “Bwana MUNGU aiambia mifupa hii...Nitatia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi. Nami nitatia mishipa juu yenu, nami nitaleta nyama iwe juu yenu, na kuwafunika ngozi, na kutia pumzi ndani yenu, nanyi mtaishi†(fu. 5-6). Mafungu 13-14 yanaongeza, “Nanyi mtajua [bado hawajui] ya kuwa Mimi ndimi BWANA, nitakapoyafunua makaburi yenu, na kuwatoa ninyi katika makaburi yenu, Enyi watu Wangu. Nami nitatia Roho Yangu ndani yenu, nanyi mtaishi, nami nitawawekeni katika nchi yenu...â€

Lini Israeli watajua kile kilichotokea? Kwenye ufufuo! Hapo ndipo Israeli “watajua†kwamba Mungu amewatoa kutoka kaburini. Wao ni sehemu ya mabilioni ambao watainuka katika ufufuo wa pili. Hiki ni kipindi ambacho kinarejelewa kama Hukumu ya Kiti Kikuu cha Enzi Cheupe (Ufu. 20:11), na huu ni wakati ambapo wanadamu wote wataonyeshwa ukweli. Mungu “ataweka Roho [Yake] ndani [yao].†Watu walio wengi watakua, kushinda na kustahili kupokea wokovu na kuungana na wale wote waliowatangulia katika ufufuo wa kwanza.

Angalizo la pembeni, nimeshauri watu kadhaa waliokuwa wanafikiria kujiua. Wale wote wanaojaribiwa kuchukua njia hii rahisi, wakifikiri kwamba itamaliza mateso yao yote na huzuni, wanapaswa wafikirie jambo lifuatalo: Wakati watu wanapokufa, hawajui kitu chochote. Hawana habari ya muda unaopita, iwe siku au karne. Kusema kweli, wataamka mara moja—pasipokuwa na ufahamu wa muda uliopita—na watagundua kwamba bado wangali na matatizo yao yote ya zamani, na wamejiongezea wenyewe hatia ya kujiua! Kujiua, basi, hakufanyi mambo yawe mazuri. Kunayafanya yawe mabaya zaidi, na, kwa hakika, inakuwa hivyo mara moja!

Kuna ufufuo mmoja wa mwisho, au wa TATU. Tuliurejelea tuliposoma Malaki 4:1-3 na Obadia 16. Ufunuo 20:14-15 inaelezea wale wanaofufuliwa na kuonyeshwa kile walichokikosa katika ufalme wa Mungu, kabla hawajatupwa kwenye ziwa kubwa la moto: “Mauti na Kuzimu zikatupwa katika lile ziwa la moto. Hii ndiyo mauti ya pili, yaani, hilo ziwa la moto. Na iwapo mtu ye yote hakuonekana ameandikwa katika kitabu cha uzima, alitupwa katika lile ziwa la moto.â€

2 Petro 3:10-12 pia inaelezea wakati ambao waovu wanateketezwa na kutimiliza Malaki 4, wakifanyika “majivu chini ya nyayo za miguu ya wenye haki.â€

Sura ya Ufufuo

1 Wakorintho 15 imeitwa “Sura ya Ufufuo.†Tumekwisha kuinukuu, lakini hebu tuichunguze zaidi sura hii. Ingawa inaongelea hasa ufufuo wa kwanza, ni muhtasari wa mpango wa Mungu wa aina tatu za ufufuo.

Fungu la 26 linasema, “ADUI wa mwisho atakayebatilishwa ni mauti.†Kwenye mazishi, watumishi wa kidunia huionyesha mauti kama “rafiki wa zamani†ambaye mtu hukutana naye mwishoni mwa “njia kuu ya maisha.†Je hujasikia hili au usemi unaofanana na huu mara nyingi kwenye matukio haya? Biblia inaita mauti ADUI!—na hakuna chochote cha “kirafiki†kuhusu maadui!

Mafungu ya 22-23 yanasema, “Kwa kuwa kama katika Adamu wote wanakufa, kadhalika na katika Kristo WOTE watahuishwa (kwa njia ya ufufuo). Lakini kila mmoja mahali pake...†Angalia pointi mbili. Kwanza kila mtu atakuwa na nafasi kwa ajili ya wokovu. Pili, kila fursa ya mtu itakuja “katika mahali pake.†Tumeona kwamba sehemu zote za mpango wa Mungu hazitimilizwi katika ufufuo mmoja.

Fungu la 23 linaendelea hadi kwenye 24: “limbuko ni Kristo; baadaye walio Wake Kristo, atakapokuja. Kisha unakuja ule mwisho...†Kristo alikuwa ule mwanzo—“limbukoâ€â€”la ufufuo wa kwanza, ambao utajumuisha watakatifu wote. Lakini, “kisha unakuja mwisho†inarejelea sehemu iliyobaki ya Mpango Mkuu wa Mungu ulio wa ajabu, ambao utaendelea wakati ufalme wa Mungu utakaposimamishwa duniani wakati wa Kurudi kwa Kristo.

Wakati huo upo hapo karibu mbeleni.

Kuuingia Ufalme

Biblia inafundisha kwamba ufalme wa Mungu unatawala juu ya watu na mataifa ya dunia. Mataifa hayawi tena sehemu ya ufalme kama raia wa kawaida wa nchi yoyote asivyokuwa sehemu ya serikali inayotawala juu yake. Ni lazima mtu AINGIE katika ufalme ili kuwa ndani yake. Kwa kuwa ni tofauti na wale wanaotawaliwa nayo, lazima tuulize, nani hasa aliye ndani ya ufalme? (sura ya Kumi-na-moja itafafanua hili kwa undani.)

Kumbuka kwamba Paulo alitamka, “Ndugu zangu, nisemayo ni haya, ya kuwa nyama na damu haziwezi kuurithi ufalme wa Mungu; wala uharibifu kurithi kutokuharibika. Angalieni, nawaambia ninyi siri...†(1 Kor. 15:50-51). Bila shaka, kama ilivyotamkwa huko nyuma, hii ni siri karibu kwa kila mmoja—kwamba wanadamu wa nyama-na-damu hawawezi kuingia ufalme wa Mungu—kwamba ni katika ufufuo pekee ambapo wanadamu waliotungwa kwa Roho huko nyuma wanapobadilishwa kutoka nyama kuwa roho. Tumeona kwamba ni katika wakati huu—na katika wakati huu pekee—kwamba Wakristo wa kweli “wanazaliwa mara ya pili.†Kama tu tungeamini ukweli dhahiri wa Biblia, ufalme wa Mungu hauwezi kuhusisha watu wa nyama-na-damu!

Uongo mwingi umefunika ufahamu halisi wa nini ni ufalme wa Mungu.

Maelezo katika Yohana 3, ambayo kwa ufupi yalirejelewa katika Sura ya Pili, kwa kawaida yanaeleweka vibaya na watu wanaoamini kwamba wanaweza “kuzaliwa mara ya pili†katika maisha haya (wakiwa wangali nyama na damu) na, kwa hiyo, “wanauona†ufalme wa Mungu katika maisha haya (fu. 3).

Katika maelezo haya, Nikodemo, Farisayo, alimwendea Kristo na kukiri katika fungu la 2, “Rabi, twajua ya kuwa u mwalimu, umetoka kwa Mungu.†Alikubali dhahiri kwamba alijua Kristo alikuwa nani na nani (Mungu) alikuwa Amemtuma duniani. Angalia kwamba Nikodemo aliongea kwa niaba ya wengi pale aliposema, “twajua.†Alikuwa akijirejelea yeye mwenyewe na Mafarisayo wengine waliotambua Yesu Kristo alikuwa nani na nini. Viongozi hawa hawakuweza kukataa uwezo wa Mungu uliodhihirika katika miujiza ambayo Yesu alikuwa akitenda.

Viongozi wa kidini—Mafarisayo—walifahamu vyema kwamba Alikuwa “mwalimu aliyetoka kwa Mungu†akiwa na ile kweli. Lakini, bado walimwita mtukanamungu, mlevi, mzushi, haini, mwanaharamu, mjinga, mwenye-pepo, nabii wa uongo, rafiki wa watoza ushuru na wenye dhambi, nk.—na wakamsulubisha!

Kristo alimwambia Nikodemo, “Mtu ASIPOZALIWA MARA YA PILI, hawezi kuuona ufalme wa Mungu†(fu. 3). Alikuwa anafafanua kwamba ni kwa mchakato wa kuzaliwa mara ya pili pekee ndipo mtu anaweza “kuuona†ufalme. Hivyo kuna mpaka juu ya kina nani wanaweza kuuona. Mtu yeyote anaweza kuona vitu vya asili. Hii siyo kweli kuhusu ufalme wa Mungu. Shika pointi hizi muhimu ambazo Kristo alizisema.

Katika fungu la 5, Kristo anasema kwamba isipokuwa mtu “amezaliwa kwa maji na kwa Roho, hawezi kamwe kuingia katika ufalme wa Mungu.†Ndiyo, ufalme ni kitu ambacho kinaweza “kuingiwaâ€â€”lakini fungu la 6 linafafanua usemi wa Kristo “kuzaliwa kwa maji na Rohoâ€. Linasema, “Kilichozaliwa kwa mwili NI mwili; na kilichozaliwa kwa Roho NI roho.†Tuliona kwamba nyama na damu haviwezi kuingia ufalme wa Mungu—lakini roho inaweza!—na ili kutoruhusu nafasi ya kuelewa isivyo, Kristo alifananisha roho na upepo.

Upepo na roho havionekani. Kristo alimwambia Nikodemo, “Upepo huvuma upendako, na sauti yake waisikia, lakini hujui unakotoka wala unakokwenda; kadhalika na hali yake kila mtu ALIYEZALIWA KWA ROHO†(fu. 8). Wale waliozaliwa kwa roho watakuwa kama upepo—watakuwa HAWAONEKANI!

Lakini lini badiliko hili kutoka kuwa wa mwili hadi kuwa wa roho litatokea?

Kumbuka 1 Wakorintho 15:49 ilisema, “Na kama tulivyoichukua sura yake yule wa udongo, kadhalika tutaichukua [wakati ujao—kwenye ufufuo] sura Yake Yeye aliye wa mbinguni.†Fungu la 53 linasema “Maana sharti huu uharibikao [nyama bila shaka inaharibika] uvae kutokuharibika [wale waliozaliwa kutokana na Mungu ni roho], nao huu wa kufa uvae kutokufa.†Ni katika pointi hii kwamba nyama inabadilishwa kuwa roho.

Hata wanadamu walioongoka bado wangali nyama—wa mavumbi ya ardhi. Mungu atabadilisha nyama yao kuwa roho kwenye ufufuo wa kwanza. Wale wote wanaouingia ufalme wa Mungu lazima watengenezwe kwa—waundwe kwa—ROHO!

Hebu tuchunguze hili zaidi. Mathayo 22:30 inasema, “Kwa maana katika ufufuo hawaoi wala hawaolewi, bali huwa kama malaika wa Mungu.†Waebrania 1:7 inaonyesha kwamba malaika wametengenezwa kwa roho. Hii ni muhimu kufahamu kuhusu kile tutakachokuwa katika ufufuo. Lakini usielewe isivyo na ukafikiri kwamba Kristo alikuwa anasema kwamba watakatifu waliofufuliwa hakika watakuwa malaika. Alimaanisha tu kwamba watakuwa “kama†malaika, kwamba si malaika wala watakatifu waliofufuliwa huoa.

Kufanyika Wenye Nia ya Rohoni

Sasa tutarudisha usikivu wetu kwa mara nyingine tena kweye ufahamu muhimu sana wa kupokea Roho ya Mungu—na jinsi gani mtu anaongozwa nayo.

Kumbuka Warumi 8:6 kwa mara nyingine. Ilisema, “Kwa kuwa nia ya mwili ni MAUTI; bali nia ya roho ni UZIMA na amani.†Mtu yeyote aliyepokea Roho ya Mungu mwishowe ana uzima ndani yake. Hii ina maana kwamba ana uwezekano wa kuwa “mrithi†pamoja na Kristo. Hebu tuseme tena kwa msisitizo: Kwa hakika huu ni ufahamu wa kustaajabisha—usiojulikana kabisa kwa wote bali wachache waliotawanyika duniani leo!

(Kipachikwa chenye kuhusiana na jambo hili lazima kiongezwe hapa. Watetezi wote wa “haki za kutoa mimba†lazima wazingatie ni lini hasa Mungu anasema maisha yanaanza—kwamba Mkristo aliyetungwa, aliye na nia ya Roho, ana uzima wa milele kiasili ndani yake. Kama vile mimba inavyoweza kuharibika kabla ya kuzaliwa, vivyo hivyo Mkristo pia anaweza “kuharibikaâ€â€”hii ni kwamba, kuiacha njia iendayo kwenye wokovu na uzima wa milele. Lakini utaratibu dhahiri wa Biblia ni kwamba maisha yanaanza wakati ule ule mimba inapotungwa kimwili kama vile yanavyoanza hakika katika muda—kitambo kile kile—cha utungwaji kiroho.)

Watu walio wengi wamelaghaiwa katika kuamini kwamba wao ni Wakristo eti kwa sababu tu “wamemkubali Yesu†au “wamefanya uamuzi kwa ajili ya Kristo†au “wametoa mioyo yao kwa Bwanaâ€â€”au aina nyingine ya kukiri imani. Wamedanganywa katika kuamini kwamba kama wakijiunga na kanisa au kujitangaza wenyewe kwamba “wamezaliwa mara ya pili,†hii inawafanya wawe Wakristo. Jinsi gani huu ni uongo kabisa na kinyume na maneno dhahiri ya Biblia!

Mkristo ni yule ANAYEONGOZWA NA Roho ya Mungu!

Kwa hakika, Biblia inasema kwamba ulimwengu wote sasa unasubiri ufufuo wa kwanza. Ni wakati huo Wana wa Mungu watafunuliwa. Angalia kwa uangalifu:

“Kwa maana viumbe [Kigiriki: uumbaji] vyote pia vinatazamia kwa shauku nyingi kufunuliwa kwa wana wa Mungu. Kwa kuwa viumbe [uumbaji] vyenyewe navyo vitawekwa huru na kutolewa katika utumwa wa uharibifu, hata viingie katika uhuru wa utukufu wa watoto wa Mungu. Kwa maana twajua ya kuwa viumbe [uumbaji] vyote pia vinaugua pamoja, navyo vina utungu pamoja hata sasa†(Rum. 8:19, 21-22). Fungu hili linaonyesha kwamba uumbaji unasubiri “kuzaliwa†kwa “Wana wa Mungu.†Uko katika “kuugua†na “utungu†(umia) hata uzaliwaji huu—KUZALIWA huku—kwa Wana wa Mungu waliotungwa, wakizaliwa mara ya pili kwenye ufufuo na Kurudi kwa Kristo.

Kanisa Huwalisha Watoto Wake

Kumbuka kwamba Kanisa la Kristo linaitwa “Yerusalemu wa juuâ€â€”“mama yetu sisi†(Gal. 4:26). Waebrania 12:22-23 inaliweka hili wazi: “Bali ninyi mmeufikilia... Yerusalemu wa mbinguni...mkutano mkuu na kanisa...walioandikwa mbinguni.†Haisemi kwamba Kanisa liko mbinguni, lakini badala yake kwamba wale walio wa Kanisa “wameandikwa mbinguni.†Hii ni kwa sababu waliokufa katika Kristo sasa wanangoja ufufuo wa kwanza.

Kama Mama, Kanisa linawalisha na kuwalea watu wa Mungu—watoto wake. Petro aliuagiza uongozi “lichungeni kundi la Mungu lililo kwenu, na kulisimamia…kwa hiari†(1 Pet. 5:2). Kumbuka kwamba Paulo aliufanya wajibu wa Kanisa kama Mama uwe wazi zaidi: “kwa kusudi la kuwakamilisha watakatifu, hata kazi ya huduma itendeke, hata mwili wa Kristo ujengwe; hata na sisi sote tutakapoufikia umoja wa imani na kumfahamu sana Mwana wa Mungu, hata kuwa mtu mkamilifu, hata kufika...kimo cha utimilifu wa Kristo†(Efe. 4:12-13).

Mafungu mawili ya nyongeza katika muktadha hapa yanaonyesha kwamba “watoto†wa Mungu, kama walivyo watoto wengine, wanapaswa “kukua.†Angalia kwamba Kanisa pia linawajibika kulilinda kundi la Mungu kutoka kwa mafundisho ya uongo: “ili tusiwe TENA WATOTO WACHANGA, tukitupwa huku na huku, na kuchukuliwa na kila upepo wa elimu, kwa hila ya watu, kwa ujanja, tukizifuata njia za udanganyifu. Lakini tuishike kweli katika upendo na KUKUA hata tumfikie Yeye katika yote, Yeye aliye Kichwa, Kristo†(fu. 14-15).

Ni jukumu la uongozi kulifundisha Kanisa ile kweli na kulionya juu ya hatari ya kudanganywa na mafundisho ya uongo.

Hivyo, mtoto wa Mungu aliyetungwa anakua tumboni mwa Mama yake—Kanisa—kama vile mtoto mwingine yeyote anavyokua wakati wa miezi-tisa ya kipindi cha mimba. Wakati wakiwa katika tumbo la uzazi la Kanisa, wana wote waliotungwa wanalishwa viini-lishe muhimu vya kiroho ili wakue kufikia kiwango cha kutosha kuweza kuzaliwa katika ufalme kama Viumbe Roho wasioweza kuharibika.

Wakristo lazima wakue na kukomaa kwa namna ya roho katika tumbo la uzazi. Vijusi vya binadamu huanza kwenye ukubwa mdogo usioonekana kwa macho na kukua hadi wakati wa kuzaliwa. Mkristo mpya aliyetungwa anakua kwa njia iyo hiyo. Anaanza akiwa hajakomaa kiroho kwa 99.9% na taratibu huendelea hadi kwenye ukomavu kiroho—na KUZALIWA!

Kristo Mzaliwa wa Kwanza—Miongoni Mwa Wengi

Wakati ikizungumzia juu ya Kristo, Warumi 1:3-4 inasema, “Yaani, habari za Mwanawe, aliyezaliwa katika ukoo wa Daudi kwa jinsi ya mwili, na kudhihirishwa kwa uweza kuwa Mwana wa Mungu, kwa jinsi ya roho ya utakatifu, kwa ufufuo kutoka kwa wafu, Yesu Kristo Bwana wetu.â€

Wengi wamesikia kwamba Yesu alikuwa Mwana wa Mungu, lakini “alitangazwa kuwa†“Mwana wa Mungu, katika hali kamilifu, “kwa ufufuo kutoka kwa wafu.†Ni kweli kwamba, tayari alikuwa Mwana wa Mungu aliyetungwa kabla ya kuzaliwa Kwake katika ufalme wakati wa Kufufuka Kwake.

Andiko hili linaonyesha kwamba Kristo alizaliwa kimwili kwa Mariamu, kutokana na Daudi “kulingana na mwili,†na alizaliwa kwa namna ya roho Mwana wa Mungu “kulingana na Roho…kwa ufufuo wa wafu.â€

Tukirudi kwa Warumi 8, tunaweza kuelewa vizuri kwa nini. Kumbuka hili linahusu kuzaliwa kwa Kristo: “Maana wale aliowajua tangu asili, aliwachagua tangu asili wafananishwe na mfano wa Mwana Wake, ili Yeye awe MZALIWA WA KWANZA MIONGONI MWA NDUGU WENGI.†(fu. 29).

Kristo ni Mwana wa Mungu wa kwanza “kuzaliwa mara ya pili.†“Ndugu wengi†(wale wote walio na Roho ya Mungu kwa miaka 6,000) wataungana Naye wakati wa Kurudi Kwake. Ufahamu huu wa kushangaza unajulikana tu kwa wale wachache walioitwa leo (Yohana 6:44, 65).

Hakuna Tumaini?

Ulimwengu haujui lolote kati ya hayo uliyosoma. Umekwamishwa chini katika utata ulioukaba wa matatizo ya mwanadamu na matukio. Hakuna wawezao kusema kwa hakika kwamba wanajua kesho ina nini—wakati wengine wengi wakitumaini tu kwamba kutakuwa na kesho, kwa ajili yao na kwa ajili ya ulimwengu.

Maumivu, mkanganyiko, vita, njaa, magonjwa, ujinga, umasikini na kukosa umoja—yote haya kwa kiwango cha dunia nzima—yanawaacha wengi wakijisikia bila tumaini. Kila mwanadamu anahitaji tumaini—anahitaji kuingiziwa sababu ya kuwepo, au hata ya kuendelea, kwa sababu ya mazingira ya ukandamizaji yanayowazunguka bila kuepukika na kufasili maisha yao.

Mataifa na watu wote wanatamani amani, furaha na ustawi. Viongozi huahidi mambo haya lakini hawatimizi kamwe. Majeshi huyapigania, lakini daima hushindwa katika kusudi hili kuu. Mamilioni huomba kwa ajili yake, lakini maombi yao huenda bila kujibiwa. Amani ya ulimwengu, furaha na ustawi kwa ajili ya wote havikamatiki kuliko wakati wowote.

Lakini Biblia inasema kwamba mambo haya yatakuja—na karibu. Sura ifuatayo na ya mwisho inafafanua ni jinsi gani!

Sura ya Kumi na Moja – Jinsi Ambavyo Amani ya Ulimwengu, Furaha na Ustawi Vitakuja

Vita vimekuwa ndiyo njia ya msingi ambayo mataifa yametumia kusuluhisha migongano katika historia yote. Imechukuliwa kuwa ndiyo hali ya asili ya ulinganifu, huku amani ikichukuliwa kama kipindi cha kukusanya nguvu kutokana na kampeni iliyopita, ambapo matayarisho yanafanywa kwa hatari inayofuata au kuteka mateka. Nukuu ya Georges Clemenceau, mzalendo wa Kifaransa wakati wa Vita ya Kwanza ya Dunia, inaakisi kwa usahihi hali hii ya mambo: “Sijui kama vita hujipenyeza wakati wa amani, au amani hujipenyeza wakati wa vita.â€

Jenerali Douglas MacArthur kwa umahili aliinena hali ya sasa ya mashaka ya mwanadamu: “Tumepata fursa yetu ya mwisho. Kama hatutatengeneza mfumo mkubwa au wa haki zaidi…Harmagenia itakuwa mlangoni mwetu†(19 Aprili, 1951, hotuba kwenye Bunge la Marekani).

Serikali Moja ya Ulimwengu?

Wakati Mungu alipoanza kuniita katika kweli Yake, nilipata fursa ya kukutana na Mbunge wangu wa Bunge la Marekani kutoka jimbo la Ohio. Nilikuwa nimeomba kujiunga na Shule ya Jeshi la Majini la Marekani na waombaji wote walipaswa kukutana ana kwa ana na Mbunge wao katika hatua za mwisho kabla ya kukubaliwa. Mwishoni mwa usaili, aliniuliza kama ningependa kumwuliza maswali yoyote. Huyu alikuwa ni mtu aliyeheshimiwa sana, Mbunge wa muda mrefu (aliyewahi kuwa Spika wa Bunge) anayenipa fursa ya kumwuliza swali lolote lililokuwa akilini mwangu.

Nilikuwa na moja tu.

Nilikuwa nikijifunza juu ya serikali inayokuja hivi karibuni, yenye kutawala dunia nzima, isiyo ya kibinadamu, itakayosimamishwa wakati wa Kurudi kwa Yesu Kristo. Nikiwa na jambo hili kwenye fikra zangu, nilimwuliza Mbunge maoni yake juu ya serikali moja ya ulimwengu mzima, kama ingekuwa katika mikono ya wanadamu. Jibu lake lilikuwa la haraka na la msisitizo, “Siamini kwamba itafanikiwa, lakini kama ningekuwa naamini, ningepaaza sauti yangu kuitangaza kutokea juu ya mapaa ya nyumba.†Kisha akaendelea kuelezea mambo mbalimbali.

Jambo hili liliniachia ushawishi wa kudumu. Sijaweza kusahau mazungumzo yangu na mbunge huyu mwenye uzoefu wa zaidi ya miaka thelathini katika serikali ya muungano.

Tangu wakati huo, wengi wamependekeza kwamba serikali moja ya ulimwengu mzima ndiyo njia pekee ya kupata amani na uthabiti. Lakini maswali mengi yanaibuka. Nani ataileta? Jinsi gani itaingizwa madarakani? Itasimamia sheria zipi? Sheria hizo zitatekelezwaje? Je, serikali za mataifa zitaiachia madaraka yao? Je, itafanikiwa, au hatimaye itawagandamiza na kuwafanya watu wote watumwa? Maswali haya daima huwaacha wenye kufikiri, wanamipango, viongozi na wanasayansi wakikuna vichwa katika harakati za kutekeleza majukumu yao.

Kwa hiyo, amani ya ulimwengu imebaki kutokuwa ya uhakika. Inavyoonekana ni kwamba kila mmoja anaitamani, lakini hakuna anayejua jinsi ya kuipata. Kwa nini? Kwa nini viongozi wenye uzoefu na wenye akili za kufikiri wa nyakati zetu hawawezi kuipata njia ya amani? Kwanini watu wanafahamu kwamba suluhisho pekee ambalo linaweza kuleta amani ni serikali moja lakini, wakati huo huo, wanakiri kwamba jambo hili haliwezekani kabisa kama litaachwa mikononi mwa wanadamu? Kama watu hawawezi kutawala maisha yao wenyewe, jinsi gani wataweza kutawala ulimwengu mzima?

SABABU ya Watu Kutoweza Kupata Amani

Mwanadamu, katika uasi wake dhidi ya Mungu, anapenda kuonyesha aina ya ustaarabu wake katika mwanga bora kadri inavyowezekana. Kwa namna hiyo hiyo, manabii wa uongo wa Israeli, kama Ezekieli alivyotabiri kuhusu nyakati zetu, wanatamka, “Amani; na hapakuwa (hakuna) amani†(13:10). Mungu anaonyesha kwamba amani haitakuwa ya kudumu kwa wale wanaoacha njia Zake.

Imesemwa kwamba mataifa yote ama yanajiandaa kwa vita, yako vitani au yanapumuzika kutoka kwenye vita. Historia inaonyesha hili—imerekodi karibu vita 15,000. Cha kushangaza, nyingi ya vita hivi vilipiganwa “katika harakati za kutafuta amani.†Lakini, matokeo ya vita kawaida yanajumuisha mkataba ambao daima hushindwa kuzalisha amani ya kudumu. Hii ni kwa sababu wanadamu hawawezi, na wao wenyewe bila msaada kutoka nje, hawataweza kamwe, kupata njia ya amani. Kwa hakika, hawana nafasi ya kuipata amani ya ulimwengu. Tena, kwa nini?

Kama sehemu ya unabii mrefu kuhusu hali ya mambo duniani katika nyakati zetu, Isaya anajibu swali hili: “NJIA ya amani hawaijui; wala hapana hukumu ya haki katika miendo yao; wamejifanyizia njia zilizopotoka; kila apitaye katika njia hizo hatajua amani†(59:8). Suluhu za wanadamu daima hupelekea kwenye vita zaidi, maangamizi, maumivu, kifo na uharibifu. Pia, Paulo aliandika, akimnukuu Isaya, “Wala njia ya amani HAWAKUIJUA†(Rum. 3:17).

Kweli jinsi gani!

Serikali za wanadamu kwa urahisi haziwezi kufanya kazi. Hazijafaulu kamwe katika kutafuta suluhu za kudumu kwa yale ambayo, kulingana nazo, yamekuwa ni matatizo yasiyotatulika. Hawana majibu kwa maswali makuu zaidi ya mwanadamu. Kwa kweli, suluhu zao zinaakisi “kutokuwa na hukumu katika miendo yao.†Wanadamu hawakupewa kujua njia ya amani—au, kwa mantiki hiyo, njia ya mafanikio, furaha, afya na ustawi. Si ajabu kwamba wenye akili wakuu, viongozi, waelimishaji na wanasayansi wameshindwa vibaya katika utafutaji wao wa amani duniani! Mungu hajawafunulia bado halaiki ya wanadamu jibu hasa kwa vita visivyokoma, na matatizo ya ulimwengu.

Swala la Serikali

Lakini Kristo aliponena juu ya “ufalme,†alimaanisha nini? Injili ya ufalme wa Mungu ina vipengele viwili tofauti.

Wengi huongea juu ya wokovu—imani katika kile kilicho baada ya maisha. Baadhi wamedhani kwamba injili imejikita tu katika “kupokea uzima wa milele†au lile wazo maarufu la “kwenda mbinguni†wakati wa kufa. Ni dhahiri kufikia hivi sasa, tumejifunza kwamba Biblia ina mengi ya kusema kuhusu wokovu. Kwa hakika, wokovu unahusiana moja kwa moja na—ni kipengele kimojawapo cha—injili ya ufalme wa Mungu.

Wengi wanadhani kwamba Mungu anajaribu kuuokoa ulimwengu sasa—kwamba leo ndiyo fursa pekee kwa ajili ya wokovu kwa wanadamu wote. Lakini kwa sababu wengi hawana wazo kwa nini walizaliwa—kwa nini waliwekwa duniani—vile vile hawafahamu kwa nini mwanadamu hawezi kupata amani, furaha, afya na mafanikio kwa njia yake mwenyewe. Ulimwengu mzima umedanganywa kuhusu wokovu na maswali muhimu zaidi pamoja na majibu ya maisha.

Kipengele kingine cha ufalme wa Mungu ni SERIKALI. Kama ilivyoonekana, neno ufalme linamaanisha serikali. Ufalme wa Mungu utakapofika, utakuwa ni SERIKALI BORA itawalayo-ulimwengu. Biblia inauelezea ufalme huu kwa undani sana.

Ujumbe Kuhusu Serikali

Sura hii itaelezea kipengele cha “serikali†cha ufalme. Sura zingine (pamoja na vitabu vyangu vingine vingi) kimsingi vinaelezea kipengele cha “wokovuâ€.

Kumbuka kwamba kabla ya kuzaliwa kwa Yesu, malaika alimtokea Mariamu, mama Yake. Mafungu haya yanaelezea kukutana huku na kile ambacho aliambiwa: “...malaika Gabrieli alitumwa na Mungu kwenda... Nazareti, kwa mwanamwali bikira aliyekuwa ameposwa na mtu, jina lake Yusufu, wa mbari ya Daudi; na jina lake bikira huyo ni Mariamu. Akaingia nyumbani kwake akasema, Salamu, uliyepewa neema...Utachukua mimba na kuzaa mtoto Mwanamume; na jina Lake utamwita YESU. Huyo atakuwa mkuu, ataitwa Mwana wa Aliye juu, na Bwana Mungu Atampa kiti cha enzi cha Daudi, baba Yake. ATAIMILIKI nyumba ya Yakobo hata milele, na UFALME Wake utakuwa hauna mwisho†(Luka 1:26-33).

Tuliona Yesu alimwambia Pilato, “Ufalme [serikali] Wangu sio wa ulimwengu huu.†Pilato akauliza “Wewe u mfalme basi?†Yesu akajibu, Wewe wasema, kwa kuwa Mimi ni mfalme. Mimi nimezaliwa kwa ajili ya haya, na kwa ajili ya haya Mimi nalikuja ulimwenguni†(Yohana 18:36-37). Yesu Kristo alizaliwa ili kuwa MFALME!

Hapa ni kile tulichoona ambacho Isaya alitabiri kuhusu Kristo: “Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto Mwanamume; Na uweza wa kifalme [SERIKALI] utakuwa begani Mwake; Naye ataitwa Jina Lake, Wa-ajabu, Mshauri, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, MFALME WA AMANI. Maongeo ya enzi [SERIKALI] Yake na AMANI hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na UFALME WAKE; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele†(9:6-7).

Kristo atakapoisimamisha serikali ya Mungu duniani, italeta amani kwa mataifa yote!

Manabii Wote wa Mungu Walihubiri Injili

Mapema, tuliona kwamba Petro alitoa kauli ya kushangaza ya historia ya Biblia. Alinena juu ya wakati ambapo “... zipate kuja nyakati za kuburudishwa kwa kuwako Kwake Bwana; Apate kumtuma Kristo Yesu mliyehubiriwa tangu zamani; Ambaye Ilimpasa kupokewa mbinguni hata zije zamani za kufanywa upya [urejeshaji] vitu vyote...†(Matendo 3:19-21). Kwa hakika, mbingu zimempokea Kristo “hata†urejeshaji wa vitu vyote. Lakini urejeshaji huu haujatokea bado—hivyo, neno “hata.â€

Katika Sura ya Pili, tulieleza kwamba kila mmoja (ilisema “woteâ€) wa watumishi wa kweli wa Mungu amehubiri kwamba wakati unakuja ambapo Kristo atarudi na “vitu vyote vitarejeshwa.†Kabla ya kuasi kwa Shetani, Serikali ya Mungu ilikuwepo duniani.

Kwa maelfu ya miaka, watumishi wa Mungu walitabiri kwa kinaganaga kurejeshwa kwake duniani. Umekwisha kuona kwamba manabii wote wa Agano la Kale na wengine walitangaza, kwa namna moja au nyingine, kuja kwa ufalme wa Mungu na “kufanywa upya vitu vyote.†Haya hapa ni maelezo katika Agano Jipya, yakimrejelea mmoja tu wa wasemaji wa Mungu wa Agano la Kale.

Kumbuka kwamba maelezo ya Yuda yanarekodi mahubri ya Babu Mkuu wa Nuhu Henoko. Haya ni maelezo ya moja kwa moja juu ya kile kilichosemwa takriban miaka 4,500 iliyopita—hata kabla ya Gharika. Fikiria UPANA wa kushangaza zaidi wa aya hii: “Na Henoko, mtu wa saba baada ya Adamu, alitoa maneno ya unabii juu ya hao, akisema, Angalia, Bwana alikuja na watakatifu Wake, maelfu maelfu, ili afanye hukumu juu ya watu wote, na kuwaadhibisha wote wasiomcha Mungu...kwa ajili ya kazi zao zote...walizozitenda...na kwa ajili ya maneno magumu yote ambayo hao wenye dhambi...wameyanena juu Yake†(fu. 14-15).

Pata maana iliyo wazi ya aya hii. Watakatifu (Wakristo wote wa kweli) wanakuja na Kristo kuuhukumu ulimwengu—kuwahukumu “wote†kulingana na mienendo yao.

Biblia ina mengi zaidi ya kusema kuhusu ufalme wa Mungu kuliko ulivyodhani. Kwa mara nyingine tena, ukweli unaduwaza kabisa—hata kushtusha—na huhitaji kutoufahamu.

Danieli Alifahamu

Kama vile Henoko alivyofahamu kwamba ufalme wa Mungu ulikuwa ni serikali halisi ambayo siku moja ingetawala juu ya watu halisi na mataifa halisi duniani, vivyo hivyo nabii Danieli. Hakushikilia fikra za uongo kwamba ufalme ulikuwa tu aina fulani ya “hisia za moyoni zisizo na uzito†au “hisia za kuchangamka†zilizo katika “mioyo ya wanadamu.†Kupitia mfuatano wa ndoto na maono (1:17), Mungu alimtumia kufafanua ufahamu maalumu kuhusu jinsi na lini ufalme Wake ungekuja duniani.

Yale yote ambayo Danieli alionyeshwa yalipaswa “kufungwa na kutiwa muhuri hata wakati wa mwisho†(12:9). SASA tuko kwenye wakati wa mwisho—na kuna uthibitisho mwingi juu ya hili. Ujumbe wake ni kwa ajili yetu, leo! Danieli aliripoti kwa upana—KWA UPANA MKUBWA!—habari ambazo zitakuathiri katika siku za maisha yako! Mapema, tuliona kwamba Danieli pia alifahamu na aliongea injili ile ile ambayo Yesu alihubiri—na ni muhimu mno tufahamu alichosema.

Danieli alitambua kwamba alikuwa mdomo tu ambao kupitia kwake MUNGU alikuwa akifunua Mpango Wake Mkuu. Katika sura ya pili, alikuwa akiongea na Mfalme wa Wakaldayo (Wababeli) Nebukadneza kuhusu mambo ambayo yalimfikia mfalme katika ndoto. Nebukadneza alikuwa mfalme wa himaya kubwa sana aliyoitawala karibia miaka mia-sita kabla ya wakati wa Kristo.

Wachawi katika mahakama ya mfalme hawakuweza kufunua kile ambacho Mungu angeweza kukifunua kupitia kwa nabii Wake Danieli. Lilikuwa ni kusudi la Mungu kufunua, kupitia yule mfalme mwanadamu wa kidunia, kwamba yuko Mwenyezi Mungu aliye hai atawalaye ulimwengu wote na wafalme wote, serikali na mataifa duniani hatimaye wako chini Yake. Mfalme mwenye hekima ya kibanadamu Nebukadneza hakuwa na maarifa ng’ambo ya uwepo wa wafalme wengine wa kibinadamu na miungu yao mingi ya uongo. Lilikuwa ni lengo la Mungu wa kweli kufunua uwepo wa serikali YAKE na kwamba inatawala ulimwengu wote. Pia alikusudia kuweka wazi KUSUDI Lake KUU la kuleta serikali hiyo duniani “katika siku za mwisho.â€

Chukua muda usome kwa makini Danieli 2:28-44. Unabii huu wa kushangaza na ulioeleza kila kitu kwa ukamilifu unafunua mambo mengi kuhusu lengo la Mungu la kurejesha serikali Yake duniani—ukijumuisha mtiririko wa matukio hadi kutokea kwa jambo hili.

Mafungu kadhaa ya mwanzo yanaelezea sanamu ya mtu mkubwa. Mafungu ya 32-33 yanasema, “Na sanamu hii kichwa chake kilikuwa ni cha dhahabu safi; kifua chake na mikono yake ni ya fedha; tumbo lake na viuno vyake ni vya shaba; miguu yake ni ya chuma; na nyayo za miguu yake nusu ya chuma na nusu ya udongo.â€

Kwa hakika hii ni sanamu ya mtu, lakini iliyojengwa kwa sehemu nne tofauti. Kisha mafungu ya 34-35 yanaelezea “jiwe lisilo la kawaida lililoipiga sanamu [na] likawa mlima mkubwa, na kuijaza dunia yote.†Angalia kwamba fungu la 34 linasema kwamba jiwe “lilichongwa bila mikono,†kwa sababu Mungu, siyo watu, alikuwa amelitengeneza.

“Jiwe†liliivunja sanamu na kuchukua mahali pake, hatimaye likaendelea kuyazingira mataifa yote—“dunia yote.†Haya yanaweza kuwa tu ni maelezo ya SERIKALI YA MUNGU ikija duniani. Danieli anatangaza tu ujumbe ule ule wa injili ya ufalme ambayo Kristo alihubiri.

Huhitaji kuniamini mimi, kwa sababu hiki ndicho kile ambacho Biblia yako inasema. Hakuna mtu anayehitaji “kukufasiria†mfuatano wa mafungu haya.

Hebu tu angalia fungu la 37. Linasema wazi, “Wewe, Ee mfalme, u mfalme wa wafalme, na Mungu wa mbinguni amekupa ufalme, na uwezo, na nguvu, na utukufu.†Fungu la 38 linafafanua, “Wewe u kichwa kile cha dhahabu.†Kumbuka, wakati wote lazima tuiache Biblia iifasiri Biblia.

Mafungu 39-40 yanaendelea kuelezea falme tatu zilizofuatana ambazo zingefuata ufalme wa Nebukadneza na Babeli.

Mafungu haya yanaonyesha mfuatano wa kihistoria wa HIMAYA ZA ULIMWENGU zilizoonyeshwa na madini tofauti ambayo kwa hayo ile sanamu kubwa ilikuwa imetengenezwa. Hizi zilikuwa ni falme halisi: (1) Himaya ya Kaldia-Babeli ya dhahabu, (2) Himaya ya Medi-Uajemi ya fedha, (3) Himaya ya Giriki-Masedonia ya shaba, na (4) Himaya ya Rumi, iliyotengenezwa kwa chuma kilichochanganyika na udongo wa mfinyanzi katika mwonekano wake wa mwisho. Ujumbe kutoka historia ni kwamba falme hizi nne (himaya) zilitawala, na ufalme wa nne utatawala tena mara moja na kuathiri ulimwengu mpaka ufalme wa Mungu utakaposimamishwa duniani.

Mungu anatufunulia kwa wazi sasa kwamba Yeye ndiye anayesimamisha na kuondoa—na kusimamisha na kuondoa, tene na tena—serikali (falme) za kidunia.

Kufasili Ufalme

Wengi wanauliza, “Lakini ni nini hasa fasili ya Biblia ya ufalme?†Wahubiri na wanateolojia wamejaribu kuifanya maana yake kuwa ya kiroho, kwa sababu hawajachunguza kwa makini fasili ya Mungu.

Hii inapatikana mwishoni mwa fungu la 39, ambalo linarejelea falme hizi “ambazo zitatawala dunia yote.†Hiki hakiwezi kuwa kielelezo cha wazo lisilo halisi kuhusu ufalme katika “mioyo ya watu.†Pia hakuna njia ya kuifanya fasili hii ikubaliane na kanisa lolote au makanisa. Inaongelea utawala wa serikali na mamlaka juu ya mataifa halisi duniani—na juu ya watu halisi. Je! Utamruhusu mtu mwingine akuambie tofauti au utaiamini fasili ya Biblia ya ufalme? Kumbuka, falme hizi “zinatawala dunia yoteâ€!

Zingatia vipengele viwili muhimu vya sanamu kubwa la madini zilizoelezewa hapa. Kwanza, madini yanapungua THAMANI kadri tunavyoshuka kutoka kichwani kwenda miguuni na nyayo za sanamu. Hii ina maana kwamba ubora wa kila ufalme/himaya unaofuata ni wa chini katika thamani kuliko ule ulioutangulia. Pili, madini yanaongezeka katika UTHABITI [nguvu] kadri tunavyoshuka kwenye mwili wa sanamu. Kwa maneno mengine, nguvu na ukubwa wa kila ufalme/himaya unaofuata ni kubwa kuliko ule ulioutangulia.

Hatimaye, tambua kwamba ile miguu miwili ya chuma inawakilisha ufalme ambao umegawanyika. Himaya ya Rumi kweli ilikuwa imegawanyika, ikiwa na makao makuu mjini Roma na Konstantinopo. Vidole kumi vya miguu nusu ni chuma na nusu ni udongo wa mfinyanzi. Chuma hakichangamani na hakiwezi kuchangamana na udongo wa mfinyanzi, hivyo hii ni picha ya hali ya kuyumba-yumba hapo mwishoni. Wakati miguu inapovunjika, mwili wote wa mtu utaanguka. Usomaji wa makini wa sura tatu lazima ufanywe ili kufahamu kwa undani mfuatano wa hizi falme nne na kuona kwa wazi zaidi kwamba vidole kumi vya miguu kwa hakika ni wafalme kumi tofauti ambao wataungana kwa muda katika siku za mwisho.

Linganisha Ufunuo 13 na 17 pamoja na Danieli 7. Kwa pamoja, zinawakilisha unabii imara na unaomfanya mtu afikiri kuhusu matukio ya siku za mwisho—matukio ambayo yatakuathiri wewe na mimi katika siku za maisha yetu! Ufunuo 17:8 inaeleza juu ya “mnyama†anayepanda kutoka kwenye “shimo la kuzimu†na ambaye amepandwa na “mwanamke.†Fungu la 12 linaonyesha kwamba mnyama huyu anahusisha WAFALME KUMI watakaopokea mamlaka na kuungana chini ya kiongozi mwenye haiba atakayechukua jukumu la “mnyama.†Huku kutakuwa ni kufufuka kwa Himaya Takatifu ya Rumi kwa mara ya saba, na ya mwisho, itakayodumu kwa muda mfupi—inayotokea SASA HIVI katikati ya Ulaya.

Muungano wa Nchi za Ulaya unakuja na uko hapo mbele kidogo. Ni muhimu kwamba uelewe unabii huu unamaanisha nini!

Kitu cha kushangaza kinatokea “katika siku za wafalme hawa†(vidole kumi vya miguu, zinazowakilisha wafalme kumi wa Ufunuo 17:12). Kuwasili kwa Kristo kunaondoa shaka yote kuhusu NINI hasa ni ufalme wa Mungu. Pia, Mungu anatuambia LINI utawasili—“katika siku za wafalme hawa.†Danieli 2:44 inasema, “Na katika siku za wafalme hao Mungu wa mbinguni atausimamisha ufalme ambao hautaangamizwa milele, wala watu wengine hawataachiwa enzi yake [Mungu hataruhusu kamwe watu kuchukua uongozi], bali utavunja falme hizi zote vipande vipande na kuziharibu, nao utasimama milele na milele.â€

Hiyo ni sawa! Mungu—siyo wanadamu—atasimamisha himaya ya mwisho na iliyo kubwa zaidi kuwahi kutawala ulimwengu wote. Na anatuambia kwamba Hataruhusu kamwe mawazo au juhudi za wanadamu kuingilia na kuikatiza, maana “itasimama milele.†Ahadi hii ni YA HAKIKA. Itatimia—bila kujali watu wanaiamini au hawaiamini!

Mwanamke wa Ufunuo 17

Kulinganisha Danieli 7 pamoja na Ufunuo 13 na 17 inafunua kuna uhuishaji mara saba wa Himaya Takatifu ya Rumi. Uhuishaji mara sita umekuja na kupita—na mmoja umebaki ambao sasa unajiunda! Utadumu kwa takribani miaka 3 1/2, wakati wa kipindi cha kutisha ambacho Biblia inakiita Dhiki Kuu (Mat. 24:21-22) na wakati wa “Taabu ya Yakobo†(Yer. 30:1-7). Ni baada ya ufufuo huu wa mwisho ambapo ufalme wa Mungu utasimamishwa.

Ni muhimu kufahamu kiunganishi kingine kwenye uhuishaji mara saba (au ufufuo) wa mfumo wa Kirumi. Ufunuo 17 inauelezea kila uhuisho kama wenye “mwanamke aliye[keti] juu ya mnyama mwekundu sana, aliyejaa majina ya makufuru, akiwa na vichwa saba na pembe kumi†(fu. 3). Vichwa saba ni uhuisho mara saba tofauti, pamoja na uhuisho wa mwisho wa pembe-kumi unaoundwa na wafalme kumi.

Kuhusu mwanamke, mafungu ya 5-6 yanasema kwamba “…katika kipaji cha uso wake alikuwa na jina limeandikwa, LA SIRI, BABELI MKUU, MAMA WA MAKAHABA NA MACHUKIZO YA NCHI. Nikamwona yule mwanamke amelewa kwa damu ya watakatifu, na kwa damu ya mashahidi wa Yesu.†Fungu la 1 linamwita “kahaba mkuu aketiye juu ya maji mengi...†pamoja na fungu la 15 likifafanua kwamba “maji†ni jamaa na makutano na mataifa na lugha.â€

Hii ni picha kielelezo ya kanisa la watu wa Mataifa ambalo ni kubwa sana na lenye nguvu ambalo ni mzaliwa wa sasa wa mfumo wa Babeli ya zamani. Yeye ni “mama†wa mabinti makanisa wengi “makahaba.†Makanisa haya yalitoka kwake kwa kupinga machache ya baadhi ya machukizo yake. Fahamu. Hili siyo kanisa dogo, bali ni kanisa “kuu†linalotawala “watu†wengi na “mataifa.†Fungu la 2 linaongelea juu ya “uasherati†wake na “wafalme wa dunia.†Na fungu la 18 linamwongelea mwanamke kama “ule mji mkubwa, unaotawala juu ya wafalme wa nchi.â€

Huyu ni mwanamke tofauti kabisa kuliko yule wa Ufunuo 12, ambaye ataolewa na Yesu Kristo (Ufu. 19:7; Math. 25:1-10; Efe. 5:23) wakati wa Kurudi Kwake. Sura hii inaelezea Kanisa la kweli la Mungu ambalo limeteswa na kanisa kuu la watu wa Mataifa kwa miaka 2,000 (17:6). Mungu atamharibu kahaba huyu mkuu na mabinti zake makahaba kwa kumgeuza mnyama anayempanda kinyume chake (17:16). Lakini kwanza lazima “aendeshe†ufufuo wa mwisho wa Himaya (Mfumo wa Kibabeli) Takatifu ya Rumi!

Hakuna muda mwigi uliobaki hadi kufikia uhuisho huu wa mwisho kutokea—unajiunda hata sasa!—na ufalme wa Mungu wa ajabu kutokea muda mfupi baada ya hapo. Serikali zote za wanadamu—ikiwa ni pamoja na zile za nchi kubwa na ndogo duniani leo—zitavunjwa na mahali pake kuchukuliwa na SERIKALI BORA ya Mungu inayokuja.

Tuliona kwamba Yesu Kristo alizaliwa kuwa mfalme—kutawala mataifa yote ya dunia milele akisaidiwa na wafalme wengine waliofanyizwa kwa roho. Angalia tena: “Na upanga mkali hutoka kinywani Mwake [Kristo] ili awapige mataifa kwa huo. Naye Atawachunga kwa fimbo ya chuma...Naye ana jina limeandikwa katika...paja Lake, MFALME WA WAFALME, NA BWANA WA MABWANA†(Ufu. 19:15-16).

Karibuni, Ufunuo 11:15 itatimia, na ulimwengu wote utaona: “Ufalme wa dunia umekwisha kuwa ufalme wa Bwana wetu na wa Kristo Wake, naye atamiliki hata milele na milele.†Kama ilivyo kwamba hakuna shaka kwamba leo hii nchi zinawakilisha falme halisi hasa (mataifa na serikali), hapawezi kuwa na shaka, kutoka kwenye fungu hili, kwamba serikali ya Mungu inayokuja pia ni halisi hasa ikitawala juu ya mataifa halisi duniani.

Ufalme Ndani ya Mioyo ya Watu?

Wengi huchagua kuamini kwamba ufalme wa Mungu huingia ndani ya watu badala ya watu kuingia katika ufalme. Tumeona kuwa ili kufikia hitimisho hili, ni lazima watu wapuuze kauli zilizo wazi za Kristo. Wanaugeuza ufalme halisi wa Mungu unaokuja kuwa “jambo la kiroho,†ili kuugeuza kuwa hisia za kufikirika katika mioyo ya wanaodai kuwa Wakristo. Waongo wamesema kwamba kuwa na Roho ya Mungu ni kuwa na ufalme wa Mungu ndani yako na kupata uzoefu wake. Karne nyingi za udanganyifu wa wazi zimewafanya mamilioni kuamini hadithi za kubuni—badala ya UKWELI DHAHIRI wa Biblia.

Tangu Kristo aliposema injili ilikuwa juu ya ufalme wa Mungu, na watu hawajui ufalme wa Mungu ni nini, basi, wamehitimisha kwamba ufalme unaweza kuwa dhehebu la kanisa fulani au Ukristo kwa pamoja. Wengine huushusha hadi kudhani ni “hisia changamfu†ndani ya “mioyo ya watu.†Bado wengine wanaamini kwamba ufalme ni “Milenia†au hata “Himaya ya Uingereza.†Baadhi hata wamehitimisha kwamba injili ya ufalme wa Mungu si kwa ajili ya wanadamu leo!

Watu wanapaswa kuamka dhidi ya udanganyifu—madanganyo makuu—ya unaodhaniwa kuwa Ukristo ambao kwa hakika unakataa KWELI DHAHIRI zote za Biblia! Mpango wa Mungu kwa ajili ya wanadamu unaduwaza—usioweza kulinganishwa na kitu chochote walichobuni wanadamu kuchukua mahali pa kile Anachokisema. Lakini ulimwengu unapuuza maandiko dhahiri, ya wazi, yaliyo bayana yanayopatikana kote katika Biblia kuhusu ufalme wa Mungu, na kuubadili ukweli na kitu cha hali ya chini mno kinachodaiwa kuwa “wokovu†mbinguni na “ufalme†ndani ya mioyo ya watu.

Kwa kuwa ni wazi kwa wengi kwamba watu wanaweza kuingia katika nchi nyingi za kisasa za iliyokuwa Himaya ya Uingereza na kwamba watu wanaweza kuingia katika kanisa, wanadini waliodanganywa walitengeneza wazo kwamba ufalme wa Mungu unakaa ndani ya “mioyo ya watu.â€

Nimewasikia mara nyingi watu wakieleza kitu kinachofanana na hiki: “Ufalme wa Mungu unaweza kusimamishwa ndani ya mioyo ya watu ikiwa Wakristo wote kila mahali watafanya kazi pamoja katika upendo ili kuleta amani ya ulimwengu na watu wote kuvumiliana.â€

Wanapata wapi wazo hili? Kiujumla ni kutokana na tafsiri isiyo sahihi ya Luka 17:20-21! Katika aya hii, Kristo alionekana kuongelea ufalme wa Mungu “ndani yenu.†Tunahitaji kuichunguza tafsiri hii isiyo sahihi. Ikiwa fungu hili kwa hakika linasema kwamba ufalme wa Mungu uko “ndani†ya watu, basi linapingana na maandiko mengine yote tuliyoyachunguza. Na kama Biblia inapingana yenyewe kwa wazi namna hii, tunaweza kuitupa, maana haiwezi kuwa Neno la Mungu.

Ufalme Ndani ya Mioyo ya Mafarisayo?

Hebu sasa tuichunguze Luka 17:20-21: “Na alipoulizwa na Mafarisayo, Ufalme wa Mungu utakuja lini? Aliwajibu akawaambia, ufalme wa Mungu hauji kwa kuuchunguza; wala hawatasema, Tazama, upo huku, au, kule, kwa maana, tazama, ufalme wa Mungu umo ndani yenu.â€

Ikiwa huelewi kitu kingine chochote katika fungu hili, elewa pointi hii moja kwa moja! Kristo alikuwa akiongea na watu wenye tabia ya mwilini, waongo, Mafarisayo wanafiki. Hata kama ile hisia ya kufikirika kwamba ufalme wa Mungu ni kitu ambacho kiko ndani ya mioyo ya watu ingekuwa ya kweli, hakuna uwezekano kabisa kwamba Kristo alikuwa akimaanisha kuwa ufalme ulikuwa ndani ya mioyo ya watu hawa! Mafarisayo walijihesabia haki na hawakuwa waongofu. Wakati wote walikuwa wakitafuta kumjaribu Kristo ili wapate kumshitaki. Ni jambo la kipumbavu kabisa na hata la mzaha kusema kwamba ufalme wa Mungu ulikuwa “ndani†yao. Usipoteze ukweli huu kwamba pale Kristo alipowajibu, inasema, “Aliwajibu.†“Aliwaambiaâ€â€”Mafarisayo. Elewa kwamba Mafarisayo hawakuwa Kanisani, na kwa hakika Kanisa la Mungu HALIKUWA ndani ya Mafarisayo. Kwa kweli, hata Kanisa la Agano Jipya lilikuwa bado halijakuwepo.

Angalia kile ambacho Kristo HAKUSEMA katika fungu hili. Hakusema, “ufalme wa Mungu utasimamishwa ndani ya mioyo ya watu†au “ndani ya mioyo yenu.†Alichosema ni, “ufalme wa Mungu NI...†Ni muhimu tufahamu kwamba katika tukio hili, Kristo alikuwa haelezei, ufalme wa Mungu, kama kitu kitakachokuja mbele, lakini badala yake Aliuzungumzia katika hali iliyopo.

Kwa nini?

Nimesema kwamba hii ni tafsiri isiyosahihi ya Kigiriki asili. Maneno halisi ya Kigiriki ambayo Luka aliyatumia hapa yanatafsiriwa vizuri zaidi “kati kati yenu†au “miongoni mwenu.†Idadi kadhaa ya tafsiri zingine zinasomeka namna hii, na Biblia nyingi zenye maelezo ya pembeni zinajumuisha semi hizi.

Biblia ya Revised Standard Version inasema, “ufalme wa Mungu uko kati kati yenu,†na tafsiri ya Moffatt inatoa hata ufahamu zaidi. Anatafsiri mafungu haya mawili kama “Aliwajibu, ‘UTAWALA wa Mungu hauji kama mnavyotumaini kuuona; hakuna yeyote atakayesema, “Huu hapa†au “Uko kule,†kwa maana UTAWALA wa Mungu sasa uko miongoni mwenu.â€â€™

Hebu tuulize, nini—au nani—anaweza kuwa yule ambaye Kristo alikuwa akimwongelea? Nini—au nani—alikuwa “kati kati†ya Mafarisayo? Nini—au nani—alikuwa “miongoni†mwao?

Mwana wa Mungu—Yesu Kristo Mwenyewe!—alikuwa amesimama katikati ya kundi hili la Mafarisayo. Fikiria kwa namna hii: Walikuwa mbele ya mwakilishi wa moja kwa moja ambaye “atatawala†katika ufalme wa Mungu ujao. Alikuwa Yesu aliyekuwa amesimama “miongoni†mwao. Ni wazi, Kristo alikuwa akiongelea juu ya ufalme wa Mungu, kupitia kwake Mwenyewe kama mwakilishi wake, akiwa pale pale walipokuwa wamesimama.

Hebu tuelewe! Mafarisayo walijua unabii mwingi wa Agano la Kale na maandiko yanayoelezea ufalme wa Mungu. Walikuwa na habari ya mafungu ambayo tumejifunza kutoka kitabu cha Danieli, na sehemu zingine. Wangeweza kuelewa kwa nini Petro baadaye angesema, “manabii wote watakatifu†walinena juu ya “kufanywa upya vitu vyote.†Waliuelewa unabii wa Isaya, Yeremia, Ezekieli, Danieli na wengine wengi. Mafarisayo walipuuzia maandiko kuhusu Kuja kwa Kristo Mara ya Kwanza kwa sababu walitaka kufokasi tu kwenye maandiko mengi yanayoelezea Kuja Kwake Mara ya Pili!

Ni wazi, Mafarisayo hawakuamini ufalme wa Mungu ulikuwa kanisa. Bila shaka hawakuamini ulikuwa ni Himaya ya Uingereza—ambayo ulimwengu usingeiona kwa karne nyingi. Na hawakuamini ulikuwa ni msisimko wa hisia katika mioyo ya watu. Walielewa kikamilifu kwamba ulihusika na serikali—UTAWALA!

Tatizo lilikuwa kwamba hawakufahamu LINI ufalme ungekuja au kwamba kusudi lake halikuwa tu kuyafukuzia mbali majeshi ya Kirumi kutoka Palestina. Kama wangefahamu Kuja kwa Kristo Mara ya Kwanza, wangefahamu vyema kuhusu “lini†kungekuwa Kuja Kwake Mara ya Pili—na kwa nini kulitakiwa kutokea baadaye sana. Hivyo, walikuwa wakitumainia Masihi mwenye kushinda ambaye angewasaidia katika hitaji lao kupindua utawala wa Kirumi ili wao wachukue mahali pa Warumi, kama mabwana juu ya Rumi.

Yesu alifafanua kosa la kufikiri kwao. Aliweka wazi kwamba kuja kwa ufalme hakukuwa tukio dogo, la mahali fulani tu, amabalo lingekuwa na kikomo cha utawala juu ya eneo Wayahudi walipoishi Palestina.

Wayahudi walikuwa wanatazamia serikali ya kibinadamu iliyoko katika taifa moja—la kwao! Hii ndiyo sababu Kristo aliwaambia wasiufikirie ufalme kama uko “kule†au “hapa.â€

Si tu kwamba Kristo alijua kwamba alizaliwa ili kuwa Mfalme, alitambua hii ilimaanisha kwamba alikuwa amekusudiwa mwishowe kuwa Mfalme juu ya Ufalme Wake. (Danieli 7:17-18 na 23 inaonyesha kwamba maneno kwa ajili ya ufalme na mfalme yanabadilishana katika Biblia.)

Kwa kuendelea kusoma zaidi muktadha wa Luka 17, tunaachwa bila shaka juu ya nini Kristo alikuwa anarejelea. Soma fungu la 24, mahali ambapo, kama Mathayo 24:27, inavyorejelea, “Kwa maana kama vile umeme utokavyo mashariki ukaonekana hata magharibi, hivyo ndivyo atakavyokuwa Mwana wa Adamu katika siku Yake.†Kristo alikuwa anaelezea tukio la kuduwaza, litakalotikisa-ulimwengu ambalo litaonekana kama umeme…Lakini, angalia msemo “katika siku Yake,â€ambao unaonyesha kwamba ni tukio la wakati ujao. Chukua muda kusoma Mathayo 24:26-30 na jinsi inavyoeleza “siku ambayo Kristo atafunuliwa.â€

Hakuna namna ya kufikiri kwamba Kristo alisema ufalme wa Mungu ulikuwa ndani ya Mafarisayo, wasio na haki, wenye nia ya mwilini, wenye chuki—walioendelea kupanga Kumwua—vile vile kama ambavyo hakusema ulikuwa kanisa.

Hapo nyuma Kristo alikuwa amewashitaki Mafarisayo kwa onyo la kutisha. Hakuna shaka, jambo hili liliwafanya wakasirike, na kuwafanya wapange kumkamata ikiwa angesema neno ambalo halikuwa sahihi kuhusu ufalme wa Mungu au jambo lingine lolote. Katika Luka 13:28-29, alikuwa amewaonya, “Ndipo kutakapokuwa na kilio na kusaga meno, mtakapomwona Ibrahimu na Isaka na Yakobo na manabii wote katika ufalme wa Mungu, nanyi wenyewe mmetupwa nje. Nao watakuja watu toka mashariki na magharibi, na toka kaskazini na kusini, nao wataketi chakulani katika ufalme wa Mungu.â€

Kristo alikuwa akiwaambia dhahiri Mafarisayo kwamba hawatakuwepo katika ufalme wa Mungu. Hawataruhusiwa kuuingia, kama vile Ibrahimu, Isaka na Yakobo watauingia—japokuwa watu hawa hawajauingia bado (Ebr. 11:13, 39-40).

Ufalme wa Mungu “Umekaribia�

Hakika mtu mmoja atanukuu Marko 1:15, mahali ambapo Kristo alikuwa amehubiri kwamba “ufalme wa Mungu umekaribia.†Kumbuka kwamba, pale alikuwa ameenda mbele kuongeza, “Tubuni na kuiamini injili.†Hivyo baadhi wamehitimisha kwamba wakati watu wanapotubu na kuiamini injili, na kuwa sehemu ya kanisa, muda huo huo pia wanauingia ufalme wa Mungu, ambao kana kwamba, ulikuwa, ukiwangoja—ulikuwa “umekaribia.â€

Kama ilivyo Luka 17:21, watu wanalisoma fungu na kulichukulia kwa namna ile wanavyotaka liseme. Kristo hakusema ufalme wa Mungu ulikuwa umesimamishwa au kusimikwa—au kwamba ulikuwa ni kanisa. Haya yote ni “mapokeo ya wanadamu†ambayo watu waliyashika badala ya Neno dhahiri la Mungu (Marko 7:7).

Luka 16:16 ilionyesha kwamba tangu wakati wa Yohana Mbatizaji, ufalme wa Mungu ulikuwa ni kitu kilichokuwa “kinahubiriwa.†Ufalme ulikuwa haujafika bado, lakini wakati huo ulikuwa unahubiriwa. Kuhubiri ufalme na kupata fursa ya kufuzu kuuingia bila shaka wakati huo (na bado sasa), “viko karibu.â€

Watakatifu Kutawala Pamoja na Kristo

Kabla ya kurudi kwa Luka, hebu tuchunguze zaidi kile ambacho Danieli alikirekodi kuhusu ufalme wa Mungu.

Kumbuka kwamba Kristo atakuja kama vile umeme ung’aavyo kutoka mashariki mpaka magharibi (Math. 24:27) katika tukio kubwa mno ambalo hakuna mtu yeyote atakayelikosa. Lakini je! Atakuja kutawala dunia pekee Yake?—au kutakuwepo na wengine watakaokuja pamoja Naye? Tungeweza kuuliza: Wakati Kristo anaposimamisha serikali Yake itawalayo ulimwengu mzima, kina nani wengine wanaweza kuwa sehemu ya muundo ule Atakaousimamisha? Ikiwa serikali za wanadamu zinahitaji nguvu za wengi, wanaomsaidia kiongozi mkuu, je serikali ya Mungu ni tofauti? Hapana!

Danieli 7:13 inaongelea juu ya Kristo akija katika “mawingu ya mbinguni.†Kumbuka kwamba, kabla ya Kurudi Kwake, Mungu Anampa rasmi madaraka ya kutawala ulimwengu anaorudi kwake. Fungu linalofuata linasema, “Naye AKAPEWA mamlaka, na utukufu, na ufalme, ili watu wa kabila zote, na mataifa yote, na lugha zote, wamtumikie; mamlaka Yake ni mamlaka ya milele, ambayo hayatapita kamwe, na ufalme Wake ni ufalme usioweza kuangamizwa†(fu. 14).

Tunauliza tena, ikiwa Kristo anatawala peke yake, au kuna wengine watatawala pamoja Naye? Namna gani hasa Mungu anakusudia kuwaongoza watu wote na mataifa yote ya dunia?

Mafungu kadhaa zaidi katika Danieli 7 lazima yarudiwe kwa sababu ni muhimu sana yakaeleweka. Kumbuka kwamba ufalme wa Mungu umetabiriwa kuchukua mahali pa falme nne zilizoelezewa huko nyuma ambazo zilitawala ulimwengu mzima, zilizoelezewa katika sura ya 2. Sasa angalia mafungu ya 17-18: “Wanyama hao wakubwa walio wanne ni wafalme wanne watakaotokea duniani. Lakini watakatifu Wake Aliye Juu wataupokea ufalme, na kuumiliki huo ufalme milele, naam hata milele na milele.â€

Amini fungu hili kwa kile linachosema! Hatima ya mwito wa Wakristo ni kuungana pamoja na Kristo ili kushiriki utawala katika ufalme wa Mungu juu ya mataifa yote na watu wote. Hakika, Kristo ni “Mfalme WA WAFALME na Bwana WA MABWANA.†Hawa wafalme na mabwana wengine wanaweza kuwa wewe au mtu yeyote ambaye yuko radhi kukubali masharti ya Mungu kwa ajili ya kuuingia ufalme Wake.

Mafungu ya 19-20 yanatoa mwanga wa ziada juu ya kile kinachotokea wakati watakatifu wanaporudi pamoja na Kristo. Wajibu wao wa kwanza ni kuchukua mahali pa kile kinachoitwa “mnyama wa nne,†anayetawala kwa msaada wa “pembe ndogo.†Pembe ndogo hii ni UFALME WA KIDINI ambao ni sawa na yule mwanamke anayemwendesha mnyama wa Ufunuo 17. Serikali hii ya kidini (iliyoko Roma) imetawala juu ya kila ufufuo au uhuisho wa Himaya Takatifu ya Rumi huko nyuma, tangu 554 BK.

Sasa soma mafungu ya 21-22: “Nikatazama, na pembe iyo hiyo ilifanya vita na watakatifu [kazi dhahiri ya kahaba wa Kibabeli wa Ufu. 17:5-6], ikawashinda; hata akaja huyo Mzee wa Siku, nao watakatifu Wake Aliye juu wakapewa hukumu; na majira yakawadia watakatifu waumiliki ufalme.â€

Hatimaye, unabii mrefu wa Danieli unahitimisha na fungu la 27 linalothibitisha zaidi uwezekano ujao wa ajabu kwa watakatifu wote wa kweli wa Mungu. Angalia: “Na ufalme, na mamlaka, na ukuu wa ufalme, chini ya mbingu zote, watapewa watu wa watakatifu Wake Aliye juu; ufalme Wake ni ufalme wa milele, na wote wenye mamlaka watamtumikia na kumtii.â€

Nini chaweza kuwa dhahiri? Si ajabu Kristo alisema, “Na yeye ashindaye, na kuyatunza matendo yangu hata mwisho, nitampa mamlaka juu ya mataifa, naye atawachunga kwa fimbo ya chuma, kama vyombo vya mfinyanzi vipondwavyo, kama Mimi Nami nilivyopokea kwa Baba Yangu†(Ufu. 2:26-27) na, mafungu machache baadaye, aliongeza, “Yeye ashindaye, nitampa kuketi pamoja Nami katika kiti Changu cha enzi...†(Ufu. 3:21).

Usemi “katika kiti Changu cha enzi†umetumika kwa sababu Kristo alijua kiti Chake cha enzi kiko katika dunia hii, tofauti na cha Baba, ambacho kiko mbinguni. Luka 1:32 inaonyesha kwamba Kristo ataketi Yerusalemu katika Kiti cha Enzi cha Daudi. (Pia angalia Ufunuo 5:10, 20:4, Mathayo 5:5, Zaburi 25:12-13 na 37:11.) Hapawezi kuwa na shaka kwamba Kristo Atakaporudi, watakatifu watatawala pamoja Naye—DUNIANI!

Hebu sasa tuchunguze mfano mpana na wa muhimu sana ambao Kristo aliutoa ili kwamba watu wapate kufahamu kuja kwa ufalme wa Mungu na wajibu wa Mkristo KUFUZU ili kuwa sehemu yake.

Mfano wa Mafungu ya Fedha

Luka 19:11-29 iliyorejelewa mapema, ina mfano ulioandikwa kuelezea kile kitakachotokea ufalme wa Mungu utakapokuja. Ndani yake, Kristo alijilinganisha na Kabaila aliyekwenda “nchi ya mbali†(mfano wa kuungana na Baba mbinguni) kwa takribani miaka 2,000, mpaka Kurudi Kwake. Wanafunzi waliamini kwamba ufalme wa Mungu “ungetokea mara moja,†na Kristo alitaka kuonyesha kwamba muda mrefu utapita kabla haujaja.

Katika mfano huu, Kristo aliondoa kabisa wazo lolote kwamba ufalme ungeonekana mara moja katika umbo la Kanisa Lake. Na, kwa hakika, bado Hajarudi kwenye dunia hii.

Yule “Kabaila†kwenye mfano “aliwaita watumishi wake kumi†(mfano wa Wakristo wakiitwa na Mungu kutoka katika ulimwengu huu) na akawaagiza kuongeza thamani ya “fungu la fedha†ambalo Alimpatia kila mmoja wao kwa ajili ya kuwekeza. Fungu la fedha kwa hakika linawakilisha aina ya kipimo cha thamani ya msingi ya kiroho. Kumbuka kwamba ulikuwa mfano, hivyo Kristo alikuwa harejelei aina yoyote ya fedha halisi. Aliwaambia watumishi Wake “Wekezeni mpaka Nitakapokujaâ€â€”au “kuzalisha†fungu la fedha kuwa pesa nyingi zaidi. Wakati Kabaila alipokuwa ameenda Zake, watumishi wake kadhaa walisema, “Hatutaki mtu huyu atawale juu yetu.†Ni muhimu kufahamu kusudi la kauli hii.

“Raia†hawa walifahamu kwamba yule Kabaila (Kristo) alikuwa anakuja “kutawala†duniani. Hawakutaka kuwa sehemu ya huu utawala na wakaikataa serikali Yake (utawala) juu yao—na hivyo sehemu yao ndani yake utakapokuja (fu. 27). Katika mfano ule, walielewa kwamba ufalme wa Mungu ungekuwa SERIKALI inayotawala juu ya dunia. Kumbuka, mfano ulikuwa umeanza na Kabaila yule (Kristo) akienda mbinguni “kuupokea ufalme Yeye binafsi na kurudi.â€

Wakati Kabaila yule aliporudi, Alimwita kila mmoja wa watumishi kuja mbele Yake kupokea ripoti ya jinsi gani alivyoongeza fungu la fedha alilokuwa amepewa. Baadhi walikuwa wamepata mafungu matano, wengine kumi, nk., lakini mtumishi mmoja alikuwa amezika fungu lake ardhini na hakulitumia kuzalisha chochote. Kristo alitaka hesabu ya jinsi ambavyo “kila mtu alikuwa amepata†wakati akiwa ameenda Zake.

Mtumishi wa kwanza alikuwa amepata mafungu kumi na Kristo alifafanua thawabu yake kwa kusema, “Vema, mtumwa mwema; kwa vile ulivyokuwa mwaminifu katika neno lililo dogo, uwe na mamlaka juu ya miji kumi†(fu. 17).

Mtumishi aliyekuwa amepata mafungu matano aliwekwa “juu ya miji mitano.†Kwa sababu mtumishi wa pili alikuwa amezalisha nusu ya yule wa kwanza, thawabu yake ilikuwa nusu vile vile. Hivyo watu hawa walipewa “mamlakaâ€â€”waliwekwa kwenye nafasi za utawala “juu ya miji.†Thawabu yao ilikuwa ni “kutawala†pamoja na Kristo (Yuda 14) katika ufalme Wake unaotawala ulimwengu mzima. Ni wazi jinsi gani!—lakini ni wazi kwa wale tu ambao wanachukua muda kuisoma Biblia!

Mtumishi aliyezika fungu lake la fedha kwenye leso alikuwa amepoteza fursa ya ajabu ya kufuzu kwa ajili ya utawala katika ufalme wa Mungu. Inasema, “Akaamwambia [Kabaila Yule, Yesu], Nitakuhukumu kwa kinywa chako, mtumwa mwovu wewe.â€

Mtumwa huyu hakukua. Hakuzalisha chochote katika maisha yake na hivyo hakufuzu kwa ajili ya utawala juu ya miji katika ufalme wa Mungu. Kristo alimpatia yule aliyepata mafungu kumi thawabu ya yule mtumwa mwovu—hivyo huyu akawa na thawabu kubwa zaidi kuliko iliyokuwa sitahili yake. Miji ambayo aliikosa kwa sababu ya mwenendo wake lazima itawaliwe na mtu mwingine. La sivyo, ingeachwa ukiwa, bila ya mtawala aliyepewa mamlaka juu yake.

Historia fupi inahitajika ili kuelewa vyema mazingira ya mfano huu. Kristo alikuwa Myahudi aliyekuwa anahubiri mfano huu katika nchi ya Yuda (Uyahudi). Yuda lilikuwa tu moja ya makabila kumi-na-mbili katika Israeli ya kale. Makabila kumi kati ya hayo yalikuwa yamepoteza utambulisho zaidi ya miaka 700 kabla, kwa sababu walikuwa wamemwasi mtoto wa Sulemani, Rehoboamu. Walikuwa wamechukuliwa mateka na Waashuru wa kale na kisha baadaye wakahamia Ulaya ya Kaskazini-magharibi, wakawa kimsingi watu wazungumzao Kiingereza-wa-nchi-za-kidemokrasia za Marekani, Uingereza, Kanada, Australia, New Zealand na baadhi ya mataifa ya Ulaya Magharibi. Ni baadhi ya watu wa makabila ya Benjamini na Lawi waliobaki na Wayahudi, ambao mji wao mkuu ulikuwa Yerusalemu.

Wakati Mfano wa mafungu ya fedha unapozungumzia juu ya raia wa Kabaila “kumchukia,†na unasema kwamba walisema, “Hatutaki Mtu huyu atutawale,†ni kielelezo kwa Wayahudi. Historia inarekodi dhahiri kwamba walikataa mamlaka ya Yesu Kristo. Hiki ndicho ambacho Yohana 1:11 inamaanisha pale inaposema kwamba “Alikuja kwa walio Wake, wala walio Wake hawakumpokea.†Wale “watumishi kumi†(wale Wakristo wanaoitwa sasa) wanakuwa kielelezo, katika mfano, kwa MAKABILA KUMI ya Israeli yaliyopotea. Kristo aliwaahidi fursa ya kutawala, kwa sababu Wayahudi walikataa mamlaka Yake juu yao.

Kwa masikitiko, baadhi hawataki Kristo wa kweli wa Biblia awaambie nini cha kufanya. Hawataki Atawale juu ya maisha na mienendo yao. Lakini wanataka wokovu—bila masharti!

Hakuna mtu atakayepewa utawala kabla hajathibitisha kwamba anaweza kutawaliwa! Hakuna yeyote anayeweza kuwa sehemu ya serikali ya Mungu itawalayo ulimwengu isipokuwa amejifunza kujisalimisha kwa serikali ya Mungu na kutawaliwa na Mungu na Yesu Kristo katika maisha haya. Hili ndilo fundisho muhimu la mfano wa talanta.

Wakati Kristo alipowaita watumishi Wake kutoa hesabu, Alikuwa anaonyesha kwamba siku moja watu wote watasimama na kutoa hesabu mbele ya kiti cha hukumu cha Kristo (2 Kor. 5:10). Kama ilivyo thawabu ya mitume kumi na wawili, ambao watawekwa juu ya makabila kumi na mbili ya Israeli (Math. 19:27-28), baadhi watapewa MAMLAKA zaidi ya kutawala juu ya miji pamoja na Kristo “katika kiti cha enzi cha utukufu Wake.â€

Ufalme Utakuja LINI?

Wote wanataka kujua Kristo atarudi lini. Wanafunzi walimwuliza, “Nayo ni nini dalili ya kuja Kwako, na ya mwisho wa dunia?†(Math. 24:3).

Mafungu yote arobaini-na-nane yanayofuata katika Mathayo 24 ni jibu la Kristo likitoa undani wa matukio mengi, kwa mfuatano, ambayo yangetangulia Kuja Kwake. Katika fungu la 36, anarejelea wakati wenyewe hasa wa Kuja Kwake, Alisema, “Walakini habari ya siku ile na saa ile hakuna aijuaye, hata malaika walio mbinguni, wala Mwana, ila Baba Yangu peke yake.â€

Majuma machache tu baadaye, katika Matendo 1:6-7, kabla ya Kristo kupaa kwa mara ya mwisho kurudi mbinguni, wanafunzi walithibitisha kwamba walikuwa bado hawajaelewa wala kukubali hasa ufafanuzi Wake wa nyuma. Hivyo, walimwuliza tena. Angalia: “...wakamwuliza, wakisema, Je! Bwana, wakati huu ndipo UNAPOWARUDISHIA Israeli ufalme? Akawaambia, Si kazi yenu kujua nyakati wala majira, Baba Aliyoyaweka katika mamlaka Yake Mwenyewe.†Kristo aliwapa jibu lile lile kama katika Mathayo—“Si kazi yenu kujua nyakati wala majira.â€

Ni muhimu kuzingatia kwamba Kanisa la Agano Jipya lingesimamishwa siku kumi tu baada ya tukio hili (2:1). Kwa nini Kristo aliwajibu, “Si kazi yenu kujua nyakati wala majira†ikiwa ufalme wa Mungu ulikuwa unaenda kuwa ni Kanisa, ambalo lilikuwa linaenda kusimamishwa mara moja (kwenye siku ya Pentekoste)—siku kumi tu baadaye?

Vivyo hivyo ni kweli kwetu leo. Hatuwezi kujua lini hasa ufalme wa Kristo utakuja, lakini tunaweza kujua makadirio ya karibu—na wakati huu uko karibu. Katika Luka 21:31, mwishoni mwa unabii mrefu unaoenda sambamba na Mathayo 24, Kristo alisema, “Nanyi KADHALIKA, mwonapo mambo hayo [matukio muhimu] yanaanza kutokea, tambueni ya kwamba ufalme wa Mungu u karibu.â€

Aliwataka wajue kwamba “mtapokea NGUVU, ikiisha kuwajilia juu yenu Roho Takatifu†(Matendo 1:8), lakini si kujua hasa lini ufalme utawasili. Ndivyo ilivyo kweli kwa wale wote wanaoongoka leo. Hatuwezi kujua lini hasa Kristo atarudi, lakini tunaweza kujua kwamba tutapokea nguvu sasa ili kukua na kushinda—na kuihubiri injili ya ufalme wa Mungu mpaka atakapokuja.

Mungu Kuingilia Kati au Ulimwengu Kuangamia

Tunaishi katika zama za hatari. Hali ya mambo ulimwenguni inaendelea kuharibika. Vita ya III ya dunia ya Nyuklia inatishia mbele ya upeo wa macho. Uwezo wa teknolojia ya kijeshi yenye uwezo wa kuangamiza wanadamu wote duniani sasa ipo. Fikra kuu za ulimwengu zinaona kwamba serikali moja ya dunia ndiyo kitu pekee ambacho kinaweza kumzuia mwanadamu asijiangamize mwenyewe. Lakini bado viongozi hawa hawa pia wanafahamu kwamba serikali ya muungano wa ulimwengu mzima haiwezekani ikiwa wanadamu wataiongoza.

Hivyo mwanadamu anakabiliwa na uchaguzi wa aina mbili; ama Mungu aingilie kati kumzuia asijiangamize mwenyewe, au ateketee.

Wakati mbaya kuliko wowote ambao ulimwengu umeshawahi kuona—Dhiki Kuu—karibu utaufikia ubinadamu usioshuku [usio tilia shaka]. Matokeo yake kama Mungu hataingilia kati—“kama siku hizo zisingalifupizwaâ€â€”ni kwamba, “asingeokoka mtu ye yote.†Mungu kwa rehema ataingilia na kumwokoa mwanadamu kwa kumtuma Kristo kusimamisha serikali Yake itawalayo ulimwengu ilete amani kwa mwanadamu. Atawalazimisha wanadamu kuishi katika mapatano na wanadamu wengine.

Serikali hii haitaongozwa na wanadamu. Yesu Kristo mwenye nguvu zote, aliye hai ataileta. Historia inarekodi kwamba serikali katika mikono ya wanadamu hushindwa kila wakati! Ni kwa uwezo wa Mungu tu ndipo serikali hii itawalayo ulimwengu mzima hatimaye inaweza kufanikiwa katika kuleta amani ya ulimwengu.

Juhudi za Wanadamu Haziwezi Kuleta Amani ya Ulimwengu

Wakristo wa kweli siyo wanaharakati wakitafuta “kuufanya ulimwengu huu mahali pazuriâ€â€”na hivyo kuuleta ufalme wa Mungu duniani. Wana “miguu yao imefungiwa utayari tupatao kwa injili ya amani†(Efe. 6:15). Wanatembea maishani huku “miguu†yao ikiwa imefunikwa na maarifa ya jinsi injili ya kweli inavyoonyesha njia pekee kuifikia amani ya dunia ya kudumu. Wanaelewa bila shaka kwamba ufalme wa Mungu—unaoleta “serikali na amani†(Isa. 9:6-7)—unakuja. Wanajua kile kilicho mbele kwa ajili ya ulimwengu huu.

Hawaendi kutumika na kuua katika vita visivyo na mwisho, vya wanadamu na mataifa, visivyo na manufaa, au kushiriki katika masuala ya serikali za wanadamu. Wala hawachukui mambo katika mikono yao wenyewe, na kujaribu kufanya kile kinachodhaniwa “kueneza ufalme,†hivyo kuhafifisha kusudi la Mungu, ambalo ni kumwonyesha mwanadamu kwamba hawezi kujitawala mwenyewe!

Badala yake, wanashiriki kwa juhudi katika kuwezesha Kazi muhimu kuliko zote juu ya uso wa dunia—Kazi ambayo umekutana nayo!

Pia wanatambua kwamba Mpango wa Mungu wa kupangilia matukio ya ulimwengu unaenda kwa ratiba Yake. Wanajua ni lazima wakue na kushinda sasa, kana kwamba hakuna kesho. Angalia kwamba Paulo alivuviwa kuandika: “Maana ninyi wenyewe mnajua yakini ya kuwa siku ya Bwana yaja kama vile mwivi ajavyo usiku. Wakati wasemapo, Kuna amani na salama, ndipo uharibifu uwajiapo kwa ghafula, kama vile utungu umjiavyo mwenye mimba, wala hakika hawataokolewa. Bali ninyi, ndugu, hammo gizani, hata siku ile iwapate kama mwivi†(1 Thes. 5:2-4).

Wale wote wanaozifahamu kweli za kitabu hiki hawahitaji kuwa gizani tena kamwe kuhusu Mpango wa Mungu au uwezekano wa jukumu lao la kustaajabisha ndani yake.

Akinukuu Isaya 52:7, Paulo pia alirekodi, “Jinsi ilivyo mizuri juu ya milima Miguu yake ahubiriye injili ya amani, Aletaye habari njema [habari njema ya injili] ya mambo mema†(Rum. 10:15). Katika fungu la 16, aliendelea mbele kunukuu aya nyingine kutoka kitabu cha Isaya: “Lakini si wote walioitii ile habari njema [injili]. Kwa maana Isaya asema, Bwana, ni nani aliyeziamini habari zetu?†(53:1).

Kwa hakika, watu wengi hawataamini “habari za Mungu†kuhusu kile kilicho mbele ya ustaarabu. Hawataamini kwamba hawawezi kuleta amani ya ulimwengu kupitia juhudi za mwanadamu. Wengi watasema kwa sauti “Amani, amani; wakati hakuna amani†(Yer. 6:14; 8:11, 14-15), na wengi wataendelea mbele kwa shauku wakiamini utabiri wao wa uongo, hata mbele ya kushidwa kuliko wazi kabisa.

Wale wanaojidai kuwa Wakristo wa ulimwengu huu wataendelea kujitahidi kuuleta ufalme wa Mungu na amani ya ulimwengu kupitia juhudi za wanadamu bila mafanikio. Viongozi wa dini waliodanganywa watawaambia kwamba huu ndio “wajibu wao wa Kikristo.†Wengi wataona huu ndio utume pekee wa kanisa lao. Mamilioni wanatazamia furaha, ustawi, amani na usalama kila mahali—lakini watakatishwa tamaa vibaya ndani ya kipindi kifupi. Hii ni kwa sababu hali ya mambo ulimwenguni, inayoelekea kwenye kipindi kibaya cha janga la ulimwengu wote, itakuwa mbaya zaidi kabla haijageuka hatimaye kuwa njema.

Jiji la Amani, Hatimaye

Lakini mwishoni, ulimwengu HAUTAKATISHWA tamaa! Habari njema iko mbele.

Makao makuu ya taifa la Kiyahudi la Israeli wakati huu ni Yerusalemu. Japokuwa jiji hili halijajua chochote bali vita katika historia yake yote, jina lake hakika linamaanisha “JIJI LA AMANI.†Linabeba jina hili kwa sababu Kristo—MFALME WA AMANI—atarudi pale kusimamisha ufalme Wake. Mfalme wa Amani atatawala kutoka Jiji la Amani. Ikianzia katika jiji hili moja, amani itaenea haraka ulimwenguni. Hatimaye, “itatokea†kila mahali!

Mwisho, amani ya kweli ya ulimwengu, furaha, ustawi na mafanikio vitakuja katika wakati wa maisha yako. Ni hakika kama lilivyo Neno la Mungu!

“Ufalme Wako Ujeâ€

Watu wengi wanaelewa kile kinachoitwa “Sala ya Bwana.†Wengi wanaweza kuikariri bila kutumia nguvu nyingi, wakiwa wamefanya hivyo mara nyingi bila kufahamu kwamba ni kielelezo tu au mwongozo wa jinsi ya kusali. Nilijifunza sala hii nilipokuwa na umri wa miaka minne. Inaanza, “Baba yetu uliye mbinguni, Jina Lako litukuzwe, Ufalme Wako uje. Mapenzi Yako yatimizwe, hapa duniani...†(Math. 6:9-27). Ombi hili fupi linaendelea kwa mafungu matatu zaidi. Lakini, kati ya mamilioni wanaoijua na kuitumia, ni wangapi hasa ambao hufikiri kuhusu usemi “Ufalme wako ujeâ€â€”au “mapenzi [Mpango Wake Mkuu] ya Mungu yatimizwe hapa dunianiâ€? Kwa miaka 2,000, kimsingi huenda wengi wametafuta kufuata maagizo ya Kristo, kuomba, “ufalme Wako uje†bila hasa kutafakari maana ya kushangaza iliyo nyuma ya usemi huu mfupi.

Wewe umetafakari?

Mafungu machache tu baadaye, katika sura hiyo hiyo, Yesu aliagiza, “Bali utafuteni kwanza ufalme wa Mungu, na haki Yake; na hayo yote mtazidishiwa†(fu. 33). Ni lazima Wakristo waendelee kutafuta ufalme wa Mungu KWANZA—juu ya kitu kingine chochote—katika maisha yao! Wanawezaje kufanya hili kama hawajui ni kitu gani—au lini utakuja—au jinsi gani unavyoathiri wokovu wao wenyewe?

Lakini sasa UNAJUA!

Je! Utasali, “ufalme Wako uje� Je! Utaufanya mwito wako na uteule wako imara†(2 Pet. 1:10)? Je! Utashinda kama Kristo alivyoshinda? Utakua, ufuzu, na kuongezeka katika tabia ya kiroho—kuzalisha fedha nyingi zaidi kuliko ulipoanza, hivyo Mungu atapata “faida†kutokana na uwekezaji Wake ndani yako? Au utazika fungu lako la fedha, na pamoja na hilo fursa yako ya kutawala juu ya mataifa yote katika ufalme wa Mungu—kuwafundisha wengine njia sahihi ya maisha?

Je! Utatimiliza UWEZEKANO wako WA KUSTAAJABISHA?

Pengine ungependa kusoma: